Mafundisho na Maagano 2021
Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu: “Familia ni ya Muhimu katika Mpango wa Muumba”


“Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu: ‘Familia ni ya Muhimu katika Mpango wa Muumba,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha

Desemba 13–19

Familia: Tangazo kwa Ulimwengu

“Familia ni ya Muhimu katika Mpango wa Muumba”

Rais Dallin H. Oaks alisema: “Ninaamini mtazamo wetu kuhusu na matumizi ya tangazo kwa familia ni [jaribio] kwa ajili ya kizazi hiki. Ninaomba kwa ajili ya Watakatifu wote wa Siku za Mwisho kusimama imara katika jaribio hilo” (“Mpango na Tangazo,” Ensign au Liahona, Nov. 2017, 31). Tafakari maneno haya unapojifunza tangazo la familia wiki hii.

Andika Misukumo Yako

Hata kabla hatujazaliwa, tulikuwa sehemu ya familia—familia ya Wazazi wetu wa Mbinguni. Wakati muda ulipofika wa kuondoka katika uwepo Wao, lazima ilikuwa ya kutia faraja kujua kwamba duniani, familia zitakuwa pia sehemu ya mpango wa Mungu. Mpangilio duniani umekusudiwa kuendeleza mpangilio mkamilifu mbinguni.

Hakuna hakikisho kwamba familia za duniani zitakuwa bora au hata za kufaa. Bali kama Rais Henry B. Eyring alivyofundisha, familia “zinawapa watoto wa Mungu nafasi nzuri zaidi kukaribishwa ulimwenguni na upendo wa pekee duniani ambao unakaribiana na kile tulichokihisi mbinguni—upendo wa mzazi” (“Kukusanya Familia ya Mungu,” Ensign au Liahona, Mei 2017, 20). Kujua kwamba familia sio kamilifu na zinakabiliwa na mashambulizi kutoka kwa adui, Mungu alimtuma Mwanaye Mpendwa kutukomboa na kuponya familia zetu. Na Aliwatuma manabii wa siku za mwisho na tangazo la kulinda na kuimarisha familia. Kama tutawafuata manabii na kuweka imani kwa Mwokozi, hata kama familia za kidunia hazifikii utukufu kamili, kuna mategemeo kwa ajili ya familia—duniani na mbinguni.

Picha

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Familia ni muhimu kwa mpango wa Muumba.”

Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” ni dhahiri kuhusu familia. Bali lina uwiano sawa na mpango wa wokovu wa Mungu. Njia mojawapo ya kujifunza tangazo ni kutafuta nini linafundisha kuhusu maisha yetu kabla ya kuja hapa duniani, maisha hapa duniani, na maisha baada ya hapa duniani. Unajifunza nini unaposoma tangazo kwa njia hii? Ni kwa jinsi gani hii inakusaidia kuelewa kwa nini ndoa na familia ni vya muhimu kwa mpango wa Mungu?

Ona pia Dallin H. Oaks, “Mpango na Tangazo,” Ensign au Liahona, Nov. 2017, 28–31.

“Furaha katika maisha ya familia itapatikana kwa urahisi ikiwa imejegwa katika mafundisho ya Bwana Yesu Kristo.

Fikiria aya ya sita na saba za tangazo la familia kama mpangilio kwa ajili ya “furaha katika maisha ya familia.” Unaposoma aya hizi, tambua kanuni za “ndoa na familia zenye mafanikio.” Kisha fikiri kuhusu uhusiano wa familia ambao ungependa kuuimarisha. Je, unajisikia kushawishiwa kufanya nini? Ni kwa jinsi gani utamhusisha Mwokozi katika juhudi zako?

Ona pia Richard J. Maynes, “Kuanzisha Nyumba Iliyolenga kwa Kristo,” Ensign au Liahona Mei 2011, 37–39); “What Matters Most,” video, ChurchofJesusChrist.org.

Mimi “nitawajibishwa mbele ya Mungu” kwa jinsi ninavyoitendea familia yangu.

Tangazo la familia linajumuisha baraka za ajabu ambazo Baba wa Mbinguni anaahidi kwa ajili ya hao wanaofuata ushauri Wake. Pia linajumuisha maonyo yenye nguvu kwa ajili ya hao wasiofuata. Fikiria kutengeneza orodha ya baraka na maonyo unayoyapata.

Je, ni kwa jinsi gani unatenda juu ya ushauri wa Mungu katika tangazo? Kama ungesimama mbele ya Mungu leo, ungejiamini kujadiliana nini na Yeye kuhusu mahusiano yako na familia? Ungehitaji kuboresha nini?

Ona pia Alma 5:15–22; Mafundisho na Maagano 42:22–25; 93:39–44.

Picha

Wazazi wanapaswa kuwalea watoto wao kwa upendo na uadilifu.

Je ninaweza kupokea baraka zilizoahidiwa kama hali ya familia yangu iko chini ya ubora?

Mzee D. Todd Christofferson alifundisha: “Kutangaza kweli za kimsingi zinazohusiana na ndoa na familia si kupuuza au kudhoofisha dhabihu na mafanikio ya wale ambao ndoa na familia si uhalisia kwa sasa. … Kila mmoja ana vipawa; kila mmoja ana talanta; kila mmoja anaweza kuchangia katika kufungua mpango wa kiungu katika kila kizazi. Mengi ambayo ni mazuri, mengi ambayo ni muhimu—hata wakati mwingine yote yaliyo ya lazima kwa sasa—yanaweza kupatikana chini ya kiwango cha hali maridhawa. … Kwa imani tunashuhudia kwamba Upatanisho wa Yesu Kristo umeshatangulia na, hatimaye, utafidia mafadhaiko na hasara kwa wale ambao wanamgeukia Yeye. Hakuna aliyepangiwa toka mwanzo kupokea kidogo kutoka kwenye chote Baba alichonacho kwa ajili ya watoto Wake.” (“Kwa nini ndoa, Kwa nini familia,” Ensign au Liahona, Mei 2015, 52).

Picha

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Nyumbani

“Jinsia ni hulka muhimu ya utambuzi wa milele wa maisha kabla ya maisha ya duniani, na maisha ya duniani ya mtu na utambulisho na dhamira.”Kama itakuwa yenye msaada kwa ajili ya familia yako kujadiliana mafundisho yanayohusiana na jinsia na mvuto wa jinsia moja, nyenzo zifuatazo zinaweza kusaidia: Dallin H. Oaks, “Ukweli na Mpango,” Ensign au Liahona, Nov. 2018, 25–28; Mada za Injili, “Mvuto wa jinsia moja,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

“Mpango mtukufu wa furaha.”Ili kuisaidia familia yako ione umuhimu wa familia katika mpango wa Baba wa Mbinguni, unaweza kuandika maisha kabla ya maisha ya duniani, maisha ya duniani, na maisha baada ya kifo kwenye sehemu tatu za kipande cha karatasi. Chunguzeni tangazo pamoja, na andikeni kwenye karatasi kile mnachojifunza kuhusu kila moja ya sehemu hizi za mpango wa Mungu. Kwa nini familia ni muhimu mno kwa Mungu?

“Familia [zinaweza] kuungana milele.” Ungeweza kuangalia video “Plan of Salvation—We’re Still a Family” (ChurchofJesusChrist.org). Chunguza tangazo la familia kwa ajili ya kweli ambazo kijana katika video alizielewa na zilizomsaidia kuwa na imani.

“Furaha ndani ya maisha ya familia.”Ili kujadiliana jinsi ya kufanikisha “furaha” zaidi katika maisha ya familia [yako],” mngeweza kuimba pamoja wimbo kuhusu familia, kama vile “Home Can Be a Heaven on Earth” (Nyimbo za kanisa, na. 298). Tunajifunza nini kutokana na wimbo na kutoka tangazo la familia ambacho kitaleta furaha zaidi kwenye familia yetu? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuhakikisha familia yetu “imejengwa juu ya mafundisho ya Bwana Yesu Kristo”? Fikiria kuchagua fundisho moja unalotaka kulifanyia kazi wiki hii.

“Imarisha familia kama kitengo cha msingi wa jamii.”Ni kwa jinsi gani shetani anajaribu kudhoofisha familia ulimwenguni? Ni kwa jinsi gani tunaweza kufanya sehemu yetu kuimarisha familia? Kwa mawazo, ona ujumbe wa Dada Bonnie L. Oscarson “Watetezi wa Tangazo la Familia,” (Ensign au Liahona, Mei 2015, 14–17).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Home Can Be a Heaven on Earth,” Nyimbo za Kanisa, na. 298.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta upendo wa Mungu. Rais M.Russell Ballard alifundisha, “Hii injili ni injili ya upendo—upendo kwa Mungu na upendo kwetu sisi kwa sisi” (“Upendo wa Mungu kwa Watoto Wake,” Ensign, Mei 1988, 59). Unaposoma tangazo la familia, fikiria kuandika au kuwekea alama uthibitisho wa upendo wa Mungu ambao hasa ni wenye maana kwako.

Chapisha