Njoo, Unifuate
Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7: ‘Alikuwa Akiwafundisha kama Mtu Mwenye Amri’


“Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7: ‘Alikuwa Akiwafundisha kama Mtu Mwenye Amri’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu Akifundisha kando ya ufukwe wa bahari

Yesu Anafundisha Watu kando ya Ufukwe wa Bahari, na James Tissot

Februari 25–Machi 3

Mathayo 6–7

“Alikuwa Akiwafundisha kama Mtu Mwenye Amri”

Tunaposoma maandiko tukiwa na swali akilini na nia ya dhati kuelewa kile ambacho Baba wa Mbinguni anatutaka tujue, tunamualika Roho Mtakatifu ili atupe mwongozo. Unaposoma Mathayo 6–7, zingatia misukumo hii.

Andika Misukumo Yako

Mahubiri ya Mlimani ni mojawapo ya mahubiri yanayojulikana-vizuri zaidi katika Ukristo. Mwokozi alifundisha kwa mifano mingi, kama vile mji juu ya mlima, maua ya mashamba, na mbwa mwitu waliojigeuza kondoo. Lakini Mahubiri ya Mlimani ni zaidi ya hotuba nzuri. Nguvu ya mafundisho ya Mwokozi kwa wafuasi Wake inaweza kubadilisha maisha yetu, hasa kama tunaishi kulingana na mafundisho hayo. Ndipo maneno Yake huwa zaidi ya maneno; yanakuwa msingi wa uhakika kwa maisha ambao, kama nyumba ya mtu mwenye busara, inaweza kuhimili pepo na mafuriko ya ulimwengu (ona Mathayo 7:24–25).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Mathayo 6–7

Napaswa kuweka moyo wangu katika mambo ya mbinguni.

Siyo rahisi kila mara kuyapa kipaumbele mambo ya Mungu kuliko mambo ya ulimwengu. Ni yapi kati ya mafundisho ya Mwokozi katika Mathayo 6–7 hukusaidia kuzingatia kwenye mambo ya mbinguni? Je, ni fikra au mawazo gani unakuwa nayo unapojifunza maneno Yake? Je, unashawishika kufanya nini? Fikiria kuandika misukumo yako. Kwa mfano:

Mathayo 6:1–4

Napaswa kujali zaidi kuhusu kile ambacho Mungu anafikiri juu yangu mimi kuliko kile ambacho wengine hunifikiria.

Mathayo 6–7

Ninaweza kusogea karibu na Mungu kupitia maombi ya dhati, ya unyenyekevu.

Mahuburi ya Mlimani yana dhamira nyingi, na dhamira unazopata zitategemea, kwa kiasi gani, na hali ya sasa ya maisha yako na kile Bwana anachotaka kuwasiliana nawe.

Dhamira moja ya Mathayo 6–7 ni maombi. Pata muda wa kutathmini maombi yako. Je, wewe unajisikia unafanya vipi katika jitihada zako za kumkaribia Mungu kupitia maombi? Je, ni mafundisho gani katika Mathayo 6–7 yanakupa mwongozo wa juu ya kuboresha jinsi unavyoomba? Andika misukumo unayopokea kupitia Roho. Kwa mfano:

Mathayo 6:9

Ninaposali, ninapaswa kulichukulia jina la Baba wa Mbinguni kwa heshima.

Mathayo 6:10

Wakati ninaposali, ninapaswa kuelezea haja yangu kwamba mapenzi ya Bwana yatimizwe.

Unaweza kufikiria kusoma Mahubiri ya Mlimani kwa mara nyingine, mara hii ukitafuta dhamira nyingine inayojirudia au ujumbe ambao hasa una matumizi kwako. Andika kumbukumbu ya kile unachopata, pamoja na fikra na maono yako katika shajara ya kujifunza.

Picha
familia kisali

Tunaweza kusogea karibu zaidi na Mungu kupitia sala.

Mathayo 6:7

Je, inamaanisha nini “kupayuka-payuka” katika maombi?

Watu mara nyingi huelewa kuwa “kupayuka- payuka” kunamaanisha kurudia maneno yale yale tena na tena. Hata hivyo, neno payuka huweza kuelezea kitu ambacho hakina thamani. “Kupayuka-payuka” katika sala huweza kumaanisha kuomba bila hisia za dhati, za moyoni (ona Alma 31:12–23).

Mathayo 6:9–13

Je, ni kwa nini hatukariri Sala ya Bwana?

Rais Russel M. Nelson alifundisha: “Bwana alitoa utangulizi wa sala Yake kwanza kwa kuwaomba wafuasi Wake kuepuka ‘kupayuka-payuka’ [Mathayo 6:7] na kwa kusali ‘salini hivi’ [Mathayo 6:9]. Hivyo, Sala ya Bwana hutumika kama mpangilio wa kufuatwa na siyo kama kipande cha kukariri na kurudia rudia. Bwana anatutaka tu tusali kwa ajili ya kuomba msaada wa Mungu wakati tukijitahidi daima kuepuka uovu na kuishi kwa haki” (“Mafundisho kutoka kwenye Sala ya Bwana,” Ensign au Liahona, Mei 2009, 46–47).

Mathayo 7:1–5

Napaswa kuhukumu kwa haki.

Katika Mathayo 7:1, Mwokozi anaweza kuonekana kana kwamba anasema tusihukumu, lakini katika maandiko mengine (ikijumuisha mistari ingine katika sura hii), Anatupatia maelekezo kuhusu jinsi ya kuhukumu. Kama hiyo inaonekana ni fumbo, Tafsiri ya Joseph Smith ya mstari huu unaweza kusaidia: “Msihukumu bila haki, msije mkahukumiwa; lakini hukumuni hukumu ya haki” (katika Mathayo 7:1, tanbihi a). Je, unapata nini katika Mathayo 7:1–5, pamoja na sura yote inayobakia, ambacho kinakusaidia kujua jinsi ya “kuhukumu hukumu ya haki”?

Ona pia “Judging Others,” Kweli kwa Imani, 90–91; Lynn G. Robbins, “Mwamuzi wa Haki,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 96–98.

Mathayo 7:21–23

Napata kumjua Yesu Kristo kwa kufanya mapenzi Yake.

Kirai “sikuwajua ninyi kamwe” Mathayo 7:23 kilibadilishwa katika Tafsiri ya Joseph Smith kuwa “Hamkunijua mimi kamwe” (Mathayo 7:23, tanbihi a). Je, ni kwa jinsi gani badiliko hili hukusaidia kuelewa vizuri zaidi kile ambacho Bwana alifundisha katika mstari 21–22 kuhusu kufanya mapenzi Yake? Je, unadhani unamjua Bwana vizuri kiasi gani? Je, unaweza kufanya nini ili kumjua vizuri zaidi?

Ona pia David A. Bednar, “Kama Mngalinijua,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 102–5.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia.

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unapojifunza Mahubiri ya Mlimani na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Mathayo 6–7

Njia mojawapo ya kujifunza kutoka katika Mathayo 6–7 kama familia ni kuangalia video “Mahubiri ya Mlimani: Sala ya Bwana” na “Mahubiri ya Mlimani: Hazina za Mbinguni” (LDS.org). Wanafamilia wanaweza kufuatilia kwenye maandiko yao na kusimamisha kwa muda video wanaposikia jambo wanalotaka kujadili. Shughuli hii inaweza kudumu kwa siku kadhaa, kama itahitajika.

Mathayo 6:5–13

Je, tunaweza kujifunza nini kuhusu sala kutokana na jinsi Mwokozi alivyosali? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kutumia sala Yake kama mfano wa kuiga ili kuboresha sala zetu binafsi na za familia? (Ona pia Luka 11:1–13.) Kama una watoto wadogo, mnaweza kufanya mazoezi ya kusali pamoja.

Mathayo 6:33

Inamaanisha nini “kutafuta … kwanza ufalme wa Mungu”? Je, ni kwa jinsi gani tunafanya hili kama familia?

Mathayo 7:1–5

Unaweza kutumia kipande kidogo cha ubao na kipande kikubwa cha ubao ili kuwakilisha kibanzi na boriti unapojadili mafundisho ya Mwokozi kuhusu kuhukumu wengine. Fikiria kusoma ingizo “Kuwahukumu Wengine” katika Kweli kwa Imani, 90–91, kama sehemu ya majadiliano haya.

Mathayo 7:24–27

Ili kusaidia familia yako kuelewa vizuri zaidi fumbo la Mwokozi wa mtu mwenye busara na mtu mpumbavu, unaweza kuwafanya wamwage maji kwenye mchanga na kisha juu ya mwamba. Je, tunawezaje kujenga misingi yetu ya kiroho juu ya mwamba?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Shiriki umaizi. Kujadiliana kanuni unazojifunza kutoka katika mafunzo yako binafsi sio tu njia nzuri ya kuwafundisha wengine; husaidia pia kuimarisha uelewa wako wewe mwenyewe. Jaribu kuelezea kanuni uliyojifunza kutokana na usomaji wa wiki hii na mwanafamilia au katika madarasa yako ya Kanisani.

Picha
Yesu akisali

Nimesali kwa Ajili Yenu, na Del Parson

Chapisha