Njoo, Unifuate
Machi 25–31. Mathayo 14–15; Marko 6–7; Yohana 5–6: ‘Msiogope’


“Machi 25–31. Mathayo 14–15; Marko 6–7; Yohana 5–6: ‘Msiogope’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Machi 25–31. Mathayo 14–15; Marko 6–7; Yohana 5–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Kristo akiwalisha makutano

Wapeni chakula, na Jorge Cocco

Machi 25–31.

Mathayo 14–15; Marko 6–7; Yohana 5–6

“Msiogope”

Unaposoma Mathayo 14–15; Marko 6–7; na Yohana 5–6, tafuta kweli ambazo zina maana kwako. Unaweza kujiuliza maswali kama vile “Je, ni kwa jinsi gani matukio katika sura hizi yananihusu” “Je, ni ujumbe gani ninapata kwa ajili ya maisha yangu?” au “Je, ni kitu gani ningependa kushiriki na familia yangu au na wengine?

Andika Misukumo Yako

Je, ni kitu gani kiliweza kumshawishi Petro atoke kwenye usalama wa mashua yake katikati ya Bahari ya Galilaya wakati wa dhoruba kali? Je, ni kitu gani kilimfanya aamini kwamba kama Yesu aliweza kutembea juu ya maji, naye angeweza pia? Hatuwezi kujua kwa hakika, lakini pengine Petro alielewa kwamba Mwana wa Mungu alikuja sio tu kufanya mambo ya ajabu kwa watu lakini kuwawezesha watu kama Petro kufanya mambo ya ajabu pia. Mwaliko wa Yesu, hata hivyo, ulikuwa “Njoo, unifuate” (Luka 18:22). Petro alikuwa amekubali mwaliko huu mara moja, na alikuwa tayari kuukubali tena, hata kama ilimaanisha kukabiliana na woga wake na kufanya jambo ambalo lilionekana kutowezekana. Pengine Bwana hatatuambia kutoka nje ya mashua katikati ya dhoruba au kuchangia akiba yetu ndogo ya mkate wakati maelfu wanapohitaji kula, lakini anaweza kututaka kukubali miongozo hata wakati hatuielewi kikamilifu. Vyovyote mialiko Yake kwetu itakavyokuwa, wakati mwingine itaonekana ya kushangaza au hata ya kuogopesha. Lakini miujiza inaweza kutokea ikiwa sisi, kama Petro, tutaweka kando woga wetu, shaka yetu, na kikomo cha uelewa wetu na kumfuata Yeye katika imani.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Yohana 5:17–47

Yesu Kristo akimtukuza Baba Yake.

Uhusiano kati ya Baba wa Mbinguni na kila mmoja wa watoto Wake unapaswa kuwa mtakatifu. Katika mistari hii, Yesu Kristo alitupatia mfano wa kuvutia wa kufuata katika uhusiano wetu na Baba wa Mbinguni. Soma Yohana 5:17–47, na uwekee alama au kuandika kila linapotamkwa neno Baba. Je, ni jinsi gani Mwana humtukuza Baba, na jinsi gani unaweza kufuata mfano Wake? Je, ni kitu gani unajifunza kuhusu jinsi Baba anavyojisikia juu ya Mwana? Ni kwa jinsi gani kuimarisha uhusiano na Baba wa Mbinguni kunaongeza utayari wako kutafuta na kutii mapenzi Yake?

Ona pia Yohana 17; Jeffrey R. Holland, “Ukuu wa Mungu,” Ensign au Liahona, Nov. 2003, 70–73.

Mathayo 14:16–21; Marko 6:33–44; Yohana 6:5–14

Mwokozi anaweza kukuza matoleo yangu haya madogo ili kufikia malengo Yake.

Je, umewahi kujisikia usiyefaa kutimiza mahitaji yote unayoona yanakuzunguka—nyumbani kwako, katika mahusiano yako, au katika jamii? Wanafunzi wa Yesu lazima walijisikia wasiofaa alipowataka kuwalisha watu elfu tano wenye njaa (ona Mathayo 14:21) wakati ilipokuwepo mikate mitano na samaki wawili tu. Unaposoma kuhusu muujiza uliofuata, tafakari jinsi gani Mungu anaweza kutumia matoleo yako madogo ya huduma kuwabariki wale wanaokuzunguka. Je, ni kwa jinsi gani Yeye anaweza kukuza jitihada zako wakati unapotumikia Kanisani? Fikiria kauli hii kutoka kwa Rais James E. Faust: “Watu wengi wasioweza kujilikana kwa majina wenye vipawa sawa tu na mikate mitano na samaki wadogo wawili hukuza miito yao na kutumikia bila kuonekana au kutambuliwa, wakiwalisha maelfu” (“Mikate Mitano na Samaki Wawili,” Ensign, Mei 1994, 5).

Mathayo 14:22–33; Marko 6:45–52; Yohana 6:15–21

Yesu Kristo ananialika kuweka kando woga na shaka yangu na kuonyesha imani yangu Kwake.

Weka taswira akilini mwako utondoti wa tukio lililoelezwa katika Mathayo 14:22–33; Marko 6:45–52; na Yohana 6:15–21. Fikiria jinsi gani Petro na wale wanafunzi wengine walivyojisikia. Je, unajifunza nini kuhusu ufuasi kutokana na maneno na matendo ya Mwokozi katika mistari hii? Je, unajifunza nini kutokana na maneno na matendo ya Petro? (Ona pia 1 Nefi 3:7.) Je, Bwana anakualika kufanya nini ambacho kinaweza kuwa sawa na kushuka chomboni? Je, unapata nini katika mistari hii ambacho kinakupa ujasiri wa kuonyesha imani yako kwa Yesu Kristo?

Yohana 6:22–71

Kama mfuasi wa Yesu Kristo, ninapaswa kuwa radhi kuamini na kukubali ukweli, hata kama ni vigumu kufanya hivyo.

Siku moja baada ya Yesu kimiujiza kutoa mkate kwa makutano huko nyikani, wafuasi Wake walimtafuta na kutaka chakula zaidi. Hata hivyo, walikatishwa tamaa na hata kukwazika Yeye badala yake aliwapa lishe ya kiroho—mkate wa uzima” (Yohana 6:48). Wengi waliona hili kama “neno gumu” (Yohana 6:60).

Je, imewahi kukutokea kwamba jambo ambalo Mwokozi au mmoja wa watumishi Wake alifundisha lilionekana kuwa “gumu” au mafundisho magumu kuyakubali? Fikiria matukio hayo wakati unaposoma tukio hili, hasa maneno ya Petro katika mstari 68–69. Je, baadhi ya “maneno ya uzima wa milele” ni yapi (John 6:68) ambayo hukusaidia kubaki kwenye ahadi uliyojiwekea ya kumfuata Mwokozi?

Ona pia M. Russell Ballard, “Twende kwa Nani?” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 90–92.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Mathayo 14:16–21

Unaposoma kuhusu kulishwa kwa watu elfu tano, unaweza kula mkate na samaki na kupata taswira ya kiasi gani ingechukua kulisha watu elfu tano. Je, ni kwa jinsi gani familia yako imelishwa kiroho na Kristo? Je, ni kwa jinsi gani amekutumia wewe kuwalisha wengine?

Picha
mikate na samaki

Yesu kimiujiza aliwalisha watu 5,000 kwa mikate mitano na samaki wawili.

Mathayo 14:22–33

Familia yako inaweza kufurahia kuigiza tena hadithi iliyo katika mistari hii. Je, kwa nini wanafunzi walikuwa wameogopa? Je, kwa nini Petro aliweza kushinda woga wake na kukiacha chombo? Je, ni kwa jinsi gani alionyesha imani hata wakati alipoanza kuzama? Je, ni kwa jinsi gani sisi wakati mwingine tuko kama Petro?

Yohana 5:1–16

Waalike wanafamilia kuandika mifano ya kirai “imekuponya” katika mistari hii. Ni katika njia zipi Yesu Kristo huwaponya watu? Lini na jinsi gani Yeye ametuponya sisi?

Yohana 6:28–58

Mpe kila mwana familia kipande cha mkate ale, na kujadili faida tunayopata kutoka kwenye mkate na vyakula vingine vyenye kutupa afya. Kisha pekueni mistari hii pamoja, mkitafuta kwa nini Yesu Kristo alijiita “mkate wa uzima” (Yohana 6:35).

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Tafuta umaizi wako mwenyewe wa kiroho. Katika kujifunza kwako binafsi na familia, usijiwekee mpaka kwenye vifungu vya maandiko yaliyoonyeshwa katika miuhtasari hii. Bwana yaelekea ana ujumbe kwa ajili yako katika sura hizo ambazo hazijaelezewa hapa. Kwa maombi zitafute.

Picha
Yesu akimwinua Petro kutoka majini.

Dhidi ya upepo, na Liz Lemon Swindle

Chapisha