Agano la Kale 2022
Desemba 19–25. Krismasi: “Ndiye Tuliyemngoja, Naye Atatuokoa”


“Desemba 19–25. Krismasi: ‘Ndiye Tuliyemngoja, Naye Atatuokoa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 19–25. Krismasi,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
mtoto Yesu amefunikwa na nguo nyeupe na kalazwa kwenye nyasi

Kwa Ajili Yetu Mtoto Amezaliwa, na Simon Dewey

Desemba 19–25

Krismasi

“Ndiye Tuliyemngoja, Naye Atatuokoa”

Wakati wa kujifunza kwako binafsi na maandalizi ya kufundisha, fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuona shangwe kuu ya kuzaliwa kwa Mwokozi. Mwalike Roho ashuhudie kwao juu ya upendo wa kukomboa wa Yesu Kristo.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati wa Krismasi unaweza kuwa fursa nzuri ya kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki jinsi kujifunza kwao Agano la Kale kulivyoimarisha imani yao katika Yesu Kristo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho Rasmi

Tunashangilia katika Mkombozi wetu.

  • Hata ingawa Krismasi inajulikana kama majira ya shangwe, kuna wengi ambao hali zao zinafanya kuwa vigumu kupata shangwe, hata katika wakati huu wa mwaka. Ujumbe muhimu wa Krismasi ni kwamba Mwokozi anaweza kuifanya myepesi mizigo yetu na kutusaidia kupata imani na hata shangwe. Ili kushiriki ujumbe huu, unaweza kuandika ubaoni marejeo ya maandiko yafuatayo: Zaburi 35:9; Isaya 25:8–9; 44:21–24; 51:11; Sefania 3:14–20; Musa 5:5–11. Kisha unaweza kuandika ubaoni swali kwa ajili ya washiriki wa darasa kutafakari wanaposoma vifungu hivi, kama vile Ni kwa sababu gani vifungu hivi vya maandiko hutoa za kuwa wenye shangwe? Waombe washiriki kile walichopata. Pengine unaweza pia kuwapa muda washiriki wa darasa kuandika kuhusu shangwe yao wenyewe katika Mwokozi. Wangeweza kupata umaizi wa ziada kutoka katika ujumbe wa Rais Russell M. Nelson katika ”Nyenzo za Ziada.”

  • Krismasi hutoa fursa za kueneza shangwe ya Kristo kwa wengine. Kabla ya darasa, unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kupitia ujumbe wa Mzee Ulisses Soares “Jeshi la Malaika wa Kisasa” (Ibada ndogo ya Urais wa Kwanza, Desemba 8, 2019, broadcasts.ChurchofJesusChrist.org) na waje wakiwa wamejiandaa kushiriki jinsi kitendo cha huduma kilimsaidia Mzee Soares na familia yake kuona shangwe ya Krismasi. Unaweza pia kushiriki sehemu za ujumbe wake katika darasa. Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki uzoefu wao wa vitendo vya kutoa au kupokea huduma wakati wa Krismasi. Ni kwa jinsi gani tunaweza kutenda juu ya mwaliko wa Mzee Soares wa kufuata mfano kamili wa Mwokozi wa upendo na ukarimu kwa binadamu”?

Ishara zinaweza kutusaidia kumkumbuka Yesu Kristo.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unaorodhesha baadhi ya ishara katika Agano la Kale ambazo zinafundisha kuhusu Yesu Kristo. Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki kile walichojifunza kuhusu Mwokozi kutoka katika ishara hizi na zingine walizozipata katika kujifunza kwao. Je, tunajifunza nini kuhusu kumpata Mwokozi katika maandiko? Ni uzoefu gani umetufundisha kwamba “vitu vyote vimeumbwa na vimefanywa ili kumshuhudia [Yeye]” (Musa 6:63).

Mungu alitupatia zawadi ya Mwana Wake.

  • Kutoa zawadi ni desturi ya Krismasi katika tamaduni nyingi. Unaweza kuongoza mjadala na washiriki wa darasa kuhusu zawadi Mungu ametupatia, hasa zawadi ya Mwanawe, Yesu Kristo. Kufanya hili, unaweza kushiriki video “He is the Gift”(ChurchofJesusChrist.org) na kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki kile zawadi ya Mwokozi inamaanisha kwao. Tunawezaje kumwonyesha Baba wa Mbinguni shukrani zetu kwa ajili ya zawadi hii?

Isaya 7:14; 9:6

“Na jina Lake litaitwa wa Ajabu.”

  • Nabii Isaya alitumia majina mengi na vyeo ili kumwelezea Masiya, ambaye angezaliwa katika Bethlehemu (ona kwa mfano, Isaya 7:14; 9:6). Labda washiriki wa darasa wanaweza kufurahia kujifunza zaidi kuhusu Mwokozi na misheni yake kuhusu vyeo hivi? Wanaweza kuchagua cheo kimoja na kutafuta vifungu vya maandiko ambavyo vitawasaidia kuelewa kile kinachomaanisha. Kwa mfano, wanaweza kujifunza zaidi kuhusu cheo “Mfalme wa Amani” (Isaya 9:6) kwa kusoma Zaburi 85:8; Isaya 52:7; Luka 2:14; au Yohana 16:33. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kupata maandiko mengine, pendekeza kwamba waangalie katika Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Vyeo hivi vinapendekeza nini kuhusu Mwokozi na kile anachotufanyia sisi?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Yesu Kristo hutoa amani na shangwe.

Rais Russell M. Nelson alifundisha:

“Wakati fokasi ya maisha yetu kwenye mpango wa Mungu wa wokovu … na Yesu Kristo na injili Yake, tunaweza kuhisi shangwe bila kujali nini kinatokea—au hakitokei—katika maisha yetu. Shangwe inakuja kutoka Kwake na kwa sababu Yake. Yeye Ndiye kiini cha shangwe yote. Tunaisikia wakati wa Krismasi pale tunapoimba, ‘Joy to the world, the Lord is come’ [Wimbo, na. 201]. Na tunaweza kuhisi hivyo mwaka mzima. Kwa Watakatifu wa Siku za Mwisho, Yesu Kristo ndiye shangwe!…

“Kama vile Mwokozi anavyotoa amani ambayo ‘inapita akili yote’[Wafilipi 4:7], Yeye pia anatoa kiwango, kina, upana wa furaha ambayo inapita uelewa wa mwanadamu au uelewa wa kimwili” (“Furaha na Kupna Kiroho,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 82).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Jitayarishe ukiwa na watu akilini. “Acha uelewa wako juu ya wale unaowafundisha uongoze mipango yako. … Walimu walio kama Kristo hawatumii mtindo au mbinu moja tu; wao hufanya kila juhudi kuwasaidia watu kujenga imani yao katika Yesu Kristo” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,7).

Chapisha