Njoo, Unifuate
Novemba 25–Desemba 1. 1 na 2 Petro: ‘Furahini sana kwa Furaha Isiyoneneka Yenye Utukufu’


“Novemba 25–Desemba 1. 1 na 2 Petro: ‘Furahini sana kwa Furaha isiyoonekana Yenye Utukufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Novemba 25–Desemba 1. Petro 1 na 2,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Yesu Kristo akihubiri injili katika ulimwengu wa roho

Kristo Akihubiri katika Ulimwengu wa Roho, na Robert T. Barrett

Novemba 25–Disemba 1

1 na 2 Petro

“Furahini sana kwa Furaha Isiyoonekana Yenye Utukufu”

Anza kujifunza kwako 1 na 2 Petro kwa sala. Kumbuka kwamba matayarisho bora ya kufundisha yatakuja kwa njia ya uzoefu wako wa kujifunza wewe binafsi na wanafamilia.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Onyesha picha iliyopo katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia, na waalike watoto wakusimulie kitu wanachojua kuhusu Petro. Wakumbushe kwamba Petro alikuwa kiongozi wa Kanisa baada ya Yesu kufufuka, na eleza kwamba 1 Petro na 2 Petro ni waraka kutoka kwake kwenda kwa waumini wa Kanisa katika siku zake.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

1 Petro 1:6–7; 3:14

Ninaweza kuwa na furaha hata wakati wa shida.

Fikiria jinsi unavyoweza kufundisha mistari hii katika njia ambazo zitawasaidia watoto kumgeukia Mwokozi wakati wanapokabiliwa na shida.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kuelezea mambo magumu ambayo Yesu alivumilia, kama vile kusulubiwa. Elezea kwamba sisi tutakuwa na nyakati ngumu katika maisha yetu. Someni 1 Petro 1:6–7; 3:14 kwa pamoja, na elezea tukio lolote ambalo wewe wakati fulani ulikabiliwa na “jaribu la imani yako.” Au unaweza kusimulia sala ya Nabii Joseph Smith katika Gereza la Liberty na faraja ambayo Mungu alimpa (ona M&M 121:1–8; 123:17). Je, ni kwa jinsi gani kuwa na imani katika Yesu Kristo kunatusaidia kupata furaha wakati wa shida?

    Picha
    Joseph Smith katika Jela ya Liberty

    Joseph Smith katika Gereza la Liberty, na Greg  K. Olsen

  • Imbeni pamoja wimbo ambao unafundisha jinsi ya kupata furaha, kama vile “I will Follow God’s Plan ” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto 164-165.

1 Petro 2:9–12

Baba wa Mbinguni ananitaka mimi niwe mfano kwa wengine.

Petro alifundisha kwamba sisi ni “watu wa milki ya Mungu” na kwamba matendo yetu mema yanaweza “kumtukuza Mungu.”

Shughuli Yamkini

  • Elezea vitu ambavyo vinajitokeza kutoka kwenye mazingira yao, au onyesha picha za vitu hivyo. Kwa mfano, hekalu limejitokeza kutoka kwenye majengo yaliyolizunguka au mlima unainuka juu ya bonde. Eleza kwamba tunapotii amri, tunajitokeza na watu wengine wanaweza kuona mifano yetu. Ongelea kuhusu baadhi ya “matendo mema” ambayo umewaona watoto wakifanya. Eleza kwamba matendo mema kama haya “yanamtukuza Mungu”—yanawasaidia wengine kuhisi upendo zaidi kwa Mungu na kutamani kumhudumia Yeye.

  • Kamilisha ukurasa wa shughuli pamoja na watoto. Je, ni kwa jinsi gani watu waliowaona katika picha wanamtukuza Mungu?

1 Petro 3:18–20; 4:6

Roho katika ulimwengu wa roho wanajifunza kuhusu injili.

Baada ya kufa, Yesu alikwenda ulimwengu wa roho na aliwatuma roho wenye haki kufundisha roho wengine ambao walikuwa bado hawajaikubali injili.

Shughuli Yamkini

  • Waeleze watoto kuhusu mtu fulani unayemjua ambaye amefariki dunia. Eleza kuwa watu wanapokufa, roho zao zinaacha miili yao na kwenda ulimwengu wa roho. Soma 1 Petro 3:19 na uelezee kwamba wakati Yesu alipokufa, alikwenda kutembelea ulimwengu wa roho. Kule, aliwaomba roho wenye haki kufundisha injili kwa roho wengine ambao walikuwa bado hawajaikubali injili (ona M&M 138:30).

  • Weka mstari wa viti katikati ya chumba kufanya kama kizuizi. Waombe baadhi ya watoto kusimama upande mmoja kuwakilisha roho katika ulimwengu wa roho ambao hawakubatizwa wakati wa maisha yao hapa duniani. Mpe mmoja wa watoto wengine ufunguo mkubwa wa karatasi lenye maneno “ubatizo kwa ajili ya wafu” yameandikwa juu yake, na muombe aondoe kizuizi hicho. Kisha eleza kwamba waumini wa Kanisa ambao wana umri wa miaka 12 na zaidi wanaweza kwenda hekaluni na kubatizwa kwa ajili ya mababu zao ambao hawakubatizwa walipokuwa duniani. Kisha hawa mababu wanaweza kuikubali injili katika ulimwengu wa roho.

  • Wasaidie watoto kujaza chati ya mti wa familia (ona mfano kwenye “Kurasa za Kupaka rangi za Historia ya Familia,” LDS.org).

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

1 Petro 3:12–17; 4:13–14, 16

Ninaweza kupata furaha na amani hata katika wakati mgumu.

Watoto unaowafundisha yawezekana wamewahi kupatwa na tukio fulani la kutaniwa au kudhihakiwa kwa sababu ya kile wanachoamini. Mistari hii inaweza kuwasaidia wakati huo.

Shughuli Yamkini

  • Fanya muhtasari wa hadithi chache kuhusu Yesu akiwa anateswa, au waombe watoto wazisome—ona, kwa mfano, Mathayo 12:9–14 au Luka 22:47–54. Waulize watoto kama wamewahi wakati wowote kutaniwa au kudhihakiwa kwa sababu wanaishi mafundisho ya injili. Kisha someni pamoja 1 Petro 3:12–14; 4:13–14 16, na waombe watoto kutafuta kile Petro alichosema kuhusu mateso “kwa ajili ya haki.” Je, ni kwa nini bado tunaweza kuwa na furaha wakati watu wengine wanatudhihaki kwa ajili ya kufanya kile kilicho sahihi.

  • Mwalike muumini wa kata kuelezea uzoefu wake wakati alipopata furaha au amani wakati wa majaribu, au kuelezea namna gani Nabii Joseph Smith alipata amani katika Gereza la Liberty (ona M&M 121:1–8; 123:17). Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kupata furaha na amani wakati wa majaribu yetu?

1 Petro 3:15

Ninapaswa daima kuwa tayari kushiriki injili na wengine.

Watoto unaowafundisha watakuwa na nafasi nyingi katika maisha yao yote kujibu maswali kutoka kwa watu wengine kuhusu imani yao. Tafakari kile unachoweza kufanya ili kuwasaidia “kuwa tayari wakati wote kutoa jibu.”

Shughuli Yamkini

  • Simulia kuhusu wakati ambapo mtu fulani alikuuliza swali kuhusu Kanisa, na eleza kama ulijisikia upo tayari kujibu. Waombe watoto kuzungumza kuhusu wakati wo wote watu walipowauliza maswali kuhusu Kanisa. Someni pamoja 1 Petro 3:15. Tunawezaje kufuata ushauri wa Petro katika aya hii?

  • Kwa msaada kutoka kwa watoto, fikiria juu ya maswali machache watu wanayoweza kuuliza kuhusu mafundisho ya Kanisa. Waache watoto wachukue zamu kuelezea jinsi ambavyo wangeweza kujibu maswali haya ili waweze “kuwa tayari siku zote”

1 Petro 3:18–20; 4:6

Roho katika ulimwengu wa roho wanajifunza kuhusu injili.

Wasaidie watoto kuelewa kwamba wakati wenye haki wanapokufa, wanakwenda ulimwengu wa roho kufundisha injili kwa wale ambao hawakuipokea wakati wakiwa duniani.

Shughuli Yamkini

  • Chora ubaoni duara na mstari ukipita katikati. Andika Paradiso ya Roho nusu moja ya duara na Gereza la Roho upande mwingine. Muombe mmoja wa watoto kusoma 1 Petro 3:18–20; 4:6 (ona 1 Petro 4:6, tanbihi a, kwa ajili ya marudio kutoka Tafsiri ya Joseph Smith). Elezea kwamba Yesu Alipokufa, alikwenda paradiso ya roho. Aliwafundisha roho wenye haki kule ili kufundisha injili kwa roho walio katika gereza la roho.

  • Mwalike mzazi au ndugu mkubwa wa mmoja wa watoto aeleze kuhusu kwenda hekaluni na kutekeleza kazi kwa ajili ya mmoja wa mababu zao.

  • Wasaidie watoto kujaza mti rahisi wa familia (ona mfano kwenye “Kurasa za Kupaka rangi za Historia ya Familia,” LDS.org.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kuelezea mti wao wa familia pamoja na wanafamila wao na waombe kusaidia kuongeza majina kwenye mti huo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tafuta kuwaelewa watoto unaowafundisha. Unawajua watoto unaowafundisha, kwa hiyo badilisha mawazo katika muhtasari huu kama ikibidi ili kukidhi mahitaji yao. Unaweza kutumia shughuli yoyote iliyopendekezwa katika muhtasari huu, sio tuu hizo zilizoandikwa kwa ajili ya kundi la umri unalofundisha. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi 7.)

Chapisha