Mafundisho na Maagano 2021
Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66: “Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali”


“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66: ‘Bwana Anahitaji Moyo na Akili yenye Kukubali,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha
shamba kwenye mawio ya jua

Wilaya ya Daviess, Missouri

Juni 14–20

Mafundisho na Maagano 64–66

“Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali”

Rais Henry B. Eyring alisema: “mara kwa mara ninaenda kwenye maandiko nikiwa na maswali ‘Ni nini Bwana anataka nifanye?’ au ‘Ni nini Yeye anataka nihisi?’ Siku zote ninapata mawazo mapya ambayo sikuwa nayo kabla” (“Jinsi Mungu Anavyozungumza Nami kupitia Maandiko,” Feb. 6, 2019, blog.ChurchofJesusChrist.org).

Andika Misukumo Yako

Katika kipindi cha joto kali la Agosti 1831, wazee kadhaa walikuwa wakisafiri kurejea Kirtland baada ya kufanyia utafiti ardhi ya Sayuni huko Missouri kama ilivyoelekezwa na Bwana. Haikuwa safari ya kufurahisha. wasafiri—Joseph Smith, Oliver Cowdery, Sidney Rigdon, Ezra Booth, na wengine—walikuwa wakihisi joto na uchovu, na mivutano punde iligeuka kuwa ugomvi. Ingeweza kuonekana kama vile kuijenga Sayuni, mji wa upendo, umoja, na amani, ingechukua muda mrefu.

Kwa bahati nzuri, kuijenga Sayuni—huko Missouri mnamo 1831 au katika mioyo na kata zetu leo—hakuhitaji sisi tuwe wakamilifu. Badala yake, “lakini ninyi mnatakiwa kusamehe,” Bwana alisema (Mafundisho na Maagano 64:10). Yeye anahitaji “moyo na akili yenye kukubali” (mstari wa 34). Na Yeye anahitaji uvumilivu na bidii, kwani Sayuni inajengwa juu ya misingi ya “mambo madogo,” yanayokamilishwa na wale ambao “hawachoki kutenda mema” (mstari wa 33).

Ona pia Saints, 1:133–34, 136–37.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mafundisho na Maagano 64:1–11

Ninahitajika kumsamehe kila mtu.

Unaposoma Mafundisho na Maagano 64:1–11, tafakari kuhusu wakati ambapo Bwana alikusamehe. Ungeweza pia kufikiria kuhusu mtu unayehitaji kumsamehe. Ni kwa jinsi gani huruma ya Mwokozi inaathiri hisia zako kuhusu wewe mwenyewe na kuhusu wengine? Kwa nini unadhani Bwana anatuamuru “kuwasamehe watu wote”? (mstari wa 10). Ikiwa unahangaika kusamehe, fikiria ni nini nyenzo zifuatazo zinafundisha kuhusu jinsi Mwokozi anavyoweza kusaidia: Jeffrey R. Holland, “Huduma ya Upatanisho,” Ensign au Liahona, Nov. 2018, 77–79; Mwongozo kwenye Maandiko, “Samehe,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org.

Mafundisho na Maagano 64:31–34

Mungu anahitaji moyo na akili yangu yenye kukubali.

Je, umewahi kuhisi “kuchoka” kwa “kutenda mema yote” unayojaribu kukamilisha? Tafuta ujumbe wa Bwana kwako katika Mafundisho na Maagano 64:31–34. Inamaanisha nini kutoa “moyo wako na akili yenye kukubali” kwa Mungu? (mstari wa 34).

Mafundisho na Maagano 64:41–43

Sayuni itakuwa “bendera kwa watu.”

Ensign ni “bendera au ishara ambayo kwayo watu hukusanyika katika umoja wa lengo au utambulisho” (Mwongozo kwenye Maandiko, “Ensign,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Ni jinsi gani Sayuni—au Kanisa la Bwana—limekuwa kama bendera kwako? Fikiria mifano hii mingine ya vitu vinavyoinuliwa juu, kama bendera, ili kubariki watu: Hesabu 21:6–9; Mathayo 5:14–16; Alma 46:11–20. Mistari hii inakufundisha nini kuhusu jinsi unavyoweza kulisaidia Kanisa kuwa bendera pale ulipo? Tafuta njia zingine Bwana anavyoielezea Sayuni katika Mafundisho na Maagano 64:41–43.

Picha
Kapteni Moroni

Kapteni Moroni na Bendera ya Uhuru, na Gary E. Smith

Mafundisho na Maagano 65

“Itengenezeni njia ya Bwana.”

Mathayo alimuelezea Yohana Mbatizaji kama mtu aliyetangaza, “Itengenezeni Njia ya Bwana” (Mathayo 3:3; ona pia Isaya 40:3). Katika Mafundisho na Maagano 65, Bwana anatumia lugha sawa na hiyo kuelezea kazi Yake ya siku za mwisho. Ni mfanano upi unauona kati ya kile Yohana Mbatizaji alichofanya (ona Mathayo 3:1–12) na kile Bwana anachotutaka tufanye leo? Ni kipi unachopata katika ufunuo huu ambacho kinakupa msukumo wa kusaidia kutimiza unabii uliomo ndani yake? Tafakari jinsi unavyoweza “kuwajulisha watu matendo ya [Mungu] ya ajabu” (mstari wa 4).

Mafundisho na Maagano 66

Bwana anajua mawazo ya moyo wangu.

Muda mfupi baada ya kujiunga na Kanisa, William E. McLellin alimuomba Joseph Smith kufunua mapenzi ya Mungu kwake. Joseph hakulijua hilo, lakini William alikuwa na maswali binafsi matano ambayo alitarajia Bwana angeyajibu kupitia Nabii Wake. Hatujui maswali ya William yalikuwa yapi, lakini tunajua kwamba ufunuo uliotolewa kwake, sasa Mafundisho na Maagano 66, ulijibu kila swali la William kwa “uridhikaji wote na ukamilifu” (“Maswali Matano ya William McLellin,” Ufunuo katika Muktadha, 138).

Unaposoma sehemu ya 66, fikiria kuhusu kile Bwana alichojua kuhusu William McLellin na wasiwasi pamoja na nia za moyo wake. Ni kwa jinsi gani Bwana amefunua kwamba Yeye anakujua wewe? Kama una baraka ya patriaki, fikiria kuisoma. Unapofanya hivyo, ni kipi Roho Mtakatifu anakusaidia kuelewa kuhusu mapenzi ya Mungu kwa ajili yako?

Ona pia Saints, 1:138–40; Mada za Injili, “Baraka za Baba Mkuu,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Mafundisho na Maagano 64:8–10.Mahusiano ya familia yanatoa fursa nyingi za kujifunza kusamehe. Pengine wanafamilia wangeweza kuzungumza kuhusu kusameheana kulivyobariki maisha ya familia yenu. Ni kwa jinsi gani Mwokozi alitusaidia kumsamehe kila mmoja? Ni kwa jinsi gani sisi “tunapata mateso” (mstari wa 8) wakati hatuwasamehi wengine?

Mafundisho na Maagano 64:33.Ni nini Baba wa Mbinguni anataka familia yako ifanye ili kutimiza “kazi Yake kubwa”? Pengine ni kwenda hekaluni, kushiriki injili na jirani, au kuepuka mabishano. Pengine kila mwanafamilia angeweza kukusanya vitu vidogo vidogo, kama mawe au vifungo au vipande vya fumbo, na kuvitumia kuwakilisha “mambo madogo” tunayoweza kufanya kila siku “[kuujenga] msingi” wa kazi kubwa ya Mungu. Kama familia, chagueni moja ya mambo haya madogo ili kuyafanyia kazi wiki hii.

Mafundisho na Maagano 66:3.Ni kwa jinsi gani unaweza kufundisha umuhimu wa kutubu? Ungeweza kuandaa chakula kwenye sahani ambayo si safi kabisa na soma maneno ya Bwana kwa William McLellin: “Wewe u safi, lakini siyo kabisa.” Kisha ungeweza kusafisha sahani na kushiriki chakula wakati mkijadili jinsi Yesu Kristo anavyofanya iwezekane kwetu kuwa wasafi kiroho.

Mafundisho na Maagano 66:10.Ni kwa jinsi gani familia yako inaweza kufuata ushauri wa Mwokozi wa “usitafute kujihangaisha,” au kuchoshwa na mambo mengi ya kufanya? Ungeweza kuzungumza kuhusu hadithi ya Mary na Martha (ona Luka 10:38–42), na kujadili jinsi familia yako inavyoweza kujiepusha kutokana na kuhangaishwa na mambo ambayo si yenye thamani ya milele.

Kwa mawazo mengine kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Help Me, Dear Father,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwa mwenye kupatikana na kufikika. Baadhi ya nyakati bora zaidi za kufundisha huanza kama maswali au wasiwasi katika mioyo ya wanafamilia. Wajulishe wanafamilia kupitia maneno na vitendo vyako kwamba una hamu ya kuwasikiliza. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 16.)

Picha
Mwanamke amepiga magoti kando ya Yesu

Kusamehewa, na Greg K. Olsen. Imetumika kwa ruhusa. www.GregOlsen.com

Chapisha