Agano Jipya 2023
Septemba 18–24. 2 Wakorintho 8–13: “Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”


“Septemba 18–24. 2 Wakorintho 8–13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2023)

“Septemba 18–24. 2 Wakorintho 8–13,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Yesu akizungumza na mtoto mdogo

Septemba 18–24

2 Wakorintho 8–13

“Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”

Kuandika misukumo yako ya kiroho kutakuwezesha kukumbuka kile unachojifunza wakati wa kujifunza maandiko. Unaweza kuandika katika shajara ya kujifunza, kuandika kwa ufupi pembeni ya maandiko yako, kuongeza kwa kuandika kwa ufupi kwenye Gospel Library app, au kujitengenezea rekodi ya kusikiliza ya mawazo yako.

Andika Misukumo Yako

Je, ungefanya nini kama ungesikia kwamba mkusanyiko wa Watakatifu katika eneo jingine ulikuwa unasumbuka katika ufukara? Hii ndiyo hali ambayo Paulo aliielezea kwa Watakatifu wa Korintho katika 2 Wakorintho 8–9. Alitumaini kuwashawishi Watakatifu wa Korintho kujitolea sehemu ya ziada yao kwa Watakatifu wenye uhitaji. Lakini zaidi ya ombi la kujitolea, maneno ya Paulo pia yalikuwa na kweli za kina kuhusu kutoa: “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima: maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” (2 Wakorintho 9:7). Katika siku yetu, bado kuna Watakatifu ulimwenguni kote ambao wanahitaji msaada. Wakati mwingine kikubwa tunachoweza kufanya kwa ajili yao ni kufunga na kutoa matoleo ya mfungo. Katika mambo mengine, kutoa kwetu kunaweza kuwa kwa moja kwa moja na binafsi zaidi. Katika mfumo wowote dhabihu zetu zitakavyokuwa, inastahili kujiuliza sababu ya kutoa kwetu. Je, dhabihu zetu ni kielelezo cha upendo? Hata hivyo, ni upendo ambao humfanya mtoaji kutoa kwa moyo mkunjufu.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

2 Wakorintho 8:1–15; 9:5–15

Ninaweza kwa moyo mkunjufu kushiriki na wengine kile nilichonacho ili kuwabariki maskini na wenye shida.

Kuna watu wengi sana wenye shida kote ulimwenguni. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuleta tofauti? Mzee Jeffrey R. Holland alitoa ushauri huu: “Tajiri au maskini, sote tunapaswa ‘kutenda tunavyoweza’ wakati wengine wakiwa katika shida [ona Marko 14:6, 8]. … [Mungu] atakusaidia na kukuongoza katika matendo ya upendo ya kiufuasi kama kwa uangalifu unataka na kuomba na kutafuta njia za kutii amri alizotupa tena na tena” (“Je, Sisi Sote Si Waombaji?,” Liahona, Nov. 2014, 41).

Soma 2 Wakorintho 8:1–15; 9:6–15, andika kwa ufupi kanuni alizofundisha Paulo kuhusu kuwajali masikini na wenye shida. Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu ushauri wa Paulo? Unaweza kuomba kwa ajili ya mwongozo kuhusu kile unachoweza kufanya ili kumbariki mtu mwenye shida. Hakikisha unaandika misukumo yoyote unayopokea na uifanyie kazi.

Ona pia Mosia 4:16–27; Alma 34:27–29; Russell M. Nelson, “Amri Kuu ya Pili,” Liahona, Nov. 2019, 96–100; Henry B. Eyring, “Je, Saumu Niliyoichagua, Siyo ya Namna Hii?,” Liahona, Mei 2015, 22–25.

2 Wakorintho 11:1–15; 13:5–9

“Jijaribuni wenyewe, kwamba mmekuwa katika imani.”

Leo, kama siku za Paulo, wapo wale ambao wanatafuta kutuongoza kwenye “kuuacha unyofu na usafi kwa Kristo” (2 Wakorintho 11:3). Kwa sababu hiyo, ni muhimu sana kufanya kile Paulo alichopendekeza: “Jijaribuni wenyewe, kwamba mmekuwa katika imani” (2 Wakorintho 13:5). Unaweza kuanza mchakato huu kwa kufikiria kuhusu kile inachomaanisha “kuwa katika imani.” Je, unajuaje kama umekuwa katika imani? Tafuta fursa ulizonazo za kujijaribu wewe mwenyewe.

Kama sehemu ya kujijaribu mwenyewe, ungeweza pia kutafakari kirai “unyofu na usafi ulio katika Kristo” ((2 Wakorintho 11:3). Ni kwa jinsi gani umepata unyofu na usafi kwa Kristo na injili Yake? Ni kwa jinsi gani fikra zako zinaweza “kuharibiwa kutokana na kuacha [ule] unyofu na usafi kwa Kristo”? Je! ni ushauri gani wenye msaada unaoupata katika 2 Wakorintho 11:1–6, 13–15?

Fikiria pia ushauri huu kutoka kwa Rais Dieter F. Uchtdorf: “Kama uliwahi kufikiria kwamba injili haifanyi kazi vizuri kwako, ninakuomba rudi nyuma, yaangalie maisha yako kwa sehemu ya juu, na rahisisha mwenendo wako wa ufuasi. Zingatia katika mafundisho ya msingi, kanuni, na matumizi ya injili. Ninawaahidi kwamba Mungu atawaongoza na kuwabariki katika njia zenu za maisha ya kuridhisha, na injili itafanya kazi vizuri kwenu” (“Inafanya kazi Vizuri Sana,” Liahona, Nov. 2015, 22).

2 Wakorintho 12:5–10

Neema ya Mwokozi yatosha kunisaidia mimi kupata nguvu katika udhaifu wangu.

Hatujui “mwiba katika mwili” wa Paulo ulikuwa nini, lakini sisi sote tunayo miiba yetu wenyewe ambayo tunatamani Mungu angeiondoa kutoka katika maisha yetu. Fikiria kuhusu miiba yako unaposoma 2 Wakorintho 12:5–10, na utafakari kile unachojifunza kuhusu Yesu Kristo katika mistari hii. Paulo alifundisha nini katika mistari hii kuhusu majaribu na udhaifu? Inamaanisha nini kwako kwamba “neema ya Mungu inatosha” kwa ajili yako?

Ona pia Mosia 23:21–24; 24:10–15; Etheri 12:27; Moroni 10:32–33.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

2 Wakorintho 8–9.Je, unagundua nini katika sura hizi ambacho kinatushawishi kuwafikia maskini na wenye shida? Huu unaweza kuwa ni wakati mzuri wa kuandaa tendo la huduma kama familia kwa mtu mwenye shida.

2 Wakorintho 9:6–7.Je, familia yako inamjua mtu ambaye anaweza kuelezewa kama “atoaye kwa moyo wa ukunjufu”? Ni kwa jinsi gani tunaweza kufanya huduma yetu kwa wengine kuwa ya moyo wa ukunjufu zaidi? Wanafamilia vijana wangeweza kutengeneza beji ambayo inasema “Mimi ni mtoaji mwenye moyo wa ukunjufu.” Ungeweza kuwatuza beji hiyo wanafamilia pale unapowaona wakitumikiana kwa moyo wa ukunjufu.

2 Wakorintho 10:3–7.Ni kwa jinsi gani unaweza kuifundisha familia yako kuhusu “vita” vyetu dhidi ya uovu? Je, familia yako itafurahia kujenga ukuta au ngome kwa kutumia viti na mablanketi? Hii inaweza kutupeleka kwenye mjadala kuhusu jinsi ya kuyadondosha mambo yanayotuongoza mbali na Mungu na jinsi ya “[kuteka] nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.” Ni “silaha” zipi za kiroho tunatumia kudhibiti mawazo yetu? (ona Waefeso 6:11–18).

2 Wakorintho 11:3.Je, familia yako inaweza kufanya nini ili kuzingatia zaidi kwenye “unyofu na usafi kwa Kristo”?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “‘Give,’ Said the Little Stream,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 236.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Andika Misukumo. Mzee Richard G. Scott alisema: “Maarifa yanayoandikwa kwa uangalifu ni maarifa unayoweza kuyatumia katika wakati wa shida. … [Kuandika mwongozo wa kiroho] huongeza uwezekano wako wa kupokea nuru zaidi” (“Kupata Maarifa ya Kiroho,” Ensign, Nov. 1993,88; ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 12, 30).

Picha
vijana wadogo wakisaidia kwenye mradi wa huduma

“Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima: maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” (2 Wakorintho 9:7).

Chapisha