Agano Jipya 2023
Oktoba 23 –29. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: “Muwe Kielelezo kwao Waaminio”


“Oktoba 23–29. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: ‘Muwe Kielelezo kwao Waaminio’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2021)

“Oktoba 23–29. 1 na 2 Wathesalonike 2–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
wanawake watatu wanatembea nje ya hekalu

Oktoba 23–29

1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni

“Muwe Kielelezo kwao Waaminio”

Soma 1na 2 Timotheo; Tito; na Filemoni ukiwa na washiriki wa darasa lako mawazoni mwako. Mawazo na misukumo inayokuja itakusaidia kuwaelekeza washiriki wa darasa kwenye maandiko husika na kumleta Roho katika darasa lako.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Itakuwa msaada kwa washiriki wa darasa kumsikia kila mmoja wao akiongea kuhusu mafanikio na changamoto katika kusoma maandiko kibinafsi na kama familia. Fikiria kuanza darasa kwa kuwaalika washiriki wa darasa kuzungumzia nini kinaenda vizuri katika kujifunza kwao maandiko.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1na 2 Timotheo; Tito

Kuelewa mafundisho ya kweli kutatusaidia kuepuka kudanganywa.

  • Washiriki wa darasa lako wanaishi katika wakati ambao inaweza kuwa vigumu kuamua kipi ni kweli na kipi ni uongo. Timotheo na Tito pia waliishi katika kipindi kama hicho, hivyo labda ushauri wa Paulo kwao ungeweza kuwanufaisha washiriki wa darasa lako. Hapa ni baadhi ya vipengele ambavyo vina ushauri wa Paulo: 1 Timotheo 1:1–7; 4:1–2, 6; 6:3–5, 20–21; 2 Timotheo 3:13–17; 4:2–4; Tito 1:7–9; 2:1, 7–8. Ungeweza kumpa kazi kila mshiriki wa darasa kusoma mojawapo ya vifungu na kushiriki nini amejifunza kuhusu umuhimu wa mafundisho ya kweli (ona pia Alma 31:5). Ni kwa jinsi gani mafundisho ya Mwokozi yanatusaidia sisi kuepuka kudanganywa? Washiriki wa darasa pia wangeweza kushiriki uzoefu wao ambapo nguvu ya mafundisho ya kweli iliwabariki.

Picha
wamisionari wawili wakiongea na mtu

“Na mtu yeyote asidharau ujana wako; bali uwe kielelezo kwao waaminio” (1 Timotheo 4:12).

1 Timotheo 4:10–16

“Uwe Kielelezo kwao Waaminio”

  • Inawezekana kwamba washiriki wa darasa lako hawatambui nguvu ya kuwa kielelezo kizuri ambacho wamekuwa. Fikiria kuwaalika kuzungumzia kuhusu jinsi gani watu wanaowajua, ikijumuisha washiriki wenzao wa darasa, wamekuwa vielelezo vya wafuasi wa Kristo. Ingeweza kusaidia katika mjadala kama ungeorodhesha kwenye ubao maneno katika mstari wa12 ambayo yanaelezea jinsi gani tunatakiwa kuwa kielelezo—kimaneno, kimaongezi (ambako pia kunaweza kumaanisha mwenendo au tabia), hisani, roho, imani, na usafi. Washiriki wa darasa wangeweza kujadili ni kwa namna gani tunaweza kuwa kielelezo kwa waaminio katika kila moja ya njia hizi.

2 Timotheo 1

“Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.”

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kuangalia katika 2 Timotheo kwa ajili ya ushauri wa Paulo alioutoa ili kumtia moyo Timotheo katika huduma yake. Waombe washiriki wa darasa kushiriki umaizi wowote walioupata. Au ungeweza kuwapa dakika chache darasani kutafuta na kushiriki baadhi ya ushauri wa Paulo (sura ya1 ina mifano mizuri). Wangeweza pia kushiriki uzoefu ambapo Mungu aliwasaidia kushinda woga wao na kuwapa roho ya … nguvu na ya upendo, na ya moyo wa kiasi” (2 Timotheo 1:7).

2 Timotheo 3

Kujifunza maandiko kunaweza kutusaidia kushinda hatari za siku za mwisho.

  • Baada ya kumwonya Timotheo kuhusu “nyakati za hatari” zitakazokuja, Paulo alishuhudia juu ya nguvu na umuhimu wa maandiko (ona 2 Timotheo 3:1, 14–17). Ili kuanzisha mjadala kuhusu umuhimu wa maandiko katika nyakati za hatari, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kurejea maelezo ya Paulo kuhusu hatari za siku za mwisho zipatikanazo katika 2 Timotheo 3:1–7. Kisha wangeweza kutafuta na kushiriki maandiko ambayo yamewasaidia wao kujikinga dhidi ya hatari kama hizi (baadhi ya mifano imeorodheshwa katika “Nyenzo za Ziada”). Ni kwa namna gani kujifunza kwetu maandiko kumetukinga dhidi ya matatizo katika ulimwengu wa leo?

  • Kujifunza ushauri wa Paulo kuhusu nguvu ya maandiko kungeweza kuwa ni nafasi kwa washiriki wa darasa kutiana moyo wao kwa wao katika juhudi zao za kujifunza neno la Mungu. Labda washiriki wa darasa wangeweza kusoma 2 Timotheo 3:14–17 na kuainisha baraka na ulinzi ambao huja kutokana na kujifunza maandiko. Kisha wangeweza kushiriki matukio wakati baraka hizi zilipotimizwa katika maisha yao kwa sababu ya kujifunza kwao maandiko. Ungeweza pia kuwapa washiriki wa darasa kiasi fulani cha muda kutafakari wanaweza kufanya nini ili kuweza kuwa na uzoefu wenye maana kwenye maandiko, vyote kibinafsi na kama familia.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Ukweli wa kimaandiko ambao hutulinda sisi dhidi ya hatari za siku za mwisho (ona 2 Timotheo 3:2.

Hatari za siku za mwisho

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Hatari za siku za mwisho

Wenye kujipenda wenyewe

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Yohana 15:12–13

Hatari za siku za mwisho

Wenye kutamani

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Mafundisho na Maagano 88:123

Hatari za siku za mwisho

Wenye kujivuna

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Mosia 2:24–25

Hatari za siku za mwisho

Wenye kiburi

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Alma 5:27–28

Hatari za siku za mwisho

Wenye kukufuru

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Mafundisho na Maagano 63:64

Hatari za siku za mwisho

Wasio watii wazazi

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Waefeso 6:1–3

Hatari za siku za mwisho

Wasio na shukrani

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Mafundisho na Maagano 78:19

Hatari za siku za mwisho

Wasio safi

Kweli Ambazo Zinatulinda Sisi

Kumbukumbu la Torati 7:6

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ukuaji wa kiroho hutokea nyumbani. Uko na washiriki wa darasa lako kwa muda mfupi tu mara mbili kwa mwezi. Wengi wao wanapitia matukio ya maana sana kiroho nje ya darasa, na matukio haya yangeweza kuwaimarisha washiriki wengine wa darasa lako. Waulize maswali ambayo yatawatia wao moyo kuelezea kile walichojifunza wakati walipokuwa wakijifunza injili nyumbani. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi18.)

Chapisha