Mafundisho na Maagano 2021
Machi 22–28. Mafundisho na Maagano 29: “Yesu Kristo Atawakusanya Watu Wake”


“Machi 22–28. Mafundisho na Maagano 29: ‘Yesu Kristo Atawakusanya Watu Wake,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Machi 22–28. Mafundisho na Maagano 29,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili

Picha
Yesu amesimama mbele ya watu waliopiga magoti

Kila Goti Litapigwa, na J. Kirk Richards

Machi 22–28

Mafundisho na Maagano 29

Yesu Kristo Atawakusanya Watu Wake

Njia muhimu zaidi ya kujiandaa kufundisha Mafundisho na Maagano 29 ni kujifunza sura hiyo kwa maombi na kutafuta mwongozo wa Roho. Fikiria njia tofauti za kualika Roho katika maisha yako, kama vile kufunga, kuhudhuria hekalu, au kuwatumikia wengine.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Katika Mafundisho na Maagano 29:5, Bwana aliwaambia watakatifu, “Inueni mioyo yenu na furahini.” Ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa washiriki kitu fulani walichojifunza katika kujifunza kwao binafsi au kama familia ambacho kinawasababisha “kuinua mioyo [yao] na kufurahi.”

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 29

Baba wa Mbinguni alitoa mpango kwa ajili ya kuinuliwa kwetu.

  • Mojawapo ya njia ya kuhimiza kujifunza nyumbani ni kuendeleza shughuli zinazopatikana katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia. Kwa mfano, unaweza kuorodhesha ubaoni sehemu za mpango wa wokovu, kama vile maisha kabla ya kuja duniani, Uumbaji, Upatanisho wa Yesu Kristo, na kadhalika. Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kitu ambacho walijifunza kutoka Mafundisho na Maagano 29 kuhusu sehemu hizi za mpango. Waweza hata kuwataka washiriki kile ambacho wangefundisha kutoka sehemu hii kwa mtu ambaye hajui kuhusu mpango wa Mungu.

Mafundisho na Maagano 29:1–8, 14–21

Yesu Kristo atawakusanya watu wake kabla ya Ujio Wake wa Pili.

  • Ili kuwasaida washiriki wa darasa kuelewa kwa nini Yesu Kristo anawakusanya watu Wake, ungeweza kuwaalika wasome mistari ya 1–8 na kujadiliana maswali kuhusu kukusanywa huko, kama vile: Ni kwa jinsi gani tumeona Kristo akitukusanya na kutulinda, kama vile kuku avikusanyavyo vifaranga vyake? Tunakusanyika namna gani kwa Mwokozi? (ona, kwa mfano, mstari wa 2). Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki namna walivyobarikiwa kwa kusanyika na kuabudu pamoja na washiriki wengine wa Kanisa.

    Picha
    kuku na vifaranga

    Mara Ngapi, na Liz Lemon Swindle

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiria kuhusu wajibu wao kumsaidia Baba wa Mbinguni kukusanya watoto Wake, unaweza kushiriki maneno ya Rais Russell M. Nelson katika “Nyenzo za Ziada.” Au ungeweza kuonyesha video “A Witness of God” (LDS.org). Je, tunajifunza nini kuhusu kukusanywa kutoka kwenye jumbe hizi? Ni kwa jinsi gani jumbe hizi zinaimarisha kile ambacho Bwana anasema katika Mafundisho na Maagano 29:1–8?

  • Baadhi ya matukio ya siku za mwisho yanayoelezewa katika Mafundisho na Maagano 29:14–21 yanaweza kuwa ya kuhuzunisha kwa washiriki wa darasa. Waache washiriki jinsi wanavyohisi. Je, ni kwa nini Bwana anatuonya kuhusu matukio haya? Ni kweli zipi za kuondoa shaka tunazojifunza kuhusu Mwokozi na kusanyiko kutoka kwenye mistari ya 1–8? Ni kwa jinsi gani kukusanyika kunatusaidia sisi kungojea matukio haya kwa imani badala ya hofu? Kama sehemu ya mjadala wenu, mnaweza kuimba wimbo wa injili kuhusu kukusanyika, kama vile “Israel, Israel, God Is Calling” (Nyimbo za Injili, na. 7), na kujadili wimbo huu unafundisha nini kuhusu kukusanywa kwa Israeli.

Mafundisho na Maagano 29:34–35

Kila amri ya Bwana ni ya kiroho.

  • Ingawaje amri zingine zinaweza kuonekana kuwa za muda, amri zote ni za kiroho kwa Bwana. Ili kuelewa ukweli huu, washiriki wa darasa wanaweza kusoma pamoja mistari ya 34–35 na kuorodhesha baadhi ya amri ubaoni, pamoja na kanuni za kiroho na baraka zinazohusiana na kila moja. Wanaweza kushiriki mifano kutoka katika maisha yao au kutoka kwenye maandiko ambayo imewasaidia kuona asili ya kiroho ya amri za Mungu. Ni kwa jinsi gani shughuli hii inaathiri jinsi tunavyozichukulia amri?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mafundisho na Maagano 29

Kushiriki katika kukusanya Israeli

Rais Russell M. Nelson alifundisha:

“Hakika hizi ni siku za mwisho, na Bwana anaharakisha kazi Yake ya kuikusanya Israeli. Kukusanywa huku ni kitu muhimu sana kinachofanyika duniani hivi leo. Hakulinganishwi na chochote katika ukubwa, hakulinganishwi na chochote katika umuhimu, hakulinganishwi na chochote katika utukufu. Na kama utachagua, kama unataka, unaweza kuwa sehemu kubwa yake. Unaweza kuwa sehemu kubwa ya kitu kikubwa, kitu kikuu, kitu kitukufu!

“Tunapozungumza kuhusu kukusanyika, kiurahisi tunamaanisha kanuni hii ya kweli: Kila mmoja wa watoto wa Baba wa Mbinguni, katika pande zote za pazia, anastahili kusikia ujumbe wa injili ya urejesho ya Yesu Kristo. Wanajiamulia wao wenyewe kama wanataka kujua zaidi. …

“Baba Yetu wa Mbinguni amehifadhi wengi wa roho zake wazuri—labda, naweza kusema, timu Yake bora zaidi—kwa ajili ya awamu hii ya mwisho. Roho hizo nzuri—wachezaji hao bora, hao mashujaa—ni wewe!” (“Hope of Israel” [ibada ya kote ulimwenguni kwa ajili ya vijana, Juni 3, 2018], ChurchofJesusChrist.org).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha kwa uwazi na kwa njia rahisi. Badala ya kujaribu kuburudisha darasa lako, fundisha mafundisho kwa uwazi na kwa njia rahisi. Unaweza kuamini ya kwamba “nguvu za neno la Mungu” zina “matokeo ya nguvu zaidi kwa akili za watu kuliko … kitu chochote kingine” (Alma 31:5).

Chapisha