Njoo, Unifuate
Desemba 23–29. Ufunuo wa Yohana 12–22: ‘Yeye Ashindaye Atayarithi Haya’


Desemba 23–29. Ufunuo wa Yohana 12–22: ‘Yeye Ashindaye Atayarithi Haya’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019.)

Desemba 23–29. Ufunuo wa Yohana 12–22,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Yesu Kristo akiwasalimia watu katika Ujio Wake wa Pili

Mji wa Milele, na Keith Larson

Desemba 23–29

Ufunuo wa Yohana 12–22

“Yeye Ashindaye Atayarithi Haya”

Je, vita kati ya wema na uovu vilivyoelezwa katika Ufunuo wa Yohana vinakufundisha nini kuhusu umuhimu wa kumfuata Kristo hapa duniani? Baada ya kutafakari kanuni hii, fikiria mahitaji ya washiriki wa darasa lako. Je, ni ukweli gani kutoka katika Ufunuo wa Yohana unaweza kuwasaidia kufanya chaguzi sahihi?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati washiriki wa darasa lako wakifikia mwisho wao wa kujifunza Agano Jipya, wahimizie kushiriki mawazo yao kuhusu Agano Jipya. Je, ni kwa namna gani kujifunza kwao maandiko kumeimarisha shuhuda zao?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Ufunuo wa Yohana 12:7–11

Tulimshinda Shetani “kwa damu ya Mwana kondoo, na kwa neno la ushuhuda [wetu].”

  • Kujifunza kuhusu Vita vya Mbinguni kunaweza kutusaidia kuelewa vizuri zaidi maisha ya hapa duniani. Washiriki wa darasa wangeweza kusoma Tafsiri ya Joseph Smith, Ufunuo wa Yohana 12:7–11 (katika muhtasari wa Biblia) na kubaini jinsi tulivyomshinda Shetani na jeshi lake katika Vita huko Mbinguni. Ni umaizi gani mwingine tunaoupata kutoka kwenye maingizo juu ya Vita huko Mbinguni katika Kamusi ya Biblia au Mada za Injili? (topics.lds.org). Je, tunajifunza nini ambacho kinaweza kutusaidia kumshinda adui katika maisha yetu ya hapa duniani?

  • Je, inamaanisha nini kwamba Mwana kondoo “alichinjwa tangu kuwekwa kwa msingi wa dunia”? (Ufunuo wa Yohana 13:8; ona pia Ufunuo wa Yohana 5:6). Fikiria kuwasaidia washiriki wa darasa lako kupata majibu ya swali hili kwa kusoma Mosia 3:13 na Musa 7:47 kama darasa. Inamaanisha nini kumshinda Shetani “kwa damu ya Mwana kondoo”? (Ufunuo wa Yohana 12:11).

Ufunuo wa Yohana 17–18

Lazima tujitenge na uovu wa ulimwengu.

  • Haivutii hasa kusoma kuhusu uovu wa Babeli na kuanguka kwake katika Ufunuo wa Yohana 17–18, lakini hii inatufundisha kwa sababu Babeli inaweza kuwa ishara ya ulimwengu ulio mwovu ambamo tunaishi leo hii. Labda ungeweza kugawanya sura hizi kwa makundi madogo madogo ya washiriki wa darasa na kuwaomba watafute majibu ya maswali kama haya: Je, ni kwa nini watu wanavutiwa na Babeli au mambo ya kiulimwengu? Je, ni kwa nini Babeli ni hatari? Je, kitaitokea nini kwa Babeli? Je, ni maonyo gani Yohana anatoa ili kutusadia sisi kuiepuka hatma ya Babeli?

  • Baada ya kusoma Ufunuo wa Yohana 18:4, washiriki wa darasa wangetaka kujadili ni kwa namna gani wanaweza “kutoka nje ya” Babeli na “kutokuwa washiriki wa dhambi zake.” Kwa mfano, ni maandiko gani au ujumbe kutoka kwa viongozi wa Kanisa umetusaidia kujizuia na majaribu ya Babeli, au ya ulimwengu? Fikiria kuangalia video “Dare to Stand Alone” au “Separating Ourselves from the World” (LDS.org) au kusoma kauli ya Mzee Quentin L. Cook katika “Nyenzo za Ziada.” Ni mawazo gani washiriki wa darasa wanaweza kutoa kuhusu jinsi ya kutumia kanuni mbili alizoorodhesha Mzee Cook? Je, ni kwa namna gani sisi “tunajitoa” Babeli? (ona, kwa mfano, Mafundisho na Maagano 133:12–14). Tunaweza kufanya nini ili kuwahamasisha wengine kufanya vivyo hivyo?

Ufunuo wa Yohana 19:5–20:15

Tunaweza kujiandaa kwa Ujio wa Pili wa Bwana na Siku ya Hukumu.

  • Ujio wa Pili wa Yesu Kristo mara nyingi huitwa “siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo” (Yoeli 2:31), na kulingana na Ufunuo wa Yohana 19–20, hii inaonekana kuwa na maelezo mazuri. Fikiria kuandika ubaoni baadhi ya matukio yaliyoelezwa katika Ufunuo wa Yohana 19:5–20:15. Waalike washiriki wa darasa kutafuta mistari ambayo inaelezea matukio haya. Je, ni kwa nini matukio haya yaliitwa makuu na yatishayo? Je, tunajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu Mwokozi na wale wanaomfuata? Je, tunaweza kufanya nini kuwa kati ya wale ambao watashangilia wakati wa ujio Wake?

  • Ili kuleta hamasa katika mjadala kuhusu kitabu cha uzima, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kutengeneza kitabu rahisi kwa kukunja kipande cha karatasi katika sehemu nne. Kisha wangesoma Ufunuo wa Yohana 20:12–15, wakitafakari nini wanakitaka kiandikwe kuhusu wao katika kitabu cha uzima, waandike vitu hivyo katika vitabu vyao. (Maana ya “kitabu cha uzima” inaweza kupatikana katika “Nyenzo za Ziada.” ) Je, tungehisi vipi kama tungeitwa mbele ya kiti cha Mungu leo hii? Fikiria kutumia Ujumbe wa Mzee Jörg Klebingat “Kukaribia Kiti cha enzi cha Mungu kwa Ujasiri” (Ensign au Liahona, Nov. 2014, 34–37) kama sehemu ya mjadala. Ungeweza pia kurejea ujumbe wa Mzee Jeffrey R. Holland “Hatimaye—Muwe Wakamilifu” (Ensign au Liahona, Nov. 2017, 40–42). Je, ujumbe huu unachangia nini katika majadiliano kuhusu kujiandaa kwa ajili ya Siku ya Hukumu?

Ufunuo wa Yohana 21:1–22:5

Kama tukiwa waaminifu, tutabarikiwa kwa kupata utukufu wa selestia.

  • Ingawa siku za mwisho zinatolewa unabii wa kujawa na uovu na majanga, thawabu ambayo Yohana aliiona kwa walio waaminifu inaizidi sana taabu ambayo wamepata mwanzoni. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuchunguza hitimisho hili zuri la Ufunuo wa Yohana, ungeweza kuwaalika kurejea Ufunuo wa Yohana 21:1–22:5, wakitafuta virai ambavyo vinawapa mwongozo wa kiungu wa kuhangaikia utukufu wa selestia. Je, ni ahadi gani zimetolewa kwa walio waaminifu? Je, ni kwa namna gani ufafanuzi huu unatusaidia kukabiliana na changamoto na majaribu yetu ya sasa?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ili kuwapa mwongozo wa kiungu washiriki wa darasa kusoma Kitabu cha Mormoni mwaka ujao—wao binafsi na pamoja na familia—elezea baadhi ya ahadi hizi za kinabii.

Rais Gordon B. Hinckley: “Bila wasiwasi ninawaahidi kwamba ikiwa kila mmoja wenu atafuata mpango huu rahisi, bila kujali mara ngapi hapo awali huenda ulisoma Kitabu cha Mormoni, kutakuja katika maisha yako na katika nyumba yako kipimo zaidi cha Roho wa Bwana, azimio la nguvu la kutembea katika kutii amri Zake, na ushuhuda wa nguvu wa uhalisi wa uhai wa Mwana wa Mungu” (“Ushuhuda wa Kusisimua na wa Kweli,” Ensign, Agosti. 2005, 6).

Rais Thomas S. Monson: “Ninawahimiza kila mmoja wetu kwa sala kujifunza na kutafakari Kitabu cha Mormoni kila siku. Tunapofanya hivyo, tutakuwa katika nafasi ya kusikia sauti ya Roho, kushinda majaribu, kushinda shaka na woga, na kupokea msaada wa mbinguni katika maisha yetu” (“Nguvu ya Kitabu cha Mormoni,” Ensign au Liahona, Mei 2017, 87).

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Ufunuo wa Yohana 12–22

Kuchagua haki badala ya uovu wa Babeli.

Mzee Quentin L. Cook alifundisha:

“Hatuwezi kuepuka ulimwengu. Maisha ya kujifungia sio suluhisho. Katika njia chanya, mchango wetu katika ulimwengu ni sehemu ya changamoto yetu na ni muhimu kama tutataka kukuza vipaji vyetu. … Waumini wa Kanisa wanahitajika kujihusisha katika ulimwengu katika njia chanya. Je, ni kwa namna gani basi tunaweka usawa hitaji la kuchangia kwa njia chanya katika ulimwengu na kutoshawishika na dhambi za ulimwengu? (Ona M&M 25:10; M&M 59:9.) Kanuni mbili zitaleta tofauti muhimu.

“1. Acha watu wajue kwamba wewe hakika ni Mtakatifu wa Siku za Mwisho. …

“2. Kuwa jasiri kuhusu na kuishi kile unachokiamini” (“Mafunzo kutoka Agano la Kale: Ulimwenguni lakini Siyo wa Kiulimwengu,” Ensign, Feb. 2006, 54–55).

Kitabu cha uzima

Wafilipi 4:3; Ufunuo wa Yohana 3:5; 17:8; 2 Nefi 29:11; Alma 5:58; Mafundisho na Maagano 127:6–7, 9; 128:6–7.

“Kwa namna moja kitabu cha uzima ni jumla ya mawazo, na matendo ya mtu—kumbukumbu ya maisha [yake]. Hata hivyo, maandiko yanaonyesha kwamba kumbukumbu ya waaminifu inatunzwa mbinguni, ambapo majina yao yameandikwa, vile vile matendo yao mema” (Kamusi ya Biblia, “Kitabu cha Uzima”).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ni SAWA kusema “Sijui.” Wakati ni kawaida kutaka kujibu kila swali, wakati mwingine ni vyema tu kusema, ‘sijui. Acha tujifunze swali hilo sisi wenyewe wiki hii, na tunaweza kulijadili wakati ujao’” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 24). Kisha waombe washiriki wa darasa kutafuta maandiko na nyenzo nyingine za Kanisa kwa ajili ya kupata majibu.

Chapisha