Agano la Kale 2022
Mei 16–22. Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34: “Jihadhari Usije Ukamsahau Bwana”


“Mei 16–22. Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34: ‘Jihadhari Usije Ukamsahau Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 16–22. Kumbukumbu la Torati 6–8;15;18; 29–30; 34 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Musa akisimama juu ya mlima

Kielelezo cha Musa juu ya Mlima Nebo, © Providence Collection/licensed kutoka goodsalt.com

Mei 16–22

Kumbukumbu la Torati 6–8; 15; 18; 29–30; 34

“Jihadhari Usije Ukamsahau Bwana”

Musa aliongozwa kiungu ili kuwafundisha watoto wa Israeli kulingana na mahitaji yao (ona Kumbukumbu la Torati 6:1). Unapojifunza Kumbukumbu la Torati, tafuta mwongozo wa kiungu wa kujua ni kanuni gani za kufundisha, kulingana na mahitaji ya washiriki wa darasa.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kwa sababu Kumbukumbu la Torati lina maneno ya mwisho ya Musa kwa wana wa Israeli, unaweza kualika washiriki wa darasa kushiriki kitu walichopata katika Kumbukumbu la Torati ambacho wangependa kukiingiza katika maneno yao ya mwisho kwa watoto wao au wajukuu. Wakiwa wanashiriki, waombe kuelezea kwa nini walichagua maneno hayo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kumbukumbu la Torati 6:4–7, 20–25; 8:2–5, 11–17; 29:18–20; 30:6–10, 15–20

Bwana anatutaka tumpende Yeye kwa mioyo yetu yote.

  • Katika Kumbukumbu la Torati, kuna vifungu ambavyo vinaweza kutusukuma kufikiria juu ya hali ya kiroho ya mioyo yetu. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kushiriki mawazo yao kuhusu vifungu hivi, ungeweza kuchora moyo ubaoni. Kisha yagawanye maandiko yafuatayo miongoni mwa washiriki wa darasa: Kumbukumbu la Torati 6:4–7, 20–25; 8:2–5, 11–17; 29:18–20; 30:6–10, 15–20. Waalike washiriki wa darasa kuandika rejeleo ndani ya moyo ikiwa inafundisha juu ya kitu ambacho tunapaswa kuwa nacho mioyoni mwetu au kuandika rejeleo nje ya moyo ikiwa inafundisha jambo ambalo tunapaswa kuepuka. Inamaanisha nini kujitoa kwa mioyo yetu yote kwa Baba wa Mbinguni?

  • Je, tunaelezeaje familia yetu na wengine kwa nini tunatii amri za Mungu? Baada ya kutafakari swali hili, washiriki wa darasa wangesoma Kumbukumbu la Torati 6:4–7, 20–25 au maelezo katika “Nyenzo za Ziada” na kushiriki mawazo yao. Ni jinsi gani utambuzi huu unavyogusa jinsi sisi tunavyojisikia kuhusu amri au maagano?

Kumbukumbu la Torati 6:4–9, 20–25

“Fundisha [maneno ya Bwana] kwa bidii kwa watoto wako.”

  • Wakati mwingine inasaidia kusikia maoni juu ya njia ambazo wengine wanafundisha na kujifunza injili katika nyumba zao. Kujadili jinsi washiriki wa darasa wanavyofuata ushauri katika Kumbukumbu la Torati 6:4–9, 20–25 inaweza kuwapa darasa lako nafasi ya kujifunza kutoka kwa kila mmoja. Tunafanya nini ili kufundisha na “kuzungumza juu ya” (mstari wa 7) neno la Mungu kama mistari hii inavyoelezea? Ni uzoefu gani tunaweza kushiriki ambao Bwana alituongoza katika juhudi zetu?

Kumbukumbu la Torati 15:1–15

Kusaidia wenye shida kunahusisha mikono ya ukarimu na mioyo iliyo tayari.

  • Bado hatujafika katika siku “ambayo hakutakuwa na maskini kati yenu” (Kumbukumbu la Torati 15:4), kwa hivyo kanuni kuhusu kuwasaidia maskini katika Kumbukumbu la Torati 15 bado ni muhimu, hata kama mazoea fulani kuhusu madeni na watumishi yamebadilika. Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kurejea upya Mistari ya 1–15 na kutafuta kanuni kuhusu kuwasaidia maskini na wenye shida ambao wangependa kujadili. Maswali kama haya yanaweza kusaidia majadiliano: Inamaanisha nini “kufungua mkono wako wazi” kwa wale walio na shida? (mstari wa 8, 11). Je, moyo wetu una nafasi gani katika kuwasaidia wengine? (ona mstari wa 7, 9–10). Tunaweza kujifunza nini kuhusu kuwasaidia wenye shida kutokana na mfano wa Bwana? (ona mstari 15).

Kumbukumbu la Torati 29:9; 30:15–20

Bwana anatualika kuchagua kati ya “maisha na mema, na kifo na uovu.”

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Tunashika maagano yetu kwa sababu tunampenda Mungu.

Rais Linda K. Burton alifundisha:

“Juu ya sababu zote tunazopaswa kuwa na bidii zaidi katika kushika agano letu, sababu hii ni ya kuvutia sana kuliko zote—upendo. …

“‘Ikiwa tunathamini kikamilifu baraka nyingi ambazo ni zetu kupitia ukombozi uliofanywa kwa ajili yetu, hakuna kitu ambacho Bwana angetaka kutoka kwetu ambacho hatungefanya kwa shauku na kwa hiari’ [Joseph Fielding Smith, “Importance of the Sacrament Meeting,” Relief Society Magazine, Oct. 1943, 592]. Kulingana na maelezo haya ya Rais Joseph Fielding Smith, kushika agano ni njia mojawapo ya kuonyesha upendo wetu kwa Upatanisho usioweza eleweka, usio na mwisho wa Mwokozi na Mkombozi wetu na upendo mkamilifu wa Baba yetu wa Mbinguni” (“The Power, Joy, and Love of Covenant Keeping,” Liahona, Nov. 2013, 114).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Sikiliza. “Kusikiliza ni tendo la upendo. … Muombe Baba wa Mbinguni akusaidie kuelewa kile washiriki wa darasa lako wanachosema. Unapotoa usikivu wa umakini kwa ujumbe wao unaozungumzwa na usiozungumzwa, utakuja kuelewa vyema mahitaji yao, mashaka yao, na matamanio yao” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 34).

Chapisha