Agano la Kale 2022
Mei 9–15. Hesabu 11–14; 20–24: “Msimwasi Bwana, Wala Msiogope”


“Mei 9–15. Hesabu 11–14; 20–24: ‘Msimwasi Bwana, Wala Msiogope ’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 9–15. Hesabu 11–14; 20–24,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
bonde la jangwani

Mei 9–15

Hesabu 11–14; 20–24

“Msimwasi Bwana, Wala Msiogope”

Moja ya njia bora ya kujua nini cha kuzingatia wakati wa darasa ni kuwauliza washiriki wa darasa kile walichoona cha maana walipojifunza maandiko. Hii itafunua kile ambacho ni muhimu kwao na nini wako tayari kujifunza.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati mwingine kinachohitajika kuwahimiza washiriki wa darasa kushiriki utambuzi waliopata kutoka kwenye masomo yao ni kuuliza swali rahisi kama “Roho Mtakatifu alikufundisha nini uliposoma maandiko wiki hii?” Kisha wape muda kutafakari na kujibu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Hesabu 12

Kusema mabaya dhidi ya nabii wa Bwana humkosea Bwana.

  • Kusoma Hesabu 12 kunaweza kusaidia washiriki wa darasa kuelewa uzito wa kusema mabaya dhidi ya nabii wa Bwana. Ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kusoma sura hii na kuongea kuhusu ni jinsi gani Bwana anajisikia kuhusu watumishi Wake. Kulingana na mstari wa 1–2, unafikiri inamaanisha nini kusema dhidi ya nabii wa Bwana? Nini hatari ya kufanya hivyo? Je, tunaweza kujifunza nini kutokana na matendo ya Musa kwa Waisraeli katika mstari wa 13 na 15?

Hesabu 12:3.

“Musa alikuwa mpole sana.”

  • Watu wengine wanaweza kushangaa kusoma kwamba kiongozi aliye hodari kama Musa, ambaye alisimama mbele ya Farao na kufanya miujiza ya kushangaza kwa nguvu za Bwana, pia alikuwa “mpole sana.” Ungeweza kutumia Hesabu 12:3 kuanzisha mjadala kuhusu upole wa kweli ni nini. Ungeweza kurejelea ufafanuzi katika “Mpole, Upole” katika Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Kama darasa, ungeweza pia kutafuta viashiria vya upole wa Musa katika Hesabu 12.

  • Ni ushahidi gani mwingine wa upole wa Musa tunaweza kujifunza? (ona, kwa mfano, Kutoka 18:13–25; Hesabu 11:26–29; Waebrania 11:24–27; Musa 1:10–11). Unaweza pia kusoma na kujadili jinsi Mwokozi alivyoonyesha upole (ona Mathayo 11:29; 27:11–14; Luka 22:41–42; Yohana 13:4–5). Mifano ya Musa na Mwokozi—au watu tunaowajua—inatufundisha nini kuhusu upole? Kwa nini Mungu anataka tuwe wapole?

Hesabu 13–14.

Kwa imani katika Bwana, tunaweza kuwa na matumaini kwa ajili ya siku zijazo.

  • Unapojadili hadithi kuhusu Waisraeli 12 walioipeleleza nchi ya ahadi na kutoa ripoti yao, fikiria kuwauliza washiriki wa darasa jinsi wanahisi hadithi hii inaweza kutumika kwa hali wanazokabiliana nazo. Kwa kusaidia, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kuorodhesha vitu kutoka Hesabu 13:23–33 ambavyo vinaweza kufananishwa na kitu fulani katika maisha yetu. Kwa mfano, nchi ya ahadi inaweza kuwakilisha kitu ambacho Bwana anataka tufanikishe, nguzo za zabibu zinaweza kuwa baraka, majitu yanaweza kuwa changamoto tutakazokabiliana nazo, na kadhalika. Watie moyo washiriki wa darasa kushiriki kile wanachohisi Bwana anaweza kutaka wajifunze kutokana na hadithi hii.

    Picha
    watu wakionesha matunda kwa Musa

    Wapelelezi kumi wa Israeli waliogopa; Yoshua na Kalebu walikuwa na imani. © Lifeway Collection/licensed from goodsalt.com

Hesabu 21:4–9

Kama tunamtazama Yesu Kristo kwa imani, Yeye anaweza kutuponya kiroho.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili hadithi katika Hesabu 21:4–9 na kujenga imani yao katika Mwokozi, unaweza kuandika maswali kama haya ubaoni: Je, nyoka wa shaba anawakilisha nini? Je, kuumwa na nyoka kunaweza kuwakilisha nini? Kwa nini watu wengine walikataa kumtazama yule nyoka wa shaba? Tunawezaje “kumuangalia” leo? Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki majibu wanayoyapata wanaposoma Hesabu 21:4–9; 1 Nefi 17:40–41; Alma 33:18–22; na Helamani 8:13–15. Ni baadhi ya mambo gani rahisi Mwokozi anatualika kufanya ili kupokea uponyaji Wake? Kwa nini wakati mwingine ni vigumu kufanya vitu hivyo rahisi? (ona “Nyenzo za Ziada” kwa maoni kadhaa juu ya hili). Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki ni kwa jinsi gani kufanya mambo haya kumeleta nguvu ya Bwana katika maisha yao.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

“Vitu vidogo na rahisi.”

Mzee L. Whitney Clayton alielezea juu ya askofu ambaye aliwashauri washiriki wa kata wanaokabiliwa na changamoto mbali mbali ngumu katika maisha yao:

“Ushauri wake kwa washiriki wa kata mara nyingi ulijumuisha kurudi kwenye mazoea rahisi ya imani, kama vile kusoma Kitabu cha Mormon[,] … kulipa zaka, na kuhudumu katika Kanisa kwa moyo wa dhati. Mara kwa mara, hata hivyo, majibu yao kwake yalikuwa ya kutiliwa shaka: ‘… Je, kufanya yoyote kati ya mambo hayo kuna uhusiano gani na maswala ambayo ninakabiliana nayo?

“… Wale ambao hufikiria sana juu ya kufanya ‘vitu vidogo na rahisi’ [Alma 37:6]—wakitii katika njia zinazoonekana kuwa ndogo—wanabarikiwa kwa imani na nguvu ambazo zinaenda mbali na matendo halisi ya utii wao wenyewe na, kwa kweli, njia hizi zinaweza kuonekana kabisa hazihusiani na maswala tunyokabiliana nayo” (“Lolote Atakalosema Kwenu, Fanyeni,” Liahona, Mei 2017, 98).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Zingatia kile kilicho muhimu zaidi. Haiwezekani kuelezea kila hadithi au kila kanuni. Mfuate Roho, na uzingatie mahitaji ya washiriki wa darasa unapoamua jinsi ya kutumia muda wa darasa. Kumbuka kwamba nyumbani, siyo darasani, ni kitovu cha kujifunza injili.

Chapisha