Njoo, Unifuate 2024
Machi 4–10: “Tunafurahia Katika Kristo.” 2 Nefi 20–25


“Machi 4–10: ‘Tunafurahia Katika Kristo.’ 2 Nefi 20–25,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Kitabu cha Mormoni 2024 (2024)

“Machi 4–10. 2 Nefi 20–25,”Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: 2024 (2024)

Picha
familia ikijifunza

Machi 4–10: “Tunafurahia Katika Kristo”

2 Nefi 20–25

Maandishi ya Isaya yanajumuisha maonyo makali, lakini pia yanatoa tumaini na furaha. Hii ni sababu moja ya kwa nini Nefi aliyajumuisha katika kumbukumbu zake: “naandika baadhi ya maneno ya Isaya,” alisema, “ili wowote … wa watu wangu watakaoona maneno haya wangeinua mioyo yao na kufurahia” (2 Nefi 11:8). Kwa namna fulani, mwaliko wa kusoma maandishi ya Isaya ni mwaliko wa kufurahia. Unaweza kufurahia, kama Nefi alivyofurahia, katika unabii wa Isaya kuhusu kukusanywa kwa Israeli, ujio wa Masiya na amani ya milenia iliyoahidiwa kwa wenye haki. Unaweza kufurahia kuishi katika siku iliyotabiriwa wakati ambapo Bwana “atawatwekea mataifa bendera na kuwakusanya watu wa Israeli waliofukuzwa” (2 Nefi 21:12). Wakati unapokuwa na kiu ya haki, unaweza “kwa furaha … kuteka maji kutoka visima vya wokovu” (2 Nefi 22:3). Kwa maneno mengine, unaweza “kufurahia katika Kristo” (2 Nefi 25:26).

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

2 Nefi 21–22

Ninaweza kupata amani katika Kristo.

Watoto wa Lehi walikuwa na tatizo la mabishano. Tatizo hilo lilikua baya sana katika vizazi vya baadaye, ikipelekea mfarakano, utumwa, huzuni na uharibifu. Na mabishano yanaendelea kuwa shida hivi leo.

Pamoja na hayo yote akilini, tafakari unabii katika 2 Nefi 21–22. Fikiria jinsi mwokozi anavyotimiza unabii huu. Utabiri kwamba mbwa mwitu “ataishi na mwana kondoo” una maana gani kwako? (2 Nefi 21:6). Tafakari kile uchachoweza kufanya kuwa mpatanishi.

Ona Dale G. Renlund, “Amani ya Kristo Huondoa Uadui,” Liahona, Nov. 2021, 83–85.

2 Nefi 21:9–12

Bwana anawakusanya watu Wake.

Nefi na familia yake walikuwa mashahidi wa utawanywaji wa Israeli (ona 2 Nefi 25:10). Sasa unaweza kushiriki kwenye ukusanyaji wa Israeli (ona 2 Nefi 21:12). Wakati unaposoma 2 Nefi 21:9– 12, fikiria jinsi unavyoweza kusaidia kutimiza unabii unaoelezwa na mistari hii.

Kwa mfano, wakati ukisoma kuhusu “bendera” (kiwango) ambayo itanyanyuliwa ili kuwakusanya watu wa Mungu, fikiria kuhusu jinsi ambayo umeona Mungu akiwakusanya watu Wake, kimwili na kiroho. Je, nini huwavutia watu kwa Bwana na Kanisa Lake.

Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya kipi ili kusaidia kuwakusanya watu wa Mungu?

2 Nefi 23–24

Mambo ya ulimwengu wa Babeli yataanguka.

Ufalme wa Babeli ulikuwa tishio kwa nguvu, kisiasa na kijeshi kwa Israeli ya kale. Lakini kwa watu wa Nefi—na kwetu sisi leo—tishio kubwa ni kile ambacho Babeli inawakilisha: mambo ya ulimwengu na dhambi. Fikiria jinsi ambavyo maonyo kwenye 2 Nefi 23–24 yangeweza kuathiri watu ambao wanaogopa au kutamani au kuamini utajiri na nguvu za Babeli (ona, kwa mfano 23:6–9, 11, 19–22; 24:10–19). Ni baadhi ya vitu gani sawa na hivyo ambavyo tunaweza kuviogopa au kuvipenda au kuvitumainia leo? Je, unahisi ujumbe wa Bwana kwako unaweza kuwa upi katika milango hii? Fikiria kuhusu jinsi unavyoweza kuonesha kwamba “unafurahia katika ukuu wa [Bwana]” (2 Nefi 23:3).

Picha
ikoni ya seminari

2 Nefi 25:19–29

“Tunazungumza kuhusu Kristo … Tunafurahia katika Kristo.”

Nefi alikuwa muwazi kuhusu kushiriki imani yake—hasa ushuhuda wake juu ya Yesu Kristo. Katika kujifunza kwako kote 2 Nefi 25, fikiria kuhusu matamanio ya Nefi “kuwashawishi watoto [wake] … kuamini katika Kristo na kupatanishwa kwa Mungu” (mstari wa 23). Je Nefi alitaka watu wajue nini kuhusu Mwokozi? (ona mistari 12–13, 16). Je, ni kwa namna ipi Nefi alijaribu kuwashawishi watu wamwamini Mwokozi? (ona mistari 19–29). Tilia maanani vifungu vya maneno katika milango hii ambavyo vinakushawishi wewe umwamini na umfuate Yesu Kristo.

Baadhi yetu tunaweza tusihisi ujasiri kama alivyokuwa Nefi kuhusu kuzungumza juu ya Kristo. Lakini unaweza kupata kitu fulani kwenye mafundisho ya Nefi kwenye 2 Nefi 25:23–26 ambacho kitakupa msukumo kuzungumza na wengine kuhusu Mwokozi kwa uwazi zaidi. Kwa mfano, tamko la Nefi “Tunafurahia katika Kristo” lingeweza kukusukuma ufikirie kuhusu jinsi ambavyo Mwokozi huleta shangwe—na jinsi unavyoweza kuishiriki shangwe hiyo na wengine.

Katika ujumbe wake “Tunazungumza Kuhusu Kristo” (Liahona, Nov. 2020, 88–91), Mzee Neil L. Andersen anapendekeza namna ambavyo tunaweza kuzungumza kwa uwazi zaidi kuhusu Kristo mahali mbalimbali. Ni pendekezo lipi ambalo linakuvutia sana? Ni fursa zipi unazo za kuzungumza kuhusu Kristo pamoja na wengine?

Je, unahisi kuvutiwa kuwaambia nini wengine kuhusu Yesu Kristo? Kama unahitaji mawazo ya namna ya kufanya hivyo ungeweza kusoma “Kristo Aliye Hai: Ushuhuda wa Mitume” (Gospel Library). Wimbo wa Dini kama “Kristo Mwokozi” (Nyimbo za Dini, na. 66) ungeweza kutoa mawazo zaidi.

Kwa mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la Liahona na magazeti ya Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana.

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

2 Nefi 21:1–5

Yesu Kristo atahukumu kwa haki.

  • Ili kuwasaidia watoto wako wapate taswira ya mistari hii, ona kama unaweza kupata mti ambao umekatwa au tawi linaloota kutoka kwenye mti (au tumia picha iliyopo hapa chini). Kama “tawi” kwenye 2 Nefi 21:1 humwakilisha Yesu Kristo, je, ni kipi mistari 2–5 hutufundisha Kumhusu?

Picha
mmea mdogo ukikuwa kutoka kwenye kisiki cha mti

2 Nefi 21:6–9

Yesu Kristo hutoa amani na shangwe.

  • Je, 2 Nefi 21:6–9 hufundisha nini kuhusu kile kinachoweza kutokea wakati kila mtu anapomfuata Mwokozi? (ona pia 4 Nefi 1:15–18). Ni kwa jinsi gani tunaweza kuzifanya nyumba zetu ziwe zaidi kama hii? Watoto wako wangeweza kufurahia kuangalia picha ya wanyama waliosemwa kwenye mistari 6–7—wanyama ambao mara nyingi ni maadui lakini hawatadhuriana wakati Yesu atakapokuja tena (ona ukurasa wa shughuli ya wiki hii). Watoto wako wangeweza kuchora picha zao wenyewe na wanyama hawa wakiishi kwa amani pamoja na Yesu.

2 Nefi 21:11–1222

Bwana anawakusanya watu Wake.

  • Isaya alisema kwamba Bwana “atawatwekea mataifa bendera” ili kuwasaidia watu wakusanyike Kwake (ona 2 Nefi 21:11–12). Wasaidie watoto wako waelewe kwamba ensign ni kama bendera. Pengine wangefurahia kuchora bendera zao wenyewe. Wangeweza kujumuisha picha au maneno ambayo yanawakilisha sababu za kwa nini wamekuja kwa Kristo na Kanisa Lake. Waruhusu wazungumze kuhusu bendera zao, na wasaidie wafikirie jinsi wanavyoweza kuwasaidia wengine “kukusanyika” kwa Kristo.

  • Baada ya kusoma 2 Nefi 22:4–5 pamoja, zungumza na watoto wako kuhusu baadhi ya “vitu vyema” Bwana alivyotenda. Ni zipi baadhi ya “kazi za Bwana miongoni [mwetu]” ambazo tunaweza kuzitangaza? Ili kuwasaidia watoto wako watafakari swali hili mnaweza kuimba pamoja wimbo kuhusu Mwokozi, kama vile “Kristo Mwokozi” (Nyimbo za Dini, na. 66). Kisha mngeweza kufanya zamu kukamilisha sentensi kama hii: “Ninaamini katika Kristo; Yeye .” Je, tunawezaje kuwasadia wengine wajue kuhusu kile ambacho Mwokozi amekifanya kwa ajili yetu?

2 Nefi 25:26

“Tunafurahia katika Kristo.”

  • Unawezaje kuwasaidia watoto wako “wafurahie katika Kristo”? Pengine ungesimulia hadithi kuhusu Yesu Kristo akileta furaha kwa wengine au ungeweza kuonesha video kama vile “Jesus Heals a Man Born Blind” au “Suffer the Little Children to Come unto Me” (Gospel Library). Watoto wako wangeweza kuonesha nyakati za shangwe zilizo kweye hadithi au video. Kisha, unaposoma 2Nefi 25:26, wangeweza kuzungumza kuhusu kwa nini “wanafurahia katika Kristo.”

Shuhudia juu ya Kristo. Usidhani kwamba familia yako inafahamu jinsi unavyohisi kuhusu Mwokozi. Waambie na ruhusu hisia zako kuhusu Mwokozi zishawishi jinsi unavyochangamana nao.

Kwa ajili ya mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la gazeti la Rafiki.

Picha
wamisionari wakiifundisha familia

Nitakwenda Utakako, na Ramon Ely Garcia Rivas

Chapisha