Rafiki
Mfano Mzuri
Machi 2024


“Mfano Mzuri,” Rafiki, Machi 2024, 32.

Rafiki kwa Rafiki

Mfano Mzuri

Kutoka kwenye Mahojiano na Haley Yancey.

Nilipokuwa mtoto sikuwa muumini wa Kanisa. Nilipokuwa mtu mzima na kuwa mfanya biashara ndipo nilipobatizwa.

Baba yangu alikuwa pia mfanya biashara. Alikuwa na wasiwasi sana wakati nilipojiunga na Kanisa. Alisema, “Hunywi pombe tena. Hiyo itakuwa vigumu katika mikutano ambapo kila mtu anakunywa pombe.”

Lakini mimi sikuwa na wasiwasi. Niliamua kwamba wakati mtu atakaponipa pombe , ningesema, “Hapana, asante.” Kisha ningeagiza kitu kingine.

Miaka ilipita, na nilifanya hivi mara nyingi sana. Baada ya muda, wafanyakazi wenzangu waligundua. Kama ningepewa pombe, wao walisema, “Mathias hanywi pombe. Mletee kitu kingine.” Wengi wao zaidi waliacha kuagizia pombe pia. “Hata mimi sitaki,” walisema.

Wakati mmoja wageni fulani walikuja kwenye mkutano. Wao pekee ndiyo walikuwa wanakunywa pombe.

Waliniuliza mimi, “Kwa nini hakuna mtu anayekunywa pombe? Wote ni waumini wa Kanisa lako?”

“Hapana,” nilisema.

Mimi sikuwahubiria wafanyakazi wenzangu kuhusu Neno la Hekima. Nilikuwa tu thabiti katika imani yangu, na wao walitambua mfano wangu.

Wewe pia unaweza kuwa mfano mzuri. Wengine watatambua wakati unapochagua kilicho chema. Unaweza tu kuwasaidia wao kwa kuishi injili.

Picha
alt text

Kielelezo na Matt Smith

Chapisha