Agano la Kale 2022
Septemba 19–25, Isaya 40–49: “Watulizeni Mioyo, Watu Wangu”


“Septemba 19–25, Isaya 40–49: ‘Watulizeni Mioyo, Watu Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Septemba 19–25, Isaya 40–49 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yesu akimponya kipofu

Yesu Akimponya Kipofu, na Carl Heinrich Bloch

Septemba 19–25

Isaya 40–49

“Watulizeni Mioyo, Watu Wangu”

Baadhi ya watu wanaweza kusitasita kushiriki fikra zao darasani kwa sababu wanahisi hawajui maandiko vizuri. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuhisi kwamba umaizi wao wa kiroho unathaminiwa?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Fikiria kuandika swali kama lifuatalo ubaoni: Je, Roho alikufundisha nini ulipokuwa unajifunza Isaiah 40–49? Washiriki wa darasa wangeweza kutafakari swali hili na kuandika majibu, na wachache wanaweza kushiriki fikra zao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Isaya 40–49

Yesu Kristo anaweza kutufariji na kutupatia matumaini.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kutafuta ujumbe wa faraja na matumaini katika Isaya 40–49 na kuorodhesha baadhi ya vifungu vya kuanzia. Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki ujumbe wo wote waliopata. Wahimize kuongea kuhusu kwa nini ujumbe huu uliweza kuwasaidia Wayahudi wakiwa utumwani na jinsi unavyoweza kutusaidia sisi leo. Ungeweza kuwaelekeza kwenye vifungu ulivyovipata katika kujifunza kwako binafsi. Je, Bwana anatutaka sisi tujue nini kuhusu Yeye? Je, Yeye hutufajiri kwa namna gani? Unaweza kuwakumbusha washiriki wa darasa kwamba “Bwana” katika Agano la Kale humrejelea Yehova, au Yesu Kristo.

  • Wimbo “How Firm a Foundation” (Wimbo, na. 85) unachukua maneno ya Isaya Isaya 41:10; 43:2–5; 46:4. Baada ya kusoma maandiko haya na kuimba aya husika za wimbo, washiriki wa darasa wanaweza kuongea kuhusu nyakati ambapo walihisi Bwana alikuwa pamoja nao na jinsi uzoefu wao ulivyowasaidia “kutoogopa.”

Picha
Yesu amekaa mchangani akiwafundisha watu

“Atalilisha kundi lake kama mchungaji” (Isaya 40:11).

Isaya 40:1– 3, 9– 11; 43:8–13; 48: 20– 21; 49:1–9

“Ninyi ni mashahidi wangu.”

  • Inamaanisha nini kuwa “mashahidi” wa Bwana? Washiriki wa darasa wanaweza kutafakari swali hili wanaposoma kifungu kimoja au zaidi kati ya vifuatavyo: Isaya 40:1–3, 9–11; 48:20–21; 49:1–9. Maelezo katika “Nyenzo za Zaida” yanaweza pia kutoa baadhi ya majibu. Je, ni “habari njema” zipi ambazo tunashiriki kama mashahidi wa Bwana? Katika mistari hii ni nini hutusaidia “kutoogopa” kushiriki ushahidi wetu? (Isaya 40:9). Washiriki wa darasa wangeweza kuongea kuhusu fursa walizonazo za kuwa mashahidi wa Bwana na ni kwa namna gani shuhuda zao zinaweza kuwabariki wengine.

  • Ili kusaidia washiriki wa darasa kutumia mafundisho katika Isaya 43:8–13, ungeweza kuwaalika wao kufikiria kwamba waliitwa kuwa mashahidi na kusimama katika mashtaka mahakamani. Katika mashtaka haya, Yesu Kristo anashitakiwa kwa kudai kama ilivyoandikwa katika Isaya 43:11. Kama tungeitwa kama mashahidi kuunga mkono madai ya Yesu (ona mstari wa10), tungetoa ushuhuda gani? Ni ushahidi gani kutoka katika maisha yetu ambao tungewasilisha?

Isaya 48–10; 49:13–16

Bwana anaweza kututakasa kupitia mateso yetu.

  • Labda washiriki wa darasa wanaweza kujadiliana jinsi maneno haya kutoka kwa Mzee Quentin L. Cook yanavyotusaidia kuelewa Isaya 48:10: “Sifa za tabia na haki ambazo hufuliwa katika tanuri la mateso hutukamilisha na kututakasa” (“Nyimbo Ambazo Hawakuweza Kuimba,” Ensign au Liahona, Nov. 2011,106). Wanaweza pia kuzungumza kuhusu jinsi “tanuri la mateso” linavyowasaidia kuwasafisha kiroho. Ni kwa jinsi gani Isaya 49:13–16 hutusaidia sisi wakati tunapoteseka? Ona pia video “The Refiner’s Fire” (ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Kusimama kama shahidi.

Rais Margaret D. Nadauld alielezea kile inachomaanisha “kusimama kama mashahidi wa Mungu nyakati zote, na katika vitu vyote na katika mahali popote” (Mosia 18:9):

“Katika kusimama kama shahidi nyakati zote, tunaahidi kumpenda Bwana, kumheshimu Yeye nyakati zote—mchana na usiku, msimu wa jua na msimu wa baridi, wakati wa furaha na wakati wa huzuni—kumpenda Bwana na kuacha upendo uonyeshe namna tunavyoishi.…

“Kusimama kama shahidi katika nyakati zote humaanisha mambo yote —mambo makubwa, mambo madogo, katika mazungumzo yote, katika mizaha, katika michezo inayochezwa na katika vitabu tunavyosoma na muziki tunaosikiliza, katika mambo yote tunayounga mkono, katika huduma tunayotoa, katika mavazi tunayovaa, katika marafiki tulionao.…

“Hatimaye, sisi tunasema kwamba tulisimama kama shahidi katika mahali pote. Hiyo inamaanisha sio tu katika sehemu za umma bali katika sehemu za faraghani, sirini, sehemu za gizani, katika sehemu za nuru; kanisani, shuleni, nyumbani, au ndani ya magari; sehemu za milimani au sehemu za pwani; mtaani au bustanini.…

“Unapofikiria juu ya ukuu wa zawadi ya [Mwokozi] kwetu, ni kitu gani kidogo tunachoweza kumfanyia Yeye na Baba yetu wa Mbinguni ambaye alimtuma? Tunaweza kusimama kama mashahidi wa upendo Wake nyakati zote, katika vitu vyote, na katika mahali popote” (“Simama kama Shahidi,” Ensign, Mei 2000, 93,95).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Alika kujifunza kwa bidii. “Wanafunzi hatimaye wanawajibika kwa kujifunza kwao wenyewe. Zingatia jinsi unavyoweza kuwasaidia wanafunzi kukubali na kutekeleza wajibu huu” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,29).

Chapisha