Agano la Kale 2022
Februari 28–Machi 6. Mwanzo 28–33: “Hakika Bwana Yuko Mahali Hapa”


“Februari 28–Machi 6. Mwanzo 28–33: ‘Hakika Bwana Yuko Mahali Hapa’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Februari 28–Machi 6. Mwanzo 28–33,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Hekalu la Tijuana Mexico

Februari 28–Machi 6

Mwanzo28–33

“Hakika Bwana Yuko Mahali Hapa”

Unaposoma Mwanzo 28–33, tafakari jinsi hadithi na kanuni katika milango hii vinaweza kuwabariki watoto unaowafundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto warushiane mpira au kuuviringisha. Mara tu watoto wanapodaka mpira, waombe washiriki kitu wanachojifunza kutoka kwenye Agano la Kale, nyumbani au katika Msingi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mwanzo 28:10–22

Maagano yananisaidia kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Katika ndoto, Yakobo aliona ngazi inayoelekea mbinguni. Hatua kwenye ngazi zinaweza kuwakilisha maagano tunayofanya na Mungu, kwa sababu maagano haya husaidia kututayarisha kurudi kwenye uwepo Wake.

Shughuli Yamkini

  • Soma Mwanzo 28:12–13 kwa watoto. Fafanua kuwa hatua zilizo kwenye ngazi zinaweza kuwakilisha maagano ambayo yanatusaidia kurudi kwa Baba wa Mbinguni. Waalike watoto kujifanya wanapanda ngazi kama unavyozungumza kuhusu nyakati tunapoahidi kumtii Mungu, kama vile tunapobatizwa, kuchukua sakramenti, au kwenda Hekaluni. Wasaidie watoto wafikirie njia ambazo wanaweza kujiandaa kutengeneza maagano wanapobatizwa.

  • Soma Mwanzo 28:15 kwa watoto, sisitiza maneno “mimi nipo pamoja nawe” na “Sitakuacha.” Fafanua kuwa Mungu ameahidi kuwa nasi kila wakati tunapojaribu kuchagua haki. Waombe watoto kufikiria vitu wanavyoweza kufanya kila siku ili kumkumbuka Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Mwanzo 29:16–28

Tunapaswa daima kutimiza ahadi zetu.

Yakobo alikubali kufanya kazi kwa Labani kwa miaka saba ili aweze kumuoa Raheli binti wa Labani. Yakobo aliyatunza makubaliano haya, lakini Labani hakufanya hivyo. Fikiria kutumia hadithi hii kufundisha watoto kuhusu umuhimu wa kutunza ahadi zetu.

Shughuli Yamkini

  • Soma Mwanzo 29:18, 20 kwa watoto, na uwaelezee kwamba Yakobo alitunza ahadi yake ya kufanya kazi kwa miaka saba kwa Labani ili aweze kumuoa Raheli, ingawa huu ulikuwa ni muda mrefu wa kufanya kazi (ona pia “Jakobo na Familia yake,” katika Hadithi za Agano la Kale). Wasaidie watoto wafikirie ahadi ambazo wanaweza kufanya kwa watu wengine. Kwa nini ni muhimu kutunza ahadi zetu? Wasaidie kuelewa kwamba agano ni ahadi takatifu kati ya Mungu na kila mmoja wetu. Toa ushuhuda kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo daima wanatunza ahadi zao.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu uaminifu, kama vile “I Believe in Being Honest” au “Stand for the Right” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 149, 159).

Mwanzo 33:1–4

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaweza kunisaidia mimi na familia yangu.

Watoto wengi wanajua jinsi inavyokuwa kuwa na hasira na ndugu. Hadithi ya jinsi Yakobo na Esau walivyoshinda hasira kati yao inaweza kuwa ya kusisimua kwao.

Picha
Yakobo na Esau wakikumbatiana

Mchoro wa kukumbatiana kwa Yakobo na Esau, na Robert T. Barrett

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kukumbuka kwanini Esau alimkasirikia Yakobo (tazama Mwanzo 27:41 au “Yakobo na Esau,” katika Hadithi za Agano la Kale). Waombe watoto wakuonyeshe sura ya hasira inaonekanaje. Fafanua kwamba baada ya miaka mingi, Yakobo aliogopa kumtembelea Esau. Waombe watoto wakuonyeshe jinsi uso wa kutisha unavyoonekana. Je, tunapaswa kufanya nini wakati tunaogopa? Waalike watoto kujifanya wanasali wakati unasoma kile alichosema Yakobo katika sala yake (ona Mwanzo 32:11). Kisha soma katika Mwanzo 33:4 nini kilitokea wakati Esau alipomwona Yakobo. Waombe watoto wakuonyeshe jinsi sura za Yakobo na Esau zilivyokuwa zinaonekana wakati walipoonana tena.

  • Onyesha picha ya Yakobo na Esau inayopatikana katika muhtasari huu. Acha watoto waelezee wanachokiona kwenye picha. Waambie kwamba kumekuwa na hisia mbaya kati ya ndugu hawa wawili, lakini waliamua kusameheana. Wasaidie watoto wafikirie jinsi wanavyoweza kuonyesha upendo zaidi kwa mtu katika familia yao, kama vile Yakobo na Esau walivyoonyesha upendo baina yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mwanzo 28:10–22

Maagano yananisaidia kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Unaweza kutumia ndoto ya Yakobo ya ngazi kwenda juu mbinguni kuwafundisha watoto kwamba kuweka maagano yetu hututayarisha kuingia katika uwepo wa Mungu.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kusoma Mwanzo 28:10–15 na kisha kuchora picha ya ndoto ya Yakobo. Waombe washiriki picha zao. Elezea kwamba ile ngazi iliwakilisha njia kwa ajili ya Yakobo kurudi kwa Mungu. Je, Ni nini Mungu ametoa ili kutusaidia kurudi Kwake? (ona ukurasa wa shughuli ya wiki hii). Wakumbushe watoto maagano yao ya ubatizo. Je, ni kwa jinsi gani kuwa mnyenyekevu hutusaidia kumkaribia Mungu?

  • Onyesha picha ya hekalu, na andika kwenye ubao maneno makuu kutoka Mwanzo 28:15–17, kama vile: “Mimi nipo pamoja nawe,” “Bwana yuko mahali hapa,” “Nyumba ya Mungu,” au “Lango la mbinguni.” Waalike watoto kutafuta vifungu hivi vya maneno. Waambie watoto jinsi hekalu na maagano ya hekalu yanavyokusaidia kujisikia karibu na Bwana.

Mwanzo 29:16–30

Ninaamini katika kuwa mwaminifu.

Yakobo alitii ahadi yake ya kumtumikia Labani kwa miaka saba, lakini Labani akamdanganya. Unawezaje kutumia hadithi hii kuwasaidia watoto kuelewa umuhimu wa kuwa waaminifu hata kama wengine sio waaminifu?

Shughuli Yamkini

  • Someni pamoja Mwanzo 29:16–30, na wasaidie watoto kufupisha matukio katika mistari hii. Je, Yakobo alijibu vipi baada ya kudanganywa? Tunajifunza nini kutoka kwenye simulizi hii?

  • Kwenye ubao andika Kinatokea nini tunapokua sio waaminifu? na kipi kinatokea tuwapo waaminifu? Alika watoto kupata majibu kwa kusoma “Honesty and Integrity” (katika Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana [2011], 19).

Mwanzo 32:6–11; 33:1–4

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaweza kunisaidia mimi na familia yangu.

Esau alimkasirikia Yakobo, na Yakobo aliogopa kumuona tena Esau, hata baada ya miaka 20 ya kuwa mbali. Lakini Yakobo alisali kuomba msaada, na Esau aliweza kushinda hasira yake. Je, unawezaje kutumia hadithi hii kuwafundisha watoto umuhimu wa kupenda familia zetu?

Shughuli Yamkini

  • Waulize watoto wanakumbuka nini kuhusu uhusiano kati ya Yakobo na Esau (ona Mwanzo 27:41 au “Jakobo na Esau,” katika Hadithi za Agano la Kale). Fafanua kwamba baada ya kuwa mbali kwa karibu miaka 20, Yakobo alikuwa akienda kuonana na Esau tena. Someni pamoja Mwanzo 32:6–11. Je, Yakobo alijisikiaje? Ni nini alifanya kupata msaada? Shuhudia kwamba tunaweza kumuomba Baba wa Mbinguni msaada wakati mahusiano yetu ya familia ni magumu. Someni pamoja Mwanzo 33:1–4 kugundua jinsi Bwana alivyojibu sala ya Yakobo.

  • Shiriki uzoefu wa kibinafsi au hadithi kutoka kwenye jarida la Kanisa kuhusu jinsi ya kuonyesha upendo mkubwa katika familia zetu. Waalike watoto kushiriki uzoefu wao pia. Je, tunaweza kufanya nini wakati mtu wa familia ametukasirikia? Ili kujifunza kuhusu kile ambacho Mwokozi ametufundisha kufanya, ona Mathayo 5:43–45.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki ukurasa wa shughuli wa wiki hii na familia zao ili kuwasaidia kujifunza na kukumbuka ndoto ya Yakobo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia picha kusaidia watoto kuelewa hadithi za maandiko. Watoto mara nyingi hujifunza vizuri wakati wanaweza kutazama picha za hadithi za maandiko au mafundisho. Kwa mfano, ungeweza kuonesha picha kutoka kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia.

Chapisha