Mafundisho na Maagano 2021
Agosti16–22. Mafundisho na Maagano 89–92: “Kanuni Yenye Ahadi”


“Agosti 16–22. Mafundisho na Maagano 89–92: ‘Kanuni Yenye Ahadi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Agosti 16–22. Mafundisho na Maagano 89–92,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili

Picha
mwanamume na mwanamke wakitayarisha chakula

Agosti 16–22

Mafundisho na Maagano 89–92

“Kanuni yenye Ahadi”

Unapojiandaa kufundisha, fikiria kuhusu kanuni ambazo zilikuvutia zaidi ulipokuwa ukisoma sehemu za 89–92 wiki iliyopita.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Haya ni maswali unayoweza kutumia kuwahimiza washiriki wa darasa kushiriki kitu kutoka kwenye kujifunza kwao maandiko: Ulisoma nini wiki hii ambacho kiliimarisha imani yako katika Yesu Kristo? Katika mwito wa kinabii wa Joseph Smith? Ulisoma nini ambacho kilikusaidia kuelewa vizuri zaidi mpango wa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya watoto Wake?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 89

Neno la Hekima ni “kanuni yenye ahadi.”

  • Watu wengi hulichukulia Neno la Hekima kuwa tu kama orodha ya vitu vya “kufanya” na “kutofanya.” Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari kanuni za msingi za elekezo hili, waalike wachunguze Mafundisho na Maagano 89 wakiwa na maswali kama yafuatayo akilini: Ni kwa nini Bwana Alitupatia Neno la Hekima? Ni nini ufunuo huu unatufundisha kuhusu Baba wa Mbinguni na Mpango wake kwa ajili yetu? Kauli katika “Nyenzo za Ziada” inaweza kuwa yenye msaada. Kama unaona inaweza kuwanufaisha washiriki wa darasa, unaweza kuwaalika waorodheshe kwenye ubao mazoea ya afya na mazoea yasiyo ya afya yaliyotambulishwa na Bwana katika Mafundisho na Maagano 89:5–17. Kisha wanaweza kufanya mapitio ya “Afya ya Mwili na Akili” katika Kwa Ajili ya Nguvu ya Vijana (25–27) na waongeze kwenye orodha zao vitu vingine wanavyovipata. Je, ni kwa namna gani ahadi katika mistari 18–21 zimetimizwa katika maisha yetu?

  • Hii ni namna nyingine ya kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili kanuni katika Neno la Hekima. Unaweza kugawa darasa katika vikundi vitatu na ukiombe kila kikundi kisome sehemu ya 89, wakitafuta majibu ya mojawapo ya maswali yafuatayo: Ni kanuni zipi zinaweza kumtia moyo mtu anayepambana kutii Neno la Hekima? Ni kanuni zipi zinaweza kutusaidia tusiwe wenye kuwahukumu wale wanaopambana kulitii? Ni kanuni zipi zinaweza kutufariji wakati tunapopata shida za kiafya licha ya kuishi Neno la Hekima? Kama sehemu ya shughuli hii, unaweza kushiriki uzoefu wa Rais Dieter F. Uchtdorf wakati akifanya mazoezi ya kuwa rubani wa ndege za kivita (ona “Endelea kwa Uvumilivu,” Ensign au Liahona, Mei 2010, 58). Wahimize washiriki wa darasa kutafakari kitu ambacho walihisi kushawishiwa kufanya wakati wa majadiliano, na uwape muda wa kuandika misukumo yao.

    Picha
    wavulana wakikimbia ufukoni

    Mungu alifunua Neno la Hekima kwa ajili ya kuwasaidia watoto Wake.

Mafundisho na Maagano 90:1–17

Urais wa Kwanza unashikilia “funguo za ufalme.”

  • Mwongozo wa wiki hii katika Njoo, Unifuate Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kuwa waumini wachunguze Mafundisho na Maagano 90:1–17 ili wajifunze kuhusu Urais wa Kwanza. Ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki kile walichojifunza nyumbani kutokana na shughuli hii, au mnaweza kuchunguza mistari hii kama darasa. Washiriki wa darasa wanaweza pia kutafuta virai katika “Come, Listen to a Prophet’s Voice” (Nyimbo za Kanisa, na. 21) au wimbo mwingine kuhusu manabii ambao unaendana na mafundisho katika mistari hii. Je, ni jinsi gani huduma ya Urais wa Kwanza imekusaidia kuwajua Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Mafundisho na Maagano 91

“Roho hufunua ukweli.”

  • Leo katika ulimwengu, tunakabiliana na jumbe ambazo zina “mambo mengi … ambayo ni ya kweli” na “mambo mengi … ambayo si ya kweli” (mistari 1–2). Waalike washiriki wa darasa waangalie katika sehemu ya 91 kwa ajili ya ushauri kuhusu Apokrifa ambao unaweza kuwasaidia kugundua ukweli katika jumbe watakazozipata. Ni mifano ya aina gani wanaweza kushiriki ya namna ambavyo Roho amewasaidia kutambua ukweli?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Neno la Hekima.

Mzee Boyd K. Packer alifundisha:

“Neno la Hekima ‘lilitolewa kwa kanuni yenye ahadi’ [Mafundisho na Maagano 89:3]. Neno hili kanuni katika ufunuo huo ni la muhimu sana. Kanuni ni kweli ya kudumu, sheria, na desturi ambayo unaweza kuitumia ili ikuongoze katika kufanya maamuzi. Kawaida kanuni huwa hazifafanuliwi kwa maelezo mengi. Hilo linakuacha uwe huru kutafuta njia yako pamoja na ukweli wa kudumu, kanuni, kama nanga yako.

“Waumini huandika wakiuliza ikiwa kitu hiki au kile ni kinyume na Neno la Hekima. Inajulikana vyema kwamba chai, kahawa, pombe, na tumbaku ni kinyume na Neno la Hekima. Haijaelezwa kwa maelezo mengi. Bali, tunafundisha kanuni pamoja na baraka zilizoahidiwa. Kuna vitu vingi vinavyosababisha mazoea, vinavyoleta uraibu ambavyo mtu anaweza kunywa au kutafuna au kuvuta au kujichoma vinavyodhuru mwili na roho ambavyo havijatajwa katika ufunuo. …

“Heshimu kanuni ya Neno la Hekima na utapokea baraka zilizoahidiwa” (“Neno la Hekima: Kanuni na Ahadi,” Ensign, Mei 1996, 17–18).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Toa ushuhuda kila mara. Ushuhuda wako rahisi, wa dhati kuhusu kweli za kiroho unaweza kuwa na ushawishi wenye nguvu kwa wale unaowafundisha. Ushahidi wako hauhitaji kuwa fasaha au mrefu. Unaweza, kwa mfano, kuwa ushuhuda rahisi wa baraka ambazo umepokea kutokana na kuishi Neno la Hekima. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 35.)

Chapisha