Agano la Kale 2022
Machi 21–27. Kutoka 1–6: “Nimekumbuka Agano Langu”


“Machi 21–27. Mwanzo 1–6; ‘Nimekumbuka Agano Langu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Machi 21–27. Kutoka 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Musa na kichaka kinachowaka moto

Musa na Kichaka Kinachowaka Moto, na Harry Anderson

Machi 21–27

Kutoka1–6

“Nimekumbuka Maagano Yangu”

Anza maandalizi yako kwa ajili ya kufundisha kwa kusoma Kutoka 1–6. Muhtasari wa Wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa sura hizi, na muhtasari huu unaweza kukupa mawazo ya kufundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Onyesha vitu kadhaa ambavyo vinahusiana na akaunti katika sura hizi – kwa mfano, kikapu kikubwa au mdoli wa mtoto. Alika watoto watumie vitu hivi kushiriki sehemu wanazopenda za hadithi ya Musa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Kutoka 1–2

Mungu anaweza kufanya kazi kupitia mimi ili kutimiza makusudi yake.

Musa alikuwa na jukumu kubwa katika kuikomboa Israeli kutoka utumwani. Lakini asingeweza kutimiza hii ikiwa mama yake, dada yake, binti wa Farao, na wanawake wengine waaminifu hawangemlinda na kumtunza.

Shughuli Yamkini

  • Tumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii na “Miriam” (katika Hadithi za Agano la Kale) kuwaambia watoto jinsi Yokebedi (mama wa Musa), Miriamu (dada yake), na binti wa Farao walivyomtunza Musa. Sisitiza kwamba kwa sababu ya hawa na wanawake na wengine waaminifu, Musa alihifadhiwa salama na siku moja angeongoza watoto wa Israeli kwenye usalama. Waalike watoto kuchora picha ya watu wanaowajali.

    Picha
    Mtoto Musa katika kikapu

    Musa katika Kikapu, © Providence Collection/licensed from goodsalt.com

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu huduma, kama vile “‘Give,’ Said the Little Stream” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 236). Wasaidie watoto kufikiria kuhusu mambo wanayoweza kufanya kusaidia wengine nyumbani, kanisani na shuleni.

Kutoka 3

Yesu atanisaidia mimi kufanya mambo mazuri.

Musa alihofia kama angeweza kuwakomboa Waisraeli kutoka Misiri. Lakini Bwana aliahidi kwamba atamsaidia Musa. Waaidie watoto kupata imani kwamba Mwokozi atawasaidia pia.

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto kuhusu jinsi Bwana alivyompa Musa kazi muhimu ya kufanya. Soma mistari iliyochaguliwa kwenye Kutoka 3, au soma “Musa Nabii” (katika Hadithi za Agano la Kale). Shiriki jinsi Musa alivyohisi (ona Kutoka 3:6, 11) na ni kitu gani Bwana alimwambia yeye (ona mistari ya 12 na 14). Waalike watoto warudie nawe kifungu cha maneno “Hakika nitakuwa nawe,” na shiriki wakati ambapo Bwana alikuwa na wewe wakati ulikuwa na jambo la muhimu kumfanyia.

  • Wasaidie watoto wafikirie hali ambazo wanaweza kuulizwa kufanya jambo ambalo linaonekana kuwa ngumu. Fafanua kwamba kama vile Yesu alivyomsaidia Musa, Yesu pia atawasaidia. Imbeni nyimbo kuhusu jinsi Yesu anavyotusaidia, kama vile “I Will Walk with Jesus” (ChurchofJesusChrist.org). Shuhudia kwamba Mwokozi atatusaidia wakati tunapokuwa na wasiwasi au tunaogopa.

  • Kata mioyo ya karatasi na uandike juu yake njia ambazo Bwana husaidia watoto. Weka mioyo ikiangalia kwenye sakafu. Waalike watoto wachukue zamu ya kuchagua mioyo, na uwasaidie kusoma yaliyoandikwa humo.

Kutoka 3:1–5

Ninaweza kuwa mnyenyekevu katika mahali patakatifu.

Tumia hadithi ya Musa na kichaka kinachowaka kuwasaidia watoto kuelewa kwa nini tunachukulia vitu vitakatifu kwa heshima.

Shughuli Yamkini

  • Soma Kutoka 3:1–5, na eleza kwamba Musa alionyesha kuheshimu kwa kuondoa viatu vyake. Tunafanya nini kuonyesha unyenyekevu kanisani? Imbeni wimbo kuhusu unyenyekevu, kama vile “Reverence Is Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,31). Wasaidie watoto kutambua maneno katika wimbo ambao unatufundisha jinsi ya kuonyesha unyenyekevu. Kwa nini Bwana anataka tuwe wanyenyekevu?

  • Onyesha picha kadhaa za hali ambazo tunapaswa kuwa waaminifu na zingine ambazo hatuhitaji kuwa wanyenyekevu, kama vile mkutano wa sakramenti, sala, uwanja wa michezo, na sherehe ya siku ya kuzaliwa. Waombe watoto wachambue picha ili kuonyesha wapi tunapaswa kuwa wanyenyekevu.

  • Waalike watoto kuchora picha zao, na waonyeshe picha zao unapojadili njia wanazoweza kuwa wanyenyekevu kwa sehemu tofauti za miili yao, kama vile macho, masikio, midomo, mikono na miguu yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Kutoka 1–2

Mungu hufanya kazi kwa kupitia kila mmoja wetu ili kutimiza madhumuni Yake.

Watu wengi walisaidia kutimiza kusudi la Mungu kwa kuhifadhi maisha ya mtoto Musa. Unawezaje kuwasaidia watoto unaowafundisha kuelewa jukumu muhimu ambalo sisi sote tunawajibika katika kutimiza mapenzi ya Mungu?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kushiriki kile wanachojua kuhusu Musa alivyokuwa mtoto. Tumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii na Kutoka 1:22; 2:1–10 ili kufanyia muhtasari wa hadithi ya utoto wa Musa. Soma marejeleo ya maandiko kwenye ukurasa wa shughuli, na uwaulize watoto ni nini kila mmoja wa wanawake alifanya kuokoa maisha ya Musa.

  • Waambie watoto kuhusu watu unaowapenda kwa sababu ya uaminifu wao katika kumtumikia Mungu na wale waliowazunguka, hata wanapotumikia kwa njia ndogo. Waalike watoto wazungumze kuhusu watu wanaowajua ambao wamemtumikia Mungu na wengine kwa uaminifu. Jukumu letu ni nini katika kazi ya Mungu?

Kutoka 3–4

Bwana atanisaidia kutimiza mapenzi Yake.

Musa alihisi kutofaa kwenye wito wake, lakini Bwana aliahidi kuwa atakuwa na Musa na kumsaidia. Je, masimulizi haya yanawezaje kuhamasisha watoto unaowafundisha?

Shughuli Yamkini

  • Tumia simulizi kwenye Kutoka 3; 4:1–17, acha watoto wachukue zamu kujifanya kuwa ni Musa. Ikiwezekana ,lete vifaa vya wao kutumia, kama tochi na mmea kuwakilisha kichaka kilichowaka moto.

  • Waombe watoto kusoma Kutoka 4:1; 4:1, 10 na ujue jinsi Musa alivyohisi kuhusu kumwuliza Farao awaachilie Waisraeli waende. Ni lini wamekuwa na hisia kama hizo? Je, ni ushauri gani ambao watoto wangemshauri Musa ili kumsaidia? Wasaidie kugundua jinsi Bwana alivyomtia moyo Musa (ona Kutoka 3:12; 4:2–9, 11–12).

  • Shiriki uzoefu wa wakati ulihisi Mungu alikuwa akikusaidia kutimiza mwito au kumtumikia kwa njia fulani. Waalike watoto kushiriki wakati ambao Bwana aliwasaidia.

Kutoka 3:1–5

Ninaweza kuwa mnyenyekevu katika mahali patakatifu.

Bwana alimtaka Musa aondoe viatu vyake kwenye kichaka kinachowaka moto kama ishara ya heshima na unyenyekevu. Unawezaje kutumia simulizi hii kuwafundisha watoto kuhusu unyenyekevu?

Shughuli Yamkini

  • Soma Musa 3:1–5, na waombe watoto wafupishe mistari hii kwa maneno yao wenyewe. Je, tunaweza kufanya nini ili kuonyesha unyenyekevu katika sehemu takatifu, kama kanisani au hekaluni? Wasaidie watoto kuunda “mifuko ya unyenyekevu” na kupeleka nyumbani iliyo na vipande vya karatasi na maoni kuhusu jinsi ya kuwa na unyenyekevu. Waalike kushiriki maoni haya na familia zao.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu unyenyekevu, kama vile “Reverence Is Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 31), na muombe kila mtoto aandike na ashiriki maana ya unyenyekevu kulingana na mistari ya wimbo.

  • Tumia picha ya Yesu akilisafisha Hekalu (Kitabu Cha Sanaa ya Injili, na. 51) kuhadithia hadithi katika Mathayo 21:12–13. Je, tabia ya Musa ilikuwaje katika Kutoka 3:1–5 tofauti na mtazamo wa wabadilishaji pesa? Je, Kwa nini Mwokozi anataka tufanye vitu vitakatifu kwa unyenyekevu?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ili kuwasaidia watoto kushiriki kile walichojifunza katika Kutoka 1–6, wahimize wachukue picha ya mmoja wa watu waliojifunza darasani ili kushiriki na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto wananufaika kutokana na marudio. Usiogope kurudia shughuli mara nyingi, hususan na watoto wadogo. Hii itawasaidia watoto kukumbuka kile unachofundisha.

Chapisha