Njoo, Unifuate
Novemba 2–8. Mormoni 7–9: “Ninawazungumzia kama Vile Mlikuwa Hapa”


“Novemba 2–8. Mormoni 7–9: ‘Ninawazungumzia kama Vile Mlikuwa Hapa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Novemba 2–8. Mormoni 7–9,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Moroni Akiandika kwenye Bamba za Dhahabu, na Dale Kilborn

Novemba 2–8

Mormoni 7–9

“Ninawazungumzia kama Vile Mlikuwa Hapa”

Rejea misukumo uliyoiandika wakati wa kujifunza kwako binafsi Mormoni 7–9 wiki hii. Ni vifungu gani vya maneno kutoka kwenye sura hizi unahisi vitakuwa na maana zaidi kurejea na darasa lako?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwapa washiriki wa darasa nafasi ya kushiriki kitu fulani walichojifunza katika kujifunza kwao binafsi au kama familia, ungeweza kuwahimiza pitia haraka haraka Mormoni 7–9 na kushiriki sentensi (au mstari) ambao wanashukuru Mormoni au Moroni aliuchagua kuujumuisha katika bamba.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mormoni 7:8–10; 8:12–22; 9:31–37

Kitabu cha Mormoni ni cha thamani kubwa.

  • Njia moja ya kutambulisha mjadala kuhusu thamani kubwa ya Kitabu cha Mormoni ni kwa kuzungumza kuhusu jinsi tunavyoamua thamani ya kitu. Ni kwa jinsi gani kujua thamani ya kitu hubadilisha jinsi tunavyokitumia? Washiriki wa darasa wangeweza kupekua Mormoni 8:12–22 na kushiriki kile Moroni alikisema kuhusu thamani ya Kitabu cha Mormoni (“maandiko haya”). Wangeweza pia kushiriki uzoefu binafsi ambao umewaonesha thamani ya Kitabu cha Mormoni. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini Kitabu cha Mormoni?

    Picha
    nakala za Kitabu cha Mormoni katika lugha tofauti

    Kitabu cha Mormoni hufafanua mafundisho yaliyofundishwa katika Biblia.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua jinsi Kitabu cha Mormoni na Biblia vinavyosaidiana, ungeweza kuwaalika kusoma Mormoni 7:8–10 na kufanyia ufupisho ufafanuzi wa Mormoni wa kumbukumbu mbili kwa maneno yao wenyewe (“maandishi ambayo yatawajia Wayunani kutoka kwa Wayahudi” humaanisha Biblia). Fikiria kuchora duara mbili zinazokutana ubaoni na kuipa moja jina Biblia na nyingine Kitabu cha Mormoni. Washiriki wa darasa wangeweza kuorodhesha mfanano kati ya vitabu viwili vya maandiko katika sehemu inayokutana na tofauti katika sehemu zingine. (Video “Bible and Book of Mormon” kwenye ChurchofJesusChrist.org hutoa utambuzi.) Kama mbadala, fikiria kuorodhesha kweli kadhaa za injili ubaoni na kuwaalika washiriki wa darasa kuangalia kwenye Mwongozo wa Maandiko kutafuta mistari kutoka katika Kitabu cha Mormoni na Biblia ambayo huwasaidia kuelewa kweli.

Mormoni 8:1–11

Tunaweza kuwa waaminifu hata wakati tuko peke yetu.

  • Baadhi ya watu katika darasa lako wanaweza kuhisi wako peke yao katika juhudi zao za kuishi injili. Nini wanaweza kujifunza kutokana na mfano wa Moroni ambacho kingeweza kuwasaidia? Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kusoma Mormoni 8:1–11 na kufikiria maswali ambayo wangependa kumuuliza Moroni ili kujifunza kuhusu jinsi alivyobaki mwaminifu licha ya hali yake ngumu. Nini kinawavutia kuhusu mfano wake? Wakati wakishiriki mawazo yao, wahimize washiriki wa darasa kushiriki uzoefu binafsi wakati ambapo wao au wengine wanaowafahamu walibaki waaminifu, hata walipohisi wako peke yao. Ni kwa namna gani Bwana aliwasaidia?

Mormoni 8:26–41; 9:1–30

Kitabu cha Mormoni kiliandikwa kwa ajili ya siku yetu.

  • Mnapokaribia mwisho wa kujifunza Kitabu cha Mormoni kwa mwaka huu, pengine washiriki wa darasa wangeweza kupata taswira juu ya kwa nini wanahisi kitabu hiki kiliandikwa kwa ajili ya siku yetu. Ungeweza kuanza majadiliano kwa kusoma maelezo ya Rais Ezra Taft Benson katika “Nyenzo za Ziada.” Washiriki wa darasa kisha wangeweza kutumia maswali ya Rais Benson kwenye Mormoni 8:26–41. Kwa nini Bwana alimshawishi Moroni kujumuisha maneno haya katika kumbukumbu? Ni kwa jinsi gani yanatusaidia katika siku zetu?

  • Kama ilivyofundishwa katika muhtasari wa wiki hii kwenye Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia, Mormoni 9:1–30 ina ujumbe wa Moroni katika kujibu ukosefu wa imani katika Yesu Kristo katika siku zetu. Pengine ungeweza kuligawa darasa katika makundi matatu na kualika kila kundi kutafuta ushauri ambao una msaada kwao katika mistari ifuatayo: 1–6 (athari za kutokuamini katika Kristo), 7–20 (umuhimu wa kuamini katika Mungu wa ufunuo na miujiza), na 21–30 (ushauri wa Moroni kwetu).

  • Japokuwa Mormoni 9:1–6 iliandikwa kwa “wale ambao hawakuamini katika Kristo,” ni yenye msaada kwetu sote kupata taswira siku moja tumesimama mbele za Mungu ili kuhukumiwa. Waombe washiriki wa darasa kurejelea mistari hii, wakitafuta maneno au vifungu vya maneno ambavyo huelezea jinsi waovu watakavyohisi siku ile. Nini tunaweza kufanya kuepuka hisia hizi? Washiriki wa darasa wanaweza kupata umaizi katika hadithi iliyosimuliwa na Rais Boyd K. Packer katika “Nyenzo za Ziada.”

  • Watu wengi leo wanaamini kwamba miujiza imekoma. Ni kwa jinsi gani unaweza kutumia mafundisho ya Moroni kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuamini katika “Mungu wa miujiza”? Ungeweza kuanza kwa kuwauliza washiriki wa darasa kurejelea Mormoni 9:7–26 na kutafuta miujiza ambayo Moroni alitusihi tuiamini. Nini tunajifunza kutoka kwenye mistari hii kuhusu Mungu na kazi Yake katika siku yetu? Nini tunapaswa kufanya ili Mungu aweze kufanya Miujiza? (ona Mormoni 9:20–21). Ni miujiza ipi ambayo tumeiona?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Je, washiriki wa darasa lako wamewahi kujiuliza jinsi wanavyoweza kuongeza imani yao katika Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo? Kama ndivyo, waalike kupekua Etheri 1–5 kwa ajili ya njia za kusaidia imani yao kukua.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Kitabu cha Mormoni kiliandikwa kwa ajili ya siku zetu.

Rais Ezra Taft Benson alisema:

“Wanefi hawakuwahi kuwa na kitabu hiki; wala hata Walamani wa kale. Kilikusudiwa kwa ajili yetu. …

“Kila mmoja wa waandishi wakuu wa Kitabu cha Mormoni alishuhudia kwamba aliandika kwa ajili ya uzao wa siku zijazo [ona 2 Nefi 25:21; Yakobo 1:3; Mormoni 7:1; 8:34–35]. …

“Kama waliona siku zetu, na wakachagua mambo yale ambayo yangekuwa ya thamani kuu kwetu, Je,, hivyo sivyo tunavyopaswa kujifunza Kitabu cha Mormoni? Tunapaswa kujiuliza wenyewe kila mara, ‘Kwa nini Bwana alimshawishi Mormoni (au Moroni au Alma) kujumuisha hayo katika kumbukumbu zake? Ni somo gani ninaweza kujifunza kutokana na hilo litakalonisaidia kuishi katika siku hii na nyakati hizi?’”(“Kitabu cha Mormoni—Jiwe la Katikati la Tao la Dini Yetu,” Ensign, Nov. 1986, 6).

Tunaweza kutokuwa na mawaa.

Rais Boyd K. Packer alisimulia kuhusu kusafiri kwa siku sita kama mvulana akiwa na wafanyakazi wa jeshi kwenye garimoshi ya mizigo yenye joto na moshi, bila namna yoyote ya kuoga au kubadili nguo. Gari moshi liliposimama, wafanyakazi wenye njaa walienda kwenye mgahawa.

“Ulikuwa umejaa, na hivyo tulijiunga katika mstari mrefu kusubiri kukaa. Nilikuwa wa kwanza, nyuma tu ya baadhi ya wanawake waliovalia kinadhifu. Hata bila kugeuka, mwanamke mwenye madaha mbele yangu mara akawa na ufahamu kwamba tulikuwa pale.

“Aligeuka na kututazama. Kisha akageuka na kunitazama kutoka kichwani hadi kidoleni. Pale nilisimama katika ile sare yenye jasho, chafu, yenye moshi, iliyokunjamana. Alisema kwa sauti ya kuchukizwa, ‘Jamani, watu wachafu kiasi gani!’ Macho yote yakatugeukia.

“Hapana shaka alitamani tusingekuwa hapo; mimi pia nilitamani vivyohivyo. Nilihisi mchafu kama nilivyokuwa, bila raha, na mwenye aibu.”

Rais Packer kisha alinukuu Mormoni 9:4 na kufananisha uzoefu wake na kuwa mchafu kiroho katika uwepo wa Mungu. Akishuhudia kwamba Upatanisho wa Yesu Kristo ulikuwa njia pekee angeweza kuwa msafi kiroho, kisha alisema:

“Unaweza kufikiria jinsi nilivyohisi wakati hatimaye nilipoweza kuona kwamba ikiwa ningefuata masharti yoyote ambayo Mkombozi aliweka, sihitaji kamwe kuvumilia maumivu ya kuwa mchafu kiroho? Fikiria hisia za faraja, za ukombozi, za kuinua ambazo zitakuja kwako pale unapoona uhalisia wa Upatanisho na thamani ya vitendo vyake vya kila siku kwako binafsi” (“Kuoshwa Safi,” Ensign, Mei 1997, 9–10).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Sali kwa ajili ya washiriki wa darasa lako. Je, kuna yeyote katika darasa lako anahangaika? Kama vile Mwokozi alivyosali kwa ajili ya Petro (ona Luka 22:31–32), unaweza kusali kwa ajili ya wale unaowafundisha ili waimarishwe (ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 6).

Chapisha