Agano la Kale 2022
Julai 25–31. Esta: “Wewe Hukuujia … kwa Ajili ya Wakati kama Huo”


“Julai 25–31. Esta: ‘Wewe Hukuujia … kwa Ajili ya Wakati kama Huo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 25–31. Esta,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Esta akisali

Esta, na James Johnson

Julai 25–31

Esta

“Wewe Hukuujia … kwa Ajili ya Wakati kama Huo”

Unaposoma Esta, tafuta misukumo kutoka kwa Roho ambayo imekusudiwa kwako, na andika misukumo unayopokea.

Andika Misukumo Yako

Matukio mengi katika kitabu cha Esta yanaweza kuonekana kama bahati nzuri au kudra. Ni kwa jinsi gani tena unaweza kueleza jinsi msichana wa Kiyahudi yatima aliweza kuwa malkia wa Uajemi kwa wakati stahiki kuokoa watu wake walipokuwa wanachinjwa? Ilitokeaje kwamba Mordekai binamu wa Esta aweze kusikia mpango wa kumuua mfalme? Je, haya yalikuwa bahati tu, au yalikuwa sehemu ya mpango mtakatifu? Mzee Ronald A. Rasband alisema: “Kile kinachoweza kuonekana kama bahati isiyo maalum, hakika, kinaonwa na Baba wa Mbinguni mwenye upendo. … Bwana yupo ndani ya vipengele vidogo vidogo vya maisha yetu” (“Kwa Usanifu Mtakatifu,” Liahona, Nov. 2017, 56). Tunaweza mara nyingi tusitambue msukumo wa Bwana katika “vipengele hivi vidogo vidogo.” Lakini tunajifunza kutokana na uzoefu wa Esta kwamba Yeye anaweza kuongoza njia zetu na kutuandaa sisi “kwa ajili ya wakati kama huo” (Esta 4:14) ambapo tunapoweza kuwa vyombo katika mikono Yake kutimiza malengo Yake.

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Kutoka, ona “Esta, kitabu cha” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Esta

Bwana anaweza kunifanya niwe chombo cha kubariki wengine.

Dada Anne C. Pingree alifundisha: “Kuwa chombo katika mikono ya Mungu ni fursa kubwa na jukumu takatifu. Popote tunapoishi, licha ya hali zetu, pasipo kujali hali zetu za ndoa au umri, Bwana anamhitaji kila mmoja wetu kutimiza sehemu [yetu] ya kipekee katika kujenga ufalme Wake katika nyakati hizi za mwisho” (“Kujua Mapenzi ya Bwana kwa Ajili Yako,” Liahona, Nov. 2005, 112).

Unaposoma hadithi ya Esta, tafakari jinsi kauli hii inavyotumika kwake. Angalia njia ambazo Bwana alizitumia kufanya iwezekane kwake kuwaokoa Wayahudi (ona, kwa mfano, Esta 2:21–23; 3:10–14; 4:14–16). Kisha tafakari namna ambayo Yeye ameongoza maisha yako katika njia ambazo zinakuwezesha wewe kubariki wengine. Ni katika baadhi ya hali zipi au mahusiano yapi ambayo unahisi Yeye amekuongoza wewe “kwa ajili ya wakati kama huo”? (Esta 4:14). Ikiwa una baraka ya patriaki, fikiria kuisoma ili ujifunze zaidi kuhusu kazi ambayo Bwana anakutaka ufanye.

Esta 3; 5:9–147

Kiburi na hasira vinaweza kuongoza kwenye anguko.

Katika kitabu cha Esta, tunajifunza kutoka katika uaminifu wa Esta na Mordekai na vile vile kutoka kwenye kiburi na hasira ya Hamani. Unaposoma Esta 3; 5:9–14, fikiria kugundua hisia za Hamani, maneno, na matendo yake. Je, yanafunua nini kumhusu yeye na hamasa zake? Ni madhara yapi aliyapata? (ona Esta 7). Kusoma kuhusu Hamani kunaweza kukuchochea kutathimini kitu gani kinahamasisha hisia na matendo yako. Je, Unashawishika kufanya mabadiliko yoyote? Unawezaje kumgeukia Baba wa Mbinguni kwa ajili ya msaada?

Ona pia Mithali 16:32; Alma 5:28.

Esta 3–4; 5:2–3; 8:11–12

Kufunga kunaonyesha utegemezi wangu kwa Mungu.

Gundua hali ambazo zilimwongoza Esta na Wayahudi wengine kufunga (ona Esta 3:13; 4:1–3, 10–17). Ni kwa namna gani kufunga kulikuwa baraka kwao? (ona Esta 5:2–3; 8:11–12). Kwa nini Bwana anatutaka tufunge? (ona Mada za Injili, “Kufunga na Matoleo ya Mfungo,” topics.ChurchofJesusChrist.org). Fikiria nini unaweza kufanya ili kufunga kuwe baraka kubwa zaidi katika maisha yako.

Ona pia Isaya 58:6–12; Mathayo 4:1–4; 17:14–21; “Fasting: Young Single Adult Ward, Amanda” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Esta 3:1–11; 4:10–17; 5:1–4

Kufanya jambo sahihi mara nyingi huitaji ujasiri mkubwa.

Wakati Mordekai na Esta waliposimamia imani yao, waliweka maisha yao hatarini. Chaguzi zetu zina matokeo ambayo yanaweza kuwa si makali, lakini kufanya jambo sahihi bado kutahitaji ujasiri. Unajifunza nini kutoka katika Esta 3:1–4; 4:10–17 kuhusu kuwa na ujasiri kufanya jambo sahihi? Gundua matokeo tofauti ambayo Mordekai na Esta waliyapata baada ya kuonyesha ujasiri (ona Esta 3:5–11; 5:1–4). Mtu atahitaji kujua nini kuhusu Mungu ili kuweza kufanya zile chaguzi Esta na Mordekai walizofanya—kufanya kilicho sahihi bila kujali matokeo?

Wakati mwingine ukifikiria matokeo ya kufanya kilicho sahihi, unaweza kutumia maneno ya ujasiri ya Esta katika Esta 4:16 katika hali yako mwenyewe. Kwa mfano, unaweza kujiambia mwenyewe, “Wakati ninapochagua mema, ikiwa [nitapoteza marafiki], na [nipoteze marafiki].”

Ona pia Thomas S. Monson, “Kuweni na Ujasiri,” Liahona, Mei 2009, 123–27.

Picha
Esta na mfalme

Esta mbele ya Mfalme, na Minerva K. Teichert

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Esta 1–10.Baada ya kupitia hadithi ya Esta (ona “Malkia Esta” katika Hadithi za Agano la Kale au video “For Such a Time as This,” ChurchofJesusChrist.org), familia yako inaweza kufurahia kutengeneza vikaragosi rahisi vya baadhi ya wahusika (ona ukurasa wa shughuli ya wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi). Wangeweza baadae kuvitumia kusimulia tena hadithi. Mngeweza pia kuimba wimbo kuhusu kuwa jasiri, na wakweli, kama vile “Dare to Do Right” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 158) au “Do What Is Right” (Nyimbo za Kanisa, na. 237). Maneno gani katika wimbo yanatukumbusha kuhusu Esta?

Esta 2:5–7.Nini tunaweza kujifunza kutokana na mfano wa Mordekai kuhusu kuwasaidia wanafamilia nyakati za majaribu? Nani katika familia yetu anahitaji usaidizi wetu? Tengenezeni mpango wa kuwasaidia.

Esta 4:15–17.Ushujaa wa Esta unaweza kuipa familia yako msukumo kujadili namna ya kukuza ujasiri wa kusimama kwenye ukweli katika hali wanazokabiliana nazo. Esta alimaanisha nini kwa “nami nikiangamia, na niangamie.”? Ni kwa jinsi gani maneno yake yanatumika kwetu tunapohitaji kuwa majasiri? Video “Courage” (ChurchofJesusChrist.org) inatoa baadhi ya mifano.

Esta 9:26–32.Sherehe ya Wayahudi ya Purimu ilianzishwa kukumbuka hadithi ya Esta. Wakati wa mlo wiki hii, fikiria kushiriki hadithi wakati wanafamilia yako, ikijumuisha mababu, walipowabariki wengine kwa kusimamia haki kama Esta alivyofanya.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Dare to Do Right,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 158.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Iga Maisha ya Mwokozi. “Nguvu za Mwokozi za kufundisha na kuwainua wengine zilikuja kutokana na jinsi Yeye alivyoishi na aina ya mtu Yeye aliyekuwa. Kadiri unavyojitahidi kwa bidii kuishi kama Yesu Kristo, ndivyo utakavyoweza zaidi kufundisha kama Yeye” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 13).

Picha
Esta

Malkia Esta, na Minerva K. Teichert, © William na Betty Stokes

Chapisha