Agano Jipya 2023
Julai 3–9. Matendo ya Mitume 1–5: “Nanyi Mtakuwa Mashahidi Wangu”


“Julai 3–9. Matendo ya Mitume 1–5: ‘Nanyi Mtakuwa Mashahidi Wangu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Julai 3–9. Matendo ya Mitume 1–5,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
umati wa watu kwenye kingo za mto na wakibatizwa mtoni

Siku ya Pentekoste, na Sidney King

Julai 3–9

Matendo ya Mitume 1–5

“Nanyi Mtakuwa Mashahidi Wangu”

Unapojifunza Matendo ya Mitume 1–5, Roho Mtakatifu anaweza kukupa mwongozo ili uzipate kweli ambazo zinahusika kwa ajili ya maisha yako. Tambua mistari inayokuvutia, na tafuta fursa za kushiriki kile unachojifunza.

Andika Misukumo Yako

Je, umewahi kujiuliza Petro alikuwa akifikiria na kuhisi nini wakati yeye, pamoja na Mitume wengine, “walipokaza macho mbinguni” wakati Yesu akipaa kwenda kwa Baba Yake? (Matendo ya Mitume 1:10). Kanisa ambalo lilianzishwa na Mwana wa Mungu sasa lilikuwa kwenye mikono ya Petro. Jukumu la kuongoza juhudi za “kufundisha mataifa yote” sasa lilikuwa juu yake (Mathayo 28:19). Lakini kama alijiona kutokustahili au kuogopa, hatupati ushahidi wowote wa hilo katika kitabu cha Matendo ya Mitume. Kile tunachokiona ni mifano ya shuhuda za ujasiri na uongofu, miujiza ya uponyaji, maonyesho ya kiroho, na ukuaji mkubwa wa Kanisa. Hili lilikuwa bado ni Kanisa la Mwokozi, bado likiongozwa Naye. Hakika, kitabu cha Matendo ya Mitume kingeweza kuitwa Matendo ya Mitume ya Yesu Kristo kupitia Mitume Wake. Akiongozwa na mbubujiko wa Roho, Petro hakuwa tena yule mvuvi asiye na elimu Yesu aliyemkuta katika fuko za Bahari ya Galilaya. Wala hakuwa mtu aliyefadhaika ambaye wiki kadhaa kabla alikuwa akilia kwa uchungu kwa sababu alikana kwamba hakumjua Yesu wa Nazareti.

Katika kitabu cha Matendo ya Mitume, utasoma matamko yenye nguvu kuhusu Yesu Kristo na injili Yake. Utaona pia ni kwa jinsi gani injili hiyo inaweza kuwabadilisha watu—ikijumuisha wewe—kuwa wafuasi mashujaa ambao Mungu anajua wanaweza kuwa.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Matendo ya Mitume 1:1–8, 15–26; 2:1–42; 4:1–13, 31–33

Yesu Kristo analiongoza Kanisa Lake kupitia Roho Mtakatifu.

Kitabu cha Matendo ya Mitume huelezea jitihada za Mitume kulijenga Kanisa la Yesu Kristo baada ya Kupaa kwa Mwokozi. Japokuwa Yesu Kristo hakuwepo tena duniani, Aliliongoza Kanisa kwa ufunuo kupitia Roho Mtakatifu. Fikiria jinsi Roho Mtakatifu alivyowaongoza viongozi wapya wa Kanisa la Kristo unaporejelea vifungu vifuatavyo: Matendo ya Mitume 1:1–8, 15–26; 2:1–42; 4:1–13, 31–33.

Kama waumini wa Kanisa la Kristo leo, kila mmoja wetu analo jukumu la kushiriki katika kazi ya wokovu na kuinuliwa—ili kuishi injili ya Yesu Kristo, kuwatunza wale walio na shida, kuwaalika wengine kuja kwa Kristo, na kuunganisha familia kwa ajili ya milele (ona Kitabu cha Maelezo ya Jumla1.2). Je, unajifunza nini kutoka kwa Mitume hawa wa mwanzo kuhusu jinsi unavyoweza kumtegemea Roho Mtakatifu kuongoza juhudi zako?

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Roho Mtakatifu.”

Matendo ya Mitume 2:36–47; 3:12–21

Kanuni na ibada za injili hunisaidia kuja kwa Kristo.

Je, umewahi kuhisi “kuchomwa moyoni [mwako],” kama wale Wayahudi katika siku ya Pentekoste? (Matendo ya Mitume 2:37). Pengine ulifanya jambo unalojutia, au labda tu unataka kubadilisha maisha yako. Unapaswa kufanya nini unapokuwa na hisia hizi? Ushauri wa Petro kwa Wayahudi unapatikana katika Matendo ya Mitume 2:38. Gundua jinsi kanuni na ibada za kwanza za injili (ikijumuisha imani, toba, ubatizo, na kipawa cha Roho Mtakatifu—au kile ambacho wakati mwingine hujulikana kama mafundisho ya Kristo) vilivyowagusa waongofu hawa, kama ilivyoandikwa katika Matendo ya Mitume 2:37–47.

Yawezekana tayari umekwisha batizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, je, ni kwa jinsi gani unaendelea kutumia mafundisho ya Kristo? Fikiria maneno haya kutoka kwa Mzee Dale G. Renlund: “Tunaweza kukamilishwa kwa kurudia rudia … kuifanyia kazi imani katika [Kristo], kutubu, kupokea sakramenti ili kufanya upya maagano na baraka za ubatizo, na kumpokea Roho Mtakatifu kama mwenza wa daima kwa kiwango kikubwa. Tunapofanya hivyo, tunakuwa zaidi kama Kristo na tunaweza kuvumilia hadi mwisho, na yote yanayoambatana na hayo” (“Watakatifu wa Siku za Mwisho Huendelea Kujaribu,” Liahona, Mei 2015, 56).

Matendo ya Mitume 3:19–21

Je, “nyakati za kuburudishwa” na “zamani za kufanywa upya vitu vyote” ni nini?

“Nyakati za kuburudishwa” humaanisha Milenia, wakati ambapo Yesu Kristo atarejea duniani. “Zamani za kufanywa upya vitu vyote” humaanisha Urejesho wa injili, ambao huuandaa ulimwengu kwa ajili ya Milenia.

Matendo ya Mitume 3; 4:1–31; 5:12–42

Wafuasi wa Yesu Kristo hupewa nguvu kufanya miujiza katika jina Lake.

Mtu kiwete alitumaini kupokea pesa kutoka kwa wale waliokuja hekaluni. Lakini watumishi wa Bwana walimpa kikubwa zaidi. Unaposoma Matendo ya Mitume 3; 4:1–31 na 5:12–42, fikiria jinsi gani muujiza uliofuata uliwagusa watu hawa:

  • Mtu kiwete

  • Petro na Yohana

  • Mashahidi hekaluni

  • Makuhani wakuu na watawala

  • Watakatifu wengine

Picha
Petro anamponya mtu

Nilicho Nacho Ndicho Nikupacho, na Walter Rane

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Matendo ya Mitume 1:21–26.Kusoma Matendo ya Mitume 1:21–26 kunaweza kuisaidia familia yako kujadili baraka ambazo huja kutokana na kuwa na Mitume duniani leo. Wanafamilia wangeweza kushiriki ni kwa namna gani wamepata ushahidi leo kwamba mitume na manabii wa leo wameitwa na Mungu. Kwa nini ushahidi huu ni muhimu?

Matendo ya Mitume 2:37.Ni nini maana ya kirai “wakachomwa mioyo yao”? Ni lini umehisi kitu sawa na hicho? Kwa nini ni muhimu kusema, “Tutendeje?” tunapopata hisia kama hizi?

Matendo ya Mitume 3:1–10.Familia yako inaweza kufurahia kuigiza tena hadithi iliyo katika mistari hii. Au mngeweza kuangalia video “Peter and John Heal a Man Crippled Since Birth” (ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa jinsi gani mtu aliyekuwa hekaluni alibarikiwa tofauti na vile alivyokuwa akitegemea? Ni kwa jinsi gani tumeona baraka za Baba wa Mbinguni zikitujia katika njia tusizotegemea?

Matendo ya Mitume 3:12–26; 4:1–21; 5:12–42.Ni nini kinakuvutia kuhusu uaminifu wa Petro na Yohana? (Ona pia video “Peter Preaches and Is Arrested” kwenye ChurchofJesusChrist.org). Tunawezaje kuwa majasiri katika shuhuda zetu juu ya Yesu Kristo? Fikiria kuwasaidia watoto wadogo kufanya mazoezi ya kushiriki shuhuda zao.

Matendo ya Mitume 4:315:4.Tunawezaje kuzisaidia familia zetu, kata, au jumuiya zetu kuwa zaidi kama kile kilichoelezewa katika Matendo ya Mitume 4:31–37? Inamaanisha nini kuwa “wa moyo mmoja na roho moja”? Ni katika njia zipi sisi wakati mwingine “[huzuia] kwa siri sehemu” ya mchango wetu? Kwa nini kufanya hivyo ni “[kumdanganya] Mungu? (Matendo ya Mitume 5:2, 4). Ni kwa jinsi gani kukosa uaminifu kunatuathiri kiroho?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Let the Holy Spirit Guide,” Nyimbo za Kanisa, na. 143.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Chagua mada. Waruhusu wanafamilia kufanya zamu kuchagua mada kutoka Matendo ya Mitume 1–5 ili kujifunza pamoja.

Picha
Mitume karibu na malaika wawili wakionyesha kidole mbinguni

Kupaa, na Harry Anderson

Chapisha