Njoo, Unifuate 2024
Oktoba 28–Novemba 3: “Ningetaka Kwamba Ningeweza Kuwashawishi Wote … Kutubu.” Mormoni 1–6


Oktoba 28–Novemba 3:‘Ningetaka Kwamba Ningeweza Kuwashawishi Wote … Kutubu.’ Mormoni 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Kitabu cha Mormoni 2024 (2023)

“Oktoba 28–Novemba 3. Mormoni 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: 2024 (2023)

Picha
Mormoni akiandika kwenye mabamba ya dhahabu

Mormoni Akifupisha Mabamba, na Tom Lovell

Oktoba 28–Novemba 3: “Ningetaka Kwamba Ningeweza Kuwashawishi Wote … Kutubu”

Mormoni 1–6

Mormoni alitunyima “maelezo kamili” ya “mandhari ya kutisha” ya uovu na umwagaji damu ambao aliuona miongoni mwa Wanefi (Mormoni 2:18; 5:8). Lakini kile alichoandika katika Mormoni 1–6 ni cha kutosha kutukumbusha ni kiasi gani watu ambao walikuwa wenye haki wanaweza kuanguka. Katikati ya uovu uliokithiri kiasi hiki, hakuna anayeweza kumlaumu Mormoni kwa kuchoka na hata kufa moyo. Na bado katika yote ambayo aliyaona na kuyapitia, hakupoteza kamwe ufahamu wake wa rehema kuu ya Mungu na msimamo wake kwamba toba ndiyo njia ya kuipokea rehema hiyo. Na ingawa watu wa Mormoni wenyewe walikataa mialiko yake ya kuwasihi watubu, alijua kwamba alikuwa na hadhira kubwa ya kuishawishi. “Tazama,” alitangaza, “Nawaandikia wote wanaoishi ulimwenguni.” Kwa maneno mengine, alikuandikia wewe (ona Mormoni 3:17–20). Na ujumbe wake kwako, leo hii, ni ujumbe sawa na ule ambao ungewaokoa Wanefi katika siku yao: “Amini injili ya Yesu Kristo. … Tubuni na mjitayarishe kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo” (Mormoni 3:21–22).

Ona pia “Mormon Preserves the Record to Bring the House of Israel to Christ” (video), Maktaba ya Injili.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Mormoni 1–6

Picha
ikoni ya seminari
Ninaweza kumfuata Yesu Kristo licha ya jambo ambalo watu wengine wanalifanya.

Kufikia wakati yeye alipokuwa na takribani miaka 10 tu, Mormoni alikuwa tofauti sana na watu wengine waliomzunguka. Unaposoma Mormoni 1 1–6, tafuta njia ambazo imani ya Mormoni katika Yesu Kristo ilimfanya yeye awe wa kipekee na kumpatia fursa za kuwatumikia na kuwabariki wengine. Mistari ifuatayo ingeweza kukuwezesha uanze:

Mormoni 1:2–3, 13–17.Je! Unaona tofauti ipi kati ya Mormoni na watu wake? Ni sifa zipi yeye alikuwa nazo ambazo zilimsaidia kubakia imara katika nyakati kama hizo?

Mormoni 2:18–19.Ni maneno yapi Mormoni aliyatumia kuelezea ulimwengu alimoishi? Ni kwa jinsi gani yeye alidumisha tumaini licha ya mazingira yake?

Mormoni 3:12.Ni kwa jinsi gani Mormoni alihisi kuhusu watu waliokuwa karibu naye? Je, unaweza kufanya nini kukuza aina ya upendo aliokuwa nao?

Ni mistari ipi mingine katika Mormoni 1–6 inaangazia imani ya Mormoni katika Yesu Kristo? Ni fursa zipi yeye alipatiwa kwa sababu alichagua kubakia mwaminifu?

Fikiria kujifunza ujumbe wa Rais Thomas S. Monson, “Kuwa Mfano na Nuru” (Liahona, Nov. 2015, 86–88) ukitafuta sababu za kwa nini ilikuwa muhimu kwa wafuasi wa Yesu Kristo kujidhihirisha au kuwa tofauti. Ni kwa jinsi gani ungekamilisha sentensi kama hizi? “ alikuwa mfano kwangu wakati [yeye] . Hii ilinisaidia nitake kufanya .”

Mormoni angeweza kuhisi kwamba mfano wake haukuwa unaleta tofuati kwa watu wake. Kama wewe ungekuwa na nafasi ya kuzungumza na Mormoni, ni kipi ungemwambia kuhusu jinsi mfano wake ulivyoleta tofauti kwako wewe.

Ona pia David A. Bednar, “Quick to Observe,” Ensign, Dec. 2006, 30–36, au Liahona, Des. 2006, 14–20; “Something Different about Us: Example” (video), Maktaba ya Injili; Mada za Injili, “Living the Gospel of Jesus Christ,” Maktaba ya Injili.

Wasaidie wengine washiriki kile wanachojifunza. Wakati watu wanaposhiriki kile walichojifunza, wanaimarisha imani yao wenyewe na imani ya wengine (ona Mafundisho na Maagano 88:122). Jaribu kuiuliza familia yako au darasa lako ni uzoefu upi walipata wakati walipokuwa wakijifunza neno la Mungu.

Picha
Wanefi na Walamani wakipigana vita wao kwa wao.

Vita, na Jorge Cocco

Mormoni 2:10–15

Huzuni kwa jinsi ya Mungu inaniongoza kwa Kristo na kwenye badiliko la kudumu.

Wakati Mormoni alipoona huzuni ya watu wake, alitumaini wangetubu. Lakini “huzuni yao haikuwa ya toba” (Mormoni 2:13)—haikuwa huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu inayoelekeza kwenye badiliko la kweli. Ili kuelewa tofauti, fikiria kuandika kile ambacho umejifunza kutoka katika Mormoni 2:10–15 katika chati kama hii:

Huzuni Iliyo kwa jinsi ya Mungu

Huzuni kwa jinsi ya Ulimwengu

Anakuja kwa Yesu (mstari wa 14)

Anamlaani Mungu (mstari wa 14)

Ni kwa jinsi gani unaweza kujua ikiwa huzuni ni kwa jinsi ya Mungu au kwa jinsi ya ulimwengu? Kama unapata huzuni kwa jinsi ya ulimwengu, ni kwa jinsi gani unaweza kuibadilisha iwe huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu?

Ona pia 2 Wakorintho 7:8–11; Mitchell D. Graig, “Kutoridhika kwa Kiungu,” Liahona, Nov. 2018, 52–55.

Mormoni 3:3, 9

“Hawakufahamu kwamba Bwana ndiye aliye warehemu.”

Mormoni aliona kwamba Wanefi hawakutambua jinsi ambavyo Bwana alikuwa amewabariki. Unaposoma Mormoni 3:3, 9, ungeweza kutafakari jinsi unavyotambua ushawishi wa Mungu katika maisha yako. Ni baraka zipi huja wakati unapotambua ushawishi Wake? Ni yapi matokeo ya kutomtambua Yeye? (ona Mormoni 2:26; Mafundisho na Maagano 59:21).

Ona Henry B. Eyring, “Ee Kumbuka, Kumbuka,” Liahona, Nov. 2007, 66-69.

Mormoni 5:8–24; 6:16–22

Yesu Kristo anasimama na mikono iliyokunjuliwa ili anipokee.

Kama umeshawahi kuhisi kukata tamaa kuhusu dhambi zako mwenyewe, maelezo ya Mormoni kuhusu Mwokozi akisimama “na mikono iliyokunjuliwa kukupokea” yangeweza kuleta hakikisho. Unaposoma Mormoni 5:8–24 na 6:16–22, unajifunza nini kuhusu hisia za Baba wa Mbinguni na Yesu kwako, na hata unapotenda dhambi? Ni kwa jinsi gani umehisi Yesu Kristo akikufikia kwa mikono iliyokunjuliwa? Je, unahisi msukumo wa kufanya nini kama matokeo?

Ona “Njoo kwa Yesu,” Nyimbo za Dini, na. 59.

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Mormoni 1:1–3; 2:1, 23–24; 3:1–3, 12, 17–22

Kama Mormoni, ninaweza kumfuata Yesu Kristo

  • Kwa sababu Mormoni alikuwa mdogo sana wakati alipokuza imani yake katika Kristo, anaweza kuwa msukumo kwa watoto wako. Pengine ungeweza kusoma Mormoni 1:1–3 na watoto wako wangeweza kusikiliza Mormoni alikuwa na umri gani wakati Amaroni alipomkabidhi jukumu maalumu. Ungeweza pia kuwasaidia wapate katika mistari hii sifa ambazo Amaroni aliziona kwa Mormoni. Je, ni kwa jinsi gani sifa hizi zinatusaidia tumfuate Yesu Kristo?

    Picha
    Mormoni akiwa mvulana mdogo

    Mormoni, Miaka 10, na Scott M. Snow

  • Kwa sababu Mormoni alimfuata Yesu Kristo, alipatiwa fursa za kuwahudumia na kuwabariki wengine. Ungeweza kuwaalika watoto wako wasome kifungu kimoja au zaidi cha maneno yafuatayo na wasaidie washiriki kile wanachojifunza kuhusu Mormoni: Mormoni 1:1–3; 2:1, 23–24; na 3:1–3, 12, 20–22 (ona pia “Mlango wa 49: Mormoni na Mafundisho Yake,” Hadithi za Kitabu cha Mormoni, 138–42). Je, ni kwa jinsi gani yeye alimfuata Yesu Kristo? Je, ni kwa jinsi gani imani yake katika Yesu Kristo inawasaidia au kuwabariki wengine? Je! ni kwa jinsi gani imani yetu inaweza kuwasaidia watu tunaowajua?

Mormoni 2:8–15

Huzuni kwa jinsi ya Mungu inaniongoza kwa Kristo na kwenye badiliko la kudumu.

  • Pengine ungeweza kutengeneza chati kama ile iliyo katika “Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani” ili kuwasaidia watoto wako waelewe tofauti kati ya huzuni iliyo kwa jinsi ya ulimwengu na huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu wakati wanaposoma Mormoni 2:8, 10–15. Waalike watoto wachunguze Mormoni 2:12 ili kupata sababu ya kwa nini toba inapaswa kuifanya “mioyo yetu … iwe na furaha.” Ni kwa jinsi gani tunaweza kuhakikisha kwamba huzuni tunayoihisi kwa ajili ya dhambi zetu inatuongoza kwenye kutafuta msaada wa Mungu na kubadilika?

Mormoni 3:3, 9

Baba wa Mbinguni hunipa baraka nyingi.

  • Kuwaalika watoto wako waorodheshe (au wachore picha ya) baadhi ya vitu wanavyovitolea shukrani ingekuwa njia nzuri ya kuwasaidia wahisi shukrani kwa Mungu. Baada ya kuwa wametengeneza orodha, ungeweza kusoma Mormoni 3:3, 9 na ueleze kwamba Baba wa Mbinguni aliwabariki Wanefi pia, lakini hawakutambua. Ni kipi tunaweza kufanya ili tuoneshe tuna shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya baraka zetu?

Mormoni 3:12

Baba wa Mbinguni ananitaka nimpende kila mtu.

  • Ingawa Wanefi walikuwa waovu, Mormoni kamwe hakukoma kuwapenda. Wasaidie watoto watafute maneno “pendwa” na “penda” katika Mormoni 3:12. Mngeweza pia kuimba pamoja wimbo kuhusu kuwapenda wengine, kama vile “Jesus Said Love Everyone” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 61), wakati ukionesha picha za watoto kutoka ulimwenguni kote. Shuhudia juu ya upendo wa Mungu kwa watoto Wake wote.

Kwa ajili ya mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la gazeti la Rafiki.

Picha
mabamba ya dhahabu

Kitabu cha Mormoni kiliandikwa ili “kwamba ninyi mpate kuamini injili ya Yesu Kristo” (Mormoni 3:21).

Chapisha