Agano la Kale 2022
Novemba 28–Desemba 4. Nahumu; Habakuki; Sefania: “Miendo Yake iIikuwa kama Siku za Kale”


“Novemba 28–Desemba 4. Nahumu; Habakuki; Sefania: ‘Miendo Yake Iikuwa kama Siku za Kale,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Novemba 28–Desemba 4. Nahumu; Habakuki; Sefania,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yesu akitazama juu kwenye nyota

“Miendo yake ilikuwa kama siku za kale” (Habakuki 3:6). Hapo mwanzo kulikuwako Neno, na Eva Timothy

Novemba 28–Desemba 4

Nahumu; Habakuki; Sefania

“Miendo yake ilikuwa kama siku za kale”

Mfano wako kama mwanafunzi wa injili unaweza kuwa baraka kwa darasa lako. Waelezee jinsi gani Roho Mtakatifu anavyokusaidia kuelewa maandiko na kuonyesha kujiamini kwako kwamba Yeye anaweza kuwasaidia wao pia.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwapa washiriki wa darasa fursa ya kuelezea umaizi kutoka katika kujifunza kwao maandiko, ungeweza kuandika Nahumu, Habakuki, na Sefania kama vichwa ubaoni. Kisha washiriki wa darasa wanaweza kuandika chini ya vichwa neno au kirai ambacho ni wazi kwao na sura na mstari ambapo wanaweza kukipata. Wape wao muda wa kuelezea kwa nini maneno haya au virai hivyo ni vya maana sana na kile ambacho Roho Mtakatifu amewafundisha.

Fundisha Mafundisho

Nahumu 1

Bwana ni mwenye nguvu na ni mwenye rehema

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia upendekeza kupekua Nahumu 1 kwa ajili ya mistari ambayo inaelezea sifa za Bwana. Unaweza kuwauliza washiriki wa darasa kitu walichojifunza kuhusu Bwana katika kujifunza kwao binafsi. Kwa mfano, tunajifunza nini kumhusu Yeye kutoka katika mstari wa 1–9? Unaweza kutaja kwamba Nahumu alitoa unabii wa hukumu ya Bwana dhidi ya Ninawi, mji mkuu wa Ashuri, na kwamba Ashuri ilikuwa imewakandamiza Waisraeli kwa miaka mingi. Kwa nini ilikuwa muhimu kwa Waisraeli kusikia ujumbe wa Nahumu kutoka kwa Mungu? Kwa nini ni muhimu kwetu sisi leo?

    Picha
    ngome ya mawe

    “Bwana ni mwema, ni ngome siku ya taabu” (Nahumu 1:7).

Habakuki 1:1–4; 2:1–4;3

Tunaweza kutumaini mapenzi ya Bwana na wakati Wake.

  • Ingekuwa msaada kwa washiriki wa darasa kujua kwamba, kama wengi wetu, Habakuki alikuwa anasumbuliwa na kile alichokiona katika ulimwengu uliomzunguka. Labda washiriki wa darasa wangeweza kusoma Habakuki 1:1–4 na kufanya muhtasari wa wasi wasi wa Habakuki. Wanaweza pia kulinganisha maswali yao na mengine katika maandiko, kama yanavyopatikana katika Marko 4:37–38 na Mafundisho na Maagano 121:1–6. Je! maswali gani yanayofanana watu wanauliza kuhusu Mungu leo? Ni ushauri gani Bwana alitoa katika Habakuki 2:1–4 ambayo hukusaidia kutumaini mapenzi Yake na wakati Wake? (Ona pia Marko 4:39–40; Mafundisho na Maagano 121:7–8). Washiriki wa darasa wanaweza kupata umaizi katika “Nyenzo za Ziada.” Wao wangeshiriki jinsi ambavyo Mwokozi amewasaidia wao “kuishi kwa imani [yao]” hata wakati wanapokuwa na maswali ambayo hayana majibu.

  • Ili kuanza majadiliano ya Habakuki 3, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kupitia sura hii na kushiriki madhihirisho ya sifa na imani waliyopata. Ili kuwasaida wao kutumia maneno haya kwa wao wenyewe, ungemwalika kila mshiriki wa darasa kuandika orodha ya baraka ambazo Mungu amempatia. Waalike kutafakari kitu ambacho kingefanyika kama angepoteza baadhi ya hizi baraka za kimwili. Someni pamoja Habakuki 3:17–19, na kujadili kwa nini ingekuwa vigumu “kufurahia katika Bwana” (mstari wa 18) wakati wa magumu kama yale yaliyoelezwa mstari wa 17. Tunawezaje kukuza imani kama Habakuki?

Sefania 3:14–20

Bwana atafurahia pamoja na watu Wake katika Sayuni.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kupata tumaini kwa ajili ya siku za usoni katika Sefania 3:14–20, ungeweza kuandika ubaoni “Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote” kwa sababu.… Kisha washiriki wa darasa wanaweza kupekua mistari hii ili kuona baraka zilizoahidiwa kwa ajili ya siku za usoni ambazo zinaweza kuwasaidia kufuruahia leo. Ni jinsi gani ahadi hizi zinatusaidia wakati wa kipindi kigumu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Imani maana yake ni kutumaini hekima, huruma, na wakati wa Bwana.

Mzee Jeffrey R. Holland alisema:

“Je, ni kwa muda gani tutasubiri kupata msaada kutokana na ugumu ambao huja juu yetu? Je, kuhusu kustahimili majaribu binafsi wakati tunaposubiri na kusubiri, na msaada kuonekana kuja pole pole sana? Kwa nini kucheleweshwa wakati mizigo inaonekana kuwa mizito kuliko tunavyoweza kuibeba?

“… Kutakuwa na nyakati katika maisha yetu ambapo hata jitihada zetu bora kabisa na za dhati, sala zetu za kusihi hazitazaa ushindi ambao tumeutamani, iwe hiyo ni kuhusu mambo mapana ya kidunia au yale madogo ya kibinafsi. Hivyo wakati tukifanya kazi na kusubiri kwa pamoja majibu kwa baadhi ya maombi yetu, ninawapeni ninyi ahadi yangu ya kitume kwamba zimesikika na zinajibiwa, ingawa pengine sio kwa wakati ule, au katika njia tunayotaka sisi. Lakini daima zinajibiwa katika wakati na katika njia ya mzazi wa milele mjua yote na mwenye huruma anavyopaswa kuyajibu.…

“… Imani maana yake ni kumtumainia Mungu katika nyakati nzuri na mbaya, hata kama hiyo inajumuisha mateso fulani hadi tunapouona mkono Wake ukifunuliwa kwa niaba yetu” (“Kumsubiria Bwana,” Ensign au Liahona, Nov. 2020, 115–16).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Uliza maswali yaliyo wazi. Unapowauliza washiriki wa darasa kuhusu uzoefu wao wa maandiko, “wajulishe kwamba hautafuti jibu mahususi bali kwamba una hamu ya kweli kujua kile wanachojifunza” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 29). Kwa baadhi ya mifano ya maswali yaliyo wazi, ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 31–32.

Chapisha