Njoo, Unifuate 2024
Machi 11–17: “Kazi ya Kushangaza na ya Maajabu.” 2 Nefi 26–30


“Machi 11–17: ‘Kazi ya Kushangaza na ya Maajabu.’ 2 Nefi 26–30,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Kitabu cha Mormoni 2024 (2024)

“Machi 11–17. 2 Nefi 26–30,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: 2024 (2024)

Picha
Yesu akimfikia mwanamke

Atakuongoza kwa Mkono Wake, na Sandra Rast

Machi 11–17: “Kazi ya Kushangaza na ya Maajabu”

2 Nefi 26–30

“Nawatolea unabii kuhusu siku za mwisho,” Nefi aliandika (2 Nefi 26:14). Kwa maneno mengine, alikuwa anaandika kuhusu siku zetu. Na kuna sababu ya kuwa na wasiwasi kuhusu kile alichokiona: watu wakikataa nguvu na miujiza ya Mungu, wivu na mabishano vikienea. Lakini pamoja na hizi “kazi za giza” za siku za mwisho (2 Nefi 26:10, 22) zikiongozwa na adui, Nefi pia alizungumzia “kazi ya kushangaza na ya maajabu” ikiongozwa na Bwana Mwenyewe (2 Nefi 27:26). Kiini katika kazi hiyo kingekuwa kitabu—kitabu ambacho kinafichua uwongo wa Shetani, na kinachowakusanya wenye haki. Kitabu hicho ni Kitabu cha Mormoni, kazi ya kushangaza ni kazi ya Kanisa la Bwana katika siku za mwisho, na maajabu—ni kwamba angalau kwa sehemu—kwamba Mungua anatualika sote, licha ya udhaifu wetu, tushiriki kwenye kukusanya.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

2 Nefi 26–27; 29–30

Mungu alikiandaa Kitabu cha Mormoni kwa ajili ya siku zetu.

Katika 2 Nefi 26–27, Nefi alichukua zaidi kutoka utabiri wa awali wa Isaya (ona Isaya 29), na akautumia kwa watu wake na kumbukumbu yao—Kitabu cha Mormoni. Nefi alijua kupitia ufunuo, hata kabla ya Kitabu cha Mormoni kumalizika kuandikwa, kwamba siku moja “kitakuwa cha thamani kuu kwa watoto wa watu” (2 Nefi 28:2). Kwa nini Kitabu cha Mormoni ni cha thamani kuu kwako? Fikiria kuhusu swali hili unaposoma 2 Nefi 29–30. Ni zipi kazi za “kushangaza” (2 Nefi 27:26) ambazo Mungu anatimiza ulimwenguni na katika maisha yako kupitia Kitabu cha Mormoni?

Ona pia Joseph Smith—Historia ya 1:62–65.

Picha
ikoni ya seminari

2 Nefi 26:23-33

Yesu Kristo anatualika sisi sote tuje Kwake.

Kuna kweli nyingi nzuri zinazopatikana katika 2 Nefi 26:23–24. Kwa mfano, ungeweza kufikiria kuhusu kile ambacho Yesu Kristo amekifanya “kwa ajili ya manufaa ya ulimwengu”—na manufaa yako. Jinsi gani Yeye “anawavuta wanadamu wote”—na wewe—“kwake”? Unahisi kuvutiwa kufanya kipi ili kuitikia dhihirisho Lake la upendo?

Endelea kusoma na kutafuta kweli kuhusu Mwokozi kwenye mistari 25–33. Zingatia hususani kwenye mialiko Yake. Je, ungefanyaje ufupisho wa ujumbe wa Yesu Kristo kwako kwa kutumia sentensi moja? Wimbo wa Dini kama “Njoo kwa Yesu” (Nyimbo za Dini, na. 59 ungeweza kufungua akili yako kwa ajili ya misukumo ya nyongeza.

Fikiria jinsi ambavyo mistari hii ingeweza kuathiri namna unavyochangamana na watu na kuwaalika waje kwa Kristo. Ungeweza kupata baadhi ya mawazo kutoka kwenye ujumbe wa Mzee D. Todd Christofferson, “Mafundisho ya Kuwa Sehemu Ya” (Liahona, Nov. 2022, 53–56).

Ona pia 3 Nefi 18:30–32; Dallin H. Oaks, “Je, Mwokozi Amefanya Nini kwa ajili Yetu?,” Liahona, Mei 2021, 75–77; Mada za Injili, “Kuwa wa Kanisa la Yesu Kristo,” Gospel Library.

Usiogope ukimya. Maswali mazuri huchukua muda kuyajibu. Yanahitaji kutafakari, kutafiti na mwongozo wa kiungu. Muda unaotumia kungoja majibu kwa swali unaweza kuwa wakati mtakatifu wa kutafakari. Epuka majaribu ya kukatiza muda huu haraka kwa kuendelea na sehemu nyingine.

2 Nefi 28

Shetani anatafuta kudanganya.

Wingi wa uwongo na mbinu za Shetani zinafichuliwa katika 2 Nefi 28. Zitafute kwenye mistari 6, 8, 21–23, 29. Je, kwa nini unahitaji kujua kuhusu uwongo wa Shetani? Utafanya nini wakati adui atakapojaribu kukudanganya?

Yalioorodheshwa hapa ni baadhi ya maandiko ambayo yanakataza uwongo wa Shetani? Anagalia kama unaweza kuoanisha mafundisho ya kweli kwenye mistari hii na mafundisho ya uwongo Nefi aliyotuonya kuhusu hayo kwenye 2 Nefi 28

Gary E. Stevenson, “Usinidanganye,” Liahona,Nov. 2019, 93–96

2 Nefi 28:27–3129

Mungu anaendelea kutoa ufunuo ili awaongoze watoto Wake.

Kama Watakatifu wa Siku za mwisho, tumebarikiwa kwa wingi wa neno la Mungu. Na bado kama Nefi alivyoonya, kamwe tusihisi kwamba “tunalo la kutosha!” Unaposoma maonyo katika 2 Nefi 28:27–31 na 2 Nei 29, fikiria kuhusu maswali kama haya:

  • Je, Bwana anataka nihisi na nitendevipi kuhusu neno Lake?

  • Kwa nini watu nyakati zingine “wana hasira” kuhusu kupokea ukweli zaidi kutoka kwa Mungu? (2 Nefi 28:28). Je, mimi nimewahi kuhisi namna hii? Kama ndivyo, Je nawezaje kubadilika?

  • Inamaanisha nini kupokea neno la Bwana? Ni kwa jinsi gani naweza kumuonesha ya kwamba nataka kupokea ziada ya neno Lake?

Kwa mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la Liahona na magazeti ya Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana.

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

2 Nefi 26:23–28, 33.

Yesu Kristo anamtaka kila mmoja aje Kwake.

  • Ili kuwafundisha watoto wako kuhusu mialiko ya Mwokozi kwenye mistari hii, ungeweza kuzungumza nao kuhusu nyakati walipowaalika watu kwenye tukio maalumu, kama sherehe ya kumbukizi ya kuzaliwa. Kisha mngeweza kusoma 2 Nefi 26:23–28 pamoja kugundua kile ambacho Bwana anatualika tukifanye. Watoto wako wangependa kutengeneza kadi kumualika mtu fulani kuja kwa Yesu Kristo. Wahimize watumie vifungu vya maneno kutoka kwenye mistari hii katika mialiko yao.

  • Picha iliyo mwisho wa muhtasari huu inaonesha watu kutoka machimbuko mengi. Pengine watoto wako wangeangalia picha hii wakati ukisoma 2 Nefi 26:33. Ungeweza kurudia kifungu cha maneno “Bwana anawaalika wote waje Kwake” wakati watoto wakimwonesha kila mtu kweye picha—na kisha wao wenyewe. Tunawezaje kuja kwake?

  • Wimbo kuhusu kuwapenda watu wengine, kama “I’ll Walk with You” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,140–41), ungeweza kusaidia kufundisha ujumbe kutoka 2 Nefi 26:33.

2 Nefi 28:2; 29:7–11; 30:3–6

Kitabu cha Mormoni ni baraka.

  • Ili kuwasaidia watoto wako wahisi kwamba Kitabu cha Mormoni ni cha “thamani kuu” (2 Nefi 28:2), ungefunga nakala kama zawadi na waruhusu wabahatishe ni nini kimefungwa. Wangeweza pia kuangalia vidokezo kutoka 2 Nefi 30:3-6. Waambie watoto wako kwa nini Kitabu cha Mormoni ni cha thamani kuu kwako, na waruhusu washiriki hisia zao pia.

  • Fikiria kuwaomba watoto wako wafikirie kwamba rafiki aliwaambia, “Sihitaji kusoma Kitabu cha Mormoni. Nimekwisha kusoma Biblia.” Je, tunaweza kusema nini kwa rafiki yetu? Someni pamoja 2 Nefi 29:7–11 kujifunza kwa nini Mungu anatutaka tuwe na vyote viwili.

2 Nefi 28:30–31

Baba wa Mbinguni hunifundisha kidogo kidogo.

  • Pengine unaweza kufikiria somo la vitendo ambalo litawasaidia watoto wako waelewe inamaanisha nini kujifunza “mstari juu ya mstari.” Kwa mfano, wangeweka vipande vya fumbo au kujenga kitu fulani kwa vitofali, kipande kimoja kwa wakati. Au ungeweza kuwafundisha ujuzi hatua kwa hatua, kama vile kutengeneza uipinde au kuchora picha. Kisha ungeweza kusoma kutoka 2 Nefi 28:30 na kujadili jinsi Baba wa Mbinguni Anavyotufundisha ukweli mmoja kwa wakati.

  • Wazo lingine ingekuwa ni kuchagua kifungu cha maneno kutoka 2 Nefi 28:30 na kufanya zamu kukiandika, neno moja kwa wakati. Ni kwa jinsi gani shughuli hii inafanana na jinsi Mungu anavyotupatia ukweli? Kwa nini Mungu anatufunulia ukweli, “mstari juu ya mstari, kanuni juu ya kanuni, hapa kidogo na pale kidogo” badala ya wote kwa mara moja? Ni kwa jinsi gani tunaweza kumwonesha Mungu kwamba tunataka kupokea kweli zaidi kutoka Kwake?

Kwa ajili ya mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la gazeti la Rafiki.

Picha
Yesu Kristo katikati ya umati

Yesu akiwa Miongoni mwa Umati, na Judith A. Mehr

Chapisha