Njoo, Unifuate
Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7: ‘Aliwafundisha Kama Mtu Mwenye Amri’


“Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7: ‘Aliwafundisha Kama Mtu Mwenye Amri’” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

“Februari 25–Machi 3. Mathayo 6–7,” Njoo,Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Yesu akifundisha pwani

Yesu Akifundisha Watu Pwani, na James Tissot

Februari 25–Machi 3

Mathayo 6–7

“Aliwafundisha Kama Mtu Mwenye Amri”

Unapojiandaa kufundisha, anza kwa kujiandaa mwenyewe. Jifunze Mathayo 6–7, na uandike misukumo wa kiroho. Hii itakusaidia kupokea ufunuo juu ya njia bora mno ya kukidhi mahitaji ya darasa lako. Kisha pekua muhtasari huu kwa mawazo ya kufundishia.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Himiza Kushiriki

Waalike washiriki wa darasa kushiriki vifungu vipi katika Mahubiri ya Mlimani wanavyohisi vinahitajika sana leo. Wahimize washiriki wa darasa kuongeza umaizi wao kwa wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mathayo 6–7

Kama tutasikia na kutenda juu ya mafundisho ya Bwana, maisha yetu yatajengwa juu ya msingi imara.

  • Ni mafundisho gani maalumu kutoka Mathayo 6–7 yatakuwa hasa yenye manufaa kwa wale unaowafundisha? Fikiria kuandika ubaoni marejeo kadha kutoka Mathayo 6–7 ambayo yana mafundisho haya. Washiriki wa darasa wanaweza kuchagua mojawapo ya marejeo kujifunza kimya kimya na kisha waandike ubaoni kweli zozote za kiroho wanazojifunza. Ni kwa jinsi gani mafundisho haya yameathiri maisha yetu?

  • Mwokozi alihitimisha mahubiri Yake na fumbo ambalo linaweza kusaidia darasa lako kuelewa vizuri umuhimu wa kuishi na mafundisho ya Mwokozi (ona Mathayo 7:24–27; ona pia Helamani 5:12). Kupata taswira ya fumbo hili, washiriki wa darasa wanaweza kufanya kazi pamoja kujenga msingi imara kwa kutumia matofali, vikombe, au vifaa vingine na kisha kupima uthabiti wa misingi yao. Labda wanaweza pia kuweka alama vifaa vyao vya ujenzi pamoja na vitu wanavyoweza kufanya kutumia mafundisho ya Mwokozi. Ni kwa jinsi gani kufanya vitu hivi kungetusaidia kustamili dhoruba za maisha?

Mathayo 6:5–13

Mwokozi alitufundisha jinsi ya kusali.

  • Kujifunza sala ya Bwana kunaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua jinsi wanavyoweza kuendeleza sala zao wenyewe kwa kufuata mfano wa Bwana. Unaweza kuwaalika waandike ubaoni virai kutoka Mathayo 6:9–13 (au Luka 11:1–4) ambavyo vinajitokeza kwao. Tunapotafakari maneno ya Mwokozi, tunajifunza nini kuhusu misimamo tunaotakiwa kuwa nayo tunaposali? Tunajifunza nini kuhusu aina ya vitu tungeomba na kuomba kuvihusu? Inaweza kuwa ya kuelemisha kwa washiriki wa darasa kufafanua baadhi ya misemo ya Mwokozi kama vitu wanavyoweza kusema katika sala zao wenyewe. Kwa mfano, “Tupe leo mkate wetu wa kila siku” ingeweza kufafanuliwa kama “Tafadhali nisaidie katika juhudi zangu za kuikimu familia yangu.”

  • Wale unaowafundisha wanaweza kunufaika kutoka kujifunza mifano mingine ya Mwokozi akisali kwa Baba Yake, kama Mathayo 26:36–42 na Yohana 17. Ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kujifunza baadhi ya vifungu hivi, kutafuta majibu kwa maswali kama “Tunajifunza nini kuhusu sala kutokana na njia Mwokozi alivyosali?” Kwa mifano mingine ya sala, ona Enoshi 1:3–17; Alma 31:26–35; 33:3–11.

  • Unao uzoefu wowote ambao unaweza kushiriki kuhusiana na sala? Kushiriki uzoefu wako kunaweza kuwatia moyo washiriki wa darasa kufanya vivyo hivyo. Rais Thomas S. Monson alishiriki uzoefu wake kadha wa kibinafsi uliohusiana na sala katika ujumbe wake “Fikiria Baraka” (Ensign, au Liahona, Nov. 2012, 86–89). Unaweza kujadili kanuni kutoka katika ujumbe huu na kutoka katika dondoo katika “Nyenzo za ziada.” Ingizo “Sala” katika Kamusi ya Biblia inaweza pia kuwa msaada.

Mathayo 7:7–11

Baba wa Mbinguni anajibu sala.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuimarisha imani yao kwamba Mungu atasikia na kujibu sala zao, unaweza kuandika omba, tafuta, na bisha ubaoni. Kisha waalike washiriki wa darasa kutafuta maandiko kwa mifano ya watu ambao “waliomba,” “walitafuta,” na “walibisha” (kwa mfano, ona 1 Nefi11:1; Etheri 2:18–3:6; Joseph Smith—Historia 1:11–17) Tunajifunza nini kutoka na mifano hii kuhusu kupata majibu kwa sala zetu?

  • Baadhi ya muktadha muhimu kwa Mathayo 7:7–11 unaweza kupatikana katika Tafsiri ya Joseph Smith ya Mathayo 7:17 (katika kiambatisho cha Biblia). Katika aya hizi, wafuasi wa Yesu walitumaini baadhi ya sababu watu wangeweza kutoa kwa kutotafuta ukweli kutoka kwa Baba wa Mbinguni. Unaweza kuwauliza washiriki wa darasa wafikirie wanaye rafiki ambaye hataki kutafuta mwongozo au baraka kutoka kwa Bwana. Washiriki wa darasa wanaweza kusema nini kumhimiza rafiki huyu? Ni kwa jinsi gani wanaweza kutumia maneno ya Mwokozi katika Mathayo 7:7–11?

Mathayo 7:15–20

Tunaweza kutambua manabii wa kweli na wa uongo kwa matunda yao.

  • Washiriki wa darasa lako wanaweza kuwa wamewahi kukumbana na falsafa za uongo na udanganyifu mwingine wa adui, ama kwenye mtandao au kutoka vianzo vingine. Wamewahi pia kusikia wengine wakiwalaumu watumishi wa Bwana. Unawezaje kuwasaidia kuelewa jinsi ya kutambua manabii na mafundisho ya uongo kutoka yale ya kweli? Unaweza kuonyesha vipande kadha vya matunda na kuuliza nini tunaweza kusadiki kuhusu miti inayoyazaa. Ni kwa jinsi gani zoezi hili linatusaidia kuelewa Mathayo 7:15–20? Mnaweza pia kusoma pamoja baadhi ya jumbe za hivi karibuni kutoka manabii wanaoishi. Ni “Matunda” au matokeo gani yanayofuata mazao ya ushauri wao?

    Picha
    tunda

    Tunaweza kuwajua manabii wa kweli kwa matunda yao.

  • Mathayo 7:15–20 inaweza kusaidia kujenga imani ya washiriki wa darasa katika kazi takatifu ya Nabii Joseph Smith. Ni matunda gani ya kazi Joseph Smith ambayo alitimiza? Kwa baadhi ya mawazo, ona ujumbe wa Mzee Neil L. Andersen “Joseph Smith” (Ensign au Liahona, Nov. 2014, 28–31). Ni kwa jinsi gani tunaweza kutumia analojia ya Mwokozi katika Mathayo 7:15–20 kutoa ushuhuda kwa marafiki zetu na familia kuhusu Nabii Joseph?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wiki hii, washiriki wa darasa wakijifunza zaidi ya miujiza Mwokozi aliyoifanya waalike watafakari mifano ya miujiza ya leo—kama ni mikubwa au midogo—ambayo wamepata uzoefu au walisikia kuihusu.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Mathayo 6–7

Nyimbo kwa matumizi ya darasani.

  • Ni kanuni gani zilizohusiana na sala washiriki wa darasa wanajifunza kutoka maneno ya wimbo “Prayer Is the Soul’s Sincere Desire”? (Wimbo, no. 146)

  • Kusoma, kuimba, au kusikiliza “Praise to the Man.” Nyimbo, no. 27, inaweza kuwasidia washiriki wa darasa kufikiria juu ya baadhi ya matunda ambayo tunaweza kujua kwamba Joseph Smith alikuwa nabii wa Mungu (ona pia M&M 135:3; “Joseph Smith” Mada za Injili, topics.lds.org).

Simulizi kuhusu sala.

Rais Boyd K. Packer alielezea juu ya sala ya familia yake waliofanya kabla hajaondoka kusafiri kwenda California. Daktari wa mifugo aliwaambia kwamba ng’ombe wao asingeweza kumaliza siku ile. “Kijana wetu mdogo alisema sala. Baada ya kumwomba Baba wa Mbinguni kumbariki Baba katika safari zake na kutubariki sisi wote,’ kisha alianza ombi la moyoni. Alisema,’Baba wa Mbinguni, tafadhali mbariki ng’ombe Bossy ili kwamba aweze kuwa sawa.’”

“Huko California, Nilisimulia juu ya tukio hili na kusema, ‘Lazima ajifunze kwamba hatupati kila kitu tunachoomba kirahisi namna ile’.

“Kulikuwa na somo la kujifunza, bali ilikuwa mimi niliyejifunza, sio mwanangu. Wakati niliporudi Jumapili usiku, Bossy ‘alikuwa salama’” (“Sala na Vishawishi,” Ensign au Liahona Nov. 2009, 45).

Kaka Mangal Dan Dipty, muumini wa Kanisa kutoka India, alisema: “Kama mtoto nilihudhuria Kanisa la Kilutheri la Ujerumani mara kwa mara. Tulikwenda milimani kusali pamoja mara kwa mara. Siku moja ya mvua, kila mtu katika kikundi cha maombi alilowa chapa chapa, na mmoja wa wahubiri alitoa sala hamasa akimsihi Bwana kuisitisha mvua. Kwa mshangao wetu mvua ilisita. Ule ulikuwa mwanzo wa imani yangu katika Mungu na sala” (“Safari Yangu kama Mwasisi kutoka India.” Ensign, Julai 2016, 67).

Kwa hadithi zingine kuhusu sala, ona sehemu ya Sauti za Watakatifu wa Siku za Mwisho la Ensign au Liahona.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Usiogope ukimya. “Maswali mazuri huchukua muda kuyajibu. Yanahitaji tafakari, kutafiti, na mwongozo. Muda unaotumia kungoja majibu kwa swali unaweza kuwa wakati mtakatifu wa kutafakari. Epukana na majaribu ya kukatiza muda huu haraka kwa kujibu swali lako mwenyewe au kwenda kwenye jambo lingine.” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 31).

Chapisha