Njoo, Unifuate 2024
Julai 8–14: ‘“Hawakuanguka Kamwe.’” Alma 23–29


“Julai 8–14: ‘“Hawakuanguka Kamwe.’” Alma 23–29,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Kitabu cha Mormoni 2024 (2023)

“Julai 8–14. Alma 23–29,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: 2024 (2023)

Picha
Waanti-Nefi-Lehi wakizika silaha zao

Waanti-Nefi-Lehi Wakizika Silaha Zao za Vita, na Jody Livingston

Alma 8–14: “Hawakuanguka Kamwe”

Alma 23–29

Je, kuna nyakati unajiuliza ikiwa kweli watu wanaweza kubadilika? Pengine una wasiwasi kuhusu ikiwa unaweza kushinda chaguzi mbaya ulizozifanya au mazoea mabaya uliyoyajenga, au unaweza kuwa na wasiwasi sawa na huu juu ya wapendwa wako. Kama ni hivyo, hadithi ya Waanti-Nefi-Lehi inaweza kukusaidia. Watu hawa walikuwa maadui wa jadi wa Wanefi. Wakati wana wa Mosia walipoamua kuwahubiria injili, Wanefi “waliwacheka [wao] kwa dharau.” Kuwaua Walamani kulionekana kama suluhu yenye kukubalika kuliko kuwaongoa. (Ona Alma 26:23–25.)

Lakini Walamani walibadilika—kupitia nguvu ya kuongoa ya Yesu Kristo. Wao wakati mmoja walijulikana kama “watu wagumu na wakali” (Alma 17:14), lakini walikuja “kutambulika kwa juhudi yao kwa Mungu” (Alma 27:27). Kwa hakika, “hawakuanguka kamwe” (Alma 23:6).

Pengine una mawazo fulani au matendo ya kubadilisha au “silaha za … uasi” za kuweka chini (Alma 23:7). Au pengine unahitaji tu kuwa na ari zaidi kwa Mungu. Bila kujali ni mabadiliko ya aina gani unahitaji, Alma 23–29 inaweza kukupatia tumaini kwamba kupitia uwezo wa Yesu Kristo wa kulipia dhambi, mabadiliko ya kudumu yanawezekana.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Alma 23–25; 27

Picha
seminary icon
Kuongoka kwangu kwa Yesu Kristo na injili Yake kutabadilisha maisha yangu.

Walamani walionekana kuwa watu wasiofaa kwa uongofu, na bado wengi wao walipata mabadiliko ya ajabu kwa sababu ya Yesu Kristo. Walamani hawa walioongoka walijiita Waanti-Nefi-Lehi.

Kusoma Alma 23–25; 27 kunaweza kukushawishi utafakari uongofu wako wewe mwenyewe. Tafuta jinsi Waanti-Nefi-Lehi walivyobadilika—jinsi walivyoongolewa “kwa Bwana” (Alma 23:6). Mistari ifuatayo inaweza kukuwezesha kuanza:

Ni katika njia zipi Yesu Kristo na injili ya Yake vimekubadilisha wewe? Ni lini umehisi kuwa karibu Naye? Je, ni kwa jinsi gani wewe unajua ikiwa umeongolewa katika Yesu Kristo? Je, Ni kipi Roho anakusukuma ufanye?

Ona pia David A. Bednar, “Kuongoka katika Bwana,Liahona, Nov. 2012, 106–9; Dale G. Renlund, “Msimamo Thabiti kwa Yesu Kristo,” Liahona, Nov. 2019, 22–25; Mada za Injili: “Kuwa kama Yesu Kristo,” Maktaba ya Injili.

Alma 24:7–19; 26:17–22

Kwa sababu Mungu ni mwenye rehema, Yeye hunisamehe ninapotubu.

Mabadiliko ambayo Waanti-Nefi-Lehi waliyapata yalikuwa zaidi ya mabadiliko katika tabia tu—yalikuwa mabadiliko ya moyo uliozaliwa kwa imani katika Yesu Kristo na toba ya uaminifu. Pengine unaweza kupata ukweli kuhusu toba katika kila mstari katika Alma 24:7–19. Je, vifungu hivi vya maneno vinafundisha nini kuhusu rehema za Mungu kwa wale wanaotubu? Je, ni kweli zipi za ziada unazojifunza kutoka katika Alma 26:17–22?

Tafakari jinsi ambavyo Mungu ameonesha rehema Zake maishani mwako. Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuonesha shukrani zetu Kwake?

Alma 26; 29

Kushiriki injili huleta shangwe kwangu.

Neno shangwe hutokea mara 24 katika Alma 23–29, likizifanya sura hizi kuwa sehemu nzuri ya kujifunza jinsi ya kupokea shangwe katika kuishi—na kuishiriki—injili ya Mwokozi. Fikiria kujifunza Alma 26:12–22, 35–37; na 29:1–17, ukitafuta kwa nini Amoni, wana wa Mosia, Alma walifurahia. Unajifunza nini kutoka kwenye vifungu hivi ambacho kinakuongoza kwenye shangwe zaidi katika maisha yako?

Mzee Marcus B. Nash alifundisha: “Kushiriki injili huleta furaha na tumaini katika mioyo ya wote, anayetoa na anayepokea. … Kushiriki injili ni furaha juu ya furaha, tumaini juu ya tumaini” (Inua Mwangaza Wako,” Liahona, Nov. 2021, 71). Ni uzoefu upi uliwahi kuupata katika kushiriki injili kwa wengine? Ni changamoto zipi unakabiliana nazo unapotaka kushiriki injili? Ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni anaweza kukusaidia ushinde changamoto hizi?

Kwa maelekezo ya kinabii juu ya jinsi ya kushiriki injili—na kupata furaha katika kufanya hivyo—fikiria kujifunza ujumbe wa Rais Dallin H. Oak “Kushiriki na Wengine Injili ya Urejesho,” (Liahona, Nov. 2016, 57–60). Ni mapendekezo yapi unapata katika ujumbe huu?

Ona pia “The Bush Family Story,” “Sharing Your Beliefs,” “Sharing the Gospel” (videos), Maktaba ya Injili.

Fikiria kutengeneza orodha ya vitu ambavyo ungeshiriki na rafiki kuhusu Kitabu cha Mormoni. Jaribu kushiriki Kitabu cha Mormoni kwa kutumia aplikesheni ya Kitabu cha Mormoni

Tafuta mifumo na dhamira. Tunapojifunza maandiko, tunaweza kupata kweli za thamani kwa kutafuta maneno, virai, au mawazo yaliyorudiwa. Mawazo hayo yaliyorudiwa yanaweza kurejelewa au kuunganishwa katika maandiko yako ili kuyafanya yawe rahisi kuonekana.

Alma 26:5–7

Ninaweza kupata kimbilio katika Yesu Kristo na injili Yake.

Wakati wa mavuno, nafaka kwa kawaida hukusanywa katika mafungu yanayoitwa miganda na kuhifadhiwa katika majengo ya kuhifadhia, wakati mwingine yakiitwa maghala. Katika Alma 26:5–7 tafakari kile ambacho miganda, maghala, na dhoruba vinaweza kuwakilisha katika maisha yako. Je, ni kwa jinsi gani unaweza kupata kimbilio katika Yesu Kristo?

Ona pia Russell M. Nelson, “Hekalu na Msingi Wako wa Kiroho,” Liahona, Nov. 2021, 93–96; David A. Bednar, “Kushikilia Jina na Msimamo kwa Heshima,” Liahona, Mei 2009, 97–100; “Jesus, Lover of My Soul,” Nyimbo za Dini, na. 102.

Kwa mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la Liahona na magazeti ya Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana.

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Alma 24:6–24

Bwana hunibariki ninapojitahidi kuzishika ahadi zangu Kwake.

  • Pengine watoto wako wangependelea kuzika “silaha” zao kama vile Waanti-Nefi-Lehi. Ungeweza kusoma vifungu vichache kutoka Alma 24:6–24 ili uwafundishe watoto kuhusu ahadi Waanti-Nefi-Lehi walizoziweka ili kumfuata Mwokozi. Kisha wangeweza kufikiria kitu gani watakachobadilisha ili kumfuata Yeye, wakiandike kwenye ukurasa wa shughuli ya wiki hii, na wajifanye wanachimba shimo na kuzika silaha zao.

  • Watoto wako wangeweza kusoma Alma 24:15–19, wakitafuta ni kipi Wanti-Nefi-Lehi walifanya “kama ushuhuda kwa Mungu.” Kisha ungezungumza nao kuhusu jinsi maagano yetu yanavyoweza kuwa “ushuhuda kwa Mungu” (mstari 18). Waruhusu watoto wako wazungumzie kuhusu jinsi watakavyomuonesha Mungu kwamba wanataka kumfuata Yeye. Kuimba wimbo kama “I Want to Live the Gospel” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 148) kungeweza kuwapa mwongozo wa kiungu.

Alma 24:7–10; 26:23–34; 27:27–30

Ninaweza kutubu.

  • Ili kuwasaidia watoto wako waone jinsi Yesu Kristo anavyoweza kutusaidia tubadilike tunapotubu, ungeweza kuwafundisha kuhusu Waanti-Nefi-Lehi. Ili kufanya hivi, ungeweza kuandika kwenye bakuli mbili “kabla” na “baada.” Kisha watoto wako wanaweza kusoma Alma 17:14–15 na 27:27–30, na waandike vile ambavyo Walamani walikuwa kabla na baada ya kutubu, na waviweke katika bakuli sahihi. Kulingana na Alma 24: 7– 10, ni kipi kiliwasaidia wao kubadilika? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonesha shukrani zetu kwa Mungu kwa ajili ya rehema Yake?

Alma 26; 29

Yesu Kristo hunipa shangwe na ninaweza kushiriki shangwe hii.

  • Pengine wewe na watoto wako mngeweza kufurahia kuchora picha za vitu katika injili ya Yesu Kristo ambavyo vinawaletea shangwe. Shiriki picha yako kwa watoto wako, na uwahimize wao washiriki picha zao kwa mtu fulani ili kumsaidia yule mtu ahisi shangwe pia.

  • Wasaidie watoto watafute maneno shangwe na furahia katika Alma 26 na 29. Ni kitu gani kiliwaletea Amoni na Alma shangwe au kuwafanya wafurahie? Swali hili lingeweza kuongoza kwenye mazungumzo kuhusu shangwe ambayo huja kutokana na kuishi au kushiriki injili ya Yesu Kristo.

Alma 27:20–30

Ninaweza kuwasaidia rafiki zangu waishi injili ya Yesu Kristo.

  • Watoto wako wanaweza kusoma Alma 27:22–23, wakitafuta ni kitu gani Wanefi walifanya ili kuwasaidia Waanti-Nefi-Lehi washike ahadi yao ya kamwe kutopigana tena. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwasaidia rafiki zetu washike ahadi zao? Watoto wako wanaweza kufanya igizo la hali kadha wa kadha. Kwa mfano, ni kipi tunaweza kusema kwa rafiki anayetaka kudanganya au kuwa mkatili?

Kwa ajili ya mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la gazeti la Rafiki.

Picha
Waanti-Nefi-Lehi wakizika silaha zao

Kielelezo cha Waanti-Nefi-Lehi wakizika silaha zao, na Dan Burr

Chapisha