Agano la Kale 2022
Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: “Yupo Nabii katika Israeli”


“Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: ‘Yupo nabii katika Israeli,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Elisha akimwonyesha mtumishi magari ya moto

Kielelezo cha Elisha akimwonyesha mtumishi wake magari ya moto, © Review & Herald Publishing/licensed from goodsalt.com

Julai 4–10

2 Wafalme 2–7

“Yupo Nabii katika Israeli”

Unaposoma maandiko, Roho anaweza kuvuta usikivu wako kwenye virai au vifungu fulani vya maandiko. Fikiria kuandika kwa nini vifungu hivyo ni vya maana kwako.

Andika Misukumo Yako

Kazi muhimu zaidi ya nabii ni kufundisha na kushuhudia juu ya Mwokozi Yesu Kristo. Kumbukumbu zetu za nabii Elisha, hata hivyo, hazijumuishi mengi sana kuhusu mafundisho yake au kushuhudia kwake. Kile ambacho kumbukumbu zinajumuisha ni miujiza Elisha aliyoifanya, ikijumuisha kumfufua kijana kutoka katika wafu (ona 2 Wafalme 4:18–37), kulisha umati kwa kiasi kidogo cha chakula (ona 2 Wafalme 4:42–44), na kumponya mkoma (ona 2 Wafalme 5:1–14). Kwa hiyo wakati hatuna maneno ya Elisha akimshuhudia Kristo, tunayo, kote katika huduma ya Elisha, maonyesho ya nguvu za Bwana yenye kuleta uhai, kustawisha na uponyaji. Maonyesho kama hayo ni mengi mno katika maisha yetu kuliko wakati mwingine tunavyofahamu. Ili kuyaona, tunahitaji kutafuta miujiza Elisha aliyoitafuta wakati aliposali kwa niaba ya mtumishi wake kijana mwoga, “Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona” (2 Wafalme 6:17).

Kwa maelezo zaidi kuhusu 2 Wafalme, ona “Wafalme, vitabu vya” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

2 Wafalme 2–6

Mungu anaweza kutenda miujiza katika maisha yangu.

Miujiza mara nyingi hutusaidia sisi kushinda magumu ya kimwili—katika nyakati za Elisha, ardhi kame ilihitaji maji safi na shoka iliyopotea ilihitaji kupatikana (ona 2 Wafalme 2:19–22; 6:4–7). Lakini miujiza pia hugeuza mioyo yetu kwa Bwana na kutufundisha masomo ya kiroho. Unaposoma 2 Wafalme 2–6, fikiria kutengeneza orodha ya miujiza uliyopata, na utafakari masomo ya kiroho uliyojifunza kutoka kwa kila mmoja. Miujiza hii inakufundisha nini kuhusu Bwana na kile Yeye anachoweza kufanya katika maisha yako?

Ona pia 2 Nefi 26:12–13; 27:23; Mormoni 9:7–21; Moroni 7:35–37; Donald L. Hallstrom, “Je, siku za Miujiza Zimekoma?Liahona, Nov. 2017, 88–90.

2 Wafalme 4:8–17; 7:1–16

Maneno ya Bwana kupitia kwa manabii Wake yatatimizwa.

Kama ilivyoandikwa katika 2 Wafalme 4:8–17; 7:1–16, Bwana alimwongoza Elisha kutoa unabii wa mambo yatakayokuja—mambo ambayo yalionekana, kutoka kwenye mitazamo ya wengine, yasingeweza kutokea. Unaposoma mistari hii, fikiria kuhusu namna unavyoitikia maneno ya Bwana kupitia manabii Wake leo. Ni mafundisho gani, unabii, au ahadi umezisikia kutoka kwa manabii walio hai? Je, unafanya nini ili kutenda kwa imani katika ahadi hizo?

Ona pia 3 Nefi 29:6; Mafundisho na Maagano 1:37–38.

2 Wafalme 5

Ikiwa mimi ni mnyenyekevu na mtiifu, Yesu Kristo anaweza kuniponya.

Wakati mwingine ni rahisi kutafuta maana binafsi katika maandiko wakati unapolinganisha vitu vya kimwili katika hadithi yenye vitu vya kiroho. Kwa mfano, wakati unaposoma 2 Wafalme 5, unaweza kulinganisha ukoma wa Naamani na changamoto ya kiroho unayokabiliana nayo. Kama Naamani, labda umetumaini kwamba Bwana “angefanya jambo kubwa” (mstari wa 13) kukusaidia wewe. Uzoefu wa Naamani unakufundisha nini? Katika maisha yako, ni nini kinaweza kuwa kisawe cha kufuata ushauri wa kawaida wa “jioshe uwe safi”?

Angalia jinsi uzoefu wa Naamani ulivyoathiri imani yake katika Mungu wa Israeli (ona mstari wa 15). Ni uzoefu gani umeimarisha imani yako katika Bwana?

Ona pia Luka 4:27; 1 Petro 5:5–7; Alma 37:3–7; Etheri 12:27; L. Whitney Clayton, “Lolote Yeye Akwambialo Wewe, Litende,” Liahona, Mei 2017, 97–99; “Naaman and Elisha” (video), ChurchofJesusChrist.org.

2 Wafalme 6:8–23

“Walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”

Je, umewahi kuhisi umezidiwa na mwoga, ukijiuliza, kama mtumishi mdogo wa Elisha alivyofanya, “Tufanyeje?” (ona 2 Wafalme 6:8–23). Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu jibu la Elisha? Ni kwa jinsi gani simulizi hii inabadilisha namna unavyofikiri na kuhisi kuhusu majaribu yako, wajibu wako, au juhudi zako za kuishi injili?

Wakati unapoafakari, fikiria maneno ya Rais Henry B. Eyring: “kama yule mtumishi wa Elisha, kuna wengi wako na wewe kuliko wale unaoweza kuwaona wako kinyume na wewe. Baadhi ambao wako na wewe wataonekana kwa macho ya kimwili. Bwana atakuinua juu na nyakati zote atafanya hivyo kwa kuwaita wengine kusimama na wewe” (“Ee Ninyi Mnaoanza,” Liahona, Nov. 2008, 58).

Ona pia Zaburi 121; Mafundisho na Maagano 84:88.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

2 Wafalme 2:1–14.Fikiria kuhusu watu walioona kwamba Elisha “alichukua” vazi la Eliya (au joho—ishara ya wito wake wa kinabii). Ni kwa namna gani hili liliathiri jinsi walivyoitikia kwenye huduma ya Elisha? (Ona pia 1 Wafalme 19:19.) Labda wanafamilia wangefanya zamu ya kuvaa “vazi” na kushuhudia njia ambazo wamemwona Bwana akiwahimili na kuwaimarisha wale wanaoitwa kuhudumu katika Kanisa Lake.

2 Wafalme 4.Ungeweza kuwaalika wanafamilia kusoma kuhusu moja ya miujiza katika 2 Wafalme 4 (ona mistari 1–7, 14–17, 32–35, 38–41, 42–44) na kuandika dokezo kuwasaidia wanafamilia wengine kubahatisha muujiza upi anauelezea. Tunajifunza nini kuhusu Bwana na miujiza Yake kutoka katika sura hii? Miujiza ipi—mikubwa au midogo—tumewahi kuiona katika maisha yetu?

2 Wafalme 5:1–15.Wakati unaposoma mistari hii na kutafakari jambo rahisi Naamani alilotakiwa kufanya, fikiria mambo rahisi ambayo nabii wetu ametutaka sisi tufanye. Ni kwa jinsi gani familia yetu inaweza kufuata ushauri wake?

Familia yako ingeweza pia kuangalia video “Naaman and Elisha” (ChurchofJesusChrist.org) au kusoma “Elisha Anamponya Naamani ” (katika Hadithi za Agano la Kale).

2 Wafalme 5:20–27.Ni kwa namna gani Gehazi angeweza kufaidika kutokana na kusoma “Uaminifu na Uadilifu” katika Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana? (ukurasa wa 19). Ni kwa jinsi gani kukosa uaminifu kunatuumiza sisi? Je, tunabarikiwa vipi tunapokuwa waaminifu?

2 Wafalme 6:13–17.Wanafamilia wanaweza kufurahia kuchora picha ya uzoefu wa Elisha na mtumishi wake iliyoelezewa katika mistari hii. Ni kwa jinsi gani mistari hii inaweza kutusaidia tunapohisi wapweke au kuelemewa?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Dearest Children, God Is Near You,” Nyimbo za Kanisa, na. 96.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Himiza maswali. Maswali ya watoto ni ishara kwamba wako tayari kujifunza. Ikiwa hujui majibu kwa maswali yao, tafuta majibu pamoja nao. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Picha
Naamani akioga katika mto

Kielelezo cha Naamani akiwa anaponywa ukoma, na Paul Mann

Chapisha