Mafundisho na Maagano 2021
Januari 25–31. Mafundisho na Maagano 6–9: “Huyu Ni Roho wa Ufunuo”


“Januari 25–31. Mafundisho na Maagano 6–9: ‘Huyu Ni Roho wa Ufunuo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Januari 25–31. Mafundisho na Maagano 6–9,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
mwandishi akiandika kwenye karatasi

Januari 25–31

Mafundisho na Maagano 6–9

“Huyu Ni Roho wa Ufunuo”

Mafundisho na Maagano 6–9 hufundisha kanuni muhimu kuhusu kupokea ufunuo. Tumia kanuni hizi kwa kutafuta ufunuo kuhusu jinsi ya kuwasaidia washiriki wa darasa wajifunze kutoka sehemu hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kuwatia moyo washiriki wa darasa waweze kushiriki uzoefu wao wakijifunza Mafundisho na Maagano 6–9, unaweza kuwaalika wajadili, inavyofaa, misukumo yoyote ya kiroho waliyopokea wakati walikuwa wakijifunza. Je, ni jumbe gani Bwana alikuwa nazo kwa ajili yao?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 6; 8–9

Baba wa Mbinguni huzungumza nami kupitia “Roho wa ukweli.”

  • Bwana ana mengi ya kutufundisha sisi kuhusu ufunuo wa binafsi katika sehemu hizi, na huenda usiweze kufundisha yote katika somo moja. Labda yaweza kusaidia kuligawa darasa katika makundi matatu na ulitake kila kundi kuchunguza sehemu ya 6, 8, au 9, wakitafuta majibu ya maswali kama haya: Ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu huzungumza nasi? Tunawezaje kutambua ufunuo wa binafsi? Tunawezaje kujitayarisha kupokea ufunuo? Mtu mmoja toka kila kundi kisha anaweza kushiriki na darasa kile ambacho kundi lake limegundua. Unaweza pia kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wao kuhusu kutambua ufunuo wa binafsi. Kwa mfano, kuna kitu chochote katika Mafundisho na Maagano 6:22–24 ambacho kinatukumbusha kuhusu uzoefu ambao tumepata awali?

  • Kuzungumza kuhusu ufunuo wa binafsi yaweza kuwavunja moyo watu katika darasa lako ambao husali kwa ajili ya kupata mwongozo lakini hawahisi kwamba wanapokea chochote. Inaweza kuwasaidia kujua ya kwamba Oliver Cowdery alisumbuliwa na hisia sawa na hizo wakati aliposhindwa kutafsiri kwa urahisi kama alivyotarajia. Labda ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kuchunguza ushauri wa Bwana kwa Oliver katika sehemu ya 9. Ni jumbe zipi katika sehenu hii zinaweza kumsaidia mtu anayehisi kwamba Bwana hajibu sala zao? Maneno katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza pia kusaidia.

    Picha
    Oliver Cowdery

    Oliver Cowdery, na Lewis A. Ramsey

Mafundisho na Maagano 6–7

“Kama unavyotaka kwangu na itakuwa hivyo.”

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kufahamu matukio ya maneno kama vile taka katika sehemu za 6–7. Pengine washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kile walichojifunza kutokana na zoezi hilo, au mnaweza kuifanya shughuli hiyo pamoja kama darasa. Ni nini vitendo vyetu vya kila siku vinatufundisha kuhusu matamanio yetu? Ni kwa jinsi gani Mungu anaweza kutusaidia kubadili matamanio zetu?

Mafundisho na Maagano 6:29–37

Tunapomtazamia Bwana, Anaweza kutusaidia kushinda shaka na hofu.

  • Kwa nini wakati mwengine sisi “[huogopa] … kufanya mema”? (mstari wa 33). Labda washiriki wa darasa wangeweza kupendekeza baadhi ya sababu, pamoja na mawazo kutoka katika Mafundisho na Maagano 6:29–37 ambayo yanawatia moyo kutenda mema.

  • Ili kuanzisha mjadala kuhusu jinsi anavyotusaidia Yesu Kristo “kutokuwa na shaka, kutokuwa na hofu” (mstari wa 36), unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kuandika juu ya makaratasi baadhi ya vitu ambavyo watu wanaweza kuogopa. (Mzee Ronald A. Rasband alitoa mifano kadhaa katika ujumbe wake “Msifadhaike” [Ensign au Liahona, Nov. 2018, 18].) Kisha unaweza kusoma kwa sauti kubwa baadhi ya makaratasi haya na kujadili jinsi ambavyo Mwokozi na uwezo Wake wa upatanisho vinaweza kutusaidia wakati tuna hofu. Mafundisho na Maagano 6:29–37 ina umaizi fulani (ona pia 1 Yohana 4:18). Inamaanisha nini “mtegemeeni [Kristo] katika kila wazo”? (mstari wa 36). Ni kwa jinsi gani kufokasi huku juu ya Mwokozi kunatusaidia wakati tunapokumbana na shaka au hofu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Kuelewa jinsi ambavyo Baba wa Mbinguni hujibu sala.

“Maishani mwangu nimejifunza kuwa wakati mwingine huwa sipati jibu la sala kwa sababu Bwana anajua kwamba siko tayari. Wakati anapojibu, mara nyingi huwa ni ‘hapa kidogo na pale kidogo’ [2 Nefi 28:30] kwa sababu hayo yote ndiyo ninayoweza kustahimili au ninayoweza kutenda” (Robert D. Hales, “Kusubiri Kutoka kwa Bwana: Mapenzi Yako Yatimizwe,” Ensign au Liahona, Nov. 2011, 73).

“Ni nini utakachofanya wakati umejitayarisha kwa makini, umesali kwa bidii, umesubiri kwa muda unaofaa kwa ajili ya kupata jibu, na bado hujapata jibu? Unaweza taka kutoa shukrani wakati hilo linapofanyika, kwani ni ushahidi wa imani Yake kwako. “Wakati unapoishi kwa haki na uchaguzi wako unabaki vilevile katika mafundisho ya Mwokozi na unahitaji kutenda, endelea kwa kuamini. … Wakati unapoishi kwa haki na kutenda kwa imani, Mungu hatakuacha uendelee mbele zaidi bila msukumo wa kukuonya kama umefanya uchaguzi mbaya” (Richard G. Scott, “Kutumia Sala Karama ya Kiungu,” Ensign au Liahona, Mei 2007, 10).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Onyesha imani katika uwezo wa wanafunzi. Baadhi ya watu katika darasa lako wanaweza kosa imani katika uwezo wao wa kujifunza injili. Fikiria jinsi unavyoweza kuwapa moyo kwamba wanapojitahidi kujifunza wao wenyewe, Roho Mtakatifu atawafundisha. (Ona Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi, 29.)

Chapisha