2022
Kumwona Zaidi Yesu Kristo Katika Maisha Yetu—Dondoo
Novemba 2022


“KumWona zaidi Yesu Kristo katika Maisha Yetu—Dondoo,” Kwaajili ya Nguvu kwa Vijana, Nov. 2022.

Kumwona Zaidi Yesu Kristo Katika Maisha Yetu

Dondoo

Picha
Nukuu ya Browning kwenye bango

Pakua PDF

Ili kutusaidia kubaki thabiti na kuelekea katika njia sahihi, Mwokozi anatualika tuyaone maisha yetu kupitia Yeye ili tumwone Yeye zaidi katika maisha yetu. …

Kama mfuasi wa mwanzo wa injili, nilikutana na wengi ambao waliona na kushuhudia mabadiliko katika tabia, desturi na chaguzi zangu baada ya kujiunga na Kanisa. …

… Kupitia juhudi kubwa ya kumwangalia Yeye na kwa ajili ya Yesu Kristo katika kila wazo na tendo langu, macho yangu yalitiwa nuru, na ufahamu wangu ulihuishwa kutambua kwamba Yesu Kristo alikuwa akiniita “nije Kwake.” …

Nilijifunza wakati huo, kama nijuavyo sasa, kwamba Mwokozi wetu, Yesu Kristo, anaelekeza miguu yetu kwenye nyumba za mikutano kila wiki ili kushiriki sakramenti Yake, kwenye nyumba ya Bwana kufanya maagano Naye, kwenye maandiko na mafundisho ya manabii ili kujifunza Maneno yake. Anaelekeza vinywa vyetu kushuhudia juu Yake, mikono yetu kuinua na kuhudumu kama vile ambavyo Yeye angeinua na kuhudumu, macho yetu kuuona ulimwengu na kila mmoja kama Yeye anavyoona—“vitu vilivyo, na … vile vitu vitakavyokuwa” [Yakobo 4:13]. Na tunapomruhusu Yeye atuelekeze katika mambo yote, tunapokea ushuhuda kwamba “vitu vyote vinaonyesha kwamba kuna Mungu” [Alma 30:44], kwa sababu tunapo mtafuta Yeye tutampata Yeye.

Chapisha