Agano la Kale 2022
Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24: “Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa”


“Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24: ‘Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Musa akimtawaza Yoshua

Kielelezo cha Musa akimtawaza Yoshua, na Darrell Thomas

Mei 23–29

Yoshua 1–8; 23–24

“Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa”

Unaposoma Yoshua 1–8 na 23–24, fikiria ushauri wa “tafakari humo mchana na usiku” (Yoshua 1:8). Zingatia mawazo yanayokujia. Haya yanaweza kukuongoza kwenye mawazo ya kufundishia kwa ajili ya darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike washiriki wa darasa kushiriki kifungu kutoka kwenye kusoma kwao wiki hii ambacho kiliongeza imani yao katika Yesu Kristo. Kwa mfano, yawezekana walitafakari njia ambazo misheni ya Yoshua ilivyowakumbusha juu ya misheni ya Yesu Kristo. Kwa nini tunashukuru kwa ajili ya hadithi zilizoko katika kitabu cha Yoshua?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Yoshua 1:1–9

“Uwe hodari na Moyo wa Ushujaa.”

  • Yoshua aliambiwa, “Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa” mara kadhaa (ona Kumbukumbu la Torati 31:7, 23; Yoshua 1:6–7, 9). Labda washiriki wa darasa wangenufaika kwa kujadili kile ambacho Bwana anamaanisha kwenye kifungu hiki. Wangeweza kuchunguza Yoshua 1:1–9 kwa ajili ya ushauri ambao Bwana alimpa Yoshua ili kumsaidia kuwa hodari na jasiri. Wanaweza pia kushiriki mifano ya watu wanaowajua ambao wana tabia hizi. Je, Yoshua alionyeshaje nguvu na ujasiri katika masimulizi yanayopatikana katika kitabu cha Yoshua? (kwa mfano, ona sura ya 3, 6, na 8). Washiriki wa darasa wangeweza kuelezea jinsi wao wanavyojaribu kuwa hodari na shujaa kwa ajili ya Kristo.

Yoshua 1:8

Neno la Mungu linaweza kuifanya njia yetu iwe yenye mafanikio.

  • Ili kuwatia moyo washiriki wa darasa katika masomo yao binafsi ya maandiko na ya familia, unaweza kusoma Yoshua 1:8 kama darasa. Tunaweza kujifunza nini kutoka kwenye mstari huu kuhusu jinsi ya kujifunza maandiko? Pengine washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kile wanachokifanya ili “kutafakari” katika maandiko “mchana na usiku.” Je, Bwana amefanyaje “njia yetu kuwa yenye mafanikio” na kutupatia “mafanikio mema” tunapojifunza neno Lake?

    Picha
    mwanamke akisoma maandiko

    Neno la Mungu linaweza “kuifanya njia [yetu] iwe yenye mafanikio” (Yoshua 1:8).

Yoshua 3–4

Tunaweza kushuhudia “maajabu” ya Mungu.

  • Labda washiriki wa darasa wangenufaika na hadithi fupi ya Waisraeli wakivuka Mto Yordani. Unaweza kugawanya darasa katika jozi na kualika kila jozi kusimuliana hadithi hii, wakipeana zamu ya kusema sentensi moja kwa wakati (wahimize waangalie katika Youshua 3 ikiwa wanahitaji msaada wa kukumbuka hadithi hiyo). Kisha, kama darasa, wangeweza kujadili maelezo yoyote ambayo yana maana kwao. Je, tunajifunza nini kutoka kwenye hadithi hii ambacho kinaweza kutusaidia kupata uzoefu wa “maajabu” ya Bwana katika maisha yetu? (verse 5). Ni “maajabu” gani aliyoyafanya kwa ajili yetu? Kwa nini ni muhimu kwamba kila kizazi kina tukio la kiroho ambalo linawafundisha wao kwamba “Bwana … ni mwenye nguvu”? (Yoshua 4:24).

  • Ingawa sisi sote tunahitaji kuwa na uzoefu wetu wenyewe wenye kujenga imani, kukumbuka kile ambacho Bwana amewafanyia mababu zetu pia ni muhimu. Kulingana na Yoshua 4, Waisraeli walifanya nini ili kuvisaidia vizazi vijavyo kukumbuka uvukaji wa Mto Yordani? (ona Yoshua 4:1–7). Je, sisi tunafanya nini kuhakikisha kwamba uzoefu wetu hausahauliki na vizazi vijavyo?

Yoshua 6–8

Utii huleta nguvu ya Mungu katika maisha yangu.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inapendekeza kulinganisha vita vya Waisraeli dhidi ya Wakanaani katika Yoshua 6–8 pamoja na vita vyetu binafsi dhidi ya majaribu. Ungeweza kuwauliza washiriki wa darasa ni mawazo au hisia gani walizokuwa nazo wakati walipokuwa wakisoma sura hizi na wazo hili la mlingano katika akili. Au unaweza kuonyesha mistari maalum ambayo inaonekana kuendana na vita vyetu ili kuepuka dhambi, na wangeweza kuzungumza juu ya kile mistari hiyo inafundisha juu ya kupata kuufikia uwezo wa Mungu katika maisha yetu. Baadhi ya mistari hii inaweza kujumuisha Yoshua 6:1–5, 18, 20; 7:11–13.

Yoshua 23–24

“Chagueni hivi leo mtakayemtumikia.”

  • Labda ingewasaidia washiriki wa darasa kutumia Yoshua 23–24 kwao wao wenyewe ikiwa watafikiria kuwa wao walikuwa Waisraeli wakimsikia Yoshua akitoa ushauri huu mwishoni mwa maisha yake. Unaweza kuwapa mistari michache kusoma kimya kimya na kisha uwaombe washiriki kitu kutoka kwenye mistari hiyo ambacho kingewahamasisha kubaki waaminifu kwa Bwana. Wanaweza pia kushiriki jinsi walivyofanya maamuzi binafsi kuhusu “nani watamtumikia” (Yoshua 24:15). Kwa nini walifanya maamuzi haya?

  • Unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kuchagua kifungu kutoka Yoshua 23–24 ambacho kinawahamasisha kuchagua kumtumikia Mungu na kisha kuunda bango au kumbukumbu yenye kifungu hiki cha maneno ili kuonyesha nyumbani au kwenye mitandao ya kijamii.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ukuaji wa kiroho hutokea nyumbani. Washiriki wa darasa lako wanahitaji kuwa na uzoefu wao wenyewe wa kiroho nje ya darasa ili kubaki kuwa wa kiroho zaidi. Tafuta njia za kutumia muda mfupi ulio nao kuwahamasisha kupata chakula cha kiroho katika maandiko nyumbani—binafsi na pamoja na familia zao. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 18.)

Chapisha