Njoo, Unifuate
Desemba 31–Januari 6. Tuna Jukumu la Mafunzo Yetu Sisi Wenyewe


Desemba 31–Januari 6. Tuna Jukumu la Mafunzo Yetu Sisi Wenyewe,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Desemba 31–Januari 6. Tuna Jukumu la Mafunzo Yetu Sisi Wenyewe,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
familia ikitazama alibamu

Desemba 31–Januari 6

Tuna Jukumu la Mafunzo Yetu Sisi Wenyewe

Unaposoma maandiko katika muhtasari huu, andika misukumo yoyote ya kiroho unayopokea. Utagundua kwamba kila muhtasari katika kitabu hiki cha kiada una shughuli za watoto wadogo na watoto wakubwa, lakini unaweza kutohoa shughuli yoyote kwa ajili ya darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Mwanzoni mwa kila darasa, wape watoto nafasi za kushiriki yale wanayojifunza kuhusu injili. Kwa mfano, wiki hii unaweza kuwaalika washiriki hadithi wanazopenda kuhusu Yesu Kristo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

Yesu Kristo anataka nimfuate Yeye.

Wewe na watoto mtasoma hadithi nyingi kutoka katika maisha ya Yesu Kristo mwaka huu. Wasaidie watoto kuelewa kwamba sababu tunajifunza hadithi hizi ni ili kwamba tuweze kufuata vyema mfano kamili wa Yesu Kristo.

Shughuli za Yakini

  • Soma mwaliko wa Mwokozi, “Njoo, unifuate,” unaopatikana katika Luka 18:22. Cheza mchezo ambapo mtoto mmoja anafanya kitendo na kisha anawaambia watoto wengine, “Njoo, unifuate.” Waalike watoto wengine kurudia kitendo hicho.

  • Onyesha picha za watu wakimfuata Mwokozi katika njia tofauti, wakati wa huduma Yake Akiwa duniani na katika siku yetu. Unaweza kupata picha katika Kitabu cha Sanaa za Injili au magazeti ya Kanisa. Unaweza pia kuonyesha video “Angaza Dunia” (LDS.org). Waache watoto watambue jinsi watu wanavyomfuata Mwokozi.

  • Wasaidie watoto kufikiria juu ya vitu wanavyofanya kumfuata Mwokozi. Kuimba “Mtafute Bwana Mapema,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 108, kunaweza kuwapa mawazo fulani. Waache wachore picha zao wenyewe wakifanya mambo haya.

Maandiko ni ya kweli.

Watoto wanaweza kupata ushuhuda kwamba maandiko ni ya kweli hata kabla hawajaweza kuyasoma. Unaposoma maandiko na watoto mwaka huu, unaweza kuwasaidia kujua wao wenyewe kwamba maandiko ni ya kweli.

Shughuli za Yakini

  • Waalike watoto waeleze kuhusu zawadi wanazozipenda walizopokea wakati wa siku za kuzaliwa au wakati mwingine. Leta nakala ya maandiko iliyofungwa kama zawadi, muache mtoto aifungue, na kushuhudia kwamba maandiko ni zawadi kwetu kutoka kwa Baba wa Mbinguni.

  • Onyesha watoto baadhi ya vitabu vyenye hadithi za ubunifu, na uwaulize kuhusu hadithi wazipendazo. Waonyeshe maandiko, na shuhudia kwamba maandiko yana neno la Mungu kwa ajili yetu na huelezea juu ya watu ambao kweli waliishi na matukio ambayo kweli yalitokea.

  • Shiriki jumbe zipatikanazo katika 2 Timotheo 3:15 na Moroni 10:3–4, ukiwasaidia watoto kurudia virai vichache. Wasaidie kuelewa kwamba wanaweza kujua maandiko ni ya kweli wao wenyewe.

  • Ficha picha ya Mwokozi, na wape watoto vidokezo vya kuwasaidia kuipata. Wasaidie watoto kuelewa jinsi kupekua maandiko kunaweza kutusaidia kumjua Yesu Kristo. Waache watoto wafiche kwa zamu picha na kutoa vidokezo kwa watoto wengine.

  • Imbeni pamoja “Mtafute Bwana Mapema,” na “Tafuta, Tafakari, na Sali.” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 108–9, na wasaidie watoto kubuni vitendo vinavyoendana na maneno. Shiriki na watoto andiko moja au mawili uyapendayo, na kuwaambia jinsi ulivyokuja kujua maandiko ni ya kweli. Kama watoto wana maandiko wayapendayo au hadithi za maandiko, waalike kushiriki.

Picha
mvulana anasoma maandiko

Watoto wanaweza kupata ushuhuda wao wenyewe wa kweli za kiroho.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

Yesu Kristo anataka nijifunze kumhusu Yeye na nimfuate Yeye.

Fikiria kuhusu jinsi umekuja kumjua Yesu Kristo. Ni kitu gani unachoweza kufanya ili kuwasaidia watoto kujifunza kuhusu na kumfuata Yeye?

Shughuli za Yakini

  • Waalike watoto wazungumze kuhusu rafiki wa karibu wanayemjua na kuelezea jinsi gani huyu mtu amekuja kuwa rafiki. Soma na jadili Yohana 5:39 na Yohana 14:15 ili kupata njia tunazoweza kuhisi tu karibu na Yesu. Waulize watoto kushiriki nyakati walipohisi kuwa karibu na Yeye.

  • Wapeleke watoto matembezini kuzunguka jumba la mikutano. Waalike watoto kunyoosha mikono yao watakapoona kitu fulani kwenye matembezi kinachowakumbusha juu ya njia ya wanayoweza kumfuata Mwokozi (kama vile kisima cha ubatizo au picha).

  • Imba pamoja na watoto “Njoo, Unifuate,” Wimbo, na. 116. Waalike watoto washiriki nyakati walipofuata mfano wa Mwokozi.

Ninaweza kujifunza maandiko kwa ajili yangu mwenyewe.

Unaposoma maandiko na watoto na kuwauliza maswali, unaweza kujenga kujiamini kwao kwamba waweze kujifunza kutoka katika maandiko na kupata hazina ya thamani ya maarifa.

Shughuli za Yakini

  • Soma kwa sauti Yohana 5:39 na Matendo ya Mitume 17:10–11, na uliza watoto ni kitu gani wameelewa kuhusu jinsi ya kujifunza maandiko.

  • Chagua maandiko rahisi machache, yenye nguvu kutoka katika Agano Jipya, andika kila moja kwenye kipande cha karatasi, na uzifiche karatasi. Tengeneza vidokezo vinavyoongoza watoto kwenye “kuwinda hazina” ndani ya darasa au jengo la kanisa ili kupata maandiko haya. Baada ya kupata kila andiko, jadili kile andiko linamaanisha na kwa nini ni hazina hasa.

  • Shiriki maandiko machache unayothamini na kuelezea kwa nini yana maana kwako. Kama darasa, wekeni orodha ya maandiko yenye thamani ambayo watoto wamepata katika Agano Jipya mwaka huu—nyumbani au wakati wa Msingi.

  • Kuwa na majadiliano na watoto kuhusu kwa nini wakati mwingine ni vigumu kusoma maandiko. Waombe watoto washiriki ushauri kwa kila mmoja kuhusu kujifunza maandiko. Waombe watoto waelezee uzoefu wowote mzuri waliopata kutokana na maandiko.

  • Wasaidie watoto kutengeneza kalenda rahisi ambazo wanaweza kutumia kuweka alama ya mara ngapi wamesoma maandiko. Kalenda hizi zinaweza kuwakumbusha kusoma maandiko kila siku.

Ninahitaji ushuhuda wangu binafsi.

Watoto unaowafundisha watahitaji ushuhuda wao wenyewe kama wataimarisha imani yao wakati shida inapokuja. Ni kitu gani unachoweza kufanya kuwahamasisha kujifunza ukweli wao binafsi?

Shughuli za Yakini

  • Shiriki hadithi ya wanawali kumi (ona Mathayo 25:1–13; ona pia “Sura 47: Wanawali Kumi.” Hadithi za Agano Jipya, 118–20. au video inayoambatana katika LDS.org). Waulize watoto jinsi gani shuhuda zetu ni kama taa? Kwa nini ni muhimu kuwa na shuhuda zetu wenyewe?

  • Jadili kile tunachoweza kufanya kuimarisha shuhuda zetu. Kwa mawazo, waalike watoto kupekua Yohana 7:17 na Moroni 10:3–5. Waalike wao washiriki vitu wanavyojua ni vya kweli.

  • Waombe watoto kukusaidia kubandika katika matofali ya kujengea virai vinavyoelezea mambo ya kufanya ili kujenga ushuhuda wetu, kama vile kuomba. Waache watoto wajenge muundo unaowakilisha ushuhuda kwa kutumia matofali.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ni kwa jinsi gani unaweza kuwahimiza watoto na wazazi wao kujifunza kutoka katika Agano Jipya nyumbani? Kwa mfano, unaweza kuwahimiza watoto kukumbuka mojawapo ya maandiko mliyojadili katika darasa (inaweza kusaidia kugawanya maandiko katika virai vifupi) na kushiriki mstari na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Badilisha shughuli kwa ajili ya umri wa watoto unaowafundisha. Watoto wadogo wanahitaji maelezo ya kina na kujifunza kutoka mbinu mbalimbali za kufundisha. Watoto wanapokomaa wanaweza kuchangia zaidi na kuwa bora katika kushiriki mawazo yao. Wape fursa ya kushiriki, kushuhudia, na kushiriki, na kutoa msaada kadiri inavyohitajika. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.

Picha
ukurasa wa shughuli: Ninajaribu Kuwa Kama Yesu

Chapisha