Mafundisho na Maagano 2021
Februari 1–7. Mafundisho na Maagano 10–11: “Kwamba Uweze Kutoka Mshindi”


“Februari 1–7. Mafundisho na Maagano 10–11: ‘Kwamba Uweze Kutoka Mshindi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Februari 1-7. Mafundisho na Maagano 10–11,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha
Muswada wa Kitabu cha Mormoni

Nakala halisi ya muswada wa Kitabu halisi cha Mormoni.

Februari 1–7

Mafundisho na Maagano 10–11

“Kwamba Uweze Kutoka Mshindi”

Kuandika misukumo wakati ukisoma maandiko ni kama kupanda mbegu; hata misukumo midogo inaweza kuongoza kwenye ufunuo binafsi wenye maana.

Andika Misukumo Yako

Wakati tafsiri ya Kitabu cha Mormoni ilipoendelea, swali kwa kawaida lilitokea: nini Joseph Smith na Oliver Cowdery wanapaswa kufanya kuhusu kurasa zile za muswada ambazo zilikuwa zimepotea? Kitu cha mantiki kinaweza kuwa kurudi nyuma na kutafsiri tena sehemu ile, lakini Bwana aliweza kuona kitu fulani ambacho wao hawakuweza kukiona—watu waovu walikuwa wanakula njama kubadilisha maneno kwenye kurasa zile ili kutilia shaka kwenye kazi ya Joseph yenye mwongozo wa kiungu. Mungu alikuwa na mpango wa kuzuia juhudi za Shetani na kufidia kile kilichopotea. Mpango huu ulianzishwa maelfu ya miaka mapema wakati nabii Nefi alipohisi msukumo kutengeneza kumbukumbu ya pili ambayo ilielezea muda sawa sawa na kipindi kile. Baadaye, Mormoni alipata msukumo kujumuisha kumbukumbu hii katika Kitabu cha Mormoni “kwa madhumuni ya busara” yaliyojulikana kwa Bwana (ona Maneno ya Mormoni 1:3–7).

“Hekima Yangu,” Bwana alimwambia Joseph, “ni kuu kuliko hila ya ibilisi” (Mafundisho na Maagano 10–43). Huo ni ujumbe wa hakikisho katika siku kama ya kwetu, wakati juhudi za adui zinazoendelea kudhoofisha imani zinapoongezeka. Kama Joseph, tunaweza kuwa “waaminifu na kuendelea” katika kazi Mungu aliyotuita kufanya (Mstari wa 3). Kisha tutakuta kwamba Yeye tayari amekwisha toa njia ili kwamba “milango ya jehanamu haitashinda” dhidi yetu (mstari wa 69).

Ona Watakatifu, 1:51–61.

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Mafundisho na Maagano 10:1–33

Shetani anatafuta kuharibu kazi ya Mungu.

Shetani angependa tusahau kwamba yupo—au kwamba angalau tushindwe kutambua majaribio yake ya kutushawishi (ona 2 Nefi 28:22–23). Lakini maneno ya Bwana katika Mafundisho na Maagano 10 yanaonesha kwamba Shetani yupo daima, upinzani hai kwa kazi za Mungu. Unaposoma Mistari 1–33, tambua jinsi Shetani alivyotafuta kuharibu kazi ya Mungu katika wakati wa Joseph Smith (ona pia Mistari 62–63). Ni mifanano gani unayoiona kwa jinsi Shetani anavyofanya kazi leo? Ungeweza kumwomba Bwana kukusaidia kuona jinsi Shetani anavyoweza kuwa anakujaribu. Unajifunza nini kutokana na sehemu ya 10 ambacho kinaweza kukusaidia kukinza juhudi za Shetani?

Mafundisho na Maagano 10:34–52

“Hekima ya Bwana ni kuu kuliko hila ya ibilisi.”

Zaidi ya miaka 2,400 kabla, Bwana alitayarisha kufidia kwa ajili ya kurasa zilizopotea za Kitabu cha Mormoni (ona 1 Nefi 9). Unajifunza nini kuhusu Bwana kutoka Mafundisho na Maagano 10:34–52? Ni ushahidi gani wa hekima ya Bwana na kujua kitu kabla hakijatokea ulivyoviona katika maisha yako?

Kumbukumbu ambayo Mungu aliitayarisha kufidia muswada uliopotea sasa inapatikana katika 1 Nefi mpaka Omni. Ni kwa jinsi gani hadithi na mafundisho katika kumbukumbu hii “[yamechangia]” mtazamo mkubwa juu [ya] injili” kwa ajili yako ? (Mafundisho na Maagano 10:45).

Picha
Mormoni akifupisha maandishi Kwenye mabamba ya dhahabu

Mormoni Akifupisha Maandishi ya Mabamba, na Tom Lovell

Mafundisho na Maagano 11

Kama nitamwomba Mungu, nitapata.

Baadhi ya wanafamilia wa Joseph Smith na marafiki walimwomba kuuliza mapenzi ya Bwana kwa niaba yao. Joseph alifurahi kufanya hivyo, bali Bwana alikuwa pia tayari kuwapa ufunuo binafsi. Katika Mafundisho na Maagano 11, ufunuo ambao Joseph alipokea kwa ajili ya kaka mkubwa Hyrum, Bwana alisema, “Nitakupa Roho wangu, … na ndipo utajua … mambo yote ambayo unahitaji kutoka kwangu” (Mafundisho na Maagano 11:13–14).

Bwana alisema maneno Yake yalikuwa kwa ajili ya “wale wote walio na matakwa yaliyo mema, na wameingiza mundu zao kuvuna” (mstari wa 27). Katika Mafundisho na Maagano 11, Bwana anajaribu kukuambia nini kuhusu ufunuo binafsi? Kuhusu kushiriki katika kazi ya Mungu? Je, ni jumbe gani zingine Alizonazo kwa ajili yako?

Mafundisho na Maagano 11:15–26

Ninapotafuta “kupata neno [la Mungu,]” Nitapokea Roho Wake na nguvu Yake.

Hata kabla Kitabu cha Mormoni hakijatafsiriwa, Hyrum Smith alikuwa na hamu ya kuhubiri injili. Unaposoma jibu la Bwana kwa matamanio yake, fikiria inamaanisha nini kwako “kupata neno [la Mungu]” (mstari wa 21) Je, ni kwa jinsi gani kupata neno la Mungu kunakusaidia kutumikia katika Kanisa? Ni kwa jinsi gani inaleta nguvu ya Mungu katika maisha yako?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Mafundisho na Maagano 10:5.Je, tunajifunza nini kutoka kwenye mstari huu kuhusu nguvu ya sala? Ni kwa jinsi gani “tunaomba daima”? (Kwa ajili ya baadhi ya mawazo, ona David A. Bednar, “Omba Daima,” Ensign au Liahona, Nov. 2008, 41–44.)

Mafundisho na Maagano 10:38–46.Kusaidia familia yako kujadili jinsi Bwana alivyofidia kurasa zilizopotea za tafsiri ya kitabu cha Mormoni, labda wanafamilia wangeweza kuzungumza kuhusu kitu fulani walichopoteza hivi karibuni. Walihisi vipi wakati walipogundua kilikuwa kimepotea? Walihisi vipi wakati kilipopatikana? Ingawa kurasa zilizopotea za Kitabu cha Mormoni hazikupatikana kamwe, ni kwa jinsi gani Bwana alifidia kupotea kwake, kulingana na Mafundisho na Maagano 10:38–46?

Mafundisho na Maagano 10:55–70.Waalike wanafamilia kutafuta au kuwekea alama virai ambavyo vinaanza na “mimi” au “Nita.” Tunajifunza nini kutoka kwenye virai vya “Mimi” kuhusu Yesu Kristo ni nani na yuko kama nani? Tunajifunza nini kutoka kwenye virai vya “Nita” kuhusu nini anafanya? Watie moyo wana familia kushiriki jinsi kweli hizi zinavyoimarisha imani yao katika Yesu Kristo.

Mafundisho na Maagano 11:12–14.Kusoma mistari hii kunaweza kuwasaidia wanafamilia yako kugundua wakati Roho anapowasiliana nao. Ungeweza kuangaza tochi kwenye sakafu na mwalike mwanafamilia kusogea kule mwanga unakoangaza. Ni kwa jinsi gani hii ni kama kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu? Ni uzoefu gani binafsi ungeweza kushiriki?

Mafundisho na Maagano 11:15–30.Fikiria kutengeneza orodha ya mambo Bwana aliyomwambia Hyrum Smith kufanya ili kwamba awe tayari kushiriki injili. Nini tunapaswa kukifanyia kazi kama familia?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Search, Ponder, and Pray,” Kitabu cha nyimbo cha watoto, 109; ona “Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwa Familia Yako.”

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia Maandiko katika Maisha Yako. Baada ya kusoma kifungu cha maandiko, waalike wanafamilia kushiriki jinsi ujumbe unavyohusiana na maisha yao. Kwa mfano, wangeweza kushiriki jinsi Roho alivyowashawishi katika njia zilizoelezwa katika Mafundisho na Maagano 11:12–13.

Picha
Joseph na Hyrum Smith

Joseph na Hyrum Smith na Ken Corbett

Chapisha