Njoo, Unifuate
Julai 22–28. Matendo ya Mitume 16–21 ‘Bwana Alituita Kuihubiri Injili’


“Julai 22–28. Matendo ya Mitume 16–21: ‘Bwana Alituita Kuihubiri Injili’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Julai 22–28. Matendo ya Mitume 16–21,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Paulo kwenye Kilima cha Maazi

Julai 22–28

Matendo ya Mitume 16–21

“Bwana Alituita Kuihubiri Injili”

Baada ya kusoma Matendo ya Mitume 16–21, fikiria jinsi ushawishi wa Roho na mawazo katika muhtasari huu vinavyoweza kukusaidia wewe kwa matayarisho ya somo. Tafuta ushauri kwenye “Kukidhi Mahitaji ya Watoto Wadogo” katika kitabu hiki cha kiada kwa ajili ya msaada wa ziada.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kukueleza jinsi Paulo alivyo kama wamisionari wa leo. Uliza, “Mmewahi wakati wowote kushiriki injili pamoja na mtu mwingine?”

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

Matendo ya Mitume 4:25–34

Wamisionari hufundisha watu kuhusu Yesu.

Je, watoto unaowafundisha wanajua wamisionari wanafanya nini? Unawezaje kuwasaidia watoto kuelewa kwamba wanaweza kushiriki injili pamoja na wengine?

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kuigiza Matendo ya Mitume 16:25–34 unapofanya muhtasari wa maelezo ya Paulo na Sila wakihubiri injili gerezani (ona pia “Sura 61: Paulo na Sila Gerezani,” Hadithi za Agano Jipya, 158–60, au video inayofanana kwenye LDS.org). Eleza kwamba wamisionari leo pia wanafundisha watu kuhusu Yesu na kuwasaidia kujitayarisha ili kubatizwa.

  • Tengeneza vibandiko vya majina vya kimisionari kwa ajili ya watoto kuvaa, na wasaidie kuandika majina yao kwenye vibandiko. Wafundishe watoto maelezo rahisi ya mafundisho ya injili ili waweze kushiriki pamoja na wengine, kama vile “Mungu ni Baba yetu wa Mbinguni anayetupenda,” “Mungu anasema kupitia nabii anayeishi,” au “Yesu Kristo ni Mwokozi Wetu.”

  • Waalike watoto kushiriki kila kitu kuhusu mtu wanaemjua ambaye yupo misheni. Wangeweza kuchora picha au kuandika barua kupeleka kwa mmisionari huyo.

Matendo ya Mitume 17:10–12

Maandiko yanashuhudia juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Ingawa baadhi ya watoto unaowafundisha wanaweza bado wasiweze kusoma, unaweza kuwasaidia kukuza upendo kwa maandiko na kuona jinsi yanavyomshuhudia Mwokozi.

Shughuli Yamkini

  • Weka nakala kadhaa za maandiko chumbani kote, na waache watoto wazitafute. Msaidie mmoja wa watoto kusoma kifungu kisemacho “Wali … yachunguza maandiko kila siku” (Matendo ya Mitume 17:11). Waalike watoto kuonyesha kila siku ya wiki kwenye kalenda wanaporudia kifungu hiki pamoja na wewe.

  • Ili kufundisha watoto kwamba maandiko yanashuhudia juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo, wasaidie kufunua kwenye sura katika maandiko, kama Matendo ya Mitume 17 au 18, na kutafuta mifano ya maneno Mungu au Bwana. Unaweza kutaka kuwekea alama maneno haya ili watoto waweze kuyapata kwa urahisi zaidi. Kila wakati wanapopata moja ya maneno haya, waalike kuelezea kitu wanachojua kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu kristo.

Matendo ya Mitume 17:22–31

Mimi ni mtoto wa Mungu.

Juu ya kilima cha Maazi, Paulo alifundisha kweli za msingi kuhusu asili ya Mungu, pamoja na kweli kwamba sisi ni watoto Wake na kwamba Yeye hawi “mbali na kila mmoja wetu” (Matendo ya Mitume 17:27). Unawezaje kuwasaidia watoto kujiona wako karibu na Baba yao wa Mbinguni?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kurudia kirai “sisi tu wazao wa Mungu” (Matendo ya Mitume 17:29), na eleza kwamba wazao maana yake mtoto. Toa ushuhuda wako kwa kila mtoto, mmoja mmoja, kwamba yeye ni mtoto wa Mungu. Waulize wanajisikiaje wanaposikia kwamba wao ni watoto wa Mungu. Waalike kushiriki jinsi wanavyojisikia kuhusu Baba yao wa Mbinguni.

  • Onyesha picha za watoto pamoja na famila zao (kama inawezekana, tumia picha za watoto katika darasa lako). Eleza kwamba sisi ni watoto wa mama na baba zetu, na sisi wote ni watoto wa kiroho wa wazazi wetu wa mbinguni.

  • Imbeni wimbo kuhusu Baba wa Mbinguni, kama vile “Najua Baba Yangu Anaishi” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto 5). Pamoja na msaada kutoka kwa watoto, andika maneno au chora picha ubaoni ambazo zinaonesha vitu tunavyojifunza kuhusu Baba wa Mbinguni kutoka kwenye wimbo huu.

  • Wasomee watoto maneno haya kutoka Matendo ya Mitume 17:27: “hawi mbali na kila mmoja wetu.” Zungumzia kuhusu wakati ulipojiona uko karibu na Baba wa Mbinguni, na waalike watoto wafanye hivyo hivyo.

Picha
mtu akimshika msichana mdogo

Kila mtu ni mtoto wa Mungu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

Matendo ya Mitume 16:14–15, 25–34; 18:7–8, 24–28

Ninaweza kuwa mmisionari sasa.

Unawezaje kuwasaidia watoto kuwa kama Paulo na kushiriki na wengine kile wanachojifunza kuhusu injili?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wasome Matendo ya Mitume 16:14–15, 25–34; 18:7–8, 24–28 na tengeneza orodha ya watu Paulo na Apollo walishiriki injili pamoja nao. Kisha waalike watengeneze orodha ya watu wanaoweza kushiriki nao injili. Waache watoto waigize jinsi ambavyo wangeweza kuwaambia watu hawa kuhusu Yesu Kristo au kuwaalika Kanisani. Unaweza pia kuwataka watoto kuandika maneno machache yanayobeba ushuhuda wa ukweli wa injili kwa watu hawa.

  • Waalike wamisionari, wamisionari waliorudi kutoka misheni zao, au wamisionari wa kata kutembelea darasa na kuzungumza kuhusu uzoefu wao kuhusu kuhubiri injili . Wahimize watoto kuuliza maswali kuhusu jinsi wanavyoweza kushiriki injili pamoja na wengine.

Matendo ya Mitume 17:2–4, 10–12; 18–28

Maandiko yanashuhudia juu ya Yesu Kristo.

Manabii wote washuhudia kuhusu Yesu Kristo. Unawezaje kuwafundisha watoto kumtafuta Yeye katika maandiko, hata kama hakutajwa kwa jina?

Shughuli Yamkini

  • Waache watoto wasome Matendo ya Mitume 17:2–4, 10–12; 18–28, na waalike kutafuta kitu gani kinafanana katika vifungu hivi. Kulingana na aya hizi, nini kiliwasaidia watu kuamini injili ya Yesu Kristo?

  • Waalike watoto kushiriki hadithi zao wanazozipenda kuhusu Yesu ambazo wamejifunza kutoka kwenye maandiko mwaka huu. Kwenye vipande vya karatasi, andika marejeo ya maandiko ambayo yanafundisha kuhusu Mwokozi, na vifiche humo chumbani. Kisha waalike watoto kuvitafuta. Wasaidie watoto kuyaangalia marejeo wanayoyapata, na watake kushiriki wao kwa wao kile kila andiko hufundisha kuhusu Yesu.

  • Waombe watoto kukusaidia kutengeneza chati rahisi ambayo wanaweza kutia alama wanaposoma kuhusu au kujifunza kuhusu Yesu kutoka katika maandiko. Ioneshe kila wiki kwa mwaka mzima, na wasaidie watoto kutafuta sehemu katika maandiko ambayo inafundisha kuhusu Yesu.

Matendo ya Mitume 17:22–31

Mimi ni mtoto wa Mungu.

Unawezaje kuwasaidia watoto kukumbuka kwamba wao ni watoto wa Mungu?

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto jiwe, na eleza kwamba katika siku za Paulo, watu waliabudu miungu waliyoitengeneza kutoka kwenye jiwe na vitu vingine. Waombe watoto kusoma Matendo ya Mitume 17: 27–29. Tunajifunza nini kuhusu Mungu kutoka aya hizi? Elezea kwamba wazao humaanisha watoto. Waulize watoto jinsi inavyowafanya wajisikie kujua kwamba wao ni watoto wa Mungu.

  • Waombe watoto kusoma Matendo ya Mitume 17: 27. Waombe watoto kuchora picha za njia wanazoweza “kujisikia baada” au kumtafuta Mungu. Lini wamejisikia kwamba Yeye “hayupo mbali [nao]”?

Picha
ikoni ya kujifunza

Wahimize Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kutafuta maandiko wiki hii ambayo yanafundisha kuhusu Yesu Kristo (hii inaweza kutokea katika wakati wao wa kujifunza maandiko binafsi au kifamilia). Wiki ijayo, waalike kushiriki kile walichokipata.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto kuwa wanafunzi wazuri. Azma yako katika kufundisha watoto sio tu kuwapa wao ukweli. Unatakiwa pia kuwasaidia kukua na kuwa watafutaji wa ukweli wa kujitegemea. Kwa mfano, badala ya kuwaambia tu watoto hadithi ya Paulo akihubiri juu ya kilima Maazi, unaweza kupanga shughuli, kama hizo zilizopendekezwa katika muhtasari huu, ambazo zitawasaidia wao wenyewe kugundua ukweli katika hadithi kwa ajili yao wenyewe.

Chapisha