Mafundisho na Maagano 2021
Januari 18–24. Mafundisho na Maagano 3–5: “Kazi Yangu Itakwenda Mbele”,


“Januari 18–24. Mafundisho na Maagano 3–5: ‘Kazi Yangu Itakwenda Mbele”, Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021) (2020)

“Januari 18–24. Mafundisho na Maagano 3–5.” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha
watu wakifanya kazi shambani

Wakati wa Mavuno Ufaransa na James Taylor Harwood

Januari 18–24

Mafundisho na Maagano 3–5.

“Kazi Yangu Itakwenda Mbele”,

Andika kile unachojifunza na kuhisi unapojifunza maandiko. Hii itakusaidia kukumbuka misukumo hiyo na ishiriki pamoja na wengine.

Andika Misukumo Yako

Wakati wa miaka yake michache kama nabii wa Bwana, Joseph Smith, bado hakujua kila kitu kuhusu “kazi ya ajabu” aliyoitwa kufanya. Bali kitu kimoja uzoefu wake wa awali ulichomfundisha ilikuwa kwamba kustahili kwa ajili ya kazi ya Mungu, jicho lake lazima kwa kweli liwe “kwenye utukufu wa Mungu” (Mafundisho na Maagano 4:1, 5). Kwa mfano, kama Bwana alimpa ushauri ambao ulikwenda kinyume na matamanio yake mwenyewe, alihitaji kufuata ushauri wa Bwana. Na hata kama alikuwa na “funuo nyingi” na … uwezo wa kufanya kazi kuu nyingi,” kama mapenzi yake mwenyewe yalikuwa muhimu zaidi machoni pake kuliko mapenzi ya Mungu, “lazima angeanguka” (Mafundisho na Maagano 3:4). Bali Joseph alijifunza kitu fulani kingine muhimu vilevile kuhusu kufanya kazi ya Mungu: “Mungu ni mwenye rehema,” na kama Joseph angetubu kwa dhati, angelikuwa “bado mteule” (mstari wa 10). Kazi ya Mungu ni, hata hivyo, kazi ya wokovu. Na kazi hiyo “haiwezi kubatilishwa” (mstari wa 1).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Mafundisho na Maagano 3:1–15

Ninapaswa kumwamini Mungu kuliko kumwogopa binadamu.

Mapema katika utumishi wa Joseph Smith, marafiki wema walikuwa wagumu kupatikana—hususani marafiki kama Martin Harris, aliyeheshimika, mtu maarufu, ambaye alikuwa katika nafasi ya kutoa msaada wenye thamani. Na Martin kwa hiyari alimsaidia Joseph, japokuwa ilimgarimu heshima ya malodi wenzake na ilihitaji kujitolea kifedha.

Kwa hiyo ni rahisi kuona kwa nini Joseph alitaka kuheshimu ombi la Martin kuchukuwa sehemu ya kwanza iliyotafsiriwa ya Kitabu cha Mormoni kumwonyesha mke wake, aliyekuwa na wasiwasi na ukweli wa Kitabu cha Mormoni. Joseph aliendelea kumwomba Bwana kuhusu ombi hili, hata wakati Bwana alipolikataa, mpaka hatimaye, baada ya Joseph kuomba mara ya tatu, Bwana alisema ndiyo. Kwa masikitiko, muswada ulipotea wakati ukiwa mkikononi mwa Martin, na Joseph na Martin walirudiwa kwa ukali sana na Bwana (ona Watakatifu, 1:51–53).

Unaposoma Mafundisho na Maagano 3:1–15, tafakari jinsi maoni ya watu wengine yanavyoweza kukuathiri. Unaweza pia kufahamu kuwa kwa kuongezea kwenye karipio la Joseph Smith, Bwana alisema maneno ya rehema. Unajifunza nini kutokana na jinsi Bwana alivyofanya vyote kumsahihisha na kumtia moyo Joseph? Unapata ushauri gani ambao unaweza kukusaidia wakati unapojaribiwa kuwaogopa watu wengine zaidi ya Mungu?

Ona pia “Michango ya Martin Harris,” Funuo katika Muktadha, 1–9 history.ChurchofJesusChrist.org.

Mafundisho na Maagano 4

Bwana ananitaka mimi kumtumikia kwa moyo wangu wote.

Sehemu ya 4 mara nyingi inatumika kwa wamisionari wa muda wote. Hata hivyo, inapendeza kufahamu kwamba ufunuo huu ulitolewa kwanza kwa Joseph Smith, Mkubwa., ambaye hakuwa ameitwa kwenye umisionari lakini bado alikuwa “anatamani kumtumikia Mungu” (mstari wa 3).

Njia moja ya kusoma sehemu hii ni kuifikiria kama maelezo ya kazi kwa ajili ya mtu fulani anayetaka kufanya kazi ya Mungu. Sifa ni zipi? Kwa nini ujuzi huu au sifa hizi bainifu ni muhimu? Pengine ungeweza kwa sala kuchagua kitu kimoja ungeweza kufanya kwa uzuri “kujipasisha [wewe mwenyewe] kwa ajili ya kazi” (mstari 5).

Mafundisho na Maagano 5

Naweza kupata ushahidi wangu mwenyewe wa Kitabu cha Mormoni.

Picha
Martin Harris

Martin Harris, na Lewis A. Ramsey

Kama ungeitwa kushuhudia mahakamani kuhusu ukweli wa Kitabu cha Mormoni, ni ushahidi gani ungeutoa? Swali kama hilo lilikuwa kwenye akili za Martin Harris wakati mke wake, Lucy, alipotoa madai kwamba Joseph Smith alikuwa akidanganya watu kwa kujifanya anatafsiri mabamba ya dhahabu (ona Watakatifu, 1:56–58). Kwa hiyo Martin alimwomba Joseph ushahidi zaidi kwamba mabamba ya dhahabu yalikuwa ya kweli . Mafundisho na Maagano 5 ni ufunuo katika kujibu ombi la Martin.

Ni nini ninachojifunza kutoka Mafundisho na Maagano 5 kuhusu yafuatayo:

Mafundisho na Maagano 5:1–10

Kizazi hiki kitapokea neno la Mungu kupitia Joseph Smith.

Ni nini Mafundisho na Maagano 5:1–10 inakufundisha kuhusu wajibu muhimu wa Joseph Smith katika wakati wetu—na katika maisha yako? Tafakari jinsi ulivyopokea neno la Mungu kupitia Nabii Joseph Smith. Fikiria kurekodi katika shajara au kushiriki na mtu fulani shukrani zako kwa ajili ya kweli ambazo zilirejeshwa kupitia kwake.

Ona pia 2 Nefi 3:6–24.)

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Mafundisho na Maagano 3:1–4.Muombe mwanafamilia kutembea katika mstari “usio mnyoofu” na kisha katika mstari “ulionyooka.” Inamaanisha nini kwa familia yetu kujua kwamba njia za “[Mungu]” zimenyooka”?

Mafundisho na Maagano 3:7–10.Wakati mtu fulani anapotushinikiza kutomtii Mungu, ni kweli zipi katika mistari hii zinaweza kutusaidia kubaki waaminifu? Pengine wana familia wangeweza kuigiza hali ambayo mtu fulani anabaki mwaminifu licha ya shinikizo la kutomtii Mungu.

Mafundisho na Maagano 4.Wanafamilia yako wanapojadiliana kile inachomaanisha kufanya kazi katika shamba la Mungu, wangeweza kufanya baadhi ya kazi katika bustani (au kujifanya wanafanya hivyo). Vifaa gani vinahitajika kwa ajili ya kufanya kazi bustanini? Ni nini Mungu anaeleza katika sehemu ya 4 ambacho kingeweza kufikiriwa ni vifaa vinavyohitajika kufanya kazi Yake? Familia yako ingeweza kujadili kwa nini kila kifaa ni muhimu katika kufanya kazi ya Mungu.

Mafundisho na Maagano 5:7.Ni ipi baadhi ya mifano ya kweli tunazoamini lakini hatuweza kuziona? Ni kwa jinsi gani tungeweza kumjibu rafiki anayetaka ushahidi kwamba Kitabu cha Mormoni ni cha kweli?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa “I Will Be Valiant,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto,162.

Kuboresha Kujifunza Kibinafsi

Kariri mstari. “Kukariri maandiko ni kubuni urafiki mpya. Ni kama kugundua mtu mpya ambaye anaweza kusaidia wakati wa shida, kutoa msukumo na faraja, na kuwa chanzo cha motisha kwa ajili ya badiliko linalohitajika” (Richard G. Scott, “Nguvu ya Maandiko,” Ensign au Liahona, Nov. 2011, 6).

Picha
Joseph Smith na wazazi wake

Uzito wa Uharibifu wa Kurasa 116, na Kwani Povi Winder

Chapisha