Kuwaimarisha Waumini Wapya
Boresha Kujifunza Injili


“Boresha Kujifunza Injili,” Njia Yangu ya Agano (2020)

“Boresha Kujifunza Injili,” Njia Yangu ya Agano

Picha
mwanaume na mwanamke wakijifunza

Boresha Kujifunza Injili

Ni muhimu kusali na kujifunza maandiko kila mara, binafsi na pamoja na familia yako (kama inawezekana). Unapofanya hivyo, utahisi Roho na kupata mwongozo katika maisha yako ya kila siku.

  • Jifunze kuhusu kukua karibu zaidi na Mwokozi kupitia kujifunza maandiko na sala kila siku. Fikiria kutumia:

  • Ikiwa bado hujapakua , pakua aplikesheni ya Gospel Library au nenda kwenye ChurchofJesusChrist.org ili kupata hotuba, makala, video na zaidi. Kama unatumia kifaa cha Android, unaweza kupakua aplikesheni hii kutoka Google Play store. Kama unatumia kifaa cha iOS, unaweza kupakua aplikesheni hii kutoka kwenye Apple App Store.

  • Magazeti ya Kanisa yanaweza kukusaidia kumfuata Mwokozi kama muumini wa Kanisa Lake.

    • Kuna magazeti matatu ya Kanisa: gazeti la Liahona kwa ajili ya watu wazima, Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana kwaa vijana, na gazeti la Rafiki kwa ajili ya watoto. Unaweza kuyapata kidigitali bila malipo katika sehemu ya “Magazeti” katika Gospel Library. Kama wewe ni muumini mpya na ungependelea nakala ya gazeti lililochapwa, wasiliana na askofu au rais wako wa tawi ili upate magazeti ya mwaka mzima bure.

  • Kama wewe ni kijana mkubwa kati ya miaka 18 na 30, jifunze kuhusu chuo kwa kusoma “The Purpose of Institute” kwenye ChurchofJesusChrist.org na jifunze kuhusu YA Weekly katika Gospel Library.

  • Azimia kujifunza maandiko kila siku, hasa kutoka katika Kitabu cha Mormoni, na sala (ona Matendo ya Mitume 17:11).

Chapisha