Njoo, Unifuate
Desemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda: ‘Mungu ni Upendo’


“Desemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda: ‘Mungu ni Upendo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

“Desemba 2–8. 1–3 Yohana; Yuda,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu Kristo akitabasamu akiwa amekaa na mtoto anayetabasamu

Upendo Mkamilifu, na Del Parson

Desemba 2–8

1–3 Yohana; Yuda

“Mungu ni Upendo”

Unaposoma nyaraka za Yohana na Yuda, tafuta mwongozo wa kiungu kuhusu jinsi unavyoweza kuonyesha upendo wako kwa Mungu. Andika misukumo hiyo na uifanyie kazi.

Andika Misukumo Yako

Wakati Yohana na Yuda walipoandika nyaraka zao, Ukengeufu uliotabiriwa ulikuwa mbioni, matokeo ya vyote mateso makali na mafundisho ya kupotosha. Baadhi ya walimu waongo walidiriki hata kutia shaka kama Yesu Kristo alikuja kweli “katika mwili” (ona, kwa mfano, 1 Yohana 4:1–3; 2 Yohana 1:7). Hivyo Mtume Yohana alianza waraka wake wa kwanza kwa kutoa ushahidi wake binafsi juu ya Mwokozi: “Huu ni ushuhuda ambao tunatoa wa lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima” (Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Yohana1:1 [katika 1 Yohana 1:1, rejeo a]). Lakini pengine ujumbe wenye nguvu zaidi wa nyaraka za Yohana ni upendo: upendo wa Mungu kwetu na upendo tunaopaswa kuwa nao Kwake na kwa watoto Wake wote. Hata hivyo, Yohana binafsi alikuwa na uzoefu wa upendo wa Mwokozi (ona Yohana 13:23; 20:2), na alitaka Watakatifu kuuona upendo kama ule wanapopitia magumu na upinzani, kwani “Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu” (1 Yohana 4:18).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

1 Yohana

Mungu ni nuru, na Mungu ni upendo.

Kama ingebidi uchague neno moja au mawili kumuelezea Mungu, maneno hayo yangekua yapi? Katika nyaraka zake, Yohana alitumia maneno “nuru” na “Upendo” (1 Yohana 1:5; 4:8, 16). Unaposoma 1 Yohana, tafakari uzoefu wa Yohana kama ilivyoandikwa katika Injili ya Yohana, na fikiria jinsi gani uzoefu huu uliweza kumfundisha Yohana kuhusu nuru na upendo wa Mungu. Ni uzoefu gani binafsi umekufundisha kwamba Mungu ni nuru na upendo?

Ona pia Yohana 3:16–21; 15:9–17; 2 Nefi 26:24; Mafundisho na Maagano 50:24; 88:6, 12–13; 93:36–37.

1 Yohana 2:24–3:3

Ninaweza kuwa kama Yesu Kristo.

Je, lengo la kuwa kama Kristo limewahi kuonekana la juu sana kwako? Fikiria ushauri wa Yohana wa kutia moyo: “Watoto wadogo, kaeni ndani yake; ili kusudi, atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri … [na] tutafanana naye” (1 Yohana 2:28; 3:2). Ni kitu gani unakipata katika 1 Yohana 2:24–3:3 ambacho kinakupa ujasiri na faraja kama mfuasi wa Yesu Kristo? Unapojifunza nyaraka za Yohana, tafuta kanuni zingine au ushauri unaoweza kukusaidia katika juhudi zako za kuwa zaidi kama Kristo.

Ona pia Moroni 7:48; Mafundisho na Maagano 88:67–68; “Kuwa Kama Mungu,” Mada za Injili, topics.lds.org.

Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Yohana 4:12

Hakuna “mtu … aliyemwona Mungu wakati wowote”?

Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Yohana 4:12 hufafanua kwamba “hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote, isipokuwa wale wanaoamini” (katika 1 Yohana 4:12, rejeo a; ona pia Yohana 6:46; 3 Yohana 1:11). Maandiko yanatoa matukio kadhaa ambapo Mungu Baba amejidhihirisha Mwenyewe kwa watu waaminifu, akiwemo Yohana mwenyewe (ona Ufunuo 4; ona pia Matendo 7:55–56; 1 Nefi 1:8; Mafundisho na Maagano 76:23; Joseph Smith—Historia ya 1:16–17).

1 Yohana 5

Ninapoonyesha imani katika Yesu Kristo na nimezaliwa upya, Ninaweza kuushinda ulimwengu.

Wazo la kuushinda ulimwengu linatokea mara nyingi katika maandishi ya Yohana. Yohana alimnukuu Yesu akisema, “Ulimwenguni mnayo dhiki: lakini jipeni moyo; Mimi nimeushinda ulimwengu” (Yohana 16:33). Na katika Ufunuo 2–3, Yohana aliandika ahadi za Bwana kwa wale wanaoushinda ulimwengu. Je, Yohana anasema nini kuhusu kuushinda ulimwengu katika 1 Yohana 5:3–5? Unaposoma 1 Yohana 5, tafuta nini tunapaswa kufanya ili kuushinda ulimwengu na kupata uzima wa milele. Kuushinda ulimwengu kunaweza kuonekanaje katika maisha yako? Unaweza pia kupata majibu na utambuzi katika ujumbe wa Mzee Neil L. Andersen “Kuushinda Ulimwengu” (Ensign au Liahona, Mei 2017, 58–62).

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

1 Yohana 2:8–11

Kuisaidia familia yako kutafakari mafundisho ya Yohana, kusanyikeni katika chumba chenye giza na wafanye wanafamilia kupata uzoefu wa tofauti kati ya kutembea “gizani” na kutembea “nuruni.” Je, ni kwa jinsi gani chuki hutusababisha kutembea gizani na kujikwaa? Je, ni kwa jinsi gani kupendana sisi kwa sisi huleta nuru katika maisha yetu?

1 Yohana 3:21–22

Ni kipi katika mistari hii huongeza “kujiamini” tulionako kwa Mungu na katika uwezo wetu wa kupokea majibu ya sala zetu? Unaweza pia kutafuta “Sala” katika Kamusi ya Biblia, Mwongozo wa Maandiko (scriptures.lds.org), au Mada za Injili (topics.lds.org).

1 Yohana 5:2–3

Je, kuna amri zo zote ambazo tunafikiria kuwa ni “kali sana” au ngumu kufuata? Ni jinsi gani upendo wetu kwa Mungu hubadilisha jinsi tunavyojisikia kuhusu amri Zake?

Picha
familia imepiga magoti pamoja katika sala

Kutii amri za Mungu hutusaidia kuushinda ulimwengu.

Yuda 1:3–4

Je, kuna hatari zozote za kiroho ambazo “zimepenyeza ndani” ya maisha yetu na familia yetu? (Yuda 1:4). Ni kwa jinsi gani tunaweza kufuata onyo la Yuda la “kwa bidii kuishindania imani” na kuepukana na hatari hizi? (Yuda 1:3). Je, tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba “amani, na upendo, vinaongezeka” katika familia yetu? (Yuda 1:2).

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta upendo wa Mungu. Mzee M. Russell Ballard alifundisha, “Hii injili ni injili ya upendo—upendo kwa Mungu na upendo kwetu sisi kwa sisi” (“Upendo wa Mungu kwa Watoto Wake ,” Ensign, Mei 1988, 59). Unaposoma maandiko, fikiria kuandika au kuwekea alama maneno na virai ambavyo huonyesha ushahidi wa upendo wa Mungu.

Picha
Kristo akitembea ufukwenii mwa ziwa

Tembea nami, na Greg K. Olsen

Chapisha