Agano la Kale 2022
Aprili 25–Mei 1. Kutoka 24; 31–34: “Uso Wangu Utakwenda pamoja na Wewe”


“Aprili 25–Mei 1. Kutoka 24; 31–34: ‘Uso Wangu Utakwenda pamoja na Wewe,’” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Aprili 25–Mei 1. Kutoka 24; 31–34,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yehova anamtokea Musa na wazee wa Israeli

Kielelezo cha Yehova akimtokea Musa na wazee 70 wa Israeli, na Jerry Harston

Aprili 25–Mei 1

Kutoka 24; 31–34

“Uso Wangu Utakwenda pamoja na Wewe”

Acha maneno haya kutoka kwa Mzee Jeffrey R. Holland yaongoze maandalizi yako ya kufundisha: “Watu wengi hawaji kanisani kutafuta tu ukweli mpya wa injili. … Wanakuja wakitafuta uzoefu wa kiroho. … Wanataka imani yao iimarishwe na tumaini lao lifanywe upya” (“A Teacher Come from God,” Ensign, Mei 1998, 26).

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Washiriki wa darasa wangeweza kufikiria kwamba rafiki anasema, “Sisomi Agano la Kale; sioni kama lina muhimu kwa maisha yangu.” Waulize ili wajibu kwa kushiriki kitu ambacho wameona kina maana katika utafiti wao wa hivi karibuni wa Agano la Kale.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kutoka 31:12–17

Tunaiheshimu Sabato kama ishara ya msimamo wetu kwa Bwana.

  • Unaweza kuanza kwa kuwauliza washiriki wa darasa ikiwa wamewahi kuelezea kwa mwanafamilia au rafiki kwa nini wao wanazichukulia Jumapili tofauti na siku zingine. Waalike washiriki kile walichosema au kile wanachoweza kusema baadaye. Kusoma Kutoka 31:12–17 au maelezo kwenye “Nyenzo za Ziada” yanaweza kuwapa mawazo ya ziada. Ni jinsi gani chaguzi zetu za siku ya Sabato zinaelezea msimamo wetu kwa Yesu Kristo?

  • Hata hivyo adhabu iliyoelezewa katika Kutoka 31:14–15 hazitumiki leo, zinaonyesha jinsi Bwana anavyohisi kuhusu Sabato. Kwa nini amri hii ni muhimu sana? Kujadili maandiko haya kunaweza kusaidia: Kutoka 31:12–17; Isaya 58:13–14; Mafundisho na Maagano 59:9–13.

    Picha
    watu wakitembea mbele ya kanisa

    Kwa kuiheshimu Sabato, tunaonyesha upendo wetu kwa Bwana.

Kutoka 32; 34:1–17

Dhambi humaanisha kuachana na Mungu, lakini Yeye hutoa njia ya kurudi.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari na kuifanya hadithi kuwa yao katika Kutoka 32, kwanza waombe kila mmoja kupitia upya sura kibinafsi au katika vikundi. Kisha waombe washiriki wa darasa wachukue nafasi ya Waisraeli ambao walikua hawana subira wakimngojea Musa arudi na wakaamua kutengeneza sanamu ya dhahabu. Je, ni hisia gani ambazo ziliweza kuwaongoza kwenye kuabudu sanamu? Washiriki wengine wa darasa wanaweza kujaribu kuwashawishi kubaki wakweli kwa Bwana na nabii Wake. Washiriki wa darasa wanaweza kuzungumza juu ya kile kinachowashawishi wao kushika maagano yao. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia wale ambao wanaweza kusumbuka katika kushika maagano yao?

  • Wakati watu wanaposoma Agano la Kale, wakati mwingine wanashangazwa na adhabu kali ambazo Bwana aliamuru kwa ajili ya dhambi. Kutoka 34:1–9 inaweza kuwasaidia kuona kwamba wakati Mungu hajali visingizio vyetu vya kutenda dhambi, Yeye pia ni mwenye huruma, akiwasamehe wale wanaotubu. Huenda washiriki wa darasa wangesoma kifungu hiki na kutafakari maswali kama haya: Je, tunajifunza nini kuhusu Bwana kutoka kwenye mistari hii? Kwa nini tunahitaji kujua vitu hivi kumhusu Yeye? Unaweza kusema kwamba Tafsiri ya Joseph Smith, Kutoka 34:7 (katika Kutoka 34:7, tanbihi e) inafafanua kwamba Mungu “hatawaondoa waasi.” Hii inaweza kumaanisha nini? Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki jinsi walivyoshuhudia rehema ya Mungu. Inawezekanaje kwa Mungu kuwa vyote mwenye rehema kamilifu na mwenye haki kamilifu? (ona Alama 42:13–15).

  • Kutoka 34: 6–17 inaweza kuonekana kama maelekezo ya kuwasaidia Waisraeli kutubu dhambi zao za kuabudu sanamu (iliyoelezewa katika Kutoka 32). Tunapata nini katika mistari hii ambacho yawezekana kiliwasaidia Waisraeli kutubu? Je, tunajifunza nini kuhusu Bwana na toba kutokana na maelekezo haya?

Kutoka 33:11–17

Tunahitaji uso wa Mungu katika maisha yetu.

  • Ni jinsi gani utawasaidia washiriki wa darasa kuyafanyia kazi yale Bwana aliyoyasema kwa Musa katika Kutoka 33:11–17? Unaweza kuanza kwa kupitia upya kazi ambayo Mungu bado alihitaji Musa kuitekeleza (ona Kutoka 33:1–3). Ni nini tunakipata katika mstari wa 11–17 ambacho kingeweza kumuimarisha na kumfariji Musa? Washiriki wa darasa wanaweza kufikiria juu ya kitu ambacho Mungu anataka wafanye—kama vile kutimiza wito wa Kanisa, jukumu la familia, au fursa ya kutumikia. Kisha wangeweza kusoma tena mistari hiyo. Je, ni utambuzi gani tunaupata kuhusu jinsi Mungu atakavyotusaidia sisi?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Sabato ni ishara.

Rais Russell M. Nelson anaelezea: “Katika miaka ya ujana wangu, nilijifunza kazi za wengine ambazo ziliorodhesha vitu vya kufanya na vya kutofanya katika Sabato. Haikuwa hadi baadaye ndipo nikajifunza kutoka katika maandiko kwamba mwenendo wangu na mtazamo wangu juu ya Sabato ilikuwa ishara kati yangu mimi na Baba yangu wa Mbinguni [ona Kutoka 31:13; Ezekieli 20:12, 20]. Kwa uelewa huo, sikuhitaji tena orodha ya vya kufanya na kutofanya. Nilipohitaji kufanya maamuzi ya kujua kama shughuli ilikuwa au haikuwa sahihi kwa ajili ya Sabato, nilijiuliza mwenyewe, ‘Ni ishara gani ninataka kumwonyesha Mungu?’ Swali hilo lilifanya uchaguzi wangu kuhusu siku ya Sabato kuwa dhahiri zaidi” (“The Sabbath Is a Delight,” Liahona, Mei 2015, 130).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha kupitia Roho. “Lengo kuu la kila kitu anachofanya mwalimu wa injili—kila swali, kila kifungu cha maandiko, kila shughuli—ni kumualika Roho Mtakatifu ajenge imani na kuwaalika wote kuja kwa Kristo” (Kufundisha katika Njia ya Bwana, 10).

Chapisha