Njoo, Unifuate
Disemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda: ‘Mungu ni Upendo’


Disemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda: ‘Mungu ni Upendo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

“Disemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Yesu Kristo akitabasamu wakati amekaa na mtoto.

Upendo mkamilifu, na Del Parson

Disemba 2–8

1–3 Yohana; Yuda

“Mungu ni Upendo”

Ni dhamira zipi na muundo ambao unaupata wakati unaposoma 1–3 Yohana na Yuda? Unawezaje kuvitumia ili uweze kuwasaidia washiriki wa darasa lako?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni kushiriki

Alika Kushiriki

Alika baadhi ya washiriki wa darasa kushiriki dhamira au kweli maalum ambazo wameziptata wakati wakisoma Waraka wa Yohana na Yuda. Ni jumbe zipi katika nyaraka hizi zilizokuwa na maana kwao na kwa familia zao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Yohana 1:5–10; 2:3–11; 3:1–3; 4:7–21; 5:1–3

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo ni mifano mikamilifu ya mwangaza na upendo.

  • Unawezaje kuwasaidia wale unaowafundisha kutambua Mwangaza wa Baba wa Mbinguni na upendo katika maisha yao? Ungeweza kuanza kwa kuandika mwangaza na upendo kwenye ubao. Waombe washiriki wa darasa kushiriki maneno ya kwanza ambayo huwajia akilini mwao wanapofikiria juu ya maneno haya mawili. Ungeweza kuligawanya darasa katika makundi na kutoa kwa kila kundi moja ya vifungu vya maandiko vifuatavyo: 1 Yohana 1:5–10; 2:3–11; 3:1–3; 4:7–12; 4:16–21; 5:1–3. Makundi yanaweza kutafuta vifungu hivi kwa ajili ya uthibitisho wa mwangaza na upendo wa Mungu na kwa vitu tunavyoweza kufanya ili kuonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa watoto Wake. Kisha washiriki wa kila kundi wangeweza kushiriki na darasa kile walichokipata. Ungeweza pia kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wakati walipohisi mwangaza na upendo wa Baba wa Mbinguni.

  • Unawezaje kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari mwangaza wa kiroho katika maisha yao? Ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kuangalia mwangaza kwenye dari au mwangaza unaokuja kupitia dirishani na kushiriki kile wanachojua kuhusu mwanga wa kawaida. Ni kwa namna gani mwangaza wa kawaida ni kama mwangaza wa kiroho? Labda ungechunguza Zaburi 27:1; Yohana 1:4–5; 1 Yohana 1:5–7; 3 Nefi 11:11; Mafundisho na Maagano 88:6–13 na uangalie umaizi wa ziada katika jinsi gani Mungu na mwana Wake hutoa mwangaza katika maisha yetu. Washiriki wa darasa wanaweza pia kushiriki uzoefu ambapo walitafuta na kupokea mwangaza wa kiroho katika maisha yao.

  • Washiriki wa darasa wangeweza kufurahia kuimba kwa pamoja au kusikiliza wimbo kuhusu mwangaza, kama vile “The Lord Is My Light” (wimbo, namba 89). Wimbo unafundisha nini kuhusu jinsi gani Bwana ni kama mwangaza? video “Choose the Light” (LDS.org) na kauli toka kwa Mzee Robert D. Hales katika “Nyenzo za Ziada” vingeweza kutoa umaizi zaidi kuhusu jinsi ya kupata mwangaza zaidi katika maisa yetu.

1 Yohana 2:18–23, 26–28; 4:3; 2 Yohana 1:7–11; 3 Yoahana 1:9–11; Yuda

Lazima tujiimarishe sisi wenyewe dhidi ya mafundisho ya uongo.

  • Baadhi ya washirirki wa darasa au wapendwa wao wanaweza kuwa wanasumbuka kukabiliana na mafundisho ya uongo ambayo yanatishia imani yao. Inaweza kuwasaidia kujifunza kile Yohana na Yuda walifundisha kuhusu ukengeufu. Fikiria kualika nusu ya darasa kutafuta maelezo juu ya mafundisho ya uongo au ukengeufu katika 1 Yohana 2:18–23, 26–28; 4:3; 2 Yohana 1:7–11; 3 Yohana 1:9–11 na nusu nyingine kutafuta maelezo hao kwenye Yuda. Au wangeweza kutafuta majibu ya maswali kama haya: Ni kwa namna gani Yohana na Yuda wanamwelezea mpinga kristo? (Ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Mpinga kristo,” scriptures.lds.org). Je, kuna chochote katika mistari hii ambacho kinaonekana hasa kinahusika katika changamoto tunazokumbana nazo leo? Ni kwa namna gani tunaweza kujiimarisha dhidi ya mafundisho ya uongo?

  • Yuda anatumia taswira ya kupendeza kuelezea walimu wa uongo au wale ambao “huyatukana mambo wasiyoyajua” (Yuda 1:10). Ungeweza kuwaalika washiriki wachache kuchora ubaoni baadhi ya taswira zilizoelezewa katika Yuda 1:12–13 wakati washiriki wengine wa darasa wakikisia ni kirai gani mtu anachora. Ni kwa namna gani taswira hizi huwakilisha walimu wa uongo na wapinga kristo? Kwa mfano, ni kwa namna gani vitendo viovu hutengeneza “mawaa katika karamu [zetu] za hisani”? Tunaweza kufanya nini ili kujiimarisha dhidi ya “wanaotudhihaki”? (ona Yuda 1:18–21). Ni kwa nini Yuda alipendekeza kwamba tuwe na huruma (Yuda 1:22) kwa wale ambao wanaidhihaki injili?

1 Yohana 5

Tunapotumia imani katika Kristo na kuzaliwa katika Mungu, tunaweza kuushinda ulimwengu

  • Mojawapo ya shughuli za wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inapendekeza kuchunguza 1 Yohana 5 ili kugundua jinsi gani tunaweza kuushinda ulimwengu. Labda ungewaalika washiriki wa darasa kushiriki nini walikipata na wakiandike ubaoni. (Ungeweza kuwapa muda kiasi darasani kupitia kwa haraka sura hii.) Au ungeweza kulialika darasa kusoma sehemu ya ujumbe wa Mzee Neil L. Andersen “Kuushinda Ulimwengu” (Ensign au Liahona Mei 2017, 58–62) na kushiriki walichojifunza. Kwa mfano, ni umaizi gani wanaoupata kutoka hadithi za Mzee Andersen akishiriki kuhusu Rais David O. McKay na Mzee Bruce D. Porter? Labda washiriki wa darasa wangeshiriki mifano yao wenyewe ya watu ambao wanahisi wamefanya juhudi kuushinda ulimwengu.

    Picha
    familia ikipiga magoti kwa pamoja kusali

    Injili ya Yesu Kristo inaweza kutusaidia sisi kupata amani katika ulimwengu wa dhiki.

3 Yohana 1:1–4

Shangwe huja pale tunapowasaidia wengine “kuenenda katika kweli.”

  • Kuna uwezekano kuna watu katika darasa lako ambao wanaweza kuhusisha na kile ambacho Yohana alikuwa akihisi aliposema kwamba hajapata “furaha kuu” zaidi ya kusikia kwamba Gaisa (mmoja wa “watoto wake”) alikuwa akienenda katika kweli. Washiriki wa darasa wanaweza kunufaika kutokana na kusikia uzoefu wa kila mmoja wao. Labda mngeweza kusoma kwa pamoja 3 Yohana 1:1–4 na maandiko katika “Nyenzo za Ziada.” Maandiko haya yanatufundisha nini kuhusu chanzo cha ukweli na furaha? Washiriki wa darasa wangeweza kuongea juu namna walivyohisi kama wazazi, wamisionari, viongozi wa kanisa, au walimu walipojua kwamba watu waliokuwa wakiwafundisha walikuwa wakienenda katika ukweli. Ungeweza kuwasiliana na washiriki wachache wa darasa kabla ya darasa na kuwaomba kuja na picha za watu ambao waliwasaidia kuwaleta kwa Kristo na kuzungumza kuhusu uzoefu wao.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ni kwa namna gani alama kama joka, mnyama pori mwenye mbawa, na mwana kondoo aliyechinjwa zinatufundisha kuhusu mpango wa Mungu kwa watoto Wake? Waalike washiriki wa darasa kufikiria kuhusu swali hili wanapojifunza Ufunuo wa Yohana ndani ya wiki ijayo.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

1–3 Yohana; Yuda

Nuru hufukuza giza.

Mzee Robert D. Hales alifundisha jinsi gani tunaweza kufukuza giza kutoka maishani mwetu na kutembea katika mwangaza.

Nilipokuwa mvulana mdogo, nilikuwa nikiendesha baiskeli yangu kwenda nyumbani kutoka kwenye mazoezi ya mpira wa kikapu usiku. Ningeweza kuunganisha vipande vya jenereta vya umbo la peasi kwenye tairi la baiskeli yangu. Kisha wakati nilipoanza kusokota pedali, tairi lingezungusha sehemu ndogo ya jenereta, ambayo ilizalisha umeme na kukaribisha mwale wa mwanga. Ulikuwa mfumo rahisi lakini wenye ufanisi. Lakini nilihitajika kusokota pedali ili kuufanya ufanye kazi! Nilijifunza haraka kwamba kama nitaacha kusokota pedali baiskeli yangu, mwanga ungekoma. Pia nilijifunza kwamba wakati nikiwa na ‘shauku kujihusisha’ [Mafundisho na Maagano 58:27] katika kusokota pedali, mwanga ungekuwa wa kung’aa zaidi na giza mbele yangu lingefukuzwa.

“Kizazi cha mwangaza wa kiroho huja kutokana na kusokota pedali baiskeli zetu za kiroho kila siku. Huja kutokana na kusali, kujifunza maandiko, kufunga, na kutumikia—kuishi injili na kutii amri” (“Kutoka kwenye Giza kwenda kwenye Nuru Yake kuu,” Ensign, Mei 2002, 71).

Maandiko kuhusu kuwasaidia wengine kuenenda katika kweli.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Sali juu ya washiriki wa darasa lako. Kama vile Mwokozi alivyosali kwa ajili ya Petro (ona Luka 22:32), unapaswa kusali kwa kutaja jina/majina ya wale unaowafundisha, ukitafuta kuelewa mahitaji yao maalum. Ufanyapo hivyo, Baba wa Mbinguni atatayarisha mioyo yao” (Alma 16:16) na kukusaidia kujua nini cha kufundisha ili kukidhi mahitaji yao (ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 6).

Chapisha