Agano Jipya 2023
Aprili 10–16. Mathayo 15–17; Marko 7–9: “Wewe Ndiwe Kristo”


“Aprili 10–16. Mathayo 15–17; Marko 7–9: ‘Wewe Ndiwe Kristo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Aprili 10–16. Mathayo 15–17; Marko 7–9,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Kugeuka sura kwa Kristo

Kugeuka Sura kwa Kristo, na Carl Heinrich Bloch

Aprili 10–16

Mathayo 15–17; Marko 7–9

“Wewe Ndiwe Kristo”

Kusoma maandiko humwalika Roho Mtakatifu katika maisha yako. Mojawapo ya huduma muhimu za Roho Mtakatifu ni kushuhudia juu ya Yesu Kristo. Unaposoma maandiko wiki hii, zingatia hisia za kiroho ambazo huimarisha ushuhuda wako juu ya Mwokozi.

Andika Misukumo Yako

Je, si ya kushangaza kwamba Mafarisayo na Masadukayo walitaka kwamba Yesu awaonyeshe “ishara kutoka mbinguni”? Je, miujiza Yake mingi iliyojulikana vyema haikutosha? Je, vipi kuhusu mafundisho Yake yenye nguvu au njia nyingi Yeye alizotimiza unabii wa kale? Hitaji lao halikuchochewa na ukosefu wa ishara bali kwa kutokuwa radhi “kutambua ishara” na kuzikubali. (Ona Mathayo 16:1–4.)

Petro, kama Mafarisayo na Masadukayo, alishuhudia miujiza ya Mwokozi na kusikia mafundisho Yake. Lakini ushuhuda wa hakika wa Petro, “Wewe Ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai,” haukuja kupitia milango yake ya fahamu za kimwili— “mwili na damu” yake. Ushuhuda wake ulifunuliwa kwake na “Baba yetu aliye mbinguni.” Ufunuo ni mwamba ambao juu yake Mwokozi alijenga Kanisa Lake wakati huo na sasa—ufunuo kutoka mbinguni kuja kwa watumishi Wake. Na huu ndio mwamba ambao juu yake tunaweza kujenga ufuasi wetu—ufunuo kwamba Yesu ndiye Kristo na kwamba watumishi Wake wanashikilia “funguo za ufalme.” Tunapokuwa tumejengwa juu ya msingi huu, “milango ya kuzimu haitatushinda [sisi]” (Mathayo 16:15–19).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mathayo 4:13–17

Ushuhuda juu ya Yesu Kristo unakuja kwa ufunuo.

Kama Yesu Kristo akiwauliza watu leo, “Watu hunena Mwana wa Mtu kuwa ni nani?” wangeweza kusema nini? Je, wewe ungejibu nini kama Yesu angekuuliza “Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?” (Ona Mathayo 16:13–15.)

Tafakari ushuhuda wako juu ya Mwokozi na jinsi gani uliupokea. Je, unajifunza nini kutoka Mathayo 16:15–17 ambacho kinaweza kuuimarisha? Kama ungependa kujifunza zaidi kuhusu ushuhuda na ufunuo binafsi, yachunguze maandiko haya: Yohana 15:26; 2 Nefi 31:17–18; Alma 5:45–48; na Mafundisho na Maagano 8:2–3.

Ona pia “Rais Nelson: Msilize Yeye—Ufunuo Binafsi” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Mathayo 16:13–19; 17:1–9; Marko 9:2–9

“Funguo za ufalme wa mbinguni” ziko duniani leo.

“Funguo za ufalme wa mbinguni” ambazo Mwokozi aliahidi kumpatia Petro ni funguo za ukuhani (Mathayo 16:19). Funguo za ukuhani ni nini? Kwa nini tunazihitaji? Tafakari maswali haya wakati unaposoma kuhusu ahadi za Mwokozi katika Mathayo 16:13–19 na utimizwaji wake katika Mathayo 17:1–9; Marko 9:2–9 (ona pia Tafsiri ya Joseph Smith, Marko 9:3 [katika Marko 9:4, tanbihi a]).

Taarifa zingine za kukusaidia kuhusu funguo za ukuhani hujumuisha Mafundisho na Maagano 65:2; 107:18–20; 110:11–16; 128: 9–11; “Funguo za Ukuhani” katika Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org); na ujumbe wa Mzee Gary E. Stevenson “Zi Wapi Funguo za Ukuhani na Mamlaka ya Ukuhani?,” (Liahona, Mei 2016, 29–32). Unapojifunza taarifa hizi, fikiria kutengeneza orodha ya kile ulichojifunza kuhusu funguo za ukuhani na baraka ambazo hutoka kwake. Kwa nini unafikiri ufunguo ni ishara nzuri kwa ajili ya haki ya kuelekeza huduma za ukuhani?

Ona pia Dallin H. Oaks, “Ukuhani wa Melkizedeki na Funguo,” Liahona, Mei 2020, 69–72; Kamusi ya Biblia, “Kugeuka Sura, Mlima wa.”

Picha
sanamu ya Petro akiwa ameshikilia funguo

Funguo za ukuhani ni mamlaka ya kuongoza matumizi ya ukuhani.

Mathayo 17:14–21; Marko 9:14–29

Katika kutafuta imani kubwa, ninaweza kuanzia na imani ambayo tayari ninayo.

Baba aliyetajwa katika Mathayo 17 na Marko 9 alikuwa na sababu za kuwa na shaka kwamba Yesu angeweza kumponya mwanawe. Aliwaomba wanafunzi wa Yesu wamponye kijana wake, na hawakuweza. Lakini alipomuomba Mwokozi muujiza, alichagua kuonesha imani. “Bwana, naamini,” alisema. Kisha, katika kutambua kwamba imani yake haikuwa kamilifu, aliongeza “Nisaidie kutokuamini kwangu.”

Je, Roho anakufundisha nini unaposoma kuhusu muujiza huu? Je, ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni amekusaidia kuzidisha imani yako? Je, unaweza kufanya nini ili kujenga juu ya imani ambayo tayari unayo? Pengine ungeweza kukusanya orodha ya maandiko, jumbe za mikutano, au uzoefu ambao umeimarisha imani yako.

Ona pia Jeffrey R. Holland, “Bwana, Naamini,” Liahona, Mei 2013, 93–95.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Mathayo 15:7–9; Marko 7:6–7.Kuna tofauti gani kati ya kumheshimu Mungu kwa midomo, au maneno yetu, na kumheshimu Yeye kwa mioyo yetu?

Mathayo 15:17–20; Marko 7:18–23..Kwa nini tunapaswa kuwa waangalifu kwa kile tunachoweka katika midomo yetu? Kulingana na kile Yesu alichofundisha katika mistari hii, kwa nini tunapaswa hata kuwa waangalifu kuhusu kile kinachotoka katika midomo yetu—na kutoka katika mioyo yetu? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuiweka mioyo yetu kuwa safi?

Mathayo 16:15–17Ni kwa jinsi gani Mungu anatufunulia sisi kwamba Yesu ndiye “Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai”? (mstari wa16). Tunawezaje kujiandaa kupokea ufunuo huu kutoka Kwake?

Mathayo 16:13–19; 17:1–9.Ili kuwafundisha watoto kuhusu funguo za ukuhani, unaweza kusimulia hadithi ya Mzee Gary E. Stevenson kuhusu kufungiwa nje ya gari lake (ona video “Zi Wapi Funguo na Mamlaka ya Ukuhani?” katika ChurchofJesusChrist.org). Unaweza kuwaacha watoto wako watumie funguo kufungua nyumba, gari, au makufuli mengine. Fikiria kuonyesha picha ya Rais wa Kanisa na kushuhudia kwamba yeye anashikilia funguo zote za ukuhani, kama ilivyokuwa kwa Petro.

Mathayo 17:20.Manabii wenye imani katika Yesu Kristo kihalisi wamehamisha milima (ona Yakobo 4:6; Musa 7:13). Lakini kwa kawaida, huo sio muujiza tunaouhitaji. Rais M. Russell Ballard alifundisha, “Ikiwa tutakuwa na imani hata ndogo kama punje ya haradali, Bwana anaweza kutusaidia kuondoa milima ya kukata tamaa na shaka katika majukumu yaliyo mbele yetu huku tukihudumu na watoto wa Mungu, ikiwa ni pamoja na wanafamilia, washiriki wa Kanisa, na wale ambao bado hawajajiunga na Kanisa” (“Zawadi za Thamani kutoka kwa Mungu,” Liahona, Mei 2018, 10). Je, baadhi ya milima gani katika maisha yetu ambayo inahitaji kuhamishwa? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha imani katika nguvu za Mungu za kutusaidia sisi kuhamisha milima hii?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa:“I Believe in Christ,,” Nyimbo za Kanisa, na.134

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kusanyikeni pamoja mara kwa mara. Rais Henry B. Eyring alifundisha: “Kamwe usipoteze nafasi ya kuwakusanya watoto pamoja ili kujifunza mafundisho ya Yesu Kristo. Nyakati kama hizo ni nadra sana ikilinganishwa na juhudi za adui” (“Nguvu ya Kufundisha Mafundisho,” Ensign, Mei 1999,74).

Picha
mtu akiwa na kijana mgonjwa mbele ya Yesu

Bwana, Nimemleta kwako Mwana Wangu, na Walter Rane

Chapisha