Agano Jipya 2023
Juni 5–11. Yohana 14–17: “Kaeni katika Pendo Langu”


“Juni 5–11. Yohana 14–17: ‘Kaeni katika Pendo Langu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2023)

“Juni 5–11. Yohana 14–17,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Karamu ya Mwisho

Karamu ya Mwisho, na William Henry Margetson

Juni 5–11

Yohana 14–17

“Kaeni Katika Pendo Langu”

Unaposoma mafundisho ya Mwokozi katika Yohana 14–17, Roho Mtakatifu atakusaidia kutambua ujumbe ambao ni kwa ajili yako. Andika misukumo unayopokea.

Andika Misukumo Yako

Leo tunaiita “Karamu ya Mwisho,” lakini hatujui kama wanafunzi wa Yesu walitambua kikamilifu, wakati walipokusanyika kwa ajili ya sherehe ya mwaka ya Pasaka, kwamba hiki kingekuwa chakula chao cha mwisho na Bwana wao kabla ya kifo Chake. Yesu, hata hivyo, “alijua kwamba saa yake imefika” (Yohana 13:1). Alikuwa karibu kukabiliana na mateso ya Gethsemane, kusalitiwa na kukataliwa na rafiki Zake wa karibu, na kifo cha maumivu msalabani. Bado pamoja na vitisho vyote hivi mbele Yake, fokasi ya Yesu haikuwa Kwake bali kwa wanafunzi Wake. Ni nini walihitajika kujua katika siku na miaka iliyoko mbele? Mafundisho ya ukarimu ya Yesu katika Yohana 14–17 yanafunua jinsi Yeye anavyohisi kuhusu wanafunzi Wake, wakati huo na sasa. Miongoni mwa kweli nyingi za kufariji Yeye alizoshiriki ilikuwa ni hakikisho kwamba, katika maana moja, Yeye kamwe hatatuacha sisi. “Mkizishika amri zangu,” Yeye aliahidi, “mtakaa katika pendo langu” (Yohana 15:10).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Yohana 14–15

Ninaonyesha upendo wangu kwa Yesu kwa kushika amri Zake.

Unaposoma Yohana 14–15, unaweza kuandika au kuwekea alama kila matumizi ya neno upendo. Unaweza kuona neno amri likirudiwa mara nyingi katika muingiliano na neno upendo katika sura hizi. Je, unajifunza nini kuhusu uhusiano kati ya upendo na amri kutoka kwenye mafundisho ya Mwokozi? Je, ni maneno gani na virai gani vingine unaona vinahusiana na neno upendo katika sura hizi?

Tafakari jinsi upendo wa Mwokozi ulivyokushawishi wewe.

Ona pia Yohana 13:34–35; D. Todd Christofferson, “Kaeni katika Pendo Langu,” Liahona, Nov. 2016, 48–51.

Picha
Yesu akizungumza na wanafunzi

Karamu ya Mwisho, na Carl Heinrich Bloch

Yohana 14–16

Roho Mtakatifu hunisaidia kutimiza lengo langu kama mfuasi wa Yesu Kristo.

Lazima ilikuwa inavunja moyo kwa wanafunzi kusikia kwamba muda wao na Mwokozi ulikuwa unakaribia kwisha. Pengine wangekuwa na wasiwasi kuhusu jinsi ambavyo wangeendelea bila Yeye. Unaposoma Yohana 14–16, tafuta kile ambacho Mwokozi alisema ili kuwatuliza. Hasa, tambua kile Yeye alichowafundisha wao kuhusu Roho Mtakatifu. Je, wewe unajifunza nini kuhusu Roho Mtakatifu kutoka katika maneno ya Mwokozi kwenye mistari ifuatayo?

Je, ni kwa nini wanafunzi walihitaji aina hii ya msaada kutoka kwa Roho Mtakatifu? Je, ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu ametimiza kazi hizi kwako? Fikiria kile unachoweza kufanya ili kwamba ushawishi Wake uwe na nguvu zaidi katika maisha yako.

Ona pia 3 Nefi 19:9; 27:20; Mafundisho na Maagano 11:12–14; Musa 6:61; Michelle D. Craig, “Uwezo wa Kiroho,” Liahona, Nov. 2019, 19–21.

Yohana 15:1–8

Ninapokaa ndani ya Kristo, Nitazaa matunda mazuri.

Unafikiri inamaanisha nini “kukaa ndani ya [Kristo]”? (Yohana 15:4). Je, ni “tunda” lako lipi huonyesha kwamba umeunganishwa kwenye mzabibu ambao humwakilisha Yesu Kristo?

Yohana 17

Yesu Kristo anaomba kwa ajili ya wanafunzi Wake.

Maneno ya Yesu yaliyoandikwa katika Yohana 17 yanajulikana kama Sala ya Maombezi. Katika sala hii, Yesu aliomba kwa ajili ya Mitume Wake na “wale watakaomuamini [Yeye] kwa sababu ya neno lao” (Yohana 17:20). Hiyo humaanisha Alikuwa akiomba kwa ajili yako. Je, Yesu aliomba nini kutoka kwa Baba Yake kwa niaba yako na waaminio wengine wote? Hii inakufundisha nini kuhusu hisia Zake kwako wewe?

Sala hii pia hufundisha kweli muhimu, za milele. Je, ni kweli zipi unazipata? Unaposoma sura hii, fikiria kuandika kile unachojifunza kuhusu yafuatayo:

  • Sala

  • Uhusiano wa Mwokozi na Baba Yake

  • Uhusiano wa Mwokozi na wanafunzi Wake

  • Jinsi gani wanafunzi Wake wanapaswa kuwa tofauti na watu wa ulimwengu

  • Kweli zingine ambazo zimejotokeza sana kwako

Yohana 17:11, 21–23

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wameungana kikamilifu.

Katika sala Yake katika Yohana 17, Yesu alisisitiza umoja Wake na Baba. Ni kwa njia zipi Baba na Mwana ni “wamoja”? (Yohana 17:11, 21–23). Tambua kwamba Mwokozi aliomba kwamba wanafunzi Wake waweze kuwa wamoja “kama vile”—au katika njia hiyo hiyo ambayo—Yeye na Baba Yake ni wamoja (Yohana 17:22). Hiyo inamaanisha nini kwako? Fikiria kuhusu uhusiano wako—kwa mfano, na mwenzi wako au wanafamilia wengine, washiriki wa kata, na Wakristo wenzako. Ni kwa jinsi gani unaweza kufanyia kazi aina ya umoja ambao Yesu anao kwa Baba?

Ona pia Quentin L. Cook, “Mioyo Iliyounganishwa kwa Haki na Umoja,” Liahona, Nov. 2020, 18–22; Sharon Eubank, “Kwa Umoja wa Kihisia Tunapata Nguvu Pamoja na Mungu,” Liahona, Nov. 2020, 55–57.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Yohana 14:5–6.Wanafamilia wanaweza kufurahia kupeana zamu ya kuongoza familia kutembea kwenye njia. Ni kwa jinsi gani Yesu ni “njia”? Yeye anatuongoza kwenda wapi?

Yohana 14:26–27.Je, ni kwa jinsi gani amani ya Yesu inatofautiana na ile “itolewayo na ulimwengu”? Wanafamilia wangeweza kushiriki njia walizopata amani na faraja kupitia Roho Mtakatifu.

Yohana 15:1–8.Ingeweza kufurahisha kusoma mistari hii nje karibu na mzabibu, mti, au mmea mwingine. Ni nini kinachotokea wakati tawi linapokatwa kutoka kwenye mmea? Mngeweza kuzungumza kuhusu jinsi ambavyo sisi ni kama matawi na inamaanisha nini “kukaa” ndani ya Mwokozi na “kuzaa matunda.”

Mathayo 15:17–27; 16:1–7.Je, ni kwa nini unafikiri Yesu Kristo aliwaonya wanafunzi Wake juu ya mateso? Je, ni kwa jinsi gani wafuasi wa Kristo wanateswa leo? Je, ni kwa jinsi gani ushauri wa Mwokozi katika mistari hii hutusaidia wakati tunapopata mateso?

Yohana 16:33.Je, ni kwa jinsi gani Yesu Kristo ameushinda ulimwengu? Je, ni namna gani Upatanisho Wake hutuletea sisi amani na furaha? (ona pia Mafundisho na Maagano 68:6).

Yohana 17:21–23.Ni kipi kingeisaidia familia kujifunza kuwa wenye kuungana zaidi kama Yesu Kristo na Baba wa Mbinguni? Pengine ungeweza kuzungumza kuhusu timu yako pendwa na jinsi inavyofanya kazi kwa lengo moja. Au mngeweza kusikiliza kwaya au okestra na kujadili jinsi wanamuziki wanavyoungana pamoja kutengeneza muziki mtamu.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa “The Holy Ghost,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 105.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia rekodi za kusikiliza. Unapoifundisha familia yako maandiko, fikiria kusikiliza kutoka katika toleo la kusikiliza la maandiko, linalopatikana kwenye ChurchofJesusChrist.org au Gospel Library app. Kusikiliza kutoka Yohana 14–17 kunaweza kuwa hasa na nguvu kwa sababu sura hizi zina maneno mengi ya Mwokozi.

Picha
zabibu kwenye mzabibu.

Yesu alifundisha, “Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi” (Yohana 15:5).

Chapisha