Mafundisho na Maagano 2021
Agosti 9–15. Mafundisho na Maagano 88: “Ijengeni … Nyumba ya Mungu”


“Agosti 9–15. Mafundisho na Maagano 88: “Ijengeni … Nyumba ya Mungu, ”,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Agosti 9–15. Mafundisho na Maagano 88,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
chumba chenye viti na mabenchi

Agosti 9–15

Mafundisho na Maagano 88)

“Ijengeni … Nyumba ya Mungu”

Mafundisho na Maagano 88:118 ushauri, “Fundishaneni maneno ya hekima.” Ni yapi “maneno ya hekima” katika Mafundisho na Maagano 88 yanayohusika zaidi kwa watoto unaowafundisha?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waambie watoto kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatutaka kuendelea kujifunza maisha yetu yote. Kisha watake kushiriki kitu fulani wanachojifunza kukihusu nyumbani, shuleni, au Kanisani.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mafundisho na Maagano 88:63

Mungu ananitaka kuwa karibu Naye.

Unaweza kufanya nini kuwasaidia watoto unaowafundisha kuhisi uwepo wa Mungu katika maisha yao?

Shughuli Yamkini

  • Unaposoma Mafundisho na Maagano 88, waalike watoto waigize baadhi ya maneno wanayosikia. Kwa mfano, wangeweza kujifanya kutafuta kitu fulani au kugonga.

  • Mtake mtoto kushikilia picha ya Yesu mbele ya chumba wakati watoto wengine wamesimama nyuma ya chumba. Watake watoto kupiga hatua mbele kila wakati unaposema kitu fulani tunachoweza kufanya ili kuja karibu zaidi kwa Mwokozi na kupiga hatua nyuma kila wakati unaposema kitu fulani ambacho kinatutenganisha sisi kutoka kwa Mwokozi. Toa ushuhuda wako kwamba wakati tunapojaribu kuwa karibu zaidi na Mwokozi, anakuja karibu zaidi kwetu.

Mafundisho na Maagano 88:118

Baba wa Mbinguni ananitaka mimi kujifunza.

Elimu ni sehemu muhimu ya mpango wa Baba wa Mbinguni kukusaidia wewe kuwa zaidi kama alivyo Yeye. … Elimu unayopata itakuwa na thamani kwako wakati wa maisha haya ya duniani na katika maisha yajayo” (Kwa Nguvu ya Vijana, 9).

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya Shule, au chora picha ubaoni, na watake watoto kuelezea ni shule gani na nini kinatokea pale. Eleza kuhusu shule Joseph Smitha aliyoanzisha (ona “Sura ya 31: Neno la Hekima,” Hadithi za Mafundisho na Maagano,119–22). Waonyeshe watoto picha za nyumba, kanisa, na hekalu, na waulize jinsi gani sehemu hizi pia ni kama shule.

  • Imba wimbo kuhusu kujifunza, kama vile “Search, Ponder, and Pray” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,109). Waulize watoto kuhusu kile wanachofurahia kujifunza.

  • Soma Mafundisho na Maagano 88:118, na sisitiza msemo “fundishaneni.” Shiriki hekima fulani uliyojifunza kutoka kwa kila mmoja wa watoto katika darasa lako, na watake kushiriki hekima waliyojifunza.

    Picha
    Watoto wakijifunza maandiko

    Tunapaswa kutafuta hekima na kujifunza.

Mafundisho na Maagano 88:119

Hekalu ni nyumba ya Mungu.

Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto kuhisi upendo wa hekalu na kutamani kumwabudu Mungu pale wakati watakapokuwa tayari.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto jinsi ya kutengeneza “mnara” wa hekalu kwa kuinua mikono yao na wakikugusa ncha za vidole vyao pamoja. Soma Mafundisho na Maagano 88:119, na watake kutengeneza mnara kila wakati unaposema neno “nyumba.” Eleza kwamba Baba wa Mbinguni alimtaka Joseph Smith na Watakatifu kujenga hekalu, au “nyumba ya Mungu.” Onyesha picha ya hekalu lililo karibu unapozungumza kuhusu tofauti kati ya hekalu na nyumba ya mkutano ya Kanisa.

  • Shiriki ushuhuda wako wa hekalu, muimbe pamoja wimbo kuhusu hekalu, kama vile “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 95). Waalike watoto wajichore picha zao wakienda hekaluni.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mafundisho na Maagano 88: 68, 74

Yesu Kristo anaweza kunifanya msafi kutokana na dhambi.

Kutakaswa kunamaanisha kufanywa msafi na mtakatifu. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kuelewa kwamba wanaweza kutakaswa wanapomfuata Yesu Kristo?

Shughuli Yamkini

  • Mwalike mtoto mmoja asome Mafundisho na Maagano 88:68 kwa sauti na mwingine asome mstari wa 74. Waombe watoto kusikiliza kwa kuzingatia msemo ambao upo katika mistari hii miwili. Jinsi gani “tunajitakasa” wenyewe? (Kama inahitajika, wasaidie watoto kutafuta “utakaso” katika Mwongozo kwenye Maandiko.) Chora picha ya moyo, mkono, na mguu ubaoni. Wasaidie watoto kufikiria juu ya kile ambacho inaweza kumaanisha “kutakasa” na “kusafisha” mioyo yetu, mikono, na miguu. Ni jinsi gani Mwokozi anatusaidia kufanya hili? Jinsi gani tunaweza kutumia mioyo yetu, mikono, na miguu kuwa zaidi kama Yesu?

  • Eleza kwamba Bwana aliwataka watu Wake kutakaswa kabla hawajaweza kwenda kwenye hekalu. Fikiria kumwalika kijana au msichana aliye na kibali cha hekaluni kutembelea darasa. Mwalike kuwaonyesha watoto kibali cha hekaluni kinaonekana vipi, jadili wanafanya nini kuishi kwa kukistahili, na shiriki kwa nini ni muhimu kuwa na kibali cha hekaluni hata kama hatuishi karibu na hekalu.

Mafundisho na Maagano 88:77–80, 118

Baba wa Mbinguni ananitaka mimi kujifunza.

Unaweza kuwasaidia watoto kuelewa kwamba kujifunza kuhusu vyote mambo ya kiroho na kidunia kunaweza kuwaandaa kumtumikia Bwana.

Shughuli Yamkini

  • Andika ubaoni Nini, Kwa nini na Jinsi gani, Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 88:77–79 wawili wawili na tengeneza orodha ya Nini Bwana anatutaka kujifunza kukihusu. Kisha watake kutafuta mstari wa 80 kupata kwanini anatutaka sisi kujifunza. Kisha wanaweza kutafuta mstari wa 118 kupata jinsi tunavyopaswa kujifunza. Je, tunajifunza nini kutoka katika mistari hii kuhusu jinsi Bwana anavyotazama elimu na kujifunza?

  • Onyesha ramani ya ulimwengu, na someni pamoja Mafundisho na Maagano 88:79. Kwa nini ni muhimu kwetu kujifunza kuhusu nchi na tamaduni zingine? Kama wewe au watoto unaowafundisha wametembelea au kuishi katika nchi nyingine, onyesha vitu ambavyo vinawakilisha utamaduni, na shiriki vitu ulivyojifunza.

Mafundisho na Maagano 88:119–26

“Ijengeni … Nyumba ya Mungu”

Maelekezo ya Bwana kuhusu “nyumba ya Mungu” yanaweza kuwa msaada wa mwongozo kwa ajili yetu tunapojijenga wenyewe na kujenga nyumba zetu.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kuchagua maneno saba ambayo yanaelezea nyumbani kwao au nyumba nyingine waliyotembelea. Kisha watake kusoma Mafundisho na Maagano 88:119 na kutafuta maneno saba Bwana anayoyatumia kuelezea Nyumba Yake. Wasaidie watoto kufikiria juu ya njia wanayoweza kufanya nyumba zao kuwa “nyumba ya Mungu.”

  • Mpe kila mtoto kifungu cha maneno kutoka Mafundisho na Maagano 88:119–26 kwa ajili ya kuchora. Wakati wanapoonyeshana picha zao, waache watoto watafute mistari kukisia ni kifungu gani cha maneno kila picha inawakilisha.

  • Andika ubaoni Fanya na Usifanye. Watake watoto kusoma Mafundisho na Maagano 88:119–26 na orodhesha vitu Bwana alivyowataka Watakatifu kufanya au kutofanya ili kujiandaa kujifunza katika hekalu. Wangeweza kutazama maneno yasiyojulikana katika kamusi. Watake watoto kuchagua kitu fulani ambacho wataanza kukifanya au kitu fulani ambacho wataacha kukifanya.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Watake watoto waandike au wachore kitu kimoja walichojifunza ambacho wangependa kushiriki pamoja na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto wadogo kushiriki katika majadiliano ya injili. Unaweza kutaka kufikiria juu ya kutengeneza njia za kuwa na majadiliano ya injili na watoto wadogo. Kwa mfano, unaweza kuleta darasani kitu fulani ambacho watoto wanaweza kushikilia wakati ni zamu yao ya kuzungumza.

Chapisha