Agano Jipya 2023
Oktoba 30–Novemba 5. Waebrania 1–6: “Yesu Kristo, ‘Sababu ya Wokovu wa Milele’”


“Oktoba 30–Novemba 5. Waebrania 1–6: ‘Yesu Kristo, “Sababu ya Wokovu wa Milele”’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Oktoba 30–Novemba 5. Waebrania 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Kristo akiwa amesimama na msichana mdogo

Zeri ya Gileadi, by Annie Henrie

Oktoba 30–Novemba 5

Waebrania 1–6

Yesu Kristo, “Sababu ya Wokovu wa Milele”

Kuandika misukumo ya kiroho hukusaidia wewe kutambua kile ambacho Roho Mtakatifu anataka kukufundisha. Kufanyia kazi misukumo yako huonyesha imani yako kwamba ushawishi huo ni halisi.

Andika Misukumo Yako

Kila mmoja wetu anatakiwa kuacha kitu fulani ili aweze kuikubali injili ya Yesu Kristo—iwe ni mazoea mabaya, imani zisizo sahihi, uhusiano usio mzuri, au kitu kingine chochote. Kwa Wayunani katika Kanisa la Kikristo la mwanzoni, uongofu mara nyingi ilimaanisha kuiacha miungu ya uongo. Kwa Waebrania (au Wayahudi), hata hivyo, uongofu ulithibitisha kuwa, kama si vigumu zaidi, ni wa kutatanisha kidogo. Hata hivyo, imani na tamaduni zao walizozipenda sana zilikuwa zimekita mizizi katika kumwabudu Mungu wa kweli na mafundisho ya manabii Wake, ikirudi nyuma maelfu ya miaka. Na bado Mitume walifundisha kwamba sheria ya Musa ilitimizwa katika Yesu Kristo na kwamba sheria ya juu zaidi sasa ilikuwa ndiyo kiwango kwa waaminio. Je, kuukubali Ukristo ingemaanisha kwamba Waebrania lazima waache imani na historia zao za mwanzo? Waraka kwa Waebrania ulitafuta kusaidia kumaliza maswali kama hayo kwa kufundisha kwamba sheria ya Musa, manabii, na ibada ni muhimu, lakini Yesu Kristo ni mkuu zaidi (ona Waebrania 1:1–4; 3:1–6; 7:23–28). Kwa kweli, mambo haya yote yanaelekeza kwa, na kushuhudia juu ya Kristo kama Mwana wa Mungu na Masiya aliyeahidiwa ambaye Wayahudi walikuwa wakimsubiri.

Uongofu, katika siku zile za zamani na leo, unamaanisha kumfanya Yesu Kristo kuwa kiini cha kuabudu kwetu na cha maisha yetu. Inamaanisha kushikilia kwa nguvu ukweli na kuachilia kile ambacho kinatuvuta mbali Naye, kwani Yeye ndiye “ sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii” (Waebrania 5:9).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Nani aliandika Waraka huu kwa Waebrania?

Baadhi ya wasomi wametia shaka ikiwa Paulo aliandika Waraka huu kwa Waebrania. Mtindo wa maandishi wa Waebrania kwa kiasi fulani ni tofauti na barua zingine za Paulo, na matoleo ya maandishi ya mwanzo kabisa hayakutaja mwandishi. Hata hivyo, kwa sababu mawazo yaliyoelezewa katika Waebrania ni sawa na mafundisho mengine ya Paulo, Watakatifu wa Siku za Mwisho, katika kuendeleza utamaduni wa Ukristo, kwa ujumla wamekubali kwamba Paulo alijihusisha kwa kiasi fulani katika kuandika waraka huu.

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Nyaraka za Paulo.”

Waebrania 1–5

Yesu Kristo ni “chapa ya nafsi” ya Baba wa Mbinguni.

Wayahudi wengi waliona vigumu kumkubali Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu. Tazama jinsi Waraka huu kwa Waebrania unavyomshuhudia Yeye. Kwa mfano, unaposoma sura tano za kwanza, ungeweza kuweka orodha ya majina ya Yesu Kristo, majukumu, sifa, na kazi ambazo unazipata zimetajwa. Je, mambo haya hukufundisha nini kuhusu Mwokozi? Je, yanakufundisha nini kuhusu Baba wa Mbinguni?

Je, kauli ifuatayo kutoka kwa Mzee Jeffrey R. Holland huongezea nini kwenye uelewa wako wa mafundisho katika sura hizi? “Yesu … alikuja kuboresha mtazamo wa mwanadamu juu ya Mungu na kuwaomba kumpenda Baba yao wa Mbinguni kama ambavyo Yeye daima amewapenda na daima atawapenda. … Hivyo kulisha wenye njaa, kuponya wagonjwa, kukemea unafiki, kuomba kwa ajili ya imani—huyu alikuwa ni Kristo akituonyesha njia ya kwenda kwa Baba” (“Sifa Kuu ya Mungu,” Liahona, Nov. 2003,72).

Waebrania 2:9–18; 4:12–16; 5:7–8

Yesu Kristo aliteseka kwa yote ili kwamba Aweze kuelewa na kunisaidia wakati ninapoteseka.

Je, unahisi kwamba unaweza “kukikaribia kwa ujasiri kiti cha neema” na kutafuta rehema? (Waebrania 4:16). Ujumbe mmoja wa Waraka kwa Waebrania ni kwamba bila kujali dhambi na udhaifu wetu, Mungu anaweza kufikiwa na neema Yake inaweza kupatikana. Je, unapata nini katika Waebrania 2:9–18; 4:12–16; 5:7–8 ambacho huimarisha kujiamini kwako kwamba Yesu Kristo atakusaidia kwenye changamoto zako za maisha? Fikiria kuandika katika shajara yako mawazo na hisia zako kuhusu yale ambayo Mwokozi amefanya kwa ajili yako.

Ona pia Mosia 3:7–11; Alma 7:11–13; 34; Matthew S. Holland, “Zawadi Nzuri Sana ya Mwana,” Liahona, Nov. 2020, 45–47.

Waebrania 3:74:11

Baraka za Mungu zinapatikana kwa wote ambao “hawashupazi mioyo [yao].”

Kwa kusimulia tena hadithi ya Waisraeli wa kale, Paulo alitumaini kuwashawishi Wayahudi kuepuka makosa waliyofanya mababu zao—kukataa baraka za Mungu kwa sababu ya kutokuamini. (Unaweza kusoma hadithi Paulo aliyoigusia katika Hesabu 14:1–12, 26–35.)

Fikiria jinsi gani Waebrania 3:74:11 inavyoweza kutumika kwako. Ili kufanya hili, unaweza kutafakari maswali kama haya:

  • Ni kwa jinsi gani Waisraeli walimkasirisha Bwana? (ona Waebrania 3:8–11). Je, matokeo ya kuwa na moyo mgumu ni nini?

  • Je, ni wakati gani nimeruhusu moyo wangu kuwa mgumu? Je, kuna baraka zozote ambazo Mungu anataka kunipa ambazo sizipokei kwa sababu ya kukosa imani?

  • Je, ninaweza kufanya nini ili kukuza moyo laini na uliopondeka? (ona Etheri 4:15; Methali 3:5–6; Alma 5:14–15).

Ona pia 1 Nefi 2:16; 15:6–11; Yakobo 1:7–8; Alma 12:33–36; Neill F. Marriott, “Kuridhia Mioyo Yetu kwa Mungu,” Liahona, Nov. 2015, 30–32.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Waebrania 1:8–9.Ni kwa njia gani Yesu ameonyesha kwamba Anapenda haki na kuchukia uovu? Kama tuna matamanio yasiyo ya haki, tunaweza kufanya nini ili kuyabadilisha?

Waebrania 2:1–4.Je, unaweza kufikiria juu ya somo la vitendo ili kuisaidia familia yako kuelewa inamaanisha nini kushika kwa uthabiti kweli za injili “ambazo tumezisikia”? Unaweza kuelezea hili kwa mfano kwa kutumia kitu ambacho ni vigumu kukishikilia. Je, ni kwa jinsi gani juhudi zetu za kudumisha ushuhuda zinafanana na kushika na kung’ang’ania kitu hiki? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuhakikisha kwamba “mambo tuliyosikia” “hayaondoki” kwetu? (mstari wa 1).

Waebrania 2:9–10.Kutafiti kirai “kiongozi mkuu wa wokovu wao,” unaweza kuanza kwa kujadili mambo ambayo kiongozi hufanya. Wokovu unamaanisha nini? Je, ni kwa kwa jinsi gani Yesu Kristo ni sawa na kiongozi wetu sisi na wokovu wetu?

Waebrania 5:1–5.Mistari hii inaweza kuwasaidia kuwa na majadiliano kuhusu inamaanisha nini kuitwa na Mungu kupitia mtu mwenye mamlaka. Je, tunaweza kujifunza nini kutoka katika mfano wa Yesu Kristo kuhusu kupokea na kutimiza miito?

Picha
Musa akimtawaza Haruni

“Na hapana mtu ajitwaliaye ​​​heshima hii, ila ​​​yeye aitwaye na Mungu, kama vile ​​​Haruni” (Waebrania 5:4). Musa Anamwita Haruni kwenye Huduma, na Harry Anderson

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “I Need Thee Every Hour,” Nyimbo za Kanisa, na. 98.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Jaribu mbinu tofauti. Badala ya daima kujifunza maandiko katika njia inayofanana, fikiria mawazo tofauti ya kujifunza. Kwa baadhi ya mawazo, ona “Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Kwako Binafsi Maandiko” mwanzoni mwa nyenzo hii.

Picha
Yesu Kristo

Nuru ya Ulimwengu, na Howard Lyon

Chapisha