Njoo, Unifuate
Oktoba 28–Novemba 3. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: ‘Muwe kielelezo kwa Waaminio’


“Oktoba 28–Novemba 3. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: ‘Muwe Kielelezo kwao Waaminio’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

“Oktoba 283. 1 na 2 Wathesalonike 2–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Wanawake watatu wamesimama nje ya hekalu

Oktoba 28–Novemba 3

1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni

“Muwe Kielelezo kwao Waaminio”

Soma 1 na 2 Timotheo; Tito; na Filemoni ukiwa na washiriki wa darasa lako mawazoni mwako. Mawazo na misukumo itakayokuja itakusaidia kuwaelekeza washiriki wa darasa kwenye maandiko husika na kumleta Roho katika darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Itakuwa msaada kwa washiriki wa darasa kumsikia kila mmoja wao akiongea kuhusu mafanikio na changamoto katika kusoma maandiko, vyote kibinafsi na kifamilia. Fikiria kuanza darasa kwa kuwaalika washiriki wa darasa kuzungumzia nini kinaenda vizuri katika kujifunza maandiko kwako.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 na 2 Timotheo; Tito

Kuelewa fundisho la kweli kutatusaidia kuepuka kudanganywa.

  • Washiriki wa darasa lako wanaishi kwenye kipindi ambacho mafundisho ya uongo yanafundishwa. Timotheo na Tito pia waliishi katika kipindi kama hicho, hivyo labda ushauri wa Paulo kwao ungeweza kuwanufaisha washiriki wa darasa lako. Baadhi ya vifungu vilivyo na ushauri wa Paulo vinapatikana katika “Nyenzo za Ziada.” Ungeweza kumpa kazi kila mashiriki wa darasa kusoma mojawapo ya vifungu na kushiriki nini amejifunza kuhusu umuhimu wa fundisho la kweli (ona pia Alma 31:5).

1 Timotheo 4:10–16

Kama sisi ni “[vi]elelezo kwa waaminio,” tunaweza kuwaongoza wengine kwa Mwokozi na injili Yake.

  • Inawezekana kwamba washiriki wa darasa lako hawatambui nguvu ya kuwa kielelezo kizuri ambacho wamekuwa. Fikiria kuwaalika kuzungumzia jinsi gani watu wanaowajua, ikijumuisha washiriki wenzao wa darasa, wamekuwa vielelezo vya wafuasi wa Kristo. Ingeweza kusaidia katika mjadala kama ungeorodhesha kwenye ubao maneno katika mstari wa 12 ambayo yanaelezea jinsi gani tunatakiwa kuwa kielelezo—neno, usemi (ambalo pia yanaweza kumaanisha mwenendo au tabia), Hisani, roho, imani, na usafi. Washiriki wa darasa wangeweza kujadili ni kwa namna gani tunaweza kuwa kielelezo kwa waaminio katika kila njia hizi.

2 Timotheo 1

“Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.”

  • Katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia, Washiriki wa darasa lako walialikwa kuangalia katika 2 Timotheo kwa ajili ya ushauri Paulo aliompa Timotheo ili kumtia moyo katika kazi yake. Waombe washiriki wa darasa kushiriki umaizi wowote walioupata, au labda ungeweza kuwapa dakika chache kutafuta na kushiriki sehemu ya ushauri wa Paulo (sura ya 1 na baadhi ya mifano mizuri). Wangeweza pia kushiriki uzoefu ambapo Mungu aliwasaidia kushinda woga wao na kuwapa roho ya … nguvu na ya upendo, na ya moyo wa kiasi” (2 Timotheo 1:7).

2 Timotheo 3

Kujifunza maandiko kunaweza kutusaidia kushinda hatari za siku za mwisho.

  • Baada ya kumwonya Timotheo kuhusu “nyakati za hatari” zitakazokuja, Paulo alishuhudia juu ya nguvu na umuhimu wa maandiko (ona 2 Timotheo 3:1, 14–17). Ili kuanzisha mjadala kuhusu umuhimu wa maandiko katika nyakati za hatari, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kurejea maelezo ya Paulo kuhusu hatari za siku za mwisho zipatikanazo katika 2 Timotheo 3:1–7. Kisha wangeweza kutafuta na kushiriki maandiko ambayo yamewasaidia kujikinga dhidi ya hatari kama hizi (baadhi ya mifano imeorodheshwa katika “Nyenzo za Ziada”). Ni kwa namna gani kujifunza kwetu maandiko kumetukinga dhidi ya shida katika dunia ya leo?

  • Kujifunza kutoka ushauri wa Paulo kuhusu nguvu ya maandiko kungeweza kuwa ni nafasi kwa washiriki wa darasa kutiana moyo wao kwa wao katika juhudi zao za kujifunza neno la Mungu. Labda washiriki wa darasa wangeweza kusoma 2 Timotheo 3:14–17 na kuainisha baraka na ulinzi ambao unaweza kuja kwa kujifunza maandiko. Kisha wangeweza kushiriki uzoefu wakati baraka hizi zilitimizwa katika maisha yao kwa sababu ya kujifunza maandiko kwao. Ungeweza pia kuwapa washiriki wa darasa muda fulani kutafakari nini wanaweza kufanya ili kuweza kuwa na uzoefu wenye maana kwenye maandiko, vyote kibinafsi na kama familia.

Filemoni

Wafuasi wa Kristo husameheana.

  • Kabla hujaanza mjadala kuhusu waraka kwa Filemoni, ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki baadhi ya taarifa kuhusu Filemoni na mtumishi wake Onesmo (kuna maelezo kwa ufupi katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia). Kisha kuligawanya darasa lako katika makundi na kuwapa kila kundi mojawapo ya maswali yafuatayo: Kuna usawa gani unaouona katika kile ambacho Paulo alikuwa radhi kukifanya kwa Onesmo na kile Mwokozi kwa radhi alikifanya kwetu? Wakati ilikuwa ngumu kwa Filemoni kumsamehe mtumwa wake aliyetoroka, ni kwa namna gani injili ya Yesu Kristo ingeweza kusababisha msamaha kuwa rahisi? Baada ya makundi kushiriki kile walichojifunza, fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki vifungu au uzoefu ambao uliwasaidia kuelewa vizuri zaidi kuhusu msamaha. Ujumbe wa Mzee Kevin R. Duncan katika “Nyenzo za Ziada” unaweza kusaidia katika mjadala huu.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ili kuwatia msukumo washiriki wa darasa kusoma waraka kwa Waebrania, waulize kama wanamjua mtu yoyote ambaye anahisi kwamba Mungu yu mbali, asiye na utu, au asiyekaribiwa. Waambie watapata mistari katika Waebrania 1–6 ambayo wangeweza kushiriki na mtu mwingine kuonyesha kuwa Mungu Baba na Yesu Kristo ni Watu wenye huruma ambao wanataka kutusaidia wakati tukiteseka.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni

Ushauri wa Paulo kuhusu fundisho la kweli.

Maandiko matakatifu ambayo hutulinda dhidi ya hatari za siku za mwisho zilizoelezewa katika 2 Timotheo 3:2.

Hatari za siku za mwisho

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Hatari za siku za mwisho

Wenye kujipenda wenyewe

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Yohana 15:12–13

Hatari za siku za mwisho

Wenye kutamani

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Mafundisho na Maagano 88:123

Hatari za siku za mwisho

Wenye kiburi

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Mosia 2:24–25

Hatari za siku za mwisho

Wenye kujivuna

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Alma 5:27–28

Hatari za siku za mwisho

Wenye kukufuru

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Mafundisho na Maagano 63:64

Hatari za siku za mwisho

Wasio heshimu wazazi

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Waefeso 6:1–3

Hatari za siku za mwisho

Wasio na shukrani

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Mafundisho na Maagano 78:19

Hatari za siku za mwisho

Wasio safi

Maandiko Ambayo Yanatulinda

Kumbukumbu la Torati 7:6

Mafuta ya uponyaji ya Upatanisho wa Mwokozi, hutusaidia kuwasamehe wengine.

Mzee Kevin R. Duncan alifundisha:

“Hakuna nafsi iishiyo ambayo haitatenda dhambi wakati mmoja au mwingine, kuwa mwathiriwa wa matendo ya uzembe ya mtu mwingine, mwenendo wa kuumiza, au hata tabia za dhambi. Hicho ni kitu kimoja ambacho sote tunalingana.

“Kwa shukrani, Mungu, kwa upendo na huruma Yake kwa watoto Wake, ameandaa njia ya kutusaidia wakati mwingine kupitia matukio ya misukosuko ya maisha. Ameandaa njia ya kuepuka kwa wale wanaoathiriwa na matendo maovu ya wengine. Ametufundisha kwamba tunaweza kusamehe! …

“Miaka mingi iliyopita, nikiwa natengeneza ua, kichane kiliingia kwenye kidole changu. Nilifanya jaribio dogo la kuondoa kichane hicho na nikafikiria nimeweza, lakini yamkini sikuwa nimeweza. Muda ukiwa unakwenda, ngozi ikawa inafunika kichane hicho, kukawa na uvimbe kwenye kidole changu. Ilikuwa inanisumbua na wakati mwingine kuuma.

“Miaka kadhaa baadaye niliamua kuchukua hatua. Nilichokifanya ilikuwa ni kupaka mafuta kwenye uvimbe na kufunga bandeji. Nilirudia zoezi hili mara kwa mara. Huwezi kuamini wakati siku moja, nilipoondoa bandeji, kipande cha mbao kilitokea kwenye kidole changu.

“Mafuta yalikuwa yamelainisha ngozi na kutengeneza njia kwa kile kitu ambacho kilinisababishia maumivu kwa miaka mingi sana. Baada ya kichane kutolewa, kidole kikapona haraka, na hadi leo, hakuna mabaki ya kuonyesha jeraha lolote.

“Kwa mfano kama huu, moyo usiosamehe hupenda sana maumivu ya bure. Tunapotumia mafuta ya uponyaji ya Upatanisho wa Mwokozi, Yeye atalainisha mioyo yetu na kutusaidia kubadilika. Anaweza kuponya nafsi iliyojeruhiwa (ona Yakobo 2:8)” (“Mafuta ya Uponyaji ya Msamaha,” Ensign au Liahona, Mei 2016, 33).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ukuaji wa kiroho hutokea nyumbani. Uko na washiriki wa darasa lako kwa muda mfupi tu kila Jumapili. Kwa muda wote uliobaki wa wiki, wengi wao wanakuwa na uzoefu wa kiroho wenye maana. Uliza maswali ambayo yatawahamasisha kushiriki kile walichojifunza nje ya darasa. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 18.)

Chapisha