Agano la Kale 2022
Aprili 18–24. Kutoka 18–20: “Yote Ambayo Bwana Amesema Tutafanya”


“Aprili 18–24. Kutoka 18–20: ‘Yote Ambayo Bwana Amesema Tutafanya,’” Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Aprili 18–24. Kutoka 18-20,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
mlima

Mlima katika Misri kimapokeo unaaminika kuwa ni Mlima Sinai.

Aprili 18–24

Kutoka 18–20

“Yote Ambayo Bwana Amesema Tutafanya”

Dada Michelle Craig alifundisha, “Kama mfuasi mwaminifu wa [Yesu Kristo], unaweza kupokea mwongozo wa kiungu wa kibinafsi na ufunuo, kulingana na amri zake ambazo zimetolewa kwako” (“Uweza wa Kiroho,” Liahona, Nov. 2019, 21). Andika na ufanyie kazi mwongozo wa kiungu unaoupokea unaposoma Kutoka 18–20.

Andika Misukumo Yako

Safari ya Waisraeli kutoka Misri hadi mwanzo mwa Mlima Sinai ilijaa miujiza—dhihirisho la wazi kabisa la nguvu, upendo, na rehema ya Bwana isiyo na mfano. Hata hivyo, Bwana alikuwa na baraka ghalani kwa ajili yao ambayo ilikuwa zaidi ya kuwatorosha kutoka Misri na kukidhi njaa yao ya kimwili na kiu. Yeye aliwataka kuwa watu Wake wa agano, “Tunu” Yake, na “taifa takatifu” (Kutoka 19:5–6). Leo, baraka ya agano hili imeenea mbali zaidi ya watu au taifa moja tu. Mungu anataka watoto Wake wote kuwa watu Wake wa agano, “kutii sauti [Yake] hasa, na kushika agano [Lake]” (Kutoka 19:5), kwani Yeye anaonyesha rehema Zake “kwa maelfu wampendao [Yeye], na kushika amri [Zake]” (Kutoka 20:6).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Kutoka 6:13–26

Mimi ninaweza kusaidia “kubeba mzigo” wa kufanya kazi ya Bwana.

Unaposoma ushauri ambao Musa alipokea kutoka kwa baba mkwe wake, Yethro, tafakari jinsi wewe unavyoweza kuwa kama “watu wa ukweli” (wakati mwingine inatafsiriwa kama “watu waaminifu”) walioelezewa katika mstari wa 21. Je, ni kwa jinsi gani wewe unaweza kusaidia “kubeba mzigo” wa viongozi wako wa Kanisa? (Mstarimstari wa 22). Kwa mfano, jinsi gani ushauri huu unaweza kutumika katika juhudi zako za kutumikia?

Unaweza pia kufikiria kwamba wewe, wakati mwingine, kama Musa, unajaribu kufanya mengi. Je, jinsi gani ushauri wa Yethro ungeweza kutumika kwako?

Ona pia Mosia 4:27; Henry B. Eyring, “The Caregiver,” Liahona, Nov. 2012, 121–24.

Picha
Mwanaume akisalimiana na mwanamke

Kuwatumikia wengine ni njia mojawapo tunayoweza kushiriki katika kazi ya Bwana.

Kutoka 19:3–6

Watu wa agano wa Mungu ni tunu ya kipekee Kwake.

Zingatia kitu inachomaanisha kwako kuwa “tunu ya kipekee” ya Bwana (Kutoka 19:5). Rais Russell M. Nelson alitoa ufafanuzi mmoja juu ya kifungu hiki cha maneno: “Katika Agano la Kale, neno la Kiebrania ambako neno kipekee lilitafsiriwa ni segullah, ambalo linamaanisha ‘mali iliyothaminiwa,’ au ‘tunu.’ … Kwa sisi kutambuliwa na watumishi wa Bwana kama watu Wake wa kipekee ni sifa ya kiwango cha juu sana” (“Children of Covenant,” Ensign, Mei 1995, 34). Je, ni jinsi gani kujua kwamba kushika kwako maagano kunakufanya wewe kuwa “tunu ya kipekee” na hivyo kushawishi namna unavyoishi?

Ona pia Gerrit W. Gong, “Kuwa wa Agano,” Liahona, Mei 2019, 80-83.

Kutoka 19:10–11, 17

Matukio matakatifu yanahitaji maandalizi.

Bwana alimwambia Musa kwamba wana wa Israeli walihitaji kuandaliwa kabla ya kuweza “kukutana na Mungu” (Kutoka 19:10–11, 17) na kushika agano na Yeye (ona Kutoka 19:5). Je, wewe unafanya nini ili kujiandaa kwa ajili ya matukio matakatifu katika maisha yako, kama vile kuhudhuria hekaluni au kula sakramenti? Je, unaweza kufanya nini ili kujiandaa kikamilifu zaidi kwa ajili ya matukio haya? Fikiria juu ya shughuli nyinginezo za kiroho ambazo zinahitaji maandalizi, na tafakari jinsi maandalizi yako yanavyoweza kuathiri aina ya uzoefu ulio nao.

Kutoka 20

Mungu ni mwenye rehema.

Unaposoma Kutoka 20, zingatia kukumbuka kati ya Amri Kumi ni amri ipi unayoona unatii na ipi unaona ungeweza kutii kwa uaminifu zaidi. Ungeweza kuchagua amri moja ili kuifanyia kazi na kisha ujifunze juu yake kwa kina zaidi kwa kusoma maandiko yanayohusiana nayo (ona Mwongozo wa Maandiko kwenye scriptures.ChurchofJesusChrist.org) au ujumbe wa mkutano mkuu (ona sehemu ya mada ya conference.ChurchofJesusChrist.org). Zingatia kujumuisha katika kujifunza kwako baraka ambazo huja kwa wale wanaotii amri. Je, baraka hizi zinaonyeshaje rehema na upendo wa Mungu kwa ajili yako?

Ona pia Carole M. Stephens, “Kama Wanipenda, Shika Amri Zangu,” Liahona, Nov. 2015, 118–20.

Kutoka 20:1–7.

Ni muhimu kumweka Mungu kwanza katika maisha yangu.

Kusoma Kutoka 20:1–7 kunaweza kukushawishi kufikiria kuhusu vipaumbele katika maisha yako—ungeweza hata kuviandika kwa kuviorodhesha. Je, ni ipi baadhi ya vinavyowezekana kuwa “miungu” au “sanamu [za] kuchongwa” (Kutoka 20:3–4) ambazo unaweza kujaribiwa kuziweka mbele ya Mungu? Je, ni kwa jinsi gani kumuweka Bwana mbele kunakusaidia wewe katika vitu vingine muhimu vya maisha yako? Je, wewe unatiwa msukumo wa kufanya nini ili kuongeza fokasi yako kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Ona pia Dallin H. Oaks, “Hakuna Miungu Wengine,” Liahona, Nov. 2013, 72–75.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Kutoka 18:8-12.Je, ushuhuda wa Musa juu ya ukombozi wa Mungu ulikuwa na matokeo gani kwa Yethro? Je, ni mambo gani makuu Bwana amefanya kwa ajili ya familia yetu? Je, ni nani tunaweza kushirikiana naye uzoefu wetu? Je, tunawezaje kuhifadhi uzoefu wetu huo kwa ajili ya vizazi vya baadaye?

Kutoka 18:13–26.Mistari hii ingeweza kuivutia familia yako kufikiria kuhusu huduma ya viongozi wa Kanisa wa eneo lenu, kama vile askofu au rais wa tawi, viongozi wa vijana au walimu wa msingi. Je, ni majukumu gani waliyonayo ambayo yanaweza kuonekana kuwa “mazito sana” (Kutoka 18:18) kwa mtu mmoja kuyabeba pekee yake? Tunaweza kufanya nini ili kusaidia kuinua mizigo yake?

Kutoka 20:3-17.Fikirieni njia nzuri ya kujadili Amri Kumi kama familia. Kwa mfano, ungeweza kuandika amri zilizoko katika Kutoka 20:3–17 kwenye vipande kumi vya karatasi. Washiriki wa familia kisha wanaweza kuzichambua katika aina mbili: (1) kumheshimu Mungu na (2) kuwapenda wengine (ona pia Mathayo 22:36–40). Zingatia kuchagua amri moja au mbili kila siku wiki hii na kujadili kwa pamoja kwa kina zaidi. Kwa mfano, ni kwa jinsi gani kutii amri hii kunaimarisha familia yetu? Je, ni kwa jinsi gani Mwokozi alitii amri hii?

Kutoka 20:12.Ili kuelewa vyema Kutoka 20:12, inaweza kusaidia kama familia yenu itatafuta maana ya neno “heshima.” Kisha wana familia wangeweza kutengeneza orodha ya mambo tunayoweza kufanya ambayo yangeleta heshima kwa wazazi wetu. Mngeweza kuimba wimbo kuhusu kuwaheshimu wazazi, kama “Quickly I’ll Obey” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 197), na kisha tumieni baadhi ya mawazo yaliyoko katika orodha yenu ili kuandika mistari mipya ya wimbo huu.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Keep the Commandments,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 146–47.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta muda ambao unafaa kwako. Mara kwa mara ni rahisi zaidi kujifunza kutoka kwenye maandiko wakati unapoweza kujifunza bila kukatizwa. Tafuta muda ambao unafaa kwako, na fanya kwa uwezo wako wote kuwa na msimamo wa kujifunza katika muda huo kila siku.

Picha
Musa ameshika mbao za mawe

Kielelezo cha Musa ameshika Amri Kumi, na Sam Lawlor

Chapisha