Mafundisho na Maagano 2021
Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114: “Nitayapanga Mambo Yote kwa Faida Yenu”


“Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114: ‘Nitayapanga Mambo Yote kwa Faida Yenu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha
Joseph Smith akihubiri

Oktoba 4–10

Mafundisho na Maagano 111–114

“Nitayapanga Mambo Yote kwa Faida Yenu”

Kwa sala omba kwa ajili ya mwongozo wa Roho unaposoma Mafundisho na Maagano 111–14, na andika misukumo yako. Kisha fikiria jinsi unavyoweza kutenda juu ya misukumo hiyo.

Andika Misukumo Yako

Je, umewahi wakati wowote kuwa na uzoefu wa kiroho ambao ulikufanya ujisikie kujiamini na salama katika imani yako—lakini kisha mateso ya maisha yakajaribu imani yako, na ukajikuta ukipata shida kuipata tena amani uliyoihisi kabla? Kitu fulani kama hicho kilitokea kwa Watakatifu huko Kirtland. Chini ya mwaka mmoja baada ya bubujiko za kiroho zilizohusishwa na kuwekwa wakfu kwa Hekalu la Kirtland, matatizo yalitokea. Hali ya hatari ya kifedha, kutoelewana ndani ya Akidi ya Wale Kumi na Wawili, na majaribu mengine yalisababisha baadhi kuyumba katika imani yao.

Hatuwezi kuepuka majaribu, kwa hiyo ni kwa jinsi gani tunaweza kuyazuia kutishia imani na ushuhuda wetu? Huenda sehemu ya jibu inaweza kupatikana katika ushauri wa Bwana katika Mafundisho na Maagano 112, uliotolewa wakati dhiki huko Kirtland ilizidi kuwa kubwa. Bwana alisema, “Itakaseni mioyo yenu mbele zangu” (mstari wa 28), “Msiasi” (mstari wa 15), “Funga viuno vyako kwa ajili ya kazi” (mstari wa 7), na “Jinyenyekeze” (mstari wa 10). Tunapofuata ushauri huu, Bwana “atatuongoza [sisi] kwa mkono” kupita dhiki na kwenda kweye uponyaji na amani (ona mistari ya 10, 13).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mafundisho na Maagano 111

Bwana anaweza “kupanga vitu vyote kwa ajili ya manufaa [yangu].”

Karibia mwaka wa 1836, Kanisa lilikuwa limelimbikiza madeni makubwa katika kufanya kazi ya Bwana. Wakati Joseph Smith na wengine walipokuwa na wasiwasi kuhusu madeni haya na kufikiria njia za kuyalipa, walisafiri kwenda Salem, Massachusetts, pengine kwa sababu kulikuwa na uvumi kwamba kiasi cha fedha kilikuwa kimeachwa katika nyumba huko (ona kichwa cha habari cha sehemu kwenye Mafundisho na Maagano 111). Baada ya kuwasili Salem, Bwana alitangaza, “Ziko hazina nyingi zaidi ya moja kwa ajili yenu katika mji huu” (mstari wa 10)—hazina ambazo ni pamoja na watu ambao Yeye “angewakusanya katika wakati wake kwa faida ya Sayuni” (mstari wa 2; ona pia Kutoka 19:5). Ingawa hakuna fedha iliyopatikana huko Salem, waongofu ambao walikuja kutokana na juhudi za baadaye za umisionari walikuwa sehemu ya utimilifu wa ahadi ya Bwana.

Unaposoma sehemu ya 111, fikiria kuhusu vitu ambavyo una wasiwasi navyo. Fikiria jinsi gani maneno ya Bwana kwa Joseph yanaweza kutumika kwako. Je, kwa jinsi gani Mungu amekusaidia kupata hazina “zisizotegemewa”? (mstari wa 10). Fikiria kuhusu kile Yeye alichokifanya “kupanga mambo yote kwa faida yako” (mstari wa 11). Kirai “haraka kadiri mtakavyoweza kuyapokea” kinakufundisha nini kuhusu Baba wa Mbinguni?

Ona pia Mathayo 6:19–21, 33; “Hazina Zaidi Kuliko Moja,” Ufunuo katika Muktadha, 229–34.

Mafundisho na Maagano 112:3–15

Bwana atawaongoza wale ambao kwa unyenyekevu hutafuta mapenzi Yake.

Umoja katika Akidi ya Wale Kumi na Wawili ulikuwa unadhoofika katika majira ya joto ya 1837. Kulikuwa na kutokukubaliana kuhusu majukumu, na baadhi ya waumini walikuwa wakizungumza dhidi ya Nabii Joseph Smith. Thomas B. Marsh, wakati huo Rais wa Akidi ya Wale Kumi na Wawili, alikuwa na mashaka, na alikuja kutoka Missouri mpaka Ohio, kutafuta ushauri kutoka kwa Nabii. Kaka Marsh aliupokea kupitia ufunuo katika sehemu ya 112. Ni kwa jinsi gani ushauri wa Bwana ungeweza kumsaidia yeye pamoja na akidi yake? Ni mafunzo gani inayo kwa ajili yako pale unapotafuta kushinda mabishano na hisia kali?

Hasa, unaweza kutafakari mstari wa 10. Inamaanisha nini kwa Bwana kukuongoza “kwa mkono”? Kwa nini unyenyekevu unatakiwa kwa ajili ya aina hii ya mwongozo?

Ona pia Ulisses Soares, “Be Meek and Lowly of Heart,” Ensign au Liahona, Nov. 2013, 9–11; “Imani na Anguko la Thomas Marsh,” Ufunuo katika Muktadha, 54–60.

Picha
watu wawili wakisali

Kama tu wanyenyekevu, Bwana atatuongoza na kujibu sala zetu.

Mafundisho na Maagano 113

Joseph Smith alikuwa “mtumishi katika mikono ya Kristo.”

Isaya alimtaja mmoja wa vizazi vya Yese kama “chipukizi” na “mzizi” (Isaya 11:1, 10). Katika sehemu ya 113, Bwana anaelezea kwamba mzao huyu, mtumishi wa Kristo, atakuwa chombo katika kukusanya watu wa Bwana katika siku za mwisho (ona Mafundisho na Maagano 113:4, 6)—Utabiri ambao unamuelezea Nabii Joseph Smith vizuri sana. Ni jinsi gani utabiri huu na kweli zingine katika sehemu ya 113 vimekuwa vikiwatia moyo Watakatifu wakati wa misukosuko waliyokuwa wanaipitia huko Kirtland? Unapata nini katika ufunuo huu ambacho kinakutia moyo kushiriki katika kazi ya Bwana leo?

Ona pia Mwongozo kwenye Maandiko, “Yese,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org; 2 Nefi 21:10–12; Joseph Smith—Historia ya 1:40.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Nyumbani

Mafundisho na Maagano 111:2, 9–12.Mistari hii ingeweza kushawishi majadiliano kuhusu nini familia yako inathamini kama “hazina” za milele. Ungeweza kutengeneza msako wa kutafuta hazina kwa kuficha vitu kuzunguka nyumba ambavyo vinawakilisha vitu Bwana anavyovithamini au kuvipa thamani. Wakati familia yako inapopata kila kimojawapo, jadilini kile mnachoweza kufanya kuonyesha kwamba mnakithamini.

Mafundisho na Maagano 112:10.Mzee Ulisses Soares alielezea watu wanyenyekevu kwa namna hii: “Wanyenyekevu hufundishika, wakitambua jinsi wanavyomtegemea Mungu na kutamani kuwa chini ya mapenzi Yake. Wanyenyekevu ni wapole na wana uwezo wa kuwashawishi wengine kuwa vivyo hivyo” (“Be Meek and Lowly of Heart,” Ensign au Liahona, nov. 2013, 10). Fikiria njia za kuisaidia familia yako kuelewa inamaanisha nini kuwa myenyekevu. Mngeweza kuimba wimbo kuhusu unyenyekevu, kama vile “Be Thou Humble” (Nyimbo za Kanisa, na.130), wakati mwanafamilia mmoja akiwashika wengine “kwa mkono” na kuwaongoza kuzunguka nyumba yenu. Au mshiriki uzoefu wenu wakati Bwana alipoongoza wanafamilia yako “kwa mkono” na kuwapa “majibu ya sala [zao].”

Mafundisho na Maagano 112:11–14, 26.Kuna tofauti gani kati ya kujua jina la mtu fulani na kuwajua? Tunajifunza nini kutoka mistari ya 11–14 kuhusu kile inachomaanisha kumjua Bwana?

Mafundisho na Maagano 112:15.Inamaanisha nini “kuasi” dhidi ya nabii? Tunapata nini katika mstari huu ambacho kinatusaidia kutaka kumuidhinisha nabii?

Mafundisho na Maagano 113:7–8.Tunajifunza nini kutoka mstari wa 8 ambacho kitasaidia “kurejesha tena Sayuni” na kukomboa Israeli?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Be thou Humble,” Nyimbo za Kanisa, na. 130.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ishi ushuhuda wako. “‘Unafundisha kile wewe ulicho,’ Mzee Neal A. Maxwell alifundisha. ‘Sifa zako zitakumbukwa zaidi … kuliko kweli fulani katika somo fulani’” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 13).

Picha
Thomas B. Marsh na Joseph Smith

Thomas B. Marsh anaandika ufunuo aliopewa kupitia Joseph Smith. Kuwa Mnyenyekevu, na Julie Rogers.

Chapisha