Agano Jipya 2023
Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai: “Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”


“Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2021)

“Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Paulo akitoa imla ya barua akiwa gerezani

Oktoba 9–15

Wafilipi; Wakolosai

“Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”

Anza kwa kusoma Wafilipi na Wakolosai, na kwa sala tafakari kuhusu mafundisho ambayo Bwana anataka wewe ufundishe. Acha Roho akuongoze unapofikiria maswali na nyenzo ambazo ungeweza kutumia katika kufundisha mafundisho haya.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Alika washiriki wa darasa kushiriki neno moja au kirai ambacho kinafupisha kile walichojifunza kutoka Wafilipi na Wakolosai na kisha waelezee kwa nini walichagua neno au kirai hicho. Wahimize kushiriki mistari kutoka maandiko kama sehemu ya maelezo yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Wafilipi 2:1–5, 14–18; 4:1–9; Wakolosai 3:1–17

Tunakuwa “wapya” tunapoishi injili ya Yesu Kristo.

  • Yawezekana ukataka kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuvuta taswira ya nini humaanisha “kuuvua utu wa kale” na “kuvaa utu upya” kupitia Yesu Kristo (Wakolosai 3:9–10). Ili kufanya hili, unaweza kuonyesha kabla au baada picha ya kitu cha zamani ambacho kimebadilishwa kuwa kitu kingine kipya (kama vile samani, nyumba au baiskeli). Washiriki wa darasa wangeweza kujadili ni kwa namna gani tunakuwa “wapya” kupitia imani yetu katika Yesu Kristo na utayari wetu wa kuishi injili Yake. Kama sehemu ya mjadala ungeweza kuwaomba nusu ya darasa kujifunza Wafilipi 2:1–5, 14–18; 4:1–9 na nusu nyingine wajifunze Wakolosai 3:1–17, wakionyesha tabia za “utu wa kale” na “utu upya.” Ungeweza pia kuwaalika washiriki wachache wa darasa kuelezea ni kwa namna gani imani katika Yesu Kristo na kuishi injili Yake kumewasaidia wao kuwa watu wapya.

Wafilipi 4:1–13

Tunaweza kupata shangwe katika Kristo, bila kujali hali zetu.

  • Ingawa hali zetu ni tofauti na za Paulo, bado tunaweza kujifunza kutokana na utayari wake wa kuridhika na kufurahia katika hali zote za maisha yake. Ili kuanza mjadala juu ya mada hii, ungeweza kurejea baadhi ya majaribu aliyoyapitia Paulo (ona, kwa mfano, 2 Wakorintho 11:23–28). Halafu ungeweza kuwauliza washiriki wa darasa kurejea Wafilipi 4:1–13 ili kupata ushauri ambao Paulo alitoa ambao unaweza kutusaidia sisi kufurahia, hata katika nyakati za majaribu.

  • Labda wangeweza kuelezea matukio ambapo walihisi “amani ya Bwana, ipitayo uelewa wote” (Wafilipi 4:7) au wakati walipohisi kuimarishwa “kupitia Kristo” (mstari wa 13) au kutimiza jambo ambalo wasingeweza kulifanya kwa namna nyingine.

  • Kama ungependa kuchunguza mada hii kwa undani, ungeweza kumuomba mshiriki wa darasa kushiriki tukio la kuhamasisha au kauli kutoka hotuba ya Rais Russell M. Nelson “Shangwe na Uhai wa Kiroho” (Liahona, Nov. 2016, 81–84). Au darasa lingeweza kuangalia video ya “Trial of Adversity” (ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa namna gani watu katika hotuba ya Rais Nelson au mwanamke katika video wanapata furaha, licha ya hali zao ngumu?

  • Kwa sababu uovu unaongezeka katika ulimwengu wa leo, washiriki wa darasa lako watanufaika kutokana na ushauri wa Paulo wa “kutafakari juu ya mambo ambayo ni safi, yenye kupendeza, yenye sifa njema, yenye staha au wema (Wafilipi 4:8). Labda ungeweza kumpa jukumu kila mshiriki wa darasa (au makundi madogo madogo ya washiriki wa darasa) moja kati ya sifa zilizoorodheshwa katika Wafilipi 4:8 au Makala ya Imani 1:13. Kila mmoja angeweza kutumia Mwongozo wa Mada ili kupata maandiko kuhusu jukumu lao walilopewa na kushiriki na wengine darasani kile walichopata. Wangeweza pia kuelezea mifano ya sifa hizo katika maisha ya watu. Je, ni kwa jinsi gani “tunayatafuta mambo hayo”?

Wakolosai 1:12–23; 2:2–8

Wakati imani yetu “imejengwa” katika Yesu Kristo, tunaimarishwa dhidi ya ushawishi wa kidunia.

  • Ushuhuda wa Paulo juu ya Mwokozi katika Wakolosai 1:12–23; 2:2–8 unatoa fursa nzuri kwa washiriki wa darasa kutafakari na kuimarisha imani zao wenyewe. Washiriki wa darasa wangeweza kuchunguza mistari hii ili kupata mambo ambayo yanaimarisha imani yao katika Yesu Kristo. Inamaanisha nini kuwa “wenye shina na kujengwa katika [Yesu Kristo]”? (Wakolosai 2:7). Picha ya mti katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia na video “Spiritual Whirlwinds” (ChurchofJesusChrist.org) vinaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili mstari huu. Nini kinaweza kuimarisha au kudhoofisha mizizi ya mti? Ni kwa namna gani kuwa “wenye shina na kujengwa katika [Yesu Kristo]” kunatuimarisha dhidi ya vishawishi vya kiulimwengu? (ona Wakolosai 2:7–8; ona pia Helamani 5:12; Etheri 12:4).

  • Ungeweza pia kuwaalika washiriki wa darasa kuorodhesha mambo ambayo Wakolosai 1:12–23; 2:2–8 inafundisha kuwa tunaweza kuepuka “madanganyo ya bure” ambayo yanaweza “kuharibu” imani yetu katika Kristo (Wakolosai 2:8). Ni kwa namna gani tunaweza kusaidiana katika jitihada zetu za kumfuata Mwokozi na kuepuka udanganyifu wa Shetani?

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia muziki. Muziki mtakatifu hukaribisha ushawishi wa Roho Mtakatifu. Unaweza kutengeneza mazingira ya utulivu na kuhamasisha uwajibikaji na matendo. Fikiria jinsi “kufundishana na kuonyana katika zaburi na nyimbo” kunavyoweza kuwa sehemu ya darasa lako (Wakolosai 3:16; ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi22).

Chapisha