Mafundisho na Maagano 2021
Aprili 26–Mei 2. Mafundisho na Maagano 45: “Ahadi … Zitatimizwa”


“Aprili 26–Mei 2. Mafundisho na Maagano 45: ‘Ahadi … Zitatimizwa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021) (2020)

“Aprili 26–Mei 2. Mafundisho na Maagano 45,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2021

Picha
vijana nje ya hekalu

Aprili 26–Mei 2

Mafundisho na Maagano 45

“Ahadi … Zitatimizwa”

Rais Russell M. Nelson alifundisha: “andika mawazo ambayo yanakuja kwenye akili yako. Andika hisia zako na fuatilia matendo yako ambayo unavuviwa kuyatenda” (“Ufunuo kwa ajili ya Kanisa, Ufunuo kwa ajili ya Maisha Yetu,” Ensign au Liahona, Mei 2018, 95).

Andika Misukumo Yako

Tunaishi katika nyakati za hatari, na hilo linaweza kuwa la kufadhaisha. Hata wanafunzi wa Yesu, wakati walipomsikia akitoa unabii wa majanga ambayo yangetokea katika siku yetu, “walifadhaika” (Mafundisho na Maagano 45:34). Watakatifu wa mwanzo huko Kirtland, Ohio, pia walifadhaishwa na nyakati za hatari walizokuwa wakiishi. Kati ya mambo mengine, kulikuwa na “taarifa nyingi za uongo … na hadithi za kijinga” ambazo zilikuwa zikifanya injili kuwa duni (Mafundisho na Maagano 45, kichwa cha habari cha sehemu). Lakini jibu la Bwana, kipindi hicho na sasa, ni “msifadhaike” (mstari wa 35). Ndiyo, kuna uovu, lakini pia kuna ushahidi kwamba Mungu anaharakisha kazi Yake. Ndiyo, hatari zilizotabiriwa kutangulia Ujio wa Pili, na tunapaswa kuzifahamu. Lakini haya si tu maonyo ya hatari; ni ishara pia kwamba ahadi za Mungu zinakaribia kutimizwa. Pengine hii ndiyo maana Mafundisho na Maagano 45—ufunuo unaoelezea nyingi za ishara hizi kwa undani—ulipokelewa “kwa shangwe ya Watakatifu” (kichwa cha habari cha sehemu).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Mafundisho na Maagano 45:1–5

Yesu Kristo ndiye Mtetezi wetu kwa Baba.

Je, umewahi kuhisi una mapungufu au usiyestahili mbele za Mungu? Unaweza kupata uthibitisho katika Mafundisho na Maagano 45:1–5. Ni nini maneno kama vile “mwombezi” na “mtetezi” yanapendekeza kwako? Ni kwa jinsi gani Mwokozi anakuombea, au kutetea mambo yako? Inamaanisha nini kwako kujua kwamba Kristo ni mwombezi wako?

Maneno yafuatayo kutoka kwa Rais Joseph Fielding Smith yangeweza kukusaidia kutafakari mistari hii: “Yesu [ni] mwombezi wetu, akitutetea kama mpatanishi kupitia huduma yake na kazi yake kutupatanisha, kutuleta kwenye makubaliano na Mungu” (katika ripoti ya mkutano, Okt. 1953, 58).

Ona pia 2 Nefi 2:8–9; Mosia 15:7–9; Moroni 7:27–28; Mafundisho na Maagano 29:5; 62:1.

Mafundisho na Maagano 45:9–10

Injili ni ishara ya ubora kwa mataifa.

Siku za kale, ishara ilikuwa ni bango au bendera iliyochukuliwa kwenda nayo vitani. Iliwaleta pamoja na kuwaunganisha askari na kuwasaidia kujua wapi pa kukusanyika na nini cha kufanya. Ishara pia ni mfano au sheria ambayo vitu vingine vinaweza kupimwa dhidi yake. Unaposoma Mafundisho na Maagano 45:9–10, tafakari jinsi ambavyo maagano ya injili yamekuwa ishara kwako. Ni kwa jinsi gani maisha yako yangekuwa tofauti kama usingekuwa na maagano haya?

Ona pia Isaya 5:26; 11:10–12; Mafundisho na Maagano 115:5–6.

Mafundisho na Maagano 45:11–75

Ahadi za Bwana zitatimizwa.

Vita, uovu, na ukiwa vitatangulia Ujio wa Pili wa Mwokozi. Lakini “msifadhaike,” Bwana amesema, “kwani haya yote yatakapokuja kutukia, ninyi muweze kujua kwamba ahadi ambazo zimefanywa kwenu zitatimizwa”(Mafundisho na Maagano 45:35).

Unapojifunza Mafundisho na Maagano 45:11–75, fikiria kufokasi si tu kwenye matukio ya kufadhaisha ambayo yametolewa unabii bali pia kwenye baraka alizoahidi Bwana (kwa mfano, ahadi katika mistari 54–59 kuhusu utawala wa Mwokozi wa miaka elfu moja). Ungeweza kufanya hili kwa kutengeneza orodha au kwa kujaza au kuwekea alama mistari. Unapata nini ambacho kinakusaidia wewe “kutofadhaika” kuhusu siku za mwisho?

Mafundisho na Maagano 45:31–32; 56–57

“Simameni katika mahali patakatifu,” na wala msiondoshwe.

Sababu moja ya Mwokozi na manabii Wake kutufundisha kuhusu ishara za Ujio wa Pili ni kutusaidia kujitayarisha. Unajifunza nini katika Mafundisho na Maagano 45: 31–32, 56–57 kuhusu kujitayarisha kwa Ujio wa Pili wa Bwana? Ingeweza kuwa yenye msaada kurejea mfano wa wanawali kumi, unaopatikana katika Mathayo 25:1–13. Mwokozi alifananisha mafuta katika mfano huu na ukweli na Roho Mtakatifu (ona Mafundisho na Maagano 45:57). Ni umaizi gani unaupata wakati unaposoma mfano katika njia hii?

Picha
wanawali kumi

Mfano wa Wanawali Kumi, na Dan Burr

Mafundisho na Maagano 45:11–15; 66–71

Sayuni ni mahali pa usalama kwa ajili ya Watakatifu wa Mungu.

Watakatifu katika kipindi cha Joseph Smith walikuwa na shauku ya kuijenga Sayuni, Yerusalemu Mpya, kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha Mormoni (ona Etheri 13:2–9) na katika toleo lenye uvuvio la Joseph Smith la Biblia (ona Musa 7:62–64). Unajifunza nini kuhusu Sayuni—jiji la kale la siku za Henoko na jiji la siku za mwisho—kutoka Mafundisho na Maagano 45:11–15, 66–71.?

Leo amri ya kuijenga Sayuni inamaanisha kuujenga ufalme wa Mungu popote tunapoishi—popote watoto wa Mungu wanapokusanyika kwenye usalama wa “agano lisilo na mwisho” (mstari wa 9). Unaweza kufanya nini ili kusaidia kujenga Sayuni mahali ulipo?

Ona pia Mada za Injili, “Sayuni,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Nyumbani

Mafundisho na Maagano 45:3–5.Ni nini mwombezi anafanya kwa ajili yetu? Ungeweza kuangalia video “The Mediator” (ChurchofJesusChrist.org) na kuzungumza kuhusu kwa nini Mwokozi anaitwa Mtetezi wetu.

Mafundisho na Maagano 45:9–10.Ikiwa familia yako ingekuwa na “ishara,” au bendera, kuwakilisha msimamo wenu kwenye injili, je, ingeonekanaje? Ingekuwa yenye kufurahisha kutengeneza bendera ya familia pamoja na kujadili jinsi mnavyoweza kuwasaidia wengine kufuata viwango vya injili.

Mafundisho na Maagano 45:32.Mahali petu “patakatifu” ni wapi? Je, inamaanisha nini “kutoondoshwa”? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuzifanya nyumba zetu kuwa mahali patakatifu?

Mafundisho na Maagano 45:39–44.Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia wanafamilia kuelewa kile inachomaanisha kutazamia Ujio wa Pili wa Mwokozi? Pengine ungeweza kufikiria juu ya tukio ambalo unalitarajia na kushiriki jinsi ambavyo “unatazamia” tukio hilo. Au mngeweza kuoka kitu pamoja na kutazamia ishara kwamba kiko tayari kuliwa. Je, nini tunafanya kutazamia Ujio wa Pili wa Mwokozi?

Mafundisho na Maagano 45:55.Kusoma 1 Nefi 22:26 na Ufunuo 20:1–3 kunaweza kuisaidia familia yako kuelewa jinsi shetani “atakavyotupwa kifungoni” wakati wa Milenia. Ni kwa jinsi gani tunaweza kumweka shetani kifungoni katika maisha yetu?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “When He Comes Again,” Kitabu cha nyimbo za watoto, 82–83 ona pia “Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwa Familia Yako.”

Kuboresha Kujifunza Kibinafsi

Tumia vielelezo vya kujifunzia. Tumia tanbihi chini ya ukurasa, Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, na Mwongozo kwenye Maandiko ili kupata umaizi kwenye maandiko.

Picha
Kristo akishuka

Ujio wa Kristo, na Jubal Aviles Saenz

Chapisha