Agano la Kale 2022
Mei 2–8. Kutoka 35–40; Mambo ya Walawi 1; 16; 19: “Utakatifu kwa Bwana”


“Mei 2–8. Kutoka 35–40: Kumbukumbu ya Torati 1; 16; 19 ‘Utukufu kwa Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 2–8. Mwanzo 35–40; Mambo ya Walawi 1; 16; 19,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Hekalu la São Paulo Brazil

Mei 2–8

Kutoka 35–40; Mambo ya Walawi 1; 16; 19

“Utukufu kwa Bwana”

Unapokuwa na uzoefu wa maana kwa kusoma maandiko, utaweza kufundisha na kushuhudia unapokutana na washiriki wa darasa siku ya Jumapili. Unaweza kufanya nini ili kuwahamasisha washiriki wa darasa kufanya vivyo hivyo?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Sura za usomaji wa juma hili hutumia alama kufundisha juu ya Yesu Kristo na dhabihu Yake ya kulipia dhambi. Unaweza kuanza darasa kwa kuwaalika washiriki wa darasa kuandika au kuchora ubaoni kitu walichopata katika Kutoka 35–40 au Mambo ya Walawi 1; 16; 19 ambayo yaliwafundisha kuhusu Mwokozi. Waalike waelezee kuhusu kile walichojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kutoka 35–40

Bwana anatutaka sisi tuwe watakatifu kama Yeye alivyo.

  • Wakati washiriki wa darasa walipojifunza Kutoka 35–40 wiki hii, wanaweza kuwa walitafakari jinsi vitu vya maskani ya kale vinavyogeuza mawazo yao kwa Yesu Kristo. Kama walifanya, wahimize washiriki mawazo yao. Jedwali katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia lingeweza kusaidia kwenye majadiliano haya. Ungeweza pia kuzungumza juu ya kile alama hizi zinazohusiana na maskani zinafundisha juu ya kuwa watakatifu zaidi. Ni kwa jinsi gani Yesu Kristo hutusaidia sisi kuwa watakatifu zaidi?

  • Kwa wengi, wazo la kuwa watakatifu zaidi linaweza kuonekana kuwa haliwezi kufikiwa. Je, utawasaidiaje washiriki wa darasa kuelewa kwamba kuwa watakatifu ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni kwetu? Mnaweza kusoma pamoja maelezo ya Rais Henry B. Eyring katika “Nyenzo za Zaida.” Inamaanisha nini kuwa mtakatifu? Ni jinsi gani mahekalu ya siku za mwisho na kazi tunazozifanya humo zinatusaidia kuwa watakatifu zaidi? (ona pia Mafundisho na Maagano 84:19–24; 109:6–26; 128:15–18). Kisha ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki jinsi vitu hivi vilivyowasaidia—au wengine wanaowajua—kuwa watakatifu zaidi.

  • Nyumba ya Bwana ya Waisraeli jangwani ni sawa kwa njia nyingi na mahekalu yetu ya siku za mwisho. Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kuorodhesha vitu walivyojifunza kuhusu nyumba ya Bwana katika Kutoka 35–40 ambavyo vinawakumbusha yale tunayoyapitia katika hekalu. Kama wanahitaji msaada, ungeweza kuwaelekeza kwenye mistari katika Mwanzo 40 ikirejelea pazia, madhabahu, mavazi matakatifu, kuoshwa, na upako. Ni kwa jinsi gani hekalu linatusaidia kuja kwa Kristo? Tunaweza kufanya nini ili kufokasi muda wetu juu Yake tuwapo hekaluni?

Mambo ya Walawi 1:1–9; 16

Kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, tunaweza kusamehewa.

  • Ingawa wazo la dhabihu ya wanyama linaweza kuonekana geni kwetu leo, kuna mengi tunayoweza kujifunza kutokana na desturi hizi kuhusu dhabihu ya Yesu Kristo ya kulipia dhambi. Ili kuanza majadiliano, unaweza kuonyesha picha za Mwokozi akiwa Gethsemane na msalabani (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na.5657). Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki maneno ambayo wanaona yanahusiana na dhabihu ya Yesu Kristo ya kulipia dhambi. Kisha alika washiriki wa darasa kupitia Mambo ya Walawi 1:1–9 au Mambo ya Walawi 16, ambayo inaelezea dhabihu za wanyama, na kupata maneno ambayo wanahisi pia yanahusiana na dhabihu ya Mwokozi. Ni kwa jinsi gani dhabihu hizi za zamani zinaweza kutusaidia kuelewa vyema Upatanisho wa Yesu Kristo? Washiriki wa darasa wanaweza kuimba wimbo kuhusu Mwokozi na kushiriki hisia zao kuhusu Yeye.

    Picha
    watu wa kale wakileta matoleo ya kujenga nyumba ya Bwana

    Wana wa Israeli walitoa matoleo kwa ajili ya nyumba ya Bwana kwa “moyo wa kupenda” (Kutoka 35:5). Kielelezo na Corbert Gauthier, © Lifeway Collection/licensed from goodsalt.com

  • Inaweza kuwa yenye msaada kwa washiriki wa darasa kulinganisha dhabihu ya Bwana iliyotakiwa katika kipindi cha Agano la Kale na dhabihu Anayoitaka kwetu leo. Kwa mfano, wangeorodhesha njia tunazotoa dhabihu kwa Bwana na kazi Yake, kama vile kuhudumu katika wito, kulipa matoleo ya mfungo, kufanya kazi ya historia ya familia, au kutumikiana. Kisha mnaweza kusoma pamoja Mambo ya Walawi 1:1–9 na uwaalike washiriki wa darasa kutafuta vitu vya matoleo viliyoelezewa katika mistari hii ambavyo vinaweza kuhusiana na matoleo ambayo Bwana anatuomba tutoe leo (ona 3 Nefi 9:19–20; Mafundisho na Maagano 64:34). Tunaweza kujifunza nini kutoka Musa 5:7 kuhusu jinsi tunavyopaswa kuona dhabihu zetu kwa ajili ya kazi ya Bwana?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mungu anaweza kutufanya kuwa watakatifu.

Rais Henry B. Eyring alifundisha:

Furaha kuu huja kutokana na utakatifu mkuu wa mtu binafsi. … Maandiko yanatufundisha kwamba miongoni mwa vitu vingine, tunaweza kutakaswa au kuwa watakatifu zaidi wakati tunapoonesha imani katika Kristo, kuonesha utiifu wetu, kutubu, kutoa dhabihu kwa ajili Yake, kupokea ibada takatifu, na kushika maagano yetu tuliyoweka Naye. …

“Wimbo ‘More Holiness Give Me’ [Nyimbo za Kanisa, na. 131] unapendekeza njia ya kusali kwa ajili ya msaada wa kuwa watakatifu zaidi. Mwandishi kwa busara anapendekeza kuwa utakatifu tunaotafuta ni zawadi kutoka kwa Mungu mwenye upendo, itolewayo baada ya muda fulani, baada ya kufanya yote tunayoweza” (“Utakatifu na Mpango wa Furaha,” Liahona, Nov. 2019, 100–101, 103).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia muziki mtakatifu. Ujumbe ulioko katika nyimbo unaweza kuimarisha mafundisho katika maandiko. Kwa mfano, kuimba wimbo kama “More Holiness Give Me” au “I Stand All Amazed” (Nyimbo za Kanisa, na. 131, 193) kunaweza kuimarisha ujumbe uliofundishwa katika Mambo ya Walawi 16 na 19.

Chapisha