Agano la Kale 2022
Novemba 7–13. Hosea 1–6; 10–14; Yoeli: “Nitawapenda kwa Ukunjufu wa Moyo”


“Novemba 7-13. Hosea 1–6; 10–14; Yoeli: ‘Nitawapenda kwa Ukunjufu wa Moyo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Novemba 7–13. Hosea 1–6; 10–14,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
bi harusi na bwana harusi katika eneo la hekalu.

Novemba 7–13

Hosea 1–6; 10–14; Yoeli

“Nitawapenda kwa Ukunjufu wa Moyo”

Alika Roho kuwa sehemu ya kujifunza kwako kwa Hosea na Yoeli. Andika muhtasari wa jumbe ambazo Roho amemkutia msukumo moyoni na akilini mwako.

Andika Misukumo Yako

Agano la Israeli na Bwana lilikuwa na maana ya kina na ya maana ambayo Bwana alililinganisha na ndoa. Agano, kama ndoa, lilijumuisha kujitolea kwa milele, uzoefu wa pamoja, kujenga maisha pamoja, uaminifu wa kipekee, na zaidi ya yote, upendo wa moyo wote. Aina hii ya kujitolea ilikuja na matarajio makubwa—na matokeo mabaya kwa uzinzi. Kupitia nabii Hosea, Mungu alielezea baadhi ya matokeo ambayo Waisraeli walipata kwa kuvunja agano lao. Na bado ujumbe Wake haukuwa “Nitakukataa milele kwa kutokuwa mwaminifu.” Badala yake ulikuwa “nitakualika urudi” (ona Hosea 2:14–15). “Nitakuposa uwe wangu katika haki,” Bwana alisema (Hosea 2:19). “Nitawaponya kurudi nyuma kwao, nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo” (Hosea 14:4). Huu ni ujumbe ule ule Anaotupatia leo tunapotafuta kuishi maagano yetu kwa upendo na kujitolea.

Yoeli alishiriki ujumbe kama huo: “Mgeukie Bwana Mungu wako: kwa kuwa yeye ndiye mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira, na mwingi wa fadhili” (Yoeli 2:13). “Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli” (Yoeli 3:16). Unaposoma Hosea na Yoeli, tafakari uhusiano wako mwenyewe na Bwana. Fikiria juu ya jinsi uaminifu wake unakuhimiza kuwa mwaminifu Kwake.

Kwa ajili ya muhtasari wa vitabu vya Hosea na Yoeli, ona “Hosea au Hoshea” na “Yoeli” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Hosea 1–3; 14

Bwana hunialika kila mara kurudi Kwake.

Mke wa Hosea, Gomeri, hakuwa mwaminifu kwake, na Mungu alionyesha tukio hili la kusikitisha kufundisha Waisraeli jinsi alivyohisi juu yao na maagano yao na Yeye. Unaposoma Hosea 1–3, tafakari jinsi Bwana anavyoona uhusiano wake na watu Wake wa agano. Unaweza kutafakari njia ambazo wewe, kama Waisraeli, unaweza kuwa haukuwa mwaminifu kwa Bwana na jinsi alivyokufikia. Kwa mfano, ni nini Hosea 2:14–23 na Hosea 14 zinakufundisha juu ya upendo na huruma ya Bwana? Je! Unamwonyeshaje upendo na uaminifu wako?

Ona pia Dieter F. Uchtdorf, “Sehemu Salama ya Kurudi Nyuma,” Liahona, Mei 2007, 99-101.

Picha
mwanamke ameketi chini na mwanamume akiweka mikono kichwani

Gomeri mwenye dhambi, ambaye anawakilisha Israeli, alipewa ukombozi na Bwana. Kielelezo na Deb Minnard, leseni kutoka goodsalt.com

Hosea 6:4–7; Yoeli 2:12–13

Kujitolea kwa Mungu lazima kuhisiwe kwa ndani, sio kuonyeshwa kwa nje tu.

Bwana alikuwa ameamuru watu wake watoe dhabihu za wanyama. Lakini hata ingawa watu katika siku za Hosea walikuwa wakitii sheria hiyo, walikuwa wakivunja amri za umuhimu zaidi (ona Hosea 6:4–7). Unafikiria inamaanisha nini kwamba Bwana “alitaka rehema, na sio dhabihu; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa”? (Hosea 6:6). Unafikiria inamaanisha nini kwa haki kuwa kama wingu au kama umande? Je! Haki yetu inapaswa kuwaje? (Ona Isaya 48:18; 1 Nefi 2:9–10).

Ungeweza pia kusoma Mathayo 9:10–13; 12:1–8 kuona jinsi Mwokozi alivyotumia Hosea 6:6 wakati wa huduma Yake. Je! Vifungu hivi vinakusaidiaje kuelewa maneno ya Hosea?

Wakati unasoma Yoeli 2:12–13, inaweza kusaidia kujua kwamba kurarua au kuchana nguo za jadi ilikuwa ishara ya nje ya maombolezo au majuto (kwa mfano, ona 2 Mambo ya Nyakati 34:14–21, 27). Je! Ni kwa jinsi gani kurarua mioyo yetu ni tofauti na kurarua mavazi yetu?

Ona pia Isaya 1:11–17; Mathayo 23:23; 1 Yohana 3:17–18.

Yoeli 2

“Nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili.”

Wakati Yoeli alipotabiri juu ya “siku ya Bwana,” aliielezea kama “siku ya giza na weusi,” “kuu na yenye kutisho sana” (Yoeli 2:1–2, 11). Israeli imekabiliwa na siku nyingi kuu na zenye kutisho katika historia yake, na watu wa agano la Mungu watakabiliwa zaidi baadaye. Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu ushauri alioutoa Bwana katika Yoeli 2:12–17? Pia angalia baraka alizoahidi katika Yoeli 2:18–32. Kwa nini baraka zilizoahidiwa katika mstari wa 27–32 zinaweza kuwa za maana sana katika siku kama zile zilizoelezewa katika Yoeli 2, pamoja na siku yetu?

Unafikiri inamaanisha nini kwamba Bwana “atamimina roho [Yake] juu ya wote wenye mwili.”? (Yoeli 2:28). Ni kwa jinsi gani unabii huu katika Yoeli 2:28–29 unavyotimizwa? (Ona Matendo ya Mitume 2:1–21; Joseph Smith—Historia 1:41.)

Unaweza kutafakari maneno haya kutoka kwa Rais Russell M. Nelson: “Katika siku zijazo, haitawezekana kunusurika kiroho bila uzoefu wa kuongoza, kuelekeza, kufariji na ushawishi endelevu wa Roho Mtakatifu.” (“Ufunuo kwa ajili ya Kanisa, Ufunuo kwa ajili ya Maisha Yetu,” Liahona, Mei 2018, 96). Kwa nini ufunuo ni muhimu kwa kunusurika kiroho? Ni kwa jinsi gani unaweza kuongeza uwezo wako ili kupokea ufunuo binafsi?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Hosea 2:19–20.Bwana alitumia sitiari ya ndoa kuelezea uhusiano wake wa agano na Israeli (ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Bwana Harusi,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Familia yako inaweza kujadili kwa nini ndoa inaweza kuwa mfano mzuri kwa maagano yetu na Mungu. Je! Ni jinsi gani Hosea 2:19–20 inatusaidia kuelewa jinsi Mungu anavyojisikia kutuhusu sisi? Je! Tunawezaje kuwa waaminifu kwa maagano yetu na Yeye?

Hosea 10:12.Watoto wanaweza kufurahia kuchora saa na kupanga njia ambazo wanaweza kumtafuta Bwana kwa nyakati tofauti kwa siku nzima.

Yoeli 2:12–13.Ili kuisaidia familia yako kuongea kuhusu Yoeli 2:12–13, unaweza kuweka picha ya Mwokozi upande mmoja wa chumba na neno dhambi upande mwingine. Alika wanafamilia kuchukua zamu kuelekea ishara na kisha kugeukia kwa Mwokozi wanaposhiriki vitu ambavyo vinaweza kutusaidia kurejea Kwake “kwa moyo [wetu] wote.” Watie moyo wanafamilia kufikiria juu ya nyanja zote za maisha yao, pamoja na shughuli, kazi, shule, na mahusiano.

Yoeli 2:28–29.Inaweza kumaanisha nini kwa Roho “kumwagwa” juu yetu? Labda unaweza kuonyesha hii kwa kumwagilia kioevu na kisha ukitofautisha na tona tona au kutiririka.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Come unto Jesus,” Nyimbo za Kanisa, na.117.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha mafundisho. “Usikose kabisa nafasi ya kuwakusanya watoto pamoja ili kujifunza kuhusu mafundisho ya Yesu Kristo. Nyakati kama hizo ni nadra sana kwa kulinganisha na juhudi za adui” (Henry B. Eyring, “Nguvu za Fundisho la Kufundisha,” Ensign, Mei 1999,74).

Picha
Yesu amesimama mlangoni

Njoo, Kwangu, na Kelly Pugh

Chapisha