Njoo, Unifuate
Novemba 25–Desemba 1. 1 na 2 Petro: “Furahini sana, kwa Furaha Isiyoneneka, Iliyojaa Utukufu”


“Novemba 25–Desemba 1. 1 na 2 Petro: ‘Furahini sana, kwa Furaha Isiyoneneka, Iliyojaa Utukufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Novemba 25–Desemba 1. 1 na 2 Petro,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu Kristo akihubiri injili katika ulimwengu wa roho

Kristo akihubiri injili katika Ulimwengu wa Roho, na Robert T. Barrett

Novemba 25–Desemba 1

1 na 2 Petro

“Furahini sana, kwa Furaha Isiyoneneka, Iliyojaa Utukufu”

Unaposoma waraka wa Petro, unaweza kupokea ushawishi wa kutenda. Andika ushawishi huo wakati ungali “bado katika Roho” (M&M 76:80) ili uweze kwa usahihi kupata kile unachofundishwa.

Andika Misukumo Yako

Muda mfupi baada ya Ufufuko Wake, Mwokozi alitoa unabii ambao yaweza kuwa ulikuwa wa kutaabisha kwa Petro. Alisema kwamba wakati Petro atakapokuwa mzee, angechukuliwa “asikotaka [yeye] … , akiashiria ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu” (Yohana 21:18–19). Wakati Petro alipoandika nyaraka zake, alijua kwamba kifo hiki kilichotabiriwa kilikuwa kimekaribia: “Kule kuwekea mbali maskani yangu kwaja upesi, kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha” (2 Petro 1:14). Kwa bahati mbaya, mateso makali kama hayo yalikuwa ya kawaida kwa Watakatifu katika jimbo la Rumi, ambalo Petro alikuwa akiliandikia (ona 1 Petro 1:1). Na bado maneno yake hayakujawa na woga au kukosa rajua. Badala yake, aliwafundisha Watakatifu “kufurahi sana,” japokuwa walikuwa “wamehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali.” Aliwashauri kukumbuka kwamba “kujaribiwa kwa imani [yao]” kungewapeleka kwenye “sifa na utukufu na heshima katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo” na kwenye wokovu wa roho [zao]” (1 Petro 1:6–7, 9). Imani ya Petro lazima ilikuwa ya kutia faraja kwa wale Watakatifu wa mwanzo, kama ilivyo ya kutia moyo kwa Watakatifu leo, ambao pia ni “washiriki wa mateso ya Kristo; ili, na katika ufunuo wa utukufu wake tufurahi kwa shangwe ” (1 Petro 4:13).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

1 Petro 1:3–9; 2:19–24; 3:14–17; 4:12–19

Ninaweza kupata furaha wakati wa majaribu na mateso.

Kwa mtazamo wa kwanza, inaweza kuonekana ya kushangaza kwamba Petro alitumia maneno kama shangilia, furaha, utukufu, na shangwe kuu katika muunganiko na maneno tunayoyahusisha hasa na ugumu: uzito, majaribu, huzuni, mateso makali, na maumivu (ona 1 Petro 1:6; 2:19; 4:12–13). Ujumbe wa Petro kwa Watakatifu wa mwanzo ulikuwa ni ujumbe sawa na ule uliofundishwa na Rais Russell M. Nelson: “Watakatifu wanaweza kuwa na furaha katika kila hali. … Wakati uzingatifu wa maisha yetu u katika mpango wa Mungu wa wokovu … na Yesu Kristo na injili Yake, tunaweza kujisikia furaha bila kujali nini kinatokea—au kisichotokea—katika maisha yetu. Furaha inakuja kutoka Kwake na kwa sababu Yake. Yeye ni chanzo cha furaha yote” (“Furaha na Kuendelea Kusalia Kiroho,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 82).

Unaposoma 1 Petro 1:3–9; 2:19–24; 3:14–17; 4:12–19, nini hukupa tumaini kwamba unaweza kupata furaha hata katikati ya nyakati ngumu?

1 Petro 3:18–20; 4:1–6

Injili inahubiriwa kwa wafu ili waweze kuhukumiwa kwa haki.

Siku moja, kila mtu atasimama mbele ya kiti cha hukumu na “kutoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na walio kufa” (1 Petro 4:5). Wengine wanaweza kustaajabu ni jinsi gani Mungu anaweza kuhukumu watu wote kwa usawa wakati fursa zao za kuelewa na kuishi injili ni tofauti sana. Ona mafundisho ambayo Petro alifundisha katika 1 Petro 3:18–20; 4:6 ili kuwasaidia Watakatifu katika siku yake kuelewa kwamba hukumu za Mungu zitakuwa za haki. Je, ni kwa jinsi gani mistari hii huimarisha imani yako katika usawa na haki ya Mungu?

Ili kujifunza mafundisho haya zaidi, chunguza Mafundisho na Maagano 138, ufunuo ambao Rais Joseph F. Smith alipokea alipokuwa akitafakari maandishi haya ya Petro. Ni baraka zipi huja kwa wale wanaofanya ibada za injili zipatikane kwa wanafamilia wao ambao wamekufa na bado wanasubiri ibada hizi?

Ona pia “Ubatizo kwa ajili ya Wafu” Mada za Injili, topics.lds.org.

2 Petro 1:1–11

Kupitia nguvu ya Yesu Kristo, ninaweza kuukuza utu wangu mtakatifu.

Je, umewahi kuhisi kwamba kuwa kama Yesu Kristo na kuwa na sifa kama Zake haiwezekani? Mzee Robert D. Hales alitoa wazo hili la kutia moyo kuhusu jinsi tunavyoweza kutengeneza sifa kama za Kristo: “Sifa za Mwokozi …ni sifa zinazojifuma, moja ikiiongeza nyingine, ambazo hukua ndani mwetu katika njia za muingiliano. Kwa maneno mengine, hatuwezi kupata sifa moja ya Kristo bila pia kupata na kuwashawishi zingine. Pale sifa moja inapokuwa na nguvu, ndivyo zinavyokuwa na nyingine zaidi” (“Kuwa Mfuasi wa Bwana Wetu Yesu Kristo,” Ensign au Liahona, Mei 2017, 46).

Picha
zulia la ukutani la changamani

Kila sifa ya Kristo tunayokuza inatusaidia kufuma zulia la kiroho la ufuasi.

Fikiria kusoma 2 Petro 1:1–11 katika muunganiko na ujumbe wa Mzee Hales. Unajifunza nini kutoka kwa Mitume hawa wawili ambacho hukusaidia katika juhudi zako za kuwa zaidi kama Kristo.

Ona pia 1 Petro 4:8; David A. Bednar, “Ahadi Kuu na za Thamani,” Ensign au Liahona, Nov. 2017, 90–93.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

1 Petro 2:5–10

Unaposoma mistari hii na familia yako, fikiria kutumia mawe ili kuwasaidia wanafamilia kupata taswira ya mafundisho ya Petro kwamba Mwokozi ni jiwe letu “kuu la pembeni.” Je, ni kwa jinsi gani sisi ni kama “mawe yaliyo hai” ambayo Mungu anatumia ili kujenga ufalme Wake? Je, tunajifunza nini kutoka kwa Petro kuhusu Mwokozi na nafasi yetu katika ufalme Wake? Je, ujumbe wa Petro kwa familia yako upi?

1 Petro 3:8–17

Je, ni kwa jinsi gani tunaweza “kuwa tayari kutoa jibu” kwa wale wanaotuuliza kuhusu imani yetu? Familia yako inaweza kufurahia kuigiza nyakati ambapo mtu huwajia na maswali kuhusu injili.

1 Petro 3:18–20; 4:6

Je, mnaweza kufanya nini kama familia ili kujifunza kuhusu mababu zenu waliofariki? Pengine katika siku ya kuzaliwa ya babu au bibi aliyefariki unaweza kupika chakula alichokipenda babu au bibi huyo, kuonyesha picha, au kusimulia hadithi kutoka katika maisha ya babu au bibi yako. Ikiwezekana, unaweza pia kupanga kupokea ibada kwa ajili ya babu au bibi huyu hekaluni.

2  Petro 1:16–21

Katika mistari hii, Petro anawakumbusha Watakatifu juu ya uzoefu wake katika Mlima wa Kugeuzwa sura (ona pia Mathayo 17:1–9). Je, tunajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu mafundisho ya manabii? (ona pia M&M 1:38). Je, ni kitu ganii hutupatia kujiamini kuwafuata manabii wetu wanaoishi leo?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

“Kuwa Tayari Daima.” Nafasi za kufundisha zisizo rasmi nyumbani huja na hupita haraka, kwa hiyo ni muhimu kuzitumia vyema wakati zinapotokea. Ni kwa jinsi gani unaweza kujitahidi “kuwa tayari daima” kufundisha wanafamilia wako kweli za injili na kuelezea “tumaini lililo ndani yako” (1 Petro 3:15) wakati nyakati za kufundisha zinapojitokeza? (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 16.)

Picha
Petro akilihubiria kundi la watu

Japokuwa Petro alikabiliwa na mateso mengi na upinzani, yeye alibaki imara katika ushuhuda wake juu ya Kristo.

Chapisha